Hizbullah ya Lebanon katika tamko lake imesisitiza kuwa: “Utamaduni wa ubaguzi wa rangi na hotuba za chuki, ambazo zimekuwa zikichochewa na mikondo ya kisiasa na vyombo vya habari vya Magharibi kwa msukumo wa tawala mfululizo za Marekani na lobi za Kizayuni kwa miongo kadhaa, zimefanya juhudi za makusudi za kupotosha taswira ya Uislamu. Hatua hizi zinafanywa kwa ajili ya kutumikia miradi ya fitna, ukoloni na uharibifu, na ndizo sababu kuu zilizowapa ujasiri watu wenye misimamo mikali kufanya vitendo hivi vya aibu.”
Katika taarifa aliyotoa, Abbott pia ametangaza kizuizi cha umiliki wa ardhi ndani ya Texas kwa Baraza la CAIR. Haya yanajiri huku serikali ya shirikisho ya Marekani ikiwa haijawahi kuiweka Ikhwanul Muslimin au CAIR katika orodha ya mashirika ya kigaidi.