Katika mazingira ya kuongezeka kwa mvutano wa kisiasa na kijeshi nchini Yemen, Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran, Sayyid Abbas Araqchi, amesisitiza ulazima wa kulindwa umoja wa ardhi na mamlaka ya kujitawala ya nchi hiyo, akionya dhidi ya madhara ya mgawanyiko na kuingilia masuala ya ndani. Kauli hiyo imetolewa kupitia mazungumzo ya simu na mawaziri wa mambo ya nje wa Saudi Arabia na Umoja wa Falme za Kiarabu, huku pia akigusia hali ya usalama nchini Yemen na kulaani uchokozi unaoendelea wa Israel dhidi ya Lebanon.
Waandamanaji walibeba mabango na kuziba baadhi ya barabara wakitaka hatua za haraka za kimataifa kuchukuliwa. Baadaye maandamano hayo yalizingira mgahawa wa OWO, ambapo baadhi ya wabunge wa Uingereza waliripotiwa kuwa na kikao, kabla ya kumalizika kwa amani kufuatia kuwasili kwa Polisi.