Msemaji wa Mfuko wa Watoto wa Umoja wa Mataifa (UNICEF) amesema kuwa, “kila dakika 17 kwa wastani, mtoto mmoja au huuawa au kupoteza uwezo fulani wa mwili,” na kueleza takwimu hizi kuwa “hazikubaliki” na “zinazoshtua.”
UNICEF imetangaza hivi karibuni kuwa takriban watoto milioni 4 nchini Afghanistan hawapati elimu kutokana na uhaba wa shule, huduma za afya, na walimu wenye sifa.
Wakati huo huo hujuma zikiendelea na ugavi wa misaada kwa Gaza ukikatizwa, Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Watoto lilionya kuhusu hali mbaya ya kibinadamu katika eneo hili na kutangaza kwamba maisha ya watoto wapatao milioni moja katika ukanda huu yako chini ya hatari na tishio kubwa.