Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran imelaani vikali kile ilichokiita “uchokozi wa kijeshi” wa Marekani dhidi ya nchi hiyo, ikisisitiza kuwa Iran haitasita kutumia haki yake ya kujilinda dhidi ya mashambulizi yoyote yanayoilenga.
Makao Makuu ya Khatam al-Anbiyaa (s) yamesema vikosi vya Jeshi la Iran na Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu vimeshambulia baadhi ya kambi za Marekani katika eneo la Mashariki ya Kati, vikieleza kuwa hatua hiyo ni jibu kwa mashambulizi ya Marekani dhidi ya maeneo ya kusini mwa Iran.