Uranium
-
Iraq: Hatutaacha urutubishaji wa urani
Iran haitakoma kurutubisha urani; ni haki yake kama taifa huru, shughuli zote zikiwa salama na zikifuatiliwa na IAEA, na mazungumzo na Marekani yanaendelea bila kujadiliwa kwenye vyombo vya habari.
-
Mazungumzo ya Marekani na Iran Yamalizika kwa Tabasamu Bila Suluhu: Iran Yakataa Kusitisha Urutubishaji wa Uranium
Mazungumzo ya nyuklia kati ya Marekani na Iran yamekamilika bila mafanikio ya msingi, huku Iran ikikataa kusitisha urutubishaji wa uranium au kuhamisha vifaa vyake nje ya nchi. Tehran imesisitiza kuwa utajirishaji ndani ya Iran ni mstari mwekundu, wakati Washington ikisisitiza haitakubali Iran kubaki na uwezo wowote wa silaha za nyuklia. Kwa hali hii, duru ijayo ya mazungumzo itaamua hatima ya diplomasia kati ya pande hizo mbili.
-
Hasira ya Lieberman kwa kushindwa kwa Israel kufikia malengo yake maovu
Hili la kusitisha mapigano ni la aibu, si mpango wa makombora wa Iran umeharibiwa wala mpango wao wa nyuklia, huu ni usitishaji mapigano usio na masharti, Iran itarutubisha Uranium (ya Nyuklia) tena.
-
Araghchi: "Kiongozi Mkuu ameweka wazi wajibu wa Iran kuhusu urani na kwamba suala la urutubishaji wa Urani (uranium enrichment) halipo mezani
Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran, Abbas Araqhchi, alizungumza kuhusu msimamo wa Marekani katika mazungumzo ya nyuklia na kusisitiza kwamba suala la urutubishaji wa urani (uranium enrichment) halipo kabisa katika meza ya majadiliano. Alisema kuwa urutubishaji si jambo ambalo linapaswa kujadiliwa, kwani haki ya Iran ya kuendeleza mpango wake wa nyuklia ni jambo la msingi na lililowekwa wazi. Aidha, aliongeza kuwa: Kiongozi Mkuu alisema wazi kuhusu hili katika majadiliano yaliyopita na hakubali kuona suala hili likiingizwa tena katika mchakato wa majadiliano.