Israel
-
Kauli ya Sheikh Naim Qassem: Makubaliano ya Mfumo kati ya Lebanon na Israel ni “Fedheha na Kusaliti Mamlaka ya Taifa”
Katibu Mkuu wa Hezbollah, Sheikh Naim Qassem, amekosoa vikali makubaliano ya mfumo yaliyofikiwa mjini Washington kati ya serikali ya Lebanon na Israel, akiyataja kuwa ni makubaliano ya fedheha yanayokiuka mamlaka ya taifa la Lebanon na kutoa fursa kwa Israel kuendeleza uvamizi wake.
-
Marekani yafichua rasimu ya makubaliano ya amani kati ya Israel na Lebanon kwa upatanishi wa Washington
Wizara ya Mambo ya Nje ya Marekani imeweka wazi maandishi ya makubaliano ya awali ya amani kati ya Israel na Lebanon yaliyofikiwa kupitia upatanishi wa Marekani mjini Washington. Makubaliano hayo yanalenga kumaliza uhasama wa muda mrefu, kuimarisha usalama wa mipaka, na kuweka utaratibu wa hatua kwa hatua wa kuimarisha mamlaka ya dola nchini Lebanon huku vikosi vya Israel vikijipanga upya kwa awamu.
-
Umoja wa Ulaya Washindwa Kufikia Makubaliano Kuhusu Kumuwekea Vikwazo Itamar Ben-Gvir
Msemaji wa masuala ya nje wa Tume ya Ulaya amesema kuwa nchi wanachama wa Umoja wa Ulaya hazikufikia mwafaka kuhusu pendekezo la kumuwekea vikwazo Waziri wa Usalama wa Ndani wa Israel, Itamar Ben-Gvir, huku zikilaani kauli zake za uchochezi dhidi ya Lebanon.
-
Wapinzani wa Serikali ya Iran Wakosolewa kwa Kushindwa; Wachambuzi Wasema Hawana Ushawishi wa Kijamii
Wanasiasa na wachambuzi kadhaa wa Iran wameeleza kuwa makundi ya upinzani wa nje yameshindwa kufikia malengo yao kwa miongo kadhaa na yamepoteza ushawishi wake ndani ya Iran, huku wakidai hata Marekani na Israel haviyaoni tena kama nguvu yenye athari ya kisiasa.
-
Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran Aikosoa Australia kwa Kuwachukulia Hatua Madaktari Wanaoikosoa Israel
Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran anayeshughulikia Masuala ya Kisheria na Kimataifa, Kazem Gharibabadi, amesema hatua dhidi ya madaktari nchini Australia wanaokosoa Israel ni shambulio dhidi ya uhuru wa kujieleza na dhamira ya taaluma ya tiba.
-
Iran Yafunga Mlango wa Bahari wa Hormuz; Yaanza Hatua za Kujibu Ukiukaji wa Makubaliano na Marekani na Israel
Khalil Nasrallah: Iran yafunga Mlango wa Bahari wa Hormuz kama hatua ya kwanza ya kujibu ukiukaji wa makubaliano unaodaiwa kufanywa na Marekani na Israel; sasa mpira uko kwa Donald Trump.
-
J.D. Vance: Trump Ndiye Mshirika Pekee Mwenye Nguvu wa Israel
Makamu wa Rais wa Marekani, J.D. Vance, amesema Rais Donald Trump ndiye mshirika pekee mwenye nguvu wa Israel kwa sasa, akiwataka viongozi wa Tel Aviv kuacha kuikosoa Washington huku akisisitiza kuwa sehemu kubwa ya silaha za Israel hutolewa na Marekani kwa fedha za walipa kodi wa Marekani.
-
Iran Yasitisha Mazungumzo ya Nyuklia na Marekani Kufuatia Mashambulizi ya Israel Lebanon
Iran imesitisha safari ya ujumbe wake kwenda Geneva kwa ajili ya duru ya kwanza ya mazungumzo ya nyuklia na Marekani, ikieleza kuwa kuendelea kwa mashambulizi ya Israel kusini mwa Lebanon kumekiuka mazingira ya kusitisha mapigano. Kufuatia msimamo huo, Makamu wa Rais wa Marekani, JD Vance, naye ameripotiwa kusitisha safari yake, huku hali hiyo ikiweka mashaka juu ya kuanza kwa mazungumzo yaliyokuwa yanatarajiwa kuwa hatua ya kwanza ya utekelezaji wa makubaliano ya hivi karibuni kati ya Tehran na Washington.
-
Sheikh Naim Qassem: Iran ni Alama ya Heshima na Nguzo ya Muqawama Dhidi ya Israel
Katibu Mkuu wa Hezbollah, Sheikh Naim Qassem, amesema katika barua yake kwa Spika wa Bunge la Iran, Mohammad Bagher Qalibaf, kwamba Iran imeonyesha kwa vitendo uungaji mkono wake kwa haki, muqawama na waliodhulumiwa. Ameeleza kuwa mchango wa Iran umeimarisha uwezo wa Lebanon kujitetea na kuitaja Iran kuwa "alama ya heshima na utukufu" katika kukabiliana na utawala wa Kizayuni.
-
Makao Makuu ya Khatam al-Anbiya (S) Yaionya Israel: Mashambulizi dhidi ya Lebanon Yakendelea, Iran Itajibu kwa Nguvu
Makao Makuu ya Khatam al-Anbiya (S) yameionya Israel kwamba ikiwa itaendelea na mashambulizi dhidi ya kusini mwa Lebanon na kukiuka makubaliano ya usitishaji mapigano, itakabiliwa na jibu kali kutoka kwa Vikosi vya Wanajeshi vya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran.
-
Al-Sisi aishutumu Israel kupanua “mstari wa njano” Gaza wakati dunia ikijishughulisha na Iran
Rais wa Misri Abdel Fattah al-Sisi ameitaka Israel kusitisha mara moja hatua ya kupanua eneo la “mstari wa njano” ndani ya Gaza, akisema inafanyika wakati macho ya dunia yameelekezwa kwenye mgogoro wa Iran.
-
Uholanzi Yazindua Kumbukumbu ya Kugusa Hisia za Wahanga wa Gaza kwa Maelfu ya Viatu vya Watoto
Maelfu ya viatu vya watoto na picha za waandishi wa habari waliouawa Gaza zimeoneshwa katika uwanja wa Den Bosch nchini Uholanzi katika tukio la kumbukumbu lililolenga kuwakumbuka zaidi ya watoto 21,000 waliopoteza maisha na kulaani ukimya wa kimataifa kuhusu janga hilo.
-
Makubaliano ya Iran na Marekani Yazua Mabadiliko Mapya ya Kisiasa Mashariki ya Kati
Makubaliano ya amani kati ya Iran na Marekani yameibua mabadiliko makubwa ya kisiasa Mashariki ya Kati, huku yakionekana kuwa ushindi wa diplomasia lakini yakizua mvutano mpya kuhusu Lebanon, Israel na mustakabali wa uhusiano wa Washington na Tel Aviv.
-
Trump: Netanyahu ni Mtu Mgumu Sana; Anapaswa Kuishukuru Marekani
Rais wa Marekani Donald Trump amesema Waziri Mkuu wa Israel, Benjamin Netanyahu, ni "mtu mgumu sana," akisisitiza kuwa anapaswa kuishukuru Marekani kwa juhudi zake za kuzuia Iran kumiliki silaha za nyuklia, akidai kuwa bila hatua hizo Israel isingekuwepo endapo Iran ingekuwa na silaha hizo.
-
Qalibaf: Muqawama wa Lebanon na Diplomasia ya Iran Vinahakikisha Uhuru na Uadilifu wa Ardhi ya Lebanon
Spika wa Bunge la Iran, Mohammad Baqer Qalibaf, amesema jihadi ya Muqawama wa Kiislamu nchini Lebanon pamoja na diplomasia madhubuti ya Iran vinahakikisha mamlaka na uadilifu wa ardhi ya Lebanon, akisisitiza kuwa maadui hawataweza kamwe kuitenga au kuisambaratisha nguzo yoyote ya Muqawama.
-
Makao Makuu ya Khatam al-Anbiyaa: Adui Hana Njia Nyingine Isipokuwa Kukubali Kushindwa na Kusalimu Amri
Makao Makuu ya Khatam al-Anbiyaa (as) yamesema wananchi wa Iran na vikosi vyao vya ulinzi, kwa msaada wa Mwenyezi Mungu na chini ya uongozi wa Amiri Jeshi Mkuu, vimethibitisha kuwa Marekani na Israel hawana njia nyingine isipokuwa kukiri kushindwa na kusalimu amri mbele ya uthabiti wa taifa la Iran.
-
Uchambuzi: Mashambulizi ya Beirut na Mvutano Mpya wa Kikanda
Kinachoendelea katika shambulizi la Israel dhidi ya Beirut ni kama ifuatavyo: Mashambulizi ya Israel Kusini mwa Beirut yanaonyesha kuendelea kwa mivutano ya kikanda, huku ukiwepo msisitizo kuwa Muqawama - Upinzani- wa Lebanon (Hezbollah) unaona una uhalali wa kukabiliana na jaribio lolote la adui Israel katika kubadilisha mlingano wa usalama katika nchi ya Lebanon.
-
Gazeti la Kizayuni: Israel Yakabiliwa na Wimbi Lisilo la Kawaida la Vikwazo vya Kimataifa
Gazeti la Yedioth Ahronoth limesema utawala wa Kizayuni wa Israel umekumbwa na ongezeko kubwa la vikwazo na shinikizo la kimataifa tangu Oktoba 2023, huku baadhi ya viongozi wake wakikabiliwa na hati za kukamatwa na marufuku ya kuingia katika nchi mbalimbali.
-
Netanyahu Awataka Raia wa Lebanon Kuungana na Israel Dhidi ya Hezbollah
Waziri Mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu ametoa wito kwa raia wa Lebanon kujitenga na Hezbollah, akidai kuwa kundi hilo limeishikilia nchi hiyo “mateka” na kusisitiza kuwa Israel haina uhasama na wananchi wa Lebanon.
-
Mchambuzi wa Zamani wa CIA: Marekani na Israel Zinajaribu Kuhujumu Mazungumzo na Iran
Mchambuzi wa zamani wa CIA Larry Johnson amesema mashambulizi dhidi ya Iran wakati mazungumzo yakiendelea yanaashiria juhudi za kuhujumu mchakato wa kidiplomasia, akionya kuwa huenda eneo hilo likashuhudia duru mpya ya mvutano katika siku zijazo.
-
Makao Makuu ya Khatam al-Anbiyaa Yatangaza Kushambulia Kambi za Marekani Kufuatia Uchokozi Dhidi ya Iran
Makao Makuu ya Khatam al-Anbiyaa (s) yamesema vikosi vya Jeshi la Iran na Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu vimeshambulia baadhi ya kambi za Marekani katika eneo la Mashariki ya Kati, vikieleza kuwa hatua hiyo ni jibu kwa mashambulizi ya Marekani dhidi ya maeneo ya kusini mwa Iran.
-
Mtandao wa Israel Wakiri: Mizani ya Kimkakati Inaendelea Kubadilika kwa Faida ya Iran
Mtandao wa Channel 12 wa Israel umekiri kuwa mashambulizi ya makombora ya Iran dhidi ya maeneo yanayokaliwa kwa mabavu yameonesha uwezo wa Tehran kuunganisha tena medani mbalimbali za mapambano, huku Israel ikikabiliwa na changamoto mpya za kimkakati.
-
Makundi ya Muqawama Iraq Yalionya Serikali ya Mpito ya Syria Dhidi ya Ushirikiano na Marekani na Israel
Makundi ya Muqawama nchini Iraq yametoa onyo kali kwa serikali ya mpito ya Syria, yakisema kuwa ushirikiano wowote wa kijeshi au kiusalama na Marekani na Israel dhidi ya Hizbullah ya Lebanon utakabiliwa na jibu la kijeshi.
-
Waziri wa Vita wa Israel Aishambulia Uturuki kwa Maneno Makali: “Israel Haiko Katika Hali ya Kusambaratika”
Waziri wa Vita wa Israel ametoa kauli kali dhidi ya viongozi wa Uturuki, akisisitiza kuwa Israel si dola inayoporomoka kama ilivyokuwa baadhi ya himaya za kihistoria. Aidha, amekosoa kile alichodai kuwa ni ndoto za kufufua Himaya ya Ottoman na kuionya Ankara dhidi ya sera zake za kikanda.
-
Mkuu wa Mahakama ya Iran: Lengo la Mashambulizi ya Israel dhidi ya Beirut ni Kubadili Muundo wa Kidemografia wa Lebanon
Mkuu wa Idara ya Mahakama ya Iran amesema kuwa lengo kuu la mashambulizi ya Israel dhidi ya Beirut ni kufanya mauaji ya halaiki dhidi ya Waislamu wa Kishia nchini Lebanon na kubadili muundo wa kidemografia wa nchi hiyo. Amesisitiza kuwa Iran na Muqawama wa Lebanon ni washirika wa muda mrefu wanaosaidiana katika nyanja za kijeshi na kiutendaji.
-
Aliyekuwa Waziri wa Ulinzi wa Marekani Aonya: Mgogoro wa Iran Unaweza Kuwa “Vietnam ya Trump”
Waziri wa zamani wa Ulinzi wa Marekani ameonya kuwa mgogoro wa sasa unaohusishwa na Iran unaweza kufanana na vita vya Vietnam, akisisitiza uwezekano wa matokeo yasiyo thabiti na hitaji la makubaliano dhaifu ambayo yanaweza kusababisha mivutano ya baadaye.
-
Iran Yalaani Marekani na Israel kwa Mauaji ya Watoto katika Migogoro ya Kivita
Iran imeishutumu Marekani na Israel kwa kile inachokiita mauaji ya watoto wasio na hatia kupitia vita, mashambulizi na ukaliaji katika maeneo mbalimbali, ikisisitiza kuwa watoto ndio wahanga wakuu wa migogoro inayoendelea duniani.
-
Naim Qassem: Hezbollah Haitasalimisha Silaha na Itaendelea Kupambana Hadi Israel Iondoke Lebanon
Katibu Mkuu wa Hezbollah, Naim Qassem, amesema Hezbollah haitasalimisha silaha zake wala kukubali makubaliano ya mazungumzo kati ya Lebanon na Israel, akisisitiza kuwa harakati hiyo itaendelea kupambana hadi majeshi ya Israel yaondoke kikamilifu katika ardhi ya Lebanon.
-
Mustafa Mahmoud: Mataifa Maskini Yasidanganywe na Ahadi za Nguvu Kubwa
Mwanafikra wa Misri, Mustafa Mahmoud, aliwahi kuonya kuwa mataifa yanayoendelea hayapaswi kutegemea ahadi na mikataba ya mataifa makubwa kama dhamana ya usalama na ustawi wao, akisisitiza umuhimu wa kujitegemea kiuchumi, kulinda rasilimali za taifa na kudumisha umoja wa kitaifa ili kukabiliana na changamoto na maslahi ya kisiasa katika mfumo wa kimataifa.
-
Iran Yatoa Onyo Kali kwa Walowezi wa Kaskazini mwa Israel Endapo Beirut Itashambuliwa
Iran imeonya kuwa kushambuliwa kwa vitongoji vya kusini mwa Beirut kutakabiliwa na majibu makali, huku ikiwataka walowezi wa Kaskazini mwa Israel kuondoka katika maeneo hayo kwa ajili ya usalama wao iwapo mashambulizi hayo yatatekelezwa.