shirika la habari la abna
-
Mwakilishi wa Ayatullah Sistani:
Licha ya juhudi zote, bado haki ya kueleza na kuonesha kikamilifu ukubwa wa Arbaeen haijatimizwa
Mwakilishi mwenye mamlaka kamili wa Ayatollah Sistani nchini Iran amesema kuwa Arbaeen ni fursa kubwa sana kwa wasimamizi na wenye dhamana wa tukio hili la kimataifa, na hawapaswi kupuuzia au kughafilika na thawabu na malipo makubwa yanayopatikana kutokana nalo.
-
Kufichuliwa kwa muundo wa siri wa utawala wa Kizayuni kwa ajili ya kukwepa uwajibikaji / Haki iko chini ya upanga wa fedha na nguvu ya utawala
Tovuti ya Kifaransa Mediapart, kwa ushirikiano na vyombo vingine nane vya habari vya Ulaya, kupitia mradi unaoitwa “Faili za Utawala wa Kizayuni”, imefichua kuundwa kwa kitengo cha siri ndani ya Wizara ya Sheria ya utawala huo.
-
Dai la Wall Street Journal: Vikosi vya Marekani Vavamia Meli Iliyokuwa Ikisafirisha Shehena ya China Kwenda Iran
Kwa mujibu wa madai ya gazeti la Wall Street Journal, vikosi maalum vya Marekani vilivamia na kuteka meli iliyokuwa ikibeba shewena ya kijeshi kutoka China kuelekea Iran katika Bahari ya Hindi mnamo Novemba 2025.
-
Tanga | Sheikh Mkuu wa T.I.C Sheikh H. Jalala Mwakindenge Aongoza Hafla ya Ndoa za Vijana 100 Katika Maadhimisho ya Mazazi ya Bibi Fatima Zahra (a.s)
Hafla hii imeendelea kuwa ishara ya umoja, upendo na kuenzi Sunna ya ndoa katika Uislamu, sambamba na kuadhimisha tukio tukufu la mazazi ya Bibi Fatima Zahra (s.a).
-
Nakuru - Kenya | Khatibu wa Sala ya Ijumaa Sheikh Abdul Ghani Khatibu Aeleza Siri ya Utukufu wa Bibi Fatima (sa) kupitia Hadithi Tukufu za Mtume(saww)
Sheikh Abdul Ghani aliweka wazi kuwa mapenzi ya Mtume (saww) kwa Bibi Fatima (sa) hayawezi kuchukuliwa kwa mtazamo wa kawaida wa mapenzi ya baba kwa binti yake. Badala yake, ni tamko la kiungu na kijamii linalobainisha nafasi yake adhimu katika Uislamu.
-
Kiongozi wa Mapinduzi: Tasnia ya Madahi inapaswa kuwa kitovu cha fasihi ya Muqawama na ufafanuzi wa mafundisho ya dini na mapinduzi
Katika hotuba yake iliyochukua takriban saa tatu, Ayatullah Sayyid Ali Khamenei aliwapongeza Wairani kwa kuadhimisha kuzaliwa kwa Bibi Fatimah (a.s) na kusema kuwa “mwananchi wa Iran, kwa kupitia msimamo wa kitaifa wa kimapinduzi, ameshindwa kabisa njama za adui kutaka kubadilisha utambulisho wa kidini, kihistoria na kiutamaduni wa taifa hili.”
-
Ubalozi wa Iran: Hatua ya Marekani dhidi ya Venezuela ni wizi katika Bahari ya Karibi
Ubalozi wa Iran mjini Caracas, huku ukilaani vikali kitendo cha Marekani cha kukamata mafuta kwenye eneo la karibu na pwani ya Venezuela, umetangaza kuwa hatua hiyo ya Marekani ya kukamata meli ya mafuta ya Venezuela bila sababu yoyote ya kisheria ni ukiukwaji mkubwa wa sheria na kanuni za kimataifa.
-
Iran na Belarus zaonyesha utayari wa kuimarisha ushirikiano katika sekta ya usafirishaji na nishati
Katika maelezo ya maafisa husika, pande zote mbili zimetaja umuhimu wa kuimarisha mahusiano katika sekta muhimu za uwekezaji na usafirishaji.
-
Iran yaadhimisha Siku ya Mwanamke na Siku ya Mama sambamba na kuzaliwa kwa Bibi Fatima Zahra (a.s)
Iran ikiadhimisha kumbukumbu hii tukufu, siku hii hubakia kuwa ukumbusho wa nafasi ya milele ya Bibi Fatima Zahra (a.s) katika nyoyo za Waislamu na nafasi yake kama taa ya uongofu, heshima na ukamilifu wa kiroho.
-
Mchambuzi wa Zamani wa CIA: Uwezo wa Kijeshi wa Iran Sasa Ni Imara Zaidi na Marekani Haiwezi Kamwe Kuilazimisha Iran Ijisalimishe
Johnson anaamini kuwa Iran sasa si tu haiko dhaifu, bali imejizatiti kama mchezaji mkuu katika masuala ya kieneo, na ina uwezo wa kushughulikia changamoto na shinikizo kutoka nje.
-
Tamko la Mkurugenzi Mkuu wa Hawza za Kiislamu Kufuatia Mauaji ya Kinyama Dhidi ya Watu Wanyonge wa Sudan
Jumuiya za Kimataifa na Mashirika ya Haki za Binadamu Waitikie Kilio cha Watu Wanaodhulumiwa Sudan
-
Mtindo wa Maisha wa Fatima (a.s) na Kauli “Jirani Kwanza Kisha Nyumba”: Kigezo cha Kiungu Kukabiliana na Ubinafsi wa Kisasa
Katika kuelekea kumbukizi ya kuzaliwa kwa Bibi Fatima Zahra (a.s), kikao cha kisayansi kuhusu “Mtindo wa Maisha wa Fatima na Mafundisho ya al-jār thumma al-dār (Jirani Kwanza Kisha Nyumba)” kiliandaliwa kwa ushirikiano na Shirika la Habari la ABNA, ambapo watafiti walibainisha changamoto za familia katika enzi ya kisasa—hususan mgongano kati ya fikra za kisasa na mwenendo wa kimapokeo. Katika kikao hicho, mfano wa Maisha wa Bibi Zahra (a.s) uliwasilishwa kama muongozo wa kiungu na wa vitendo unaojenga maadili ya kuwajali wengine na kuleta mizani kati ya haki na wajibu ndani ya familia.
-
Zelenskyy Akataa Shinikizo la Kuachia Ardhi: Avunja Pendekezo la Marekani Kuhusu Suluhu ya Vita
Zelenskyy ameweka wazi kwamba nchi yake haitakubali kuachia ardhi yoyote kwa Urusi — haoni pendekezo lolote la “kuzielezea” maeneo uliopewa na nguvu. “Hatuwezi kuachia mambo yoyote,” amesema, akiongeza kwamba sheria ya Ukraine — na katiba — haina ridhaa ya kuichukua ardhi yake.
-
Kauli ya Mwenyekiti wa Jumuiya ya Maridhiano na Amani Tanzania - Sheikh Dkt.Alhad Mussa Salum katika Kumbukizi ya Miaka 64 ya Uhuru wa Tanganyika
Tanganyika ilipata Uhuru kwa njia ya Amani; na sisi leo hii tunalo jukumu la kuuimarisha na kuurithisha kwa vizazi vijavyo. Kwa niaba ya Jumuiya ya Maridhiano na Amani Tanzania, Nawatakia Kumbukumbu Njema ya Miaka 64 ya Uhuru wa Tanganyika. Hongera Tanganyika, Hongera Tanzania! Amani na Maridhiano Daima.
-
CAIR Yapinga Uamuzi wa Gavana wa Florida na Kumkabili Kisheria
Shirika la Uhusiano wa Kiraia-Kiislamu la Marekani (CAIR) limetoa taarifa ikisema: “Tangu pale Ron DeSantis, Gavana wa Florida, alipochukua madaraka, kipaumbele chake kilikuwa kuwatumikia serikali ya Israeli, si watu wa Florida. Aliongoza kikao chake cha kwanza cha baraza la mawaziri katika ardhi za makoloni, akatenga mamilioni ya dola ya kodi ya wananchi kwa waraka wa serikali ya Israeli, na hata kutishia kufunga vyama vyote vya wanafunzi vinavyounga mkono Palestina katika vyuo vikuu vya Florida; tishio ambalo lilijibidiwa baada ya CAIR kulirekebisha kortini.”
-
Ayatollah Nouri Hamedani: Hakuna Mbinu Yenye Ufanisi Zaidi ya Tablighi ya Kienyeji (Ya Kawaida) / Umuhimu wa Kumfahamu Mhusika Unayemhubiria
Ayatollah al-‘Uzma Hussein Nouri Hamedani, mmoja wa Marjaa wakubwa wa Kishia, amesisitiza kuwa licha ya manufaa makubwa ya mbinu mpya za tablighi kama vile kutumia mitandao ya kijamii, kutengeneza video na programu za kuvutia, bado hakuna mbinu iliyo na athari pana na ya kudumu kama tablighi ya kitamaduni—ya uso kwa uso na kupitia mimbari.
-
Florida Yatangaza “Ikhwan al-Muslimin” na “Baraza la Mahusiano ya Kiislamu-Kimarekani (CAIR)” kuwa Mashirika ya Kigaidi
Jimbo la Florida nchini Marekani limetangaza rasmi kwamba kundi la Ikhwan al-Muslimin na Baraza la Mahusiano ya Kiislamu–Kimarekani (CAIR) ni mashirika ya kigaidi ya kigeni.
-
Kulipiza Kisasi kwa Marekani dhidi ya Uchaguzi wa Wananchi na Kundi la Muqawama nchini Iraq / Uhandisi Usio wa Moja kwa Moja wa Mamlaka Baghdad
Kwa kukaribia kutangazwa kwa kifurushi kikubwa zaidi cha vikwazo dhidi ya wanasiasa, makampuni na watu wanaohusishwa na Iran, wachambuzi wanaona hatua hii kuwa ni kulipiza kisasi kwa Marekani dhidi ya matokeo ya uchaguzi wa Iraq na kuongezeka kwa nguvu za makundi ya muqawama (upinzani wa Kiiraqi).
-
Rais Mstaafu Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete Aendelea Kuitangaza Tanzania Katika Ajenda ya Elimu Duniani Kupitia Global Partnership for Education
Ushiriki wa Rais Mstaafu Dkt. Jakaya Kikwete katika majukwaa haya ya kimataifa unaonesha kwa vitendo dhamira yake endelevu ya kuitetea elimu kama nguzo kuu ya maendeleo ya binadamu, sambamba na kuendeleza diplomasia ya elimu kwa manufaa ya mataifa duniani, hususan Afrika.
-
Mtazamo wa Mapambano ya Sheikh Ghazal Dhidi ya Serikali ya Kigaidi ya Al-Jolani: Kuanzia Kukabidhi Silaha hadi Mwito wa Mgomo wa Kitaifa
Baada ya mabadiliko ya hivi karibuni nchini Syria, Sheikh Ghazal Ghazal, Rais wa Baraza Kuu la Kiislamu la Waalawi, amekuwa akitoa misimamo mbalimbali akidai kulindwa kwa haki za Mashia wa Syria. Katika siku za hivi karibuni, ametoa mwito wa mgomo wa kitaifa wa amani kama sehemu ya kupinga mauaji na dhulma zinazotekelezwa na serikali ya mpito ya Al-Jolani.
-
Mufti wa Tanzania Atoa Wito wa Kulinda Amani na Kuepuka Uchochezi wa Kidini na Maandamano Yanayopangwa Kufanyika 9 Disemba
"Tuepuke upepo mbaya unaosambazwa kwa chuki za kidini. Sisi Waislamu hatukatazwi kuishi kwa wema na wasiokuwa Waislamu. Maisha ya watu lazima yalindwe,” alisema Mufti.
-
Ushindi wa Jukwaa la Upinzani (Muqawama) ni Kudhihirika kwa Utabiri wa Qur’an
Kushindwa kwa Israel na Marekani katika mapambano ya hivi karibuni kunatokana na uongozi wa busara wa Ayatullah Khamenei, Kiongozi Mkuu wa Mapinduzi ya Kiislamu.
-
Je, Senario ya Maafa ya Al-Fasher Inarejelewa Tena Katika Mji wa Babanusa, Sudan?
Shirika la Umoja wa Mataifa limeonya kuwa hali ya kibinadamu katika mji wa Babanusa, uliopo katika jimbo la West Kordofan nchini Sudan, iko katika hatari kubwa ya kushuhudia janga kama lililotokea katika mji wa Al-Fasher, Kaskazini mwa Darfur, endapo hali ya sasa itaendelea kuzorota.
-
Joseph Aoun ataka Israel ishinikizwe ijiondoe Lebanon
Rais wa Lebanon, Joseph Aoun, ameitaka jumuiya ya kimataifa kuishinikiza Israel ili itekeleze kikamilifu makubaliano ya usitishaji vita na ijiondoe katika ardhi ya Lebanon.
-
Ustadhi Rajai Ayoub na Wasomi wa Qur'an kutoka Tanzania Wawasili Salama Bangladesh kwa Ajili ya Mahfali Makubwa ya Kimataifa ya Qur'an +Picha
Mahfali hayo ya kimataifa yanakusudiwa kuwa jukwaa muhimu la kiroho na kielimu, ambapo wasomaji bingwa na mahiri wa Qur'an Tukufu kutoka Tanzania watapata fursa ya kuonesha vipaji vyao katika kusoma Aya Tukufu za Mwenyezi Mungu (SWT), kwa mapito na mitindo mbalimbali ya usomaji wa Qur'an (Qira’at).
-
JMAT Yatoa Wito wa Maridhiano na Amani, Funga ya Siku Tatu na Maombi ya Kitaifa kwa ajili ya Umoja wa Kitaifa
Mwenyekiti wa JMAT, Sheikh Dkt. Alhad Mussa Salum, amesema: "Matukio ya baada ya Uchaguzi yameacha majeraha ya kisaikolojia na kuchochea hisia za kidini, hivyo kunahitajika hatua za haraka kuimarisha umoja wa kitaifa. Amehimiza maombi hayo yashirikishe waumini wa madhehebu zote na kufanyika kwa mfumo mmoja na Kwa siku moja kitaifa".
-
Mkutano wa Balozi wa China mjini Kabul na Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa Taliban kuhusu vifo vya raia wa China mpakani mwa Afghanistan na Tajikistan
“Balozi wa China mjini Kabul, katika mkutano na Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa Taliban, alitaja mashambulio ya hivi karibuni dhidi ya wafanyakazi wa China katika eneo la mpakani kati ya Tajikistan na Afghanistan — ambayo yamesababisha vifo vya watu 5 na kuwajeruhi wengine kadhaa — kuwa ‘kitendo cha maadui kwa ajili ya kuleta kutokuaminiana’. Pia aliishukuru Taliban kwa kuanzisha uchunguzi kuhusu tukio hilo.
-
Marafiki wa Ukweli Wako Wengi Zaidi Upande wa Pili | Kifo cha Kishahidi kwao hakileti upweke kwao Bali ni Daraja la kukutana na Msafara wa Waumini
"Katika ugeni hakuna hofu ya upweke; marafiki wapendwa wako wengi zaidi upande ule mwingine.” Kwa maana kwamba: Shahidi anapovuka kutoka dunia hii, haogopi kutengwa, kwa sababu anatambua wazi kuwa upande wa pili kuna kundi kubwa la wacha-Mungu, wakweli, watu wema, na mashahidi waliomtangulia, walio tayari kumpokea katika safu yao.
-
Je, Taurati imebadilishwa? Angalia jibu la Qur’an hapa!
Kuhusu taarifa (maelezo) ya Qur’an Tukufu kuhusu ubadilishaji wa maneno ya Taurati, kuna mjadala wa kiitihadi kama ifuatavyo: 1. Mtazamo maarufu (ushahidi unaoonekana wazi kabisa katika Quran) Watafiti wengi na wafuasi wa mtazamo huu wanaona kwamba Qur’an inazungumzia ubadilishaji wa maneno kwa uwazi jabisa. Qur’an inataja maneno yaliyopinduliwa au kuharibiwa na baadhi ya Watu wa Kitabu (Ahlul-kita'bi): «يُحَرِّفُونَ الْكَلِمَ عَن مَوَاضِعِهِ» (An-Nisa 46) Hapa (kwa mujibu wa Aya hiyo Tukufu) , ubadilishaji huo unahusiana na maneno yenyewe, na si tafsiri tu. 2. Mtazamo wa wapinzani (Mukhalifuna) Wao wanasema kuwa Qur’an inazungumzia ubadilishaji wa maana, si maneno ya kifasihi: Wanasema kuwa maneno ya msingi hayajabadilishwa, lakini maana au tafsiri potofu ndizo zilizobadilishwa au kutumika vibaya. Hii inaitwa ubadilishaji wa maana (tafsiri) badala ya ubadilishaji wa maneno.
-
Madrid itakuwa mwenyeji wa Mahakama ya Umma kuhusu Ushirikiano na Mauaji ya Kimbari ya Wapalestina / Imeitaka Kuvunja Mahusiano na Israel
Katika Siku ya Uunganisho na Palestina, Madrid ilikuwa mwenyeji wa Mahakama ya Umma dhidi ya ushirikiano wa Hispania na pia ikashuhudia maandamano makubwa yaliyoikosoa kukosekana kwa heshima ya mapumziko ya silaha kwa mfumo.