23 Desemba 2025 - 12:29
"Tetemeko la Vitisho" – Amiri Jeshi Mkuu wa Jeshi la Jamhuri ya Kiislamu ya Iran Atoa Onyo Kali dhidi ya “Ndoto” za Mashambulizi ya Israel!

Wachambuzi wa kijeshi wanasema lugha iliyotumiwa leo si vitisho vya kawaida, bali ni tamko rasmi kwamba Iran sasa inamiliki silaha “inayovunja mizani ya nguvu”, ambayo inaweza kufichuliwa moja kwa moja katika uwanja wa vita endapo Israel itathubutu kuchukua hatua. Ngoma za vita zinapigwa… na simba wa Iran ameonyesha meno yake!

Shirika la Habari la Kimataifa la Ahlul-Bayt (as) -ABNA- Tehran imevunja ukimya wake kwa kutuma ujumbe mzito na wa kutisha kupitia Kamanda wa Vikosi vya Kijeshi Meja Jenerali Hatami akisema: “Benki yetu mpya ya malengo (shabaha) itashangaza dunia!”. Katika kauli zilizotajwa kuwa hatari na nzito zaidi kwa mwaka huu, Meja Jenerali Hatami, amevuruga kabisa mipango yote ya maadui, akitoa tahadhari kali zilizojaa nguvu na moto.
 Mambo makuu katika ‘bomu’ la kauli hizi:
1_ “Zaidi ya ufuatiliaji wa kawaida”
Waziri huyo amesema kuwa rada mpya za Iran zilizoanza kufanya kazi leo zina uwezo wa kugundua hata harakati za karibu kabisa za ndege za kivita zisizoonekana (stealth) kabla hazijakaribia mipaka ya Iran. Hii, kwa mujibu wake, inamaanisha kuwa faida ya kijeshi ya ndege aina ya F-35 imepotea kabisa. 
2_ “Kupanua duara la moto”
Kwa mara ya kwanza, waziri amedokeza kuwa “Benki ya malengo” ya Iran imesasishwa na sasa inajumuisha maeneo nyeti ambayo adui hakuyatarajia hata kidogo, akisisitiza kuwa jibu la Iran litakuwa
“la jumla, la haraka, na la kusikika duniani kote.” 
3_ “Vidole viko kwenye trigger (kifute cha kubonyeza”
Ujumbe wa moja kwa moja kwa uwanja wa vita: Iran imehama kutoka hali ya kujilinda na kuingia kwenye hali ya “kuchukua hatua ya kuzuia (deterrence proactive)”. Kosa lolote litakabiliwa na
dhoruba ya makombora” isiyokoma hadi tishio lifutwe kabisa kwenye ramani.

Kwa nini kauli hii imekuwa gumzo sasa?
Wachambuzi wa kijeshi wanasema lugha iliyotumiwa leo si vitisho vya kawaida, bali ni tamko rasmi kwamba Iran sasa inamiliki silaha “inayovunja mizani ya nguvu”, ambayo inaweza kufichuliwa moja kwa moja katika uwanja wa vita endapo Israel itathubutu kuchukua hatua.

Ngoma za vita zinapigwa… na simba wa Iran ameonyesha meno yake!
Kwa mujibu wa wachambuzi, kauli hii ni ishara kwamba hatua yoyote ya kijeshi dhidi ya Iran itakuwa na gharama kubwa na isiyotabirika.

"Tetemeko la Vitisho" – Amiri Jeshi Mkuu wa Jeshi la Jamhuri ya Kiislamu ya Iran Atoa Onyo Kali dhidi ya “Ndoto” za Mashambulizi ya Israel!

Tags

Your Comment

You are replying to: .
captcha