Israel
-
Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani atazuru Qatar kesho
Gazeti la Washington Post, likinukuu maafisa wawili wa serikali ya eneo hilo, limeripoti kuwa Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani anatarajiwa kufanya ziara nchini Qatar kesho, siku ya Jumanne.
-
-
Uhamaji wa Waisraeli 11,000 Baada ya Vita na Iran | Walihama ili kukimbia Makombora ya Iran
Kwa Mujibu wa Taarifa, kurejea kikamilifu kwa wakimbizi hawa majumbani mwao kutachukua miaka kadhaa.
-
Wimbi la Kukatisha Ushirikiano wa Vyuo Vikuu Duniani na Israel
Chuo Kikuu cha Amsterdam kimefuta mpango wa kubadilishana wanafunzi na Chuo Kikuu cha Kiebrania cha Yerusalemu, huku Jumuiya ya Ulaya ya Wanaanthropolojia wa Kijamii ikitangaza marufuku ya aina yoyote ya ushirikiano na Israel.
-
Kuhukumiwa Myahudi wa Kiyahudi Orthodox nchini Israel kwa shtaka la kushirikiana na Iran
Moja ya majukumu hayo lilikuwa kutuma kifurushi cha vitisho kwa mwakilishi wa Israel katika Shirika la Kimataifa la Nishati ya Atomiki. Mahakama imesema ingawa Stern hakutekeleza baadhi ya majukumu hayo, lakini kwa sababu alikubali na kuanza kuyafuatilia, ametambuliwa kuwa na hatia
-
Watu wa Iran na Jeshi Watasimama na Qatar: Kamanda Mkuu
Shambulio dhidi ya Qatar lisingeweza kutokea bila kupata idhini kutoka Washington.
-
Spika Mike Johnson Asisitiza Kuzuia Vurugu za Kisiasa Kufuatia Kifo cha Charlie Kirk
Shambulio dhidi ya Qatar lisingeweza kutokea bila kupata idhini kutoka Washington.
-
Hezbollah: Uhalifu wa Wavamizi Dhidi ya Yemen Unaonesha Kiwango cha Kufilisika Kwao
Hezbollah imetoa tamko likisema kuwa: "Uhalifu na mashambulizi yanayofanywa na wavamizi (yaani utawala wa Kizayuni wa Israel) dhidi ya Yemen ni ishara ya wazi ya kufilisika kwao kisiasa, kiakhlaqi na kijeshi."
-
Israel imefanya mashambulizi ya anga dhidi ya Sanaa (Mji Mkuu wa Yemen) na Mkoa wa Al-Jawf
Kwa mujibu wa wizara ya afya ya Yemen, mashambulizi ya Israeli yaliyoelekezwa Sanaa na Mkoa wa Al-Jawf yamesababisha watu wasiopungua 35 kuuawa na zaidi ya 130 kujeruhiwa.
-
Sheikh Naeem Qassem:
Uvamizi wa Wazayuni Dhidi ya Qatar Ni Sehemu ya Mradi wa "Israeli Kubwa"/ Msimamo wa Iran wa Kuunga Mkono Palestina Ni Miongoni mwa Nguzo Kuu za Umoja
Akiwahutubia viongozi wa nchi za Kiarabu, Sheikh Qassem alisema: "Pendekezo langu la pili ni hili: Msisimame pamoja na Israel, msiisaliti Harakati ya Mapambano kwa kujaribu kuipokonya silaha au kukubali masharti ya utawala wa Kizayuni."
-
Majibu ya kwanza ya Qatar kufuatia shambulizi la Israel dhidi ya Qatar: Uchunguzi unafanyika katika ngazi ya juu kabisa!!!
Qatar imelaani shambulizi la Israel dhidi ya Hamas mjini Doha.
-
Prof. Pillar | "Kutambuliwa kwa Palestina na Ulaya Ni Ishara Tu ya Kidiplomasia"
“Ahadi za kuitambua Palestina bado ni hatua ya kidiplomasia tu. Mradi tu Israel inaendelea kuikalia ardhi ya Palestina, taifa la kweli la Palestina haliwezi kusimama"
-
Jeshi la Yemen Lashambulia Tel Aviv kwa Makombora ya “Falastin-2” na “Dhulfikar”
"Adui wa Kizayuni hatapata usalama wala utulivu. Mashambulizi yetu yataendelea kwa kasi kubwa zaidi katika hatua ijayo.”
-
Chama cha Kimataifa cha Utafiti wa Mauaji ya Kimbari: Israel Imetekeleza Mauaji ya Kimbari Gaza
Rais wa chama kikubwa zaidi duniani cha wataalamu wa masuala ya mauaji ya kimbari (IAGS) ametangaza kuwa taasisi hiyo imepitisha azimio linalothibitisha kuwa vitendo vya Israel katika Ukanda wa Gaza vinaendana na vigezo vya kisheria vya mauaji ya kimbari.
-
Wayemen hawawezi kushindwa
Gazeti la Kizayuni Jerusalem Post, katika ripoti yake, limesisitiza kuwa Taifa la Yemen haliwezi kushindwa na likabainisha wazi kuwa Israel haitaki vita vya moja kwa moja na Yemen.
-
Israel imeushambulia tena Mji Mkuu wa Yemen, Sanaa / Milipuko 10 Mfululizo imetokea katika Mji wa Sanaa
Katika muktadha wa mzozo unaoongezeka kati ya Israel na vikosi vya kijeshi vya Yemen, jeshi la Israel limefanya mashambulizi makubwa ya anga dhidi ya Sanaa.
-
Katibu Mkuu wa Hizbullah: Kama siyo Muqawama, Israel ingeingia Beirut / Kamwe hatutaweka silaha chini
Sheikh Qasim alieleza kuwa ramani ya njia ya baadaye ni: kufukuza adui kutoka ardhi ya Lebanon, kusimamisha uvamizi, kuwaachia huru wafungwa, kuanza upya ujenzi wa taifa na kisha kushughulika na mkakati wa ulinzi wa kitaifa.
-
Shambulio Kubwa la Anga la Israel Dhidi ya Mji Mkuu wa Yemen – Ansarullah Yasema Itaendelea Kuunga Mkono Gaza
Vyombo vya habari vya Israel vimeripoti kuwa vyombo vya ujasusi vya Tel Aviv vinaandaa orodha kubwa ya malengo mapya nchini Yemen kwa mashambulizi yajayo.
-
Abdulmalik al-Houthi Awashutumu Waislamu Bilioni Mbili kwa “Kukaa Kimya” Kuhusu Matukio ya Gaza
Katika hotuba yake, al-Houthi alieleza kwa masikitiko na ghadhabu hali ya “kutochukua hatua” kwa Waislamu zaidi ya bilioni mbili duniani, akisema kuwa ukimya huo ni “aibu na fedheha” inayoweza kuleta madhara si tu kwa Palestina, bali pia kwa ulimwengu mzima wa Kiislamu.
-
Jeshi la Israel lawageukia Wayahudi wa Kigeni ili kutatua uhaba wa wanajeshi
Kwa mujibu wa ripoti hiyo, jeshi la Israel linapanga kuwalenga zaidi Wayahudi vijana wenye umri wa miaka 18 hadi 25 kutoka Marekani na Ufaransa, kuwahimiza wahamie katika ardhi zinazokaliwa kwa mabavu na kujiandikisha jeshini kwa kipindi cha miaka kadhaa.
-
Mmiliki wa Mawkibu Muiraq Katika Mahojiano na ABNA:
Arubaini ni fursa yenye thamani kubwa ya kubainisha uhalisia wa Jamhuri ya Kiislamu na tabia ya kinyama ya Israel
Mmiliki wa Mawkibu kutoka Iraq, akisisitiza umuhimu wa Jihadi ya Kuelimisha katika siku za Arubaini ya Imam Hussein (a.s), amesema kuwa siku hizi ni fursa muhimu ya kuwapa uelewa mataifa mbalimbali.
-
Mufti wa Oman:
“Inasikitisha kuwa waandishi wa habari wanauawa Gaza na baadhi wanaendelea kuwaunga mkono wavamizi”
Mufti wa Oman amelaani mauaji ya waandishi wa habari katika mji wa Gaza yaliyofanywa na jeshi la Israel, na kutamka masikitiko yake juu ya kuendelea kwa baadhi ya watu na nchi kuunga mkono wavamizi.
-
Alim wa Kishia wa Pakistan:
Waarabu kwa Usaliti Wao Wameiacha Palestina Ikiwa na Majeraha Makubwa Yasiyotibika
Mmoja wa maulamaa mashuhuri wa Kishia nchini Pakistan amesema kuwa usaliti wa Uturuki, baadhi ya nchi za Kiarabu na washirika wao umeacha majeraha makubwa yasiyoweza kupona katika mwili wa Palestina.
-
Sudan Kusini na Israel: Ushirikiano wa Kistratejia au Mgongano wa Maslahi?
Kwa ziara rasmi ya Waziri wa Mambo ya Nje wa Sudan Kusini nchini Israel, uhusiano wa muda mrefu lakini wa kimya wa mataifa haya mawili umeingia katika hatua mpya.
-
Jeshi la Mapinduzi la Iran Laonya Marekani na Israel: Jibu Litakuwa Kali Mno Kuliko Mnavyodhani
Iran iko tayari kwa Operesheni Kubwa Dhidi ya Wachokozi kwa muda wowote ule.
-
Makelele ya Maafisa wa Kijeshi wa Zamani wa Israel dhidi ya Vita ya Gaza: "Tuko Kwenye Ukingo wa Kushindwa kwa Kihistoria"
Amos Malka, aliyewahi kuwa mkuu wa idara ya ujasusi wa kijeshi, pia alitoa onyo kuwa:"Tuko karibu na ukingo wa kushindwa. Malengo ya awali ya kijeshi yalitimia muda mrefu uliopita, lakini kwa sababu za kisiasa – si za kijeshi – mapigano yanaendelea, na hali hii inaiathiri vibaya Israel kisiasa na kiusalama."
-
Jeshi la Yemen Latangaza Awamu ya Nne ya Kufunga Njia za Baharini, Latoa Onyo kwa Ndege Zinazosaidia Israel
Ndege yoyote, iwe ya kijeshi au kibiashara, itakayojihusisha na shughuli za kusaidia Israel, tutaiangamiza. Itaingia kwenye historia.
-
Ayatollah Sistani Aitaka Dunia ya Kiislamu Kuchukua Hatua Haraka Kuhusu Njaa Inayoikumba Gaza
Kauli ya Ayatollah Sistani inakuja wakati ambapo mashirika ya misaada ya kibinadamu yanaonya kuwa njaa inasambaa kwa kasi kote Gaza, huku takwimu za Umoja wa Mataifa zikionesha kuwa karibu watu nusu milioni wanakumbwa na viwango vya juu vya njaa kali.
-
Rais wa Iran: Mashambulizi ya Israel na Marekani dhidi ya Iran Yameleta Umoja wa Kitaifa Usio na Mfano
"Leo tunashuhudia kwa macho yetu kuwa kila Muirani - awe ni mfuasi wa Serikali au mpinzani wake - amekuwa sauti moja katika kutetea hadhi, uhuru, na mamlaka ya nchi yetu".
-
Mwanamke Mmoja akamatwa kwa tuhuma za kujaribu kumuua Netanyahu
Duru za Israel zimeripoti kukamatwa kwa Mwanamke mmoja kwa tuhuma za kujaribu kumuua Waziri Mkuu wa utawala huo haram wa kizayuni.