Msemaji wa Makao Makuu ya Khatam al-Anbiya (s) amesema Iran haitaruhusu Marekani kuingilia Mlango wa Hormuz na ameonya kuwa endapo miundombinu ya Iran itashambuliwa, Vikosi vya Ulinzi vya Iran vitajibu kwa mashambulizi makubwa dhidi ya miundombinu iliyosalia katika eneo.
Kiongozi Mkuu wa Mapinduzi ya Kiislamu amesisitiza umuhimu wa kulinda umoja wa wananchi, akionya kuwa adui anatumia mbinu za kueneza mifarakano ya kijamii baada ya kushindwa kufikia malengo yake kupitia mashinikizo ya kijeshi, kiuchumi na kisiasa.