shirika la habari la abna
-
Iran: “Udhibiti wa Hormuz ni Chombo cha Nguvu Chenye Ufanisi Kuliko Silaha za Nyuklia” – The Atlantic
Jarida la Marekani The Atlantic limesema Iran imeonyesha uwezo wa kusimama bila kufanya makubaliano makubwa na Marekani, likidai kuwa udhibiti wa Mlango wa Hormuz umeifanya Tehran kuwa na turufu yenye nguvu ya kimkakati. Wakati huo huo, Iran imeonya kuwa ushiriki wowote katika vita vya kiuchumi vya Marekani dhidi yake utachukuliwa kuwa kitendo cha kivita.
-
New York Times: “Msidharaueni Houthi Kamwe” na Kumbukeni Silaha Zao
Gazeti la New York Times limeonya dhidi ya kuendelea kuwapuuza Houthi wa Yemen, likisisitiza kuwa wamegeuka kuwa nguvu muhimu ya kikanda yenye uwezo wa kuathiri hesabu za vita na amani, huku eneo la Yemen la kimkakati likiwapa uwezo wa kutumia njia za baharini kama silaha ya kimkakati.
-
Kamanda wa Jeshi la Pakistan aelekea Tehran kwa mazungumzo na viongozi wa Iran
Chanzo cha kidiplomasia kimesema Kamanda wa Jeshi la Pakistan, Field Marshal Asim Munir, ameondoka Islamabad kuelekea Tehran kwa ajili ya kukutana na viongozi wakuu wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran.
-
Ayatollah Dajkam: Uhalifu wa Lamerd Ufikishwe Duniani Kama Janga la Hiroshima
Ayatollah Lotfollah Dajkam amesema tukio la Lamerd, ambapo watu 21 waliuawa ndani ya sekunde 35, linapaswa kufikishwa katika kiwango cha kimataifa kama janga la Hiroshima. Amesisitiza kwamba mamlaka ziachane na visingizio na urasimu na zifuatilie kwa dhati suala hilo kama jinai ya kivita.
-
Kesi ya Mufti wa Zamani wa Syria Yakabiliwa na Hukumu; Waendesha Mashtaka Wadai Adhabu ya Kifo
Kesi ya Ahmad Badr al-Din Hassoun, Mufti Mkuu wa zamani wa Syria, imeingia hatua ya mwisho baada ya kikao cha tano katika Mahakama ya Jinai ya Nne mjini Damascus. Waendesha mashtaka wamewahi kuomba apewe adhabu ya kifo kwa tuhuma za kuchochea vurugu na kuunga mkono ukandamizaji wa serikali iliyopita, huku tarehe 24 Agosti ikiwekwa kwa ajili ya mapitio ya mwisho na kutolewa kwa hukumu.
-
Mohsen Rezaei: Nchi yoyote itakayounga mkono vita vya kiuchumi dhidi ya Iran tutachukulia hatua hiyo kuwa kitendo cha kivita
Katibu wa Baraza Kuu la Usalama wa Taifa la Iran, Meja Jenerali Mohsen Rezaei, ameonya kuwa Iran itachukulia ushiriki au uungaji mkono wa nchi yoyote katika kile alichokiita vita vya kiuchumi vya Marekani dhidi ya wananchi wa Iran kuwa “kitendo cha kivita.”
-
Iran: Vita la hivi karibuni yaweka upya vipaumbele na mwelekeo wa viwanda vya ulinzi
Waziri wa Ulinzi wa Iran amesema vita la hivi karibuni limeibua hitaji la kuainisha upya vipaumbele vya sekta ya ulinzi, huku uzalishaji wa baadhi ya vifaa vya kijeshi ukiongezeka hadi mara kadhaa licha ya vita.
-
Jenerali Qaani: Dira ya Palestina Kutoka Bahari hadi Mto Bado Iko Hai na Inazidi Kufikiwa
Kamanda wa Kikosi cha Quds cha Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu (IRGC), Brigedia Jenerali Esmail Qaani, amesema suala la Palestina bado ni dira hai na isiyobadilika, akisisitiza kuwa ndoto ya Palestina kutoka baharini hadi mto iko hai zaidi kuliko wakati mwingine wowote.
-
Mwanamke Anayehusishwa na Daesh Akamatwa New York kwa Tuhuma za Kupanga Shambulio
Mamlaka za shirikisho nchini Marekani zimemkamata mwanamke mwenye umri wa miaka 35 mjini Albany, New York, kwa tuhuma za kujaribu kutoa msaada wa kimaada kwa Daesh (ISIS) na kupanga shambulio dhidi ya jengo la Bunge la Jimbo la New York.
-
Zaidi ya Watu Milioni Mbili Wamtembelea Imam Shahidi kwa Niaba Yake Katika Ziara ya Arbaeen
Mwakilishi wa Kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu katika Masuala ya Hija na Ziara, Hujjatul-Islam Sayyid Abdulfattah Nawab, amesema zaidi ya mahujaji milioni mbili walifanya ziara ya Arbaeen kwa niaba ya Imam Shahidi mwaka huu. Pia amesimulia ushauri wa Imam Shahidi kwamba ibada ya Hija ya Sunnah isifanywe kwa niaba yake pekee, bali waumini wengine washirikishwe katika thawabu yake.
-
Iran: Baadhi ya Mabomu Yalikuwa Yametengenezwa Maalum kwa Ajili ya Kuishambulia Iran
Kaimu Waziri wa Ulinzi wa Iran, Brigedia Jenerali Ibn al-Ridha, amesema adui alitumia mchanganyiko wa zana za kijeshi, mtandao, vikosi vya vibaraka na wapinzani wa ndani katika vita dhidi ya Iran, huku baadhi ya silaha zikitumiwa kwa mara ya kwanza na baadhi ya mabomu yakitengenezwa mahsusi kwa ajili ya kuishambulia Iran.
-
Uturuki Yatoa Ombi la Kumtafuta Netanyahu Kimataifa Kupitia Interpol kwa “Red Notice”
Wizara ya Sheria ya Türkiye imeanza mchakato wa kuomba Interpol itoe Red Notice dhidi ya Waziri Mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu na Afek Moskowitz, kufuatia kesi inayohusiana na shambulio dhidi ya “Global Sumud Flotilla” iliyokuwa ikipeleka misaada ya kibinadamu Gaza.
-
Iran Yatishia Kushambulia Nchi Itakayoisaidia Marekani
Iran imetoa onyo kwamba nchi yoyote itakayoisaidia Marekani katika hatua za kijeshi dhidi yake inaweza kuchukuliwa kuwa mshirika wa Marekani na kulengwa na hatua za kijeshi.
-
Kiongozi wa Iran: Wageni wa Kigeni Wanaofanya Uvamizi Ghuba ya Uajemi Hawana Mahali Isipokuwa Chini ya Maji Yake
Kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu amesema kuwa wageni kutoka maelfu ya kilomita mbali wanaoingilia na kufanya vitendo vya uchokozi katika Ghuba ya Uajemi hawana nafasi katika eneo hilo, isipokuwa chini ya maji yake. Kauli hiyo ilitolewa katika ujumbe wake wa kuadhimisha Siku ya Kitaifa ya Ghuba ya Uajemi.
-
Waziri Mkuu wa Canada: Tulisitisha Mazungumzo na Marekani kwa Sababu ya Madai Yao Mengi
Waziri Mkuu wa Canada, Mark Carney, amesema Ottawa ilisitisha mazungumzo ya kibiashara na Marekani baada ya Washington kutoa madai mengi huku ikitoa masharti machache ya manufaa kwa Canada. Amesema waendelezaji wa mazungumzo wa Canada waliagizwa kurejea Ottawa.
-
Mtaalamu wa Kisiasa: Kulipiza Kisasi cha Kiongozi Shahidi Lazima Kugeuke Kuwa Mkakati wa Kisiasa
Profesa Fouad Izadi amesema suala la kulipiza kisasi cha kiongozi shahidi halipaswi kubaki katika kiwango cha kauli na misemo, bali linapaswa kufuatiliwa kwa njia za kisheria na kisiasa. Ameonya pia kwamba Marekani inaweza kuwa inarudia mbinu ya kutumia mazungumzo na ahadi za makubaliano kama njia ya kudhibiti mwenendo wa Iran na kuandaa mazingira ya hatua nyingine.
-
Kutoka Hofu hadi Kuvutiwa: Kwa nini Mrengo Mpya wa Kulia Marekani Unavutiwa na Uislamu?
Baadhi ya watu mashuhuri katika mrengo mpya wa kulia nchini Marekani wameanza kuutazama Uislamu si kama tishio kwa ustaarabu wa Magharibi, bali kama mfano wa nidhamu, nguvu, familia, utambulisho na mshikamano wa kijamii wanaodai kuwa Magharibi imevipoteza.
-
Admirali Sayyari: Sekta ya ulinzi ya Iran imepata uwezo endelevu wa kuzuia mashambulizi
Mkuu wa Majeshi na Naibu Mkuu wa Uratibu wa Jeshi la Iran, Admirali Habibullah Sayyari, amesema sekta ya ulinzi ya nchi hiyo imevuka kipindi cha vikwazo na vizuizi kwa kutegemea imani, elimu, teknolojia na uwezo wa wataalamu wa ndani, na hivyo kufanikisha uwezo endelevu wa kuzuia mashambulizi na kuimarisha nguvu za ulinzi.
-
Khatibzadeh: Wananchi wa Iran pia watashinda dhidi ya ugaidi wa kiuchumi
Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran, Saeed Khatibzadeh, amesema serikali ya Iran imedhamiria kukabiliana na vikwazo vya Marekani na kupunguza athari zake, huku akisisitiza kuwa wananchi wa Iran wana uwezo wa kushinda changamoto za kile alichokiita ugaidi wa kiuchumi.
-
Baqerzadeh: Hali ya marubani wa Iran wanaoshikiliwa Qatar ni mbaya sana
Brigedia Jenerali Mohammad Baqerzadeh amesema hali ya kiafya ya marubani wa Iran wanaoshikiliwa nchini Qatar ni mbaya sana, akitoa wito kwa Kamati ya Kimataifa ya Msalaba Mwekundu kupeleka ndege ya matibabu nchini Qatar ili kuhakikisha majeruhi hao wanarejeshwa Iran haraka iwezekanavyo.
-
Waziri wa Sayansi: Iran imethibitisha uwezo wa kusimamia migogoro wakati wa vita vya hivi karibuni
Waziri wa Sayansi, Utafiti na Teknolojia wa Iran, Hossein Simaei Saraf, amesema Jamhuri ya Kiislamu ya Iran ilikabiliana na moja ya majeshi makubwa zaidi duniani wakati wa vita vya hivi karibuni na ikaonyesha uwezo wake wa kusimamia migogoro huku ikiendelea kutoa huduma kwa wananchi.
-
Msemaji wa Serikali ya Iran: Kuunga mkono Vikosi vya Ulinzi ni wajibu na jukumu la kulinda usalama wa nchi
Msemaji wa Serikali ya Iran, Fatemeh Mohajerani, amesema kuunga mkono Vikosi vya Ulinzi ni wajibu na jukumu la serikali katika kuhakikisha usalama wa nchi, akisisitiza kuwa msaada huo unahusisha mahitaji ya ulinzi, kuboresha hali za wanajeshi na familia zao, pamoja na kuimarisha uratibu na taasisi za ulinzi.
-
Vita vya kiuchumi vya Marekani dhidi ya Iran ni ukiukaji wa mamlaka ya kitaifa na tangazo la vita dhidi ya serikali zote
Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran, Ismail Baghaei, amesema vikwazo vipya vya Marekani dhidi ya Iran vinaenda mbali zaidi ya kile kinachoitwa “vita vya kiuchumi”, akivitaja kuwa jaribio la Marekani kulazimisha mamlaka yake nje ya mipaka yake dhidi ya nchi zote huru wanachama wa Umoja wa Mataifa.
-
Msemaji wa Jeshi la Iran: Vita vya hivi karibuni vimeleta mwamko wa kijio-siasa nchini Iran
Msemaji wa Jeshi la Jamhuri ya Kiislamu ya Iran, Brigedia Jenerali Mohammad Akrami-Nia, amesema vita vya hivi karibuni vimesababisha mabadiliko katika mtazamo wa kijeshi na kuleta mwamko mkubwa wa kijio-siasa miongoni mwa wananchi wa Iran.
-
Vyombo vya habari vya Kiebrania: Israel ilishambulia kituo cha Abu al-Duhur kuchunguza mienendo ya Uturuki
Vyombo vya habari vya Kiebrania vimeripoti kuwa shambulio la anga la utawala wa Israel dhidi ya kituo cha kijeshi cha Abu al-Duhur, kusini mwa Idlib nchini Syria, lililenga kuchunguza na kujaribu nia za Uturuki, huku taasisi za usalama za Israel zikiwa zimeonya dhidi ya kufungua mzozo mpya na Ankara.
-
Qalibaf: Ushirikiano wa kiuchumi kati ya Iran na Iraq waingia hatua ya utekelezaji
Spika wa Bunge la Iran, Mohammad Baqer Qalibaf, amesema ushirikiano wa kiuchumi kati ya Iran na Iraq umeingia katika hatua ya utekelezaji, huku akieleza matumaini kwamba kuondoka kwa vikosi vya kigeni nchini Iraq kutaimarisha mamlaka na uhuru kamili wa taifa hilo.
-
Iran: Ulinzi wa raia na miundombinu muhimu wawekwa kuwa kipaumbele
Mkuu wa Shirika la Ulinzi wa Raia la Iran, Gholam Reza Jalali, amesisitiza umuhimu wa kuimarisha utayari wa jumla, kudumisha mshikamano wa kitaifa na kuhakikisha ulinzi wa raia pamoja na miundombinu muhimu katika mazingira hatarishi.
-
Qalibaf Atembelea Haram Tukufu za Imam Musa al-Kadhim na Imam al-Jawad mjini Kadhimayn
Spika wa Bunge la Iran, Mohammad Baqer Qalibaf, ametembelea Haram Tukufu za Maimamu wawili, Imam Musa al-Kadhim (as) na Imam Muhammad al-Jawad (as), mjini Kadhimayn nchini Iraq wakati wa ziara yake rasmi nchini humo.
-
Aoun Aomba Shinikizo la Kimataifa dhidi ya Israel Kutekeleza Makubaliano na Kuondoka Lebanon
Rais wa Lebanon Joseph Aoun amemtaka Papa Leo XIV kusaidia kuongeza shinikizo la kimataifa kwa utawala wa Israel ili utekeleze “Makubaliano ya Mfumo”, usitishe mashambulizi na kuondoka kikamilifu katika maeneo ya Lebanon inayoyakalia.
-
Qalibaf: Hatutafuti vita, lakini hatutaruhusu heshima yetu ikanyagwe
Spika wa Bunge la Iran, Mohammad Baqer Qalibaf, amesema Iran haitafuti vita, lakini haitaruhusu mtu yeyote kukanyaga heshima na utu wake, huku akisisitiza kuwa Iran iko tayari kujitolea na kusimama imara mbele ya vitisho, mashambulizi na vikwazo visivyo vya haki.