shirika la habari la abna
-
Donald Trump awasili katika Mji Mkuu wa Saudi Arabia / Kuanza kwa ziara ya kikanda ya Rais wa Marekani
Rais wa Marekani, katika mwanzo wa ziara yake ya kwanza ya nje ya nchi, amewasili katika jiji la Riyadh.
-
Kufanyika kwa Tamasha la Ushairi wa Amani katika mji wa Parachinar, Pakistan / Mkutano wa washairi wa Kishia na Kisunni wenye ujumbe wa umoja
Washairi Mashuhuri wa Kishia na Kisunni kutoka maeneo yote ya Kurram wamekusanyika katika tamasha lenye mada ya amani lililofanyika katika mji wa Parachinar, Pakistan.
-
Mkutano wa kihistoria wa Marjaa wa Kidini:
Najaf Ashraf: Ayatollah Jawadi Amuli akutana na Ayatollah Sistani / Zawadi ya Qur'an yatolewa katika Mkutano wa Viongozi hawa wawili wa juu wa Kidini
"Ayatollah al-Udhma Jawadi Amuli — ambaye yuko ziarani nchini Iraq kwa ajili ya kutembelea maeneo matakatifu — amekutana na kufanya mazungumzo na Ayatollah al-Udhma Sistani huko Najaf Al-Ashraf."
-
Kwa nini Qur'an inahitaji Tafsiri? | Sehemu ya Kwanza
Ili kuelewa Aya za Mutashabihat, tunahitaji wataalamu (wajuzi) wa Tafsiri ambao wanaweza kufafanua kwa kutumia Aya nyingine au zingine na elimu ya dini.
-
Shahriari: Vitabu Vipya vya Jumuiya ya Kimataifa ya Taqrib ya Madhehebu za Kiislamu, vinaangazia Umoja na Ustaarabu Mpya wa Kiislamu
Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Kimataifa ya Taqrib baina ya Madhehebu ya Kiislamu, Dkt. Hamid Shahriari, alieleza kuwa: “Kwa bahati nzuri, kwa kuweka vitabu katika mfumo wa kielektroniki kupitia tovuti ya maonyesho ya vitabu, mazingira mazuri yameandaliwa kwa ajili ya kutoa huduma kwa wadau na wageni wanaopendelea kufanya manunuzi yao kwa njia za kidijitali.”
-
Madhimisho ya Miaka 14 ya "Kujihami Kutakatifu" ya Bahrain: Mwangaza wa Uhuru Usiozimika
Mnamo tarehe 12 Mei, Wabahrain wanasherehekea miaka 14 tangu kuanza kwa awamu ya "Ulinzi Takatifu" – harakati ya wananchi iliyozaliwa kutokana na upinzani wa kisiasa na kijamii. Harakati hii haikuwa tu jibu la dhuluma na ukandamizaji, bali pia ilikuwa ni hatua muhimu katika kutetea heshima, thamani za kidini na binadamu, na haki za kimsingi za raia wa Bahrain. Hii ilikuwa ni mapinduzi ya wananchi, na kwa miaka 14, inabaki kuwa kipengele muhimu katika historia ya mapambano ya watu wa Bahrain, ikionyesha nguvu ya umoja wa wananchi katika kukabiliana na ukandamizaji wa kisiasa na kijamii. Ulinzi Takatifu umejenga msingi wa mapambano ya kidemokrasia, na ingawa changamoto bado zipo, kumbukumbu hii inawakilisha azma na matumaini ya watu wa Bahrain katika kuendelea kutafuta haki na uhuru.
-
"Maarifa ya Nahjul Balagha (3) / Dua za Imam Ali (a.s)"
Hata ingawa seti ya dua zinazosimuliwa kutoka kwa Imam Ali (a.s) inafikia takriban dua 700, lakini kwa kuzingatia msisitizo wa Sayyid Razi katika kuchagua baadhi ya maneno ya Imam Ali (a.s) katika kitabu cha Nahjul Balagha, kuna takriban dua 50 zinazohusishwa na Amir al-Mu'minin (a.s) ambazo zinahusisha mada mbalimbali.
-
"Kutoka 'Juhudi Zisizoisha' hadi kwenye 'Diplomasia ya Muqawamah'; Wiki ya Kuwapa Heshima Mashahidi wa Huduma"
"Saeed Ohadi, Mkuu wa Kamati ya Maadhimisho ya Kumkumbuka Shahidi Ayatollah Sayyid Ebrahim Raisi na Mashujaa wengine wa Huduma, ameeleza kwa kina ratiba ya maadhimisho ya kumbukumbu ya mwaka wa kwanza ya mashahidi wa huduma."
-
"Ayatollah Ramezani: Dini inapaswa kuwa na ufanisi katika nyanja mbalimbali za kitamaduni, kisiasa na kiuchumi"
"Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Kimataifa ya Ahlul-Bayt (a.s) alisema: Tunapaswa kuwa na mtazamo jumuishi kuhusu dini ili tuone athari kamili za dini; mtazamo jumuishi maana yake ni kwamba dini ina sura ya nje na ya ndani, ina wajibu wa mtu binafsi na pia wajibu wa kijamii. Haiwezekani dini iwe na hukumu nyingi za kijamii lakini isiwe na Serikali."
-
"Kuna Wivu wa Husuda na Wivu Ghibta | Je, Tuwe na Wivu wa Aina ya Ghibta au Tusiwe nao?"
Husuda ni kutamani neema ya mtu mwingine itoweke, iwe neema hiyo itamfikia mwenye husuda au la. Kinyume cha husuda ni 'Ghibta', ambapo mtu hatamani neema ya mwingine ipotee, bali anatamani kuwa na neema kama hiyo bila kumtakia mwingine mabaya.
-
"Vita vya Gaza vimesababisha Wapalestina 1,500 kupoteza uwezo wa kuona"
Wizara ya Afya ya Palestina imetangaza leo Jumapili kuwa, kutokana na vita na kuzidi kwa mzingiro unaoendelea wa jeshi la utawala wa Kizayuni dhidi ya Gaza, Wapalestina 1,500 wamepoteza uwezo wao wa kuona.
-
"Wadau wa sekta ya utamaduni wa Afghanistan watilia mkazo juu ya ukarabati wa "Gonbad-e-Begum" / 'Kubba ya Malkia' katika Mkoa wa Ghazni"
"Baadhi ya wadau wa sekta ya utamaduni wa Afghanistan wametilia mkazo umuhimu wa ukarabati na urejeshwaji wa jengo la kihistoria la 'Kubba ya Malkia' katika Mkoa wa Ghazni."
-
Bilal Muslim Mission - Kanda ya Pangani - Hafla ya Mazazi ya Imam Ridha (as) na Maonyesho ya Wanafunzi wa Madrasa
Hafla hii imehudhuriwa na Madrasat kutoka Bilal Muslim – Kanda ya Pangani pamoja na baadhi ya Madrasa kutoka kwa ndugu zetu wa Kisuni. Hili ni jambo la faraja kubwa, linaloashiria mshikamano wa kijamii na wa kidini katika maeneo yetu.
-
Ayatollah Sheikh Jawadi Amuli Atembelea Makao ya Maimamu wa Ahlul-Bayt (as) Samarra, Akaribishwa kwa Heshima Kubwa
Katika heshima ya ziara hii tukufu, Haram ilifanya hafla maalum ya kumuenzi Sheikh Jawadi Al-A'muli, sambamba na kuzinduliwa kwa kitabu chake kipya chenye kichwa: Sharh Ziyarat Al-Jami'a Al-Kabira
-
Faida ya kuingiza furaha katika moyo wa mtu mwenye matatizo
"Huna hasara yoyote hata chembe mbele ya Mwenyezi Mungu endapo utamsapoti Mwalimu kwa kumlipia mtoto wake ada ya shule na kumuepushia tatizo la mtoto wake kufukuzwa shule kwa ajili ya ada (school fees), au ukamlipia Mwalimu kodi ya nyumba"
-
Katika mkutano na maelfu ya wafanyakazi kutoka kote nchini:
Kiongozi wa Mapinduzi ametoa uungaji mkono kamili kwa jamii ya wafanyakazi / Fikira zisikengeushwe kutoka kwenye suala la Palestina
Ayatollah Khamenei pia alisisitiza kuwa, pamoja na kuendelea kwa jinai na mauaji ya kikatili dhidi ya watu wa Gaza na Palestina yanayofanywa na utawala wa Kizayuni kwa msaada wa Marekani na Uingereza, mataifa yanapaswa kusimama dhidi ya utawala wa Kizayuni na wafuasi wake, na wasiruhusu masuala yanayohusu Palestina kusahaulika.
-
Majlis ya Mazazi ya Imam Ridha (as) yafanyika Jamiat Al-Mustafa(s), Tanzania | Hadithi Toka Vyanzo vya Kisunni Zinathibitisha Makhalifa Kumi na Wawili
Lengo la Mazungumzo Haya ni: Kuleta maelewano baina ya Madhehebu za Kiislamu na kuonyesha kuwa msingi wa Uimamu na Ukhalifa wa Maimam Kumi na Wawili wa Ahlul-Bayt (a.s), wanaofuatwa na Waislamu wa Madhehebu ya Shia Ithna Ashari, una mizizi pia katika vyanzo vinavyokubalika vya Kisunni.
-
Swala ya Ijumaa Yaswaliwa katika Chuo Cha Jamiat Al-Mustafa (s), Dar-es-Salaam:Khatibu wa Ijumaa Sheikh Bakari Mtulia Azungumzia "Umuhimu wa Kusamehe"
Kutoa Msamaha, hakupunguzi Heshima ya Mtu, Bali kunaongeza Heshima ya Mtu mbele ya Mwenyezi Ahlul-Bayt (as), Familia ya Mtume Muhammad (s.a.w.w) walikuwa mfano wa Hali ya Juu ya huruma, subira, na Kusamehe.
-
Watu 5 Wauawa Katika Shambulio la Mizinga la Jeshi la India katika eneo la Kashmir
Watu 5 Wasio Wanajeshi, Wakiwemo Mtoto Mmoja, Wauawa Katika Shambulio la Mizinga la Jeshi la India Katika Eneo la Kashmir Linalodhibitiwa na Pakistan.
-
Sheikh Dkt. Abdul- Razak Amiri Atoa Kisa Halisi Cha Mwanamke wa Kiislamu aliyedai Talaka kisa Mume Wake Kaoa Mke wa 2, Hatimaye naye akawa Mke wa Pili
Ndoa ni heshima, ndoa ni stara ya kijamii, na ndio maana Qur'an Tukufu ikasema: «هُنَّ لِبَاسٌ لَّكُمْ وَأَنتُمْ لِبَاسٌ لَّهُنَّ» kwamba "Mwanamke ni vazi kwa Mwanaume, na Mwanaume ni vazi kwa Mwanamke". Katika kazi za vazi (nguo) ni heshima, kupendeza, kuheshimika, vazi kawaida yake linaleta heshima katika jamii, na Ndoa vile vile inaleta heshima katika Jamii.
-
Kardinali Robert Prevost Achaguliwa Papa Mpya – Achukua Jina la Leo XIV
Katika hotuba yake ya kwanza kwa umma kutoka kwenye roshani ya Basilika ya Mtakatifu Petro, Papa Leo XIV alitoa salamu kwa kusema, "Amani iwe nanyi nyote!" Alisisitiza umuhimu wa umoja, amani, na mazungumzo, akitoa wito kwa Kanisa kuwa daraja linalounganisha watu wote. Alitoa salamu maalum kwa watu wa Peru, akionyesha uhusiano wake wa karibu na nchi hiyo kutokana na huduma yake ya muda mrefu kama mmisionari.
-
Mkutano na Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Dkt. Batlida Burian, pamoja na baadhi ya Masheikh wa Kishia na Kisunni.
"Tanga ni mfano wa kuigwa kwa utulivu wa kidini. Tuendelee kudumisha hali hii na kushirikiana kwa ajili ya maendeleo ya jamii yetu."
-
"Ayatollah Ramezani: Chuo cha Dini cha Qom kina uwezo wa kuunda ustaarabu wa Kiislamu / Mapinduzi ya Kiislamu yamebadilisha mlingano wa dunia."
Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Kimataifa ya Ahlul-Bayt (a.s) alisema: Leo hii, fursa ya kipekee imepatikana kwa vyuo vya kidini, ambayo haijawahi kushuhudiwa katika vipindi vya nyuma. Tunapaswa kuweza kuitambulisha dini ya Uislamu kwa dunia kwa kutumia lugha na istilahi za kimataifa, na kwa hakika tutafaulu katika njia hii.
-
Ujumbe wa Kiongozi Mkuu wa Mapinduzi kwa mkutano wa kumbukumbu ya miaka mia moja (100) ya kuanzishwa upya kwa Chuo cha Dini cha Qom:
Ayatollah Khamenei: Jukumu la (Hawza) Chuo cha Kidini ni Kuchora Mipaka Mikuu na Midogo ya Ustaarabu mpya wa Kiislamu
"Kazi kuu na ya msingi ya Hawza ni (البَلاغُ المُبین) kufikisha ujumbe wa dini kwa uwazi na ufasaha (ubalighi wa wazi - Kwa maana: Kufikisha ujumbe kwa uwazi na uthabiti na kwa namna ambayo haiachi shaka yoyote -). Miongoni mwa vielelezo vyake muhimu kabisa ni kuchora na kueleza kwa uwazi mistari (mipaka) mikuu na ya kando ( au midogo) ya ustaarabu mpya wa Kiislamu, pamoja na kuifafanua, kuieneza, na kuikuza katika jamii kama sehemu ya utamaduni."
-
Kwa mujibu wa Qur'an Tukufu: Kundi la Mwenyezi Mungu, linalomtii Mwenyezi Mungu, Mtume Wake, na waliokuwa Waumini wa kweli, Hao ndio washindi wa kweli
"Hezbollah" humaanisha: Kundi lililojifunga na miongozo ya Mwenyezi Mungu, linalosimama na kutetea haki, hata likiwa ni dogo au linakabiliwa na maadui wakubwa. Aya hii imekuwa nembo ya Harakati za Muqawama (Upinzani wa Kiislamu) kama vile Hezbollah ya Lebanon, Ansarullah ya Yemen, na wengineo wanaopambana dhidi ya dhulma ya mabeberu ya Kimataifa.
-
Kushindwa kwa Wamarekani Mbele ya Msimamo wa Wayemen Katika Kipindi cha Siku 50 / Ansarullah Yabadilisha Mlinganyo wa Dunia kwa Manufaa ya Muqawama
Katika kipindi cha siku 50 za mapambano ya kistratejia baharini, harakati ya Ansarullah ya Yemen imeweza kusimama imara dhidi ya mashinikizo ya kijeshi na kisiasa ya Marekani na washirika wake, na hatimaye kuwadhihirishia ulimwengu kwamba dhamira ya mataifa huru inaweza kuvunja nguvu za mabeberu.
-
Hasira za Wafuasi wa Uzayuni Kufuatia Matokeo ya Uchaguzi wa Canada / Mark Carney na Msimamo Wake wa Kizayuni Dhidi ya Palestina
Matokeo ya uchaguzi wa karibuni nchini Canada yamezua ghadhabu miongoni mwa wafuasi wa utawala wa Kizayuni, hasa baada ya ushindi wa Mark Carney, mwanasiasa ambaye anajulikana kwa msimamo wake wa kihafidhina zaidi kuhusu suala la Palestina. Mabadiliko haya katika mwelekeo wa siasa za Canada yamewafanya baadhi ya wafuasi mashuhuri wa Kizayuni kuonesha hali ya kukata tamaa, huku wakitoa ukosoaji mkali dhidi ya mazingira mapya ya kisiasa yanayoweza kuathiri uhusiano wa karibu wa Canada na Israel.Hofu kuu ya makundi hayo ni kwamba sera mpya zinaweza kupunguza uungaji mkono wa wazi kwa Israel, na kufungua nafasi kwa mijadala mikali zaidi kuhusu haki za Wapalestina katika siasa za ndani na nje ya Canada.
-
Onyo Kuhusu Mradi wa "Kuisahau Palestina" – Njama ya Kimataifa kwa Ushirikiano wa Viongozi wa Kiarabu
Kiongozi wa Harakati ya Kuamsha Ummah wa al-Mustafa: Kusahau Kadhia ya Palestina ni Njama Hatari na Usaliti Usiosameheka. Kiongozi wa Harakati ya Kuamsha Ummah wa Mustafa, katika hotuba yake ya hivi karibuni mjini Lahore, amekosoa vikali ukimya wa ulimwengu wa Kiislamu mbele ya uhalifu wa utawala wa Kizayuni dhidi ya watu wa Palestina. Amesema kuwa kusahaulika kwa suala la Palestina ni njama hatari na usaliti usiosameheka, na akasisitiza kwamba ukimya huu – kuanzia vyombo vya habari hadi baadhi ya Serikali za Kiarabu – ni sehemu ya mradi wa kufuta kwa taratibu Palestina kutoka kwenye kumbukumbu ya Ummah wa Kiislamu.
-
Mwanamume Shujaa Kazini | Burkina Faso Yavunja Rekodi Katika Uzalishaji wa Vitunguu!
Burkina Faso sasa imeizidi Senegal katika uzalishaji wa vitunguu na kuwa nchi ya tatu kwa uzalishaji mkubwa wa vitunguu katika eneo la Afrika Magharibi.Mafanikio haya yamechangiwa kwa kiasi kikubwa na uongozi bora wa Rais Ibrahim Traoré, ambaye ameweka mkazo katika kuimarisha sekta ya kilimo na kuinua maisha ya wakulima wa kawaida.
-
Sheikh Hemed Jalala:
Kwa nini Mashia wanatoa Salam za Krismasi kwa Wakristo?! | Pata jawabu maridhawa la swali hilo
Katika maisha ya Mtume wetu Muhammad (saww) ambaye ndiye Kiongozi wetu sisi kama Waislamu, bali Kiongozi wa walimwengu wote, tunapata mifano mingi ya uhusiano mwema na Wakristo, bali watu wote wasiokuwa Waislamu.