Katibu Mkuu wa Hezbollah, Sheikh Naim Qassem, amekosoa vikali makubaliano ya mfumo yaliyofikiwa mjini Washington kati ya serikali ya Lebanon na Israel, akiyataja kuwa ni makubaliano ya fedheha yanayokiuka mamlaka ya taifa la Lebanon na kutoa fursa kwa Israel kuendeleza uvamizi wake.
Balozi wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran nchini Iraq, Bw. Muhammad Kazim Al-Sadiq, ametuma tamko maalum la shukrani kwa Marjaa wa kidini, serikali, wananchi, hasa makabila, vijana na vyombo vya ulinzi na usalama vya Iraq kwa kufanikisha maadhimisho ya Arubaini ya Imam Hussein (a.s).