Inaonekana wazi kuwa vyombo vya habari pinzani, hususan mitandao ya Kifarsi inayohusishwa na Wazayuni na Magharibi, kwa makusudi vimeepuka kuzingatia madai halisi ya wafanyabiashara na badala yake vinalenga kuchochea mivutano na machafuko ya kijamii.
Katika dunia ya sasa, ni vigumu kujua ukweli kamili kwa urahisi, hivyo ni muhimu kuwa na vyombo vya habari vya kuaminika vinavyotumia vyanzo vya haki na kuthibitisha taarifa kabla ya kuzisambaza. Hivyo ndio Vyombo vya kufuatilia na kusikiliza. Na sio kufuata kila chombo cha Habari bila kujua kuwa hiki chombo kinatumiwa na waovu wa uistikbari wa Dunia au la.