silaha
-
Kutoka Mafuta hadi Silaha: Vita dhidi ya Iran Vinaathirije Masoko na Uwezo wa Marekani?
Vita vya Marekani dhidi ya Iran vimeathiri zaidi ya uwanja wa mapambano, huku usumbufu katika usambazaji wa mafuta, gesi, malighafi na mbolea ukitikisa masoko ya dunia. Wachambuzi wanaonya kuwa athari za kiuchumi na changamoto za vita vya muda mrefu zinaweza kuendelea hata baada ya vita kumalizika.
-
Mwakilishi wa Nujaba Iran: Hatutaacha uwanja wa mapambano wala kukabidhi silaha zetu
Mwakilishi wa Katibu Mkuu wa Harakat al-Nujaba nchini Iran, Hujjatul-Islam Sayyid Abbas Mousavi, amesema kuwa kwa misingi ya wajibu wa kidini, uwajibikaji na uaminifu kwa kiongozi wao aliyefariki shahidi, hawataondoka katika uwanja wa mapambano wala kukabidhi silaha zao, akisisitiza kuwa wataendelea na njia yake.
-
Kiongozi Shahidi: Sina Wasiwasi na Silaha Zinazonunuliwa na Saudi Arabia; Zitaangukia Mikononi mwa Mujahidina wa Kiislamu
Kiongozi Shahidi Ayatollah Sayyid Ali Khamenei alisema kuwa hana wasiwasi kuhusu vifaa na silaha ambazo Saudi Arabia inanunua, akisisitiza kuwa hatimaye vifaa hivyo vitaangukia mikononi mwa mujahidina wa Kiislamu.
-
New York Times: Iran Yaongeza Kujiamini Katika Kukabiliana na Marekani
Tathmini za kijasusi za Marekani zinaonyesha kuwa baada ya miezi sita ya mapigano, Iran imepata uelewa mpana zaidi wa uwezo wake wa kijeshi na udhaifu wa nguvu za Marekani.
-
Mwakilishi wa Hamas Tehran: Uamuzi wa Silaha ni Haki Huru na ya Kimsingi ya Wapalestina
Mwakilishi wa Harakati ya Hamas nchini Iran, Khaled Qadoumi, amesema kuwa uamuzi kuhusu silaha za upinzani ni suala la kitaifa na la mamlaka ya Wapalestina, akisisitiza kuwa hakuna harakati ya upinzani inayoweza kukubali kujinyang’anya silaha wakati mashambulizi dhidi ya Gaza yakiendelea.
-
Dkt. Hossam Matar: “Rais wa Jamhuriya si Dola, na tunakataa kujisalimisha”
Dkt. Hossam Matar amemkosoa Rais wa Lebanon kuhusu namna anavyotekeleza madaraka yake, akisisitiza kuwa rais ni sehemu ya mamlaka ya nchi anayefungwa na Katiba. Amesema suluhu ya kisiasa inapaswa kulinda mamlaka na haki za Lebanon, badala ya kuwa “kujisalimu” mbele ya shinikizo la Marekani.
-
Iran: Vita la hivi karibuni yaweka upya vipaumbele na mwelekeo wa viwanda vya ulinzi
Waziri wa Ulinzi wa Iran amesema vita la hivi karibuni limeibua hitaji la kuainisha upya vipaumbele vya sekta ya ulinzi, huku uzalishaji wa baadhi ya vifaa vya kijeshi ukiongezeka hadi mara kadhaa licha ya vita.
-
Mkuu wa Walinzi wa Mapinduzi: Mujahidina wa Kiislamu Walililazimisha Jeshi Lenye Silaha Nyingi Zaidi Duniani kunyenyekea (kusalimu amri)
Meja Jenerali Ahmad Vahidi amesema wapiganaji wa Kiislamu, kwa kumtegemea Mwenyezi Mungu na kwa kujitolea kwao, waliweza kulazimisha jeshi lenye silaha nyingi zaidi duniani kusalimu amri.
-
Moscow na Tehran Zafanya Mashauriano ya Kuimarisha Ushirikiano katika Usalama wa Kimataifa
Iran na Urusi zimefanya mashauriano mjini Moscow kuhusu kuimarisha ushirikiano katika masuala ya usalama wa kimataifa, yakiwemo udhibiti wa silaha, upokonyaji wa silaha na kuzuia kuenea kwa silaha za nyuklia.
-
-
IRGC: Mpango wa Kuivua Hamas Silaha Umeshindwa Kimkakati, Hautafanikiwa
Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu (IRGC) limesema mpango wa kuivua Hamas silaha umeshindwa tangu mwanzo, likisisitiza kuwa harakati za muqawama zitaendelea hadi kufikiwa kwa malengo ya ukombozi wa Palestina.
-
Kama tukio la Ashura lingetokea leo, ni simulizi gani lingekuwa gumzo zaidi kwenye mitandao ya kijamii?
Ashura haikuwa tu vita ya kijeshi iliyopiganwa katika jangwa, bali ilikuwa uwanja mkubwa wa mapambano kati ya ukweli mtupu na uongo uliopambwa kwa sura ya kuvutia. Ikiwa tukio hili lingetokea katika zama za mawasiliano ya kisasa, bila shaka mashine ya propaganda ya kambi ya batili ingetumia nguvu zake zote za kishetani kupotosha mapinduzi ya Sayyid al-Shuhadaa (a.s.), kwa lengo la kubadilisha nafasi za dhalimu na mwenye kudhulumiwa.
-
Muqawama wa Kiislamu Iraq: Jibu kwa Marekani Halitakwepeka Baada ya Arbaeen, Yatoa Onyo kwa Serikali ya Iraq
Muqawama wa Kiislamu nchini Iraq umetangaza kuwa utatoa jibu dhidi ya kile ulichokiita mashambulizi ya Marekani baada ya kumalizika kwa ibada za Arbaeen ya Imam Hussein (as), huku ukitoa muda kwa serikali ya Iraq hadi tarehe 23 Safar kuchukua msimamo kuhusu usalama na suala la silaha za makundi ya Muqawama.
-
Trump: Tuna silaha nyingi zaidi kuliko mahitaji yetu
Rais wa Marekani, Donald Trump, amekanusha madai kwamba nchi hiyo inakabiliwa na upungufu wa silaha, akisema kuwa Marekani ina akiba kubwa ya risasi na vifaa vya kijeshi, hata zaidi ya mahitaji yake ya kioperesheni.
-
Vyombo vya Habari vya Iran:
Picha za Satelaiti Zinaonyesha Jengo la Amazon Nchini Bahrain Likilengwa kwa Silaha ya Kupenya Malengo Magumu Katika Shambulio la Iran
Picha za satelaiti zenye ubora wa juu zinaonyesha kuwa jengo la kampuni ya Amazon nchini Bahrain lilipigwa na kuharibiwa kwa kutumia silaha yenye uwezo wa kupenya malengo magumu, katika shambulio linalodaiwa kufanywa na Iran.
-
Mwanazuoni wa Kisunni na Imamu wa Swala ya Ijumaa Auawa Shahidi katika Shambulio la Kigaidi Kusini-Mashariki mwa Iran
Mwanazuoni wa Kisunni na Imamu wa Swala ya Ijumaa katika Msikiti wa Ali Ibn Abi Talib, Molavi Mohammad Anwar Rigi, ameuawa Shahidi baada ya kushambuliwa na watu wenye silaha wasiojulikana katika mji wa Mirjaveh, kusini-mashariki mwa Iran. Mamlaka za eneo hilo zimesema uchunguzi unaendelea kubaini wahusika wa shambulio hilo, huku wananchi wakitakiwa kudumisha utulivu na kutoruhusu tukio hilo kuchochea migawanyiko ya kidini.
-
Makubaliano ya nyuklia kati ya Marekani na Saudi Arabia yazua wasiwasi wa kuenea kwa silaha za Nyuklia
Utawala wa Trump uliandaa makubaliano ya ushirikiano wa nyuklia na Saudi Arabia ambayo yangeruhusu ufalme huo kurutubisha urani kwa ajili ya programu yake ya nyuklia ya kiraia. Ingawa makubaliano hayo yamekamilika, bado hayajasainiwa na Rais Trump wala kuwasilishwa kwa Bunge la Marekani. Pendekezo hilo limezua mjadala kwa sababu halihitaji Saudi Arabia kupitisha Itifaki ya Ziada ya Shirika la Kimataifa la Nishati ya Atomiki (IAEA), bali linategemea makubaliano tofauti ya dhamana kati ya Marekani na Saudi Arabia. Wakosoaji wanaonya kuwa hatua hiyo inaweza kurahisisha Saudi Arabia kuendeleza uwezo wa kutengeneza silaha za nyuklia katika siku zijazo.
-
Macron: Hezbollah Ikabidhi Silaha Zake, Israel Iondoe Vikosi Vyake Lebanon
Rais wa Ufaransa, Emmanuel Macron, amesisitiza kuwa Hezbollah inapaswa kukabidhi silaha zake kwa mamlaka ya Lebanon, huku akitaka pia Israel iondoe vikosi vyake kutoka maeneo ya kusini mwa Lebanon ili kuimarisha amani na utulivu wa kudumu katika eneo hilo.
-
Makubaliano ya Iran na Marekani Yazua Mabadiliko Mapya ya Kisiasa Mashariki ya Kati
Makubaliano ya amani kati ya Iran na Marekani yameibua mabadiliko makubwa ya kisiasa Mashariki ya Kati, huku yakionekana kuwa ushindi wa diplomasia lakini yakizua mvutano mpya kuhusu Lebanon, Israel na mustakabali wa uhusiano wa Washington na Tel Aviv.
-
Trump: Netanyahu ni Mtu Mgumu Sana; Anapaswa Kuishukuru Marekani
Rais wa Marekani Donald Trump amesema Waziri Mkuu wa Israel, Benjamin Netanyahu, ni "mtu mgumu sana," akisisitiza kuwa anapaswa kuishukuru Marekani kwa juhudi zake za kuzuia Iran kumiliki silaha za nyuklia, akidai kuwa bila hatua hizo Israel isingekuwepo endapo Iran ingekuwa na silaha hizo.
-
IRGC Yadai Kuilenga na Kuiangusha Ndege Ndege Isiyo na Rubani ya Marekani MQ-9 Nchini Bushehr
Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu ya Iran (IRGC) wametangaza kuuangusha ndege isiyo na rubani ya kijeshi ya Marekani aina ya MQ-9 katika Mkoa wa Bushehr kusini mwa Iran.
-
Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran: Vikosi vya Iran Havitasita Kuilinda Nchi na Kujibu Uchokozi
Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran, Esmaeil Baqaei, amesema matukio ya usiku uliopita yameonyesha wazi kuwa vikosi vya ulinzi vya Iran viko tayari kuitetea nchi wakati wowote, huku akiilaumu Marekani kwa kudhoofisha mchakato wa kidiplomasia kupitia ujumbe unaokinzana na ukiukaji wa mara kwa mara wa usitishaji vita.
-
Putin: Iran Haina Nia ya Silaha za Nyuklia, Aunga Mkono Kusitishwa kwa Hatua za Kijeshi
Rais wa Urusi Vladimir Putin amesema kuwa Iran haina mpango wa kutengeneza silaha za nyuklia na ina haki ya kutumia urani kwa madhumuni ya amani. Aidha, ameunga mkono kusitishwa kwa hatua za kijeshi akilielezea hilo kuwa ni hatua ya busara kuelekea amani ya kudumu.
-
Njama ya Aibu: Upinzani wa India walaani ziara ya Modi nchini Israel
Ziara ya siku ya Jumatano ya Narendra Modi, Waziri Mkuu wa India, kwenda Israel, imezua ukosoaji mkubwa kutoka kwa vyama na makundi ya mrengo wa kushoto nchini humo. Makundi hayo yamemshutumu kiongozi huyo wa kitaifa mwenye msimamo wa Uhindu kwa kushirikiana au kuunga mkono vita vinavyoendelea vya Israel dhidi ya Wapalestina katika Ukanda wa Gaza. Wakosoaji wanasema kuwa ziara hiyo inapingana na msimamo wa kihistoria wa India wa kuunga mkono haki za Wapalestina na suluhisho la mataifa mawili, na wameitaka serikali kutoa maelezo ya wazi kuhusu madhumuni ya safari hiyo pamoja na makubaliano yaliyofikiwa.
-
Wasiwasi Mbili Kuu za Marekani Kuhusu Hatua ya Kijeshi Dhidi ya Iran
Kwa mujibu wa ripoti ya Politico, Marekani inajizuia kuchukua hatua ya kijeshi dhidi ya Iran kutokana na hofu ya kupungua kwa akiba ya silaha na uwezekano wa wanajeshi wake kuuawa au kujeruhiwa, huku mazungumzo yasiyo ya moja kwa moja yakiendelea mjini Geneva kwa upatanishi wa Oman.
-
Mazungumzo yaendelea kwa ajili ya kufikia makubaliano ya kunyang’anya silaha Gaza / Kikosi cha Indonesia chatarajiwa kuwasili mwezi Machi
Katika muktadha wa kunyang’anya silaha huko Gaza, mapendekezo mengi yamewasilishwa. Inabakia kuonekana iwapo Hamas na makundi ya muqawama watakubali kikamilifu suala hili. Hapo awali, mazungumzo yalihusu tu silaha nzito, lakini sasa yanajumuisha pia silaha za mtu binafsi.
-
Iran Yatoa Onyo kwa Meli: Mazoezi ya Kijeshi ya Moto wa Moja kwa Moja Yaanza katika Lango la Bahari la Hormuz
Kipeo cha Hormuz ni moja ya njia kuu za kimataifa za kusafirisha mafuta na bidhaa, hivyo zoezi lolote la kijeshi katika eneo hilo huweza kuleta athari pana za kiuchumi na kiusalama duniani.
-
Osama Hamdan: Kuzungumzia kukabidhi silaha za Muqawama ni jambo lisilo na maana
Katika mwendelezo wa matamko yanayofichua malengo ya kweli ya utawala wa Kizayuni wa Israel, mwanachama mwandamizi wa Harakati ya Hamas, Osama Hamdan, amesisitiza kuwa mazungumzo kuhusu kukabidhi silaha za Muqawama hayana msingi wowote. Ameeleza kuwa wakati Israel inakiuka ahadi zake zote, lengo lake kuu linaendelea kuwa ni kuwahamisha kwa nguvu Wapalestina kutoka Ukanda wa Gaza na Ukingo wa Magharibi.
-
Katika kumbukumbu maalumu ilielezwa;
Mahmoud Al-Hashimi: Hoja 23 Muhimu Kuhusu Mradi wa Kiamerika wa “Kuhodhi Silaha Mikononi mwa Serikali”
Mchambuzi wa masuala ya Iraq, katika kumbukumbu maalumu kwa Shirika la Habari la ABNA, aliandika: “‘Kuhodhi silaha mikononi mwa serikali’ kunahitaji kuwepo kwa serikali halisi; lakini ni vipi raia wa Iraq anaweza kuamini kuwepo kwa serikali kama hiyo, ilhali wabunge wengi wa Bunge la Taifa, chini ya shinikizo la Marekani, waliondoka kwenye ukumbi wa Bunge ili kuzuia upigaji kura kuhusu sheria ya Hashd al-Shaabi?”
-
Uchambuzi wa New York Times;
Je, , Beirut inaweza kuipokonya silaha Hezbollah ifikapo mwishoni mwa mwaka 2025?
Wachambuzi wanaonya kuwa ikiwa Beirut itaharakisha zoezi la kuipokonya silaha bila kupata mafanikio sambamba kutoka kwa Israel - kama vile kusitishwa kwa mashambulizi ya anga- hatua hiyo inaweza kuimarisha nafasi ya kisiasa na kijamii ya Hezbollah. Hii ni kwa sababu Hezbollah si kundi la kijeshi pekee, bali pia ni chama cha kisiasa chenye ushawishi mpana.