Kamanda wa Makao Makuu ya Khatam al-Anbiyaa (s), Meja Jenerali Abdollahi, amesema ushiriki mkubwa wa wananchi katika kipindi cha siku 100 zilizopita umeonyesha umoja wa kipekee wa taifa la Iran na kuwa sehemu muhimu ya nguvu za kimkakati za kuzuia maadui wa nchi hiyo.
Makao Makuu ya Khatam al-Anbiyaa (s) yamesema vikosi vya Jeshi la Iran na Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu vimeshambulia baadhi ya kambi za Marekani katika eneo la Mashariki ya Kati, vikieleza kuwa hatua hiyo ni jibu kwa mashambulizi ya Marekani dhidi ya maeneo ya kusini mwa Iran.