Jenerali Amir Hatami amesema adui sasa ametambua kuwa hana budi kuheshimu Taifa la Iran na mfumo wa Jamhuri ya Kiislamu, akisisitiza kuwa msimamo na uthabiti wa wananchi wa Iran umebadili hesabu za wapinzani wao.
Wachambuzi wa kijeshi wanasema lugha iliyotumiwa leo si vitisho vya kawaida, bali ni tamko rasmi kwamba Iran sasa inamiliki silaha “inayovunja mizani ya nguvu”, ambayo inaweza kufichuliwa moja kwa moja katika uwanja wa vita endapo Israel itathubutu kuchukua hatua.
Ngoma za vita zinapigwa… na simba wa Iran ameonyesha meno yake!
Ziara hii inakuja wakati Iran inasisitiza kuimarisha usalama wa mipaka yake na kuonyesha utayari wa jeshi katika kukabiliana na changamoto za kijeshi bila kukosa tahadhari ya kisiasa, hasa kutokana na mvutano uliopo katika eneo la Mashariki ya Kati.