Israel
-
Waziri wa Ulinzi Pakistan: Ulimwengu wa Kiislamu lazima uungane kukabiliana na tishio la Israel
Waziri wa Ulinzi wa Pakistan, Khawaja Muhammad Asif, amesema kuwa Israel ni tishio kwa nchi za Kiislamu na kutoa wito kwa ulimwengu wa Kiislamu kuungana na kuchukua hatua za pamoja kukabiliana na tishio hilo.
-
Mahakama ya Israel Yasitisha Pendekezo la Ben Gvir la Kuweka Mamba Kuzunguka Gereza la Ketziot
Mahakama ya Israel imesitisha pendekezo la Waziri wa Usalama wa Taifa, Itamar Ben Gvir, la kuweka mamba kuzunguka Gereza la Ketziot linalowashikilia wafungwa wa Kipalestina, kufuatia kesi iliyowasilishwa na shirika la kutetea haki za wanyama.
-
Mvutano Wazidi kati ya Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Israel Baada ya Jeshi Kukataa Amri ya Kufukuzwa kwa Kamanda
Mvutano umeibuka kati ya Waziri wa Ulinzi wa Israel na uongozi wa jeshi baada ya jeshi kukataa kutekeleza amri ya kumfukuza Kamanda wa Kikosi cha Kanda ya Kati, likisema waziri huyo hana mamlaka ya kufanya uamuzi huo.
-
Mwandishi wa Marekani: Trump Hana Ujasiri wa Kuanzisha Vita Dhidi ya Iran
Mwandishi na mwanahabari wa Marekani Ethan Levins amesema kuwa Rais Donald Trump hana uwezo wa kuanzisha vita dhidi ya Iran, akidai kuwa matamshi yake ya vitisho yana lengo la kuiridhisha Israel kuliko kuonyesha nia ya kuchukua hatua za kijeshi.
-
Mhadhiri wa Sala ya Ijumaa Tehran: Makombora na Diplomasia Vimeimarisha Mizani ya Nguvu kwa Manufaa ya Iran
Mhadhiri / Khatibu wa Sala ya Ijumaa mjini Tehran amesema uwezo wa makombora ya Iran pamoja na diplomasia madhubuti ndivyo vilivyoimarisha mizani ya nguvu kwa manufaa ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran, huku akisisitiza umuhimu wa kulinda mshikamano wa kitaifa na kuimarisha imani ya wananchi.
-
Mamlaka ya Palestina: Serikali ya Netanyahu Inawajibika Kikamilifu kwa Kuongezeka kwa Mvutano Katika Ukingo wa Magharibi
Mamlaka ya Palestina imeishutumu serikali ya Netanyahu kwa kuhusika kikamilifu na uhalifu wa kila siku unaofanywa na walowezi wa Kizayuni dhidi ya Wapalestina, huku ikionya kuwa upanuzi wa makazi ya walowezi na kuongezeka kwa hatua za kijeshi kunaweza kuusukuma Ukingo wa Magharibi kuelekea mlipuko mkubwa wa hali ya mambo.
-
Araghchi: Iran Iliingia Katika Mazungumzo Ili Kuthibitisha Kuwa Marekani na Israel Hawawezi Kujadiliana kwa Uaminifu
Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran, Abbas Araghchi, amesema kuwa Iran iliingia katika mazungumzo baada ya kutumia njia zote za kidiplomasia, ili kuthibitisha kwamba tatizo halikutokana na kutokuwepo kwa mazungumzo.
-
Haaretz: Enzi ya utawala wa Marekani na zama za Netanyahu zimefikia mwisho
Gazeti la Kiebrania la Haaretz limesema kuwa baada ya vita vya hivi karibuni, Iran imekaribia zaidi nafasi ya kuwa nguvu kuu ya kikanda katika Ghuba ya Uajemi, huku likidai kuwa enzi ya utawala wa Marekani, mfumo wa dunia wa upande mmoja na zama za Waziri Mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu zimefikia mwisho.
-
Afisa wa Lebanon: Makubaliano Mapya na Israel Hayana Uhalali wa Kisheria
Afisa wa Lebanon, Bassam Al-Hashem, amesema kuwa makubaliano ya mfumo yaliyopendekezwa na Israel hayana thamani ya kisheria bila kuidhinishwa na Baraza la Mawaziri na Bunge la Lebanon, akionya kuwa baadhi ya vipengele vyake vinakiuka mamlaka ya taifa.
-
Seneta wa Marekani Lindsey Graham afariki dunia akiwa na umri wa miaka 71
Ofisi ya Seneta Lindsey Graham imetangaza kuwa mwanasiasa huyo wa Chama cha Republican amefariki dunia akiwa na umri wa miaka 71 baada ya kile kilichoelezwa kuwa "ugonjwa wa ghafla wa muda mfupi."
-
Macron: Hezbollah Ikabidhi Silaha Zake, Israel Iondoe Vikosi Vyake Lebanon
Rais wa Ufaransa, Emmanuel Macron, amesisitiza kuwa Hezbollah inapaswa kukabidhi silaha zake kwa mamlaka ya Lebanon, huku akitaka pia Israel iondoe vikosi vyake kutoka maeneo ya kusini mwa Lebanon ili kuimarisha amani na utulivu wa kudumu katika eneo hilo.
-
Kauli ya Sheikh Naim Qassem: Makubaliano ya Mfumo kati ya Lebanon na Israel ni “Fedheha na Kusaliti Mamlaka ya Taifa”
Katibu Mkuu wa Hezbollah, Sheikh Naim Qassem, amekosoa vikali makubaliano ya mfumo yaliyofikiwa mjini Washington kati ya serikali ya Lebanon na Israel, akiyataja kuwa ni makubaliano ya fedheha yanayokiuka mamlaka ya taifa la Lebanon na kutoa fursa kwa Israel kuendeleza uvamizi wake.
-
Marekani yafichua rasimu ya makubaliano ya amani kati ya Israel na Lebanon kwa upatanishi wa Washington
Wizara ya Mambo ya Nje ya Marekani imeweka wazi maandishi ya makubaliano ya awali ya amani kati ya Israel na Lebanon yaliyofikiwa kupitia upatanishi wa Marekani mjini Washington. Makubaliano hayo yanalenga kumaliza uhasama wa muda mrefu, kuimarisha usalama wa mipaka, na kuweka utaratibu wa hatua kwa hatua wa kuimarisha mamlaka ya dola nchini Lebanon huku vikosi vya Israel vikijipanga upya kwa awamu.
-
Umoja wa Ulaya Washindwa Kufikia Makubaliano Kuhusu Kumuwekea Vikwazo Itamar Ben-Gvir
Msemaji wa masuala ya nje wa Tume ya Ulaya amesema kuwa nchi wanachama wa Umoja wa Ulaya hazikufikia mwafaka kuhusu pendekezo la kumuwekea vikwazo Waziri wa Usalama wa Ndani wa Israel, Itamar Ben-Gvir, huku zikilaani kauli zake za uchochezi dhidi ya Lebanon.
-
Wapinzani wa Serikali ya Iran Wakosolewa kwa Kushindwa; Wachambuzi Wasema Hawana Ushawishi wa Kijamii
Wanasiasa na wachambuzi kadhaa wa Iran wameeleza kuwa makundi ya upinzani wa nje yameshindwa kufikia malengo yao kwa miongo kadhaa na yamepoteza ushawishi wake ndani ya Iran, huku wakidai hata Marekani na Israel haviyaoni tena kama nguvu yenye athari ya kisiasa.
-
Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran Aikosoa Australia kwa Kuwachukulia Hatua Madaktari Wanaoikosoa Israel
Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran anayeshughulikia Masuala ya Kisheria na Kimataifa, Kazem Gharibabadi, amesema hatua dhidi ya madaktari nchini Australia wanaokosoa Israel ni shambulio dhidi ya uhuru wa kujieleza na dhamira ya taaluma ya tiba.
-
Iran Yafunga Mlango wa Bahari wa Hormuz; Yaanza Hatua za Kujibu Ukiukaji wa Makubaliano na Marekani na Israel
Khalil Nasrallah: Iran yafunga Mlango wa Bahari wa Hormuz kama hatua ya kwanza ya kujibu ukiukaji wa makubaliano unaodaiwa kufanywa na Marekani na Israel; sasa mpira uko kwa Donald Trump.
-
J.D. Vance: Trump Ndiye Mshirika Pekee Mwenye Nguvu wa Israel
Makamu wa Rais wa Marekani, J.D. Vance, amesema Rais Donald Trump ndiye mshirika pekee mwenye nguvu wa Israel kwa sasa, akiwataka viongozi wa Tel Aviv kuacha kuikosoa Washington huku akisisitiza kuwa sehemu kubwa ya silaha za Israel hutolewa na Marekani kwa fedha za walipa kodi wa Marekani.
-
Iran Yasitisha Mazungumzo ya Nyuklia na Marekani Kufuatia Mashambulizi ya Israel Lebanon
Iran imesitisha safari ya ujumbe wake kwenda Geneva kwa ajili ya duru ya kwanza ya mazungumzo ya nyuklia na Marekani, ikieleza kuwa kuendelea kwa mashambulizi ya Israel kusini mwa Lebanon kumekiuka mazingira ya kusitisha mapigano. Kufuatia msimamo huo, Makamu wa Rais wa Marekani, JD Vance, naye ameripotiwa kusitisha safari yake, huku hali hiyo ikiweka mashaka juu ya kuanza kwa mazungumzo yaliyokuwa yanatarajiwa kuwa hatua ya kwanza ya utekelezaji wa makubaliano ya hivi karibuni kati ya Tehran na Washington.
-
Sheikh Naim Qassem: Iran ni Alama ya Heshima na Nguzo ya Muqawama Dhidi ya Israel
Katibu Mkuu wa Hezbollah, Sheikh Naim Qassem, amesema katika barua yake kwa Spika wa Bunge la Iran, Mohammad Bagher Qalibaf, kwamba Iran imeonyesha kwa vitendo uungaji mkono wake kwa haki, muqawama na waliodhulumiwa. Ameeleza kuwa mchango wa Iran umeimarisha uwezo wa Lebanon kujitetea na kuitaja Iran kuwa "alama ya heshima na utukufu" katika kukabiliana na utawala wa Kizayuni.
-
Makao Makuu ya Khatam al-Anbiya (S) Yaionya Israel: Mashambulizi dhidi ya Lebanon Yakendelea, Iran Itajibu kwa Nguvu
Makao Makuu ya Khatam al-Anbiya (S) yameionya Israel kwamba ikiwa itaendelea na mashambulizi dhidi ya kusini mwa Lebanon na kukiuka makubaliano ya usitishaji mapigano, itakabiliwa na jibu kali kutoka kwa Vikosi vya Wanajeshi vya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran.
-
Al-Sisi aishutumu Israel kupanua “mstari wa njano” Gaza wakati dunia ikijishughulisha na Iran
Rais wa Misri Abdel Fattah al-Sisi ameitaka Israel kusitisha mara moja hatua ya kupanua eneo la “mstari wa njano” ndani ya Gaza, akisema inafanyika wakati macho ya dunia yameelekezwa kwenye mgogoro wa Iran.
-
Uholanzi Yazindua Kumbukumbu ya Kugusa Hisia za Wahanga wa Gaza kwa Maelfu ya Viatu vya Watoto
Maelfu ya viatu vya watoto na picha za waandishi wa habari waliouawa Gaza zimeoneshwa katika uwanja wa Den Bosch nchini Uholanzi katika tukio la kumbukumbu lililolenga kuwakumbuka zaidi ya watoto 21,000 waliopoteza maisha na kulaani ukimya wa kimataifa kuhusu janga hilo.
-
Makubaliano ya Iran na Marekani Yazua Mabadiliko Mapya ya Kisiasa Mashariki ya Kati
Makubaliano ya amani kati ya Iran na Marekani yameibua mabadiliko makubwa ya kisiasa Mashariki ya Kati, huku yakionekana kuwa ushindi wa diplomasia lakini yakizua mvutano mpya kuhusu Lebanon, Israel na mustakabali wa uhusiano wa Washington na Tel Aviv.
-
Trump: Netanyahu ni Mtu Mgumu Sana; Anapaswa Kuishukuru Marekani
Rais wa Marekani Donald Trump amesema Waziri Mkuu wa Israel, Benjamin Netanyahu, ni "mtu mgumu sana," akisisitiza kuwa anapaswa kuishukuru Marekani kwa juhudi zake za kuzuia Iran kumiliki silaha za nyuklia, akidai kuwa bila hatua hizo Israel isingekuwepo endapo Iran ingekuwa na silaha hizo.
-
Qalibaf: Muqawama wa Lebanon na Diplomasia ya Iran Vinahakikisha Uhuru na Uadilifu wa Ardhi ya Lebanon
Spika wa Bunge la Iran, Mohammad Baqer Qalibaf, amesema jihadi ya Muqawama wa Kiislamu nchini Lebanon pamoja na diplomasia madhubuti ya Iran vinahakikisha mamlaka na uadilifu wa ardhi ya Lebanon, akisisitiza kuwa maadui hawataweza kamwe kuitenga au kuisambaratisha nguzo yoyote ya Muqawama.
-
Makao Makuu ya Khatam al-Anbiyaa: Adui Hana Njia Nyingine Isipokuwa Kukubali Kushindwa na Kusalimu Amri
Makao Makuu ya Khatam al-Anbiyaa (as) yamesema wananchi wa Iran na vikosi vyao vya ulinzi, kwa msaada wa Mwenyezi Mungu na chini ya uongozi wa Amiri Jeshi Mkuu, vimethibitisha kuwa Marekani na Israel hawana njia nyingine isipokuwa kukiri kushindwa na kusalimu amri mbele ya uthabiti wa taifa la Iran.
-
Uchambuzi: Mashambulizi ya Beirut na Mvutano Mpya wa Kikanda
Kinachoendelea katika shambulizi la Israel dhidi ya Beirut ni kama ifuatavyo: Mashambulizi ya Israel Kusini mwa Beirut yanaonyesha kuendelea kwa mivutano ya kikanda, huku ukiwepo msisitizo kuwa Muqawama - Upinzani- wa Lebanon (Hezbollah) unaona una uhalali wa kukabiliana na jaribio lolote la adui Israel katika kubadilisha mlingano wa usalama katika nchi ya Lebanon.
-
Gazeti la Kizayuni: Israel Yakabiliwa na Wimbi Lisilo la Kawaida la Vikwazo vya Kimataifa
Gazeti la Yedioth Ahronoth limesema utawala wa Kizayuni wa Israel umekumbwa na ongezeko kubwa la vikwazo na shinikizo la kimataifa tangu Oktoba 2023, huku baadhi ya viongozi wake wakikabiliwa na hati za kukamatwa na marufuku ya kuingia katika nchi mbalimbali.
-
Netanyahu Awataka Raia wa Lebanon Kuungana na Israel Dhidi ya Hezbollah
Waziri Mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu ametoa wito kwa raia wa Lebanon kujitenga na Hezbollah, akidai kuwa kundi hilo limeishikilia nchi hiyo “mateka” na kusisitiza kuwa Israel haina uhasama na wananchi wa Lebanon.