Kwa mujibu wa Shirika la Habari la Kimataifa la Ahlul-Bayt (as) -ABNA-, Makao Makuu ya Kijeshi ya "Khatam al-Anbiyaa (s)" yametangaza kuwa yamelenga baadhi ya kambi za kijeshi za Marekani katika eneo la Mashariki ya Kati kufuatia kile ilichokitaja kuwa ni uchokozi wa jeshi la Marekani dhidi ya maeneo ya kusini mwa Iran alfajiri ya Jumatano.
Katika taarifa iliyotolewa alfajiri ya leo, makao hayo yalisema kuwa hatua hiyo imechukuliwa kujibu mashambulizi ya jeshi la Marekani dhidi ya maeneo ya kusini mwa Iran kwa madai ya kuangusha helikopta yake. Taarifa hiyo ilieleza kuwa vikosi vya Jeshi la Iran pamoja na walinzi wa Islamic Revolutionary Guard Corps (IRGC) vilitekeleza mashambulizi makali dhidi ya baadhi ya vituo vya Marekani katika eneo hilo.
Makao Makuu ya Khatam al-Anbiyaa (s) yalisisitiza kuwa Iran haitasita kujibu kwa nguvu hatua yoyote ya kijeshi itakayolenga usalama na mamlaka yake ya kitaifa, huku yakionya kuwa matokeo ya vitendo vya uchokozi yatawabebesha wahusika gharama kubwa.
Your Comment