3 Septemba 2025 - 11:58
Kutoka kwenye Kampeni ya "Ziara kwa Njia ya Mbali" hadi Kuachiwa kwa Wafungwa: Maandalizi ya Wiki ya Umoja Mkoani Gilan

Sheikh Hujjatul Islam wal-Muslimin Mujtaba Ashjari, Mwenyekiti wa Baraza la Uratibu wa Matangazo ya Kiislamu mkoa wa Gilan, amesema kuwa wiki ya Umoja itashuhudia mfululizo wa shughuli za kiroho, kijamii na kusaidia wahitaji, ikiwa ni pamoja na kampeni za ibada, misafara ya furaha, utoaji wa misaada kwa familia zisizojiweza, na kusaidia wanafunzi masikini.

Kwa mujibu wa Shirika la Habari la Kimataifa AhlulBayt (a.s) -ABNA- Ashjari amesema kuwa Mtume Muhammad (s.a.w.w) ni Mtume wa huruma kwa ulimwengu wote, na umuhimu wa Umoja unaendelea kuwa urithi wa thamani uliotolewa na Mtume kwa Waislamu wote duniani.

Umoja wa Kiislamu: Silaha Dhidi ya Maadui

Ashjari alibainisha kuwa wiki ya Umoja ni fursa muhimu ya kuimarisha mshikamano kati ya Waislamu wote duniani dhidi ya maadui wa Uislamu kama vile Marekani na utawala dhalimu wa Kizayuni wa Israel. Alisema kuwa:

"Hakuna nguvu yoyote iliyo juu ya Allah au iliyo na uwezo mkubwa kuliko umoja wa taifa lenye imani thabiti katika ujumbe wa Mtume Muhammad (s.a.w)."

Akaongeza kuwa ikiwa mataifa ya Kiislamu yatasimama pamoja na kuunda safu ya pamoja, mabeberu wa dunia hawatakuwa na nafasi ya kuchochea fitina na migawanyiko.

Kaulimbiu ya Wiki ya Umoja

Sheikh Ashjari alieleza kuwa kamati ya maadhimisho ya wiki ya Umoja imeshaundwa katika mikoa yote ya Gilan, na kaulimbiu kuu kwa mwaka huu (kuadhimisha miaka 1500 ya kuzaliwa kwa Mtume) ni:

"Kwa Mapenzi ya Ahmad (s.a.w), Umoja wa Taifa, Umoja wa Umma."

Kampeni za Kiimani na Kijamii

Kampeni ya kitaifa yenye kauli mbiu: "Kwa Mapenzi ya Mtume (s.a.w) Nasamehe" imeanzishwa rasmi mkoani Gilan. Katika muktadha huu, kwa mujibu wa makubaliano kati ya Baraza la Uratibu na taasisi ya kitaifa ya kuachilia wafungwa, wafungwa wa makosa yasiyo ya jinai wataachiliwa huru na kurejea katika familia zao wakati wa wiki ya Umoja.

Sherehe, Misaada, na Huduma kwa Wenye Mahitaji

Ashjari alieleza kuwa wiki ya Umoja (kuanzia Ijumaa 14 Shahrivar hadi Jumatano 19 Shahrivar) itajumuisha:

  • Sherehe za kuzaliwa Mtume Muhammad (s.a.w.) na Imam Ja’far Sadiq (a.s) zitakazofanyika katika barabara ya kitamaduni ya "Mashahidi Dhahab" mjini Rasht na maeneo mengine, zikijumuisha hotuba, qaswida, nyimbo za kidini, muziki wa moja kwa moja, maonesho ya furaha, na fataki.

  • Matembezi ya kifamilia, misafara ya magari na pikipiki za furaha.

  • Kampeni ya "Ziara kwa Njia ya Mbali", ambapo Waislamu watasoma dua na ziara za Mtume Muhammad (s.a.w) na Imam Ali (a.s) katika misikiti na maeneo matakatifu yaliyochaguliwa.

  • Kufanyika kwa maonesho ya burudani katika vituo vya kitamaduni, kuwekwa kwa vituo vya huduma kwa jina la Mtume (s.a.w) mijini na vijijini.

  • Ununuzi na ugawaji wa vifaa vya shule na mahitaji kwa wanafunzi wa maeneo ya pembezoni.

  • Huduma za bure au zenye punguzo kutoka kwa taasisi mbalimbali.

  • Kutoa zawadi za ndoa, vifaa vya nyumbani (jahazi), na misaada ya chakula kwa familia zenye uhitaji.

Vipindi vya Runinga, Mashindano, na Maonesho

Sheikh Ashjari pia alieleza kuwa:

  • Vipindi vya runinga na redio vya kuelimisha na kufurahisha vitatayarishwa na kurushwa hewani.

  • Kutazalishwa maudhui ya kidijitali kama vile filamu fupi, video za muziki wa kidini, mabango, picha zenye maandishi, motion graphics na infographics.

  • Mashairi ya jioni (asr al-shi’r), mashindano ya utamaduni, sanaa, uandishi, na michezo, pamoja na maonesho ya sanaa na maandiko, na burudani mbalimbali kama:

    • Bendi za nyimbo za kidini.
    • Mchoro wa picha ukutani.
    • Urembeshaji wa maeneo ya wazi kwa mabango na matangazo ya kimazingira.

Tags

Your Comment

You are replying to: .
captcha