Ubalozi wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran nchini Austria umesisitiza kuwa historia inaonyesha uimara wa wananchi wa Iran dhidi ya wavamizi, ukieleza kuwa maadui wa haki na wahalifu wanaotafutwa kimataifa hawatapata chochote isipokuwa fedheha na aibu.
Mwenyekiti wa Baraza la Wanazuoni wa Kiislamu wa Bahrain alisisitiza kuwa kuacha njia ya Muqawama (mapambano dhidi ya wavamizi na dhulma) hakuzai chochote isipokuwa fedheha, udhalilishaji na utumwa.
Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Kimataifa ya AhlulBayt (a.s) akieleza kuwa tabia njema ya Mtume (s.a.w.w) ilikuwa ndiyo sababu kuu ya ushawishi wake, aliongeza: "Popote palipo na maadili ya Mtume, hakika yataacha athari yake.