shirika la habari la abna
-
Kuimarishwa kwa uhusiano wa kibiashara kati ya Iran na Afrika / Isfahan kuwa mwenyeji wa Mkutano wa Ushirikiano wa Kiuchumi kati ya Iran na Afrika
Waziri wa Viwanda wa Mali, katika hafla ya kufunga Mkutano wa Ushirikiano wa Kiuchumi kati ya Iran na Afrika, alisisitiza umuhimu wa kuimarisha uhusiano wa kibiashara na uwekezaji wa pamoja katika nyanja mbalimbali. Alieleza matumaini kwamba mkutano huu utasababisha mshikamano na maingiliano yenye tija kati ya pande hizo mbili, na akatambua kuwa sekta binafsi ina nafasi muhimu katika mchakato huu.
-
Hakim: Hashd al-Shaabi ina Jukumu la msingi katika kuilinda Iraq
Kiongozi wa Harakati ya Hekima ya Kitaifa ya Iraq amesisitiza umuhimu wa Hashd al-Shaabi katika kulinda nchi ya Iraq na ametoa wito wa kuendelezwa kwa juhudi za kiusalama pamoja na matumizi ya teknolojia za kisasa katika uwanja huo. Sayyid Ammar Hakim pia ameashiria kujitolea kwa Hashd al-Shaabi na nafasi yake katika kuleta uthabiti nchini Iraq, na amesisitiza ulazima wa kulinda heshima na sifa njema ya taasisi hiyo.
-
Raundi ya Nne ya Mazungumzo kati ya Iran na Marekani Kufanyika Jumatano, Mei 7, 2025
Kwa mujibu wa Mwandishi wa Wall Street Journal, muda unaotarajiwa kwa ajili ya mazungumzo yajayo ni tarehe 7 Mei, 2025 (Siku ya Jumatano).
-
Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Kimataifa ya Ahlul-Bayt (a.s):
Mapinduzi ya Kiislamu ni miale ya fikra ya Ahlul-Bayt (a.s) / Magharibi wanapotosha Uislamu, sisi tunapaswa kusimulia ukweli halisi ulivyo
Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Kimataifa ya Ahlul-Bayt (a.s) amesema kuwa Mapinduzi ya Kiislamu ya Iran ni mwangaza unaotokana na fikra na mafundisho ya Ahlul-Bayt (a.s), na kuongeza kuwa: Magharibi wanajitahidi kupotosha taswira ya Uislamu mbele ya dunia, hivyo ni jukumu letu kusimulia ukweli halisi wa Uislamu Sahihi na wa Haki kwa kutumia njia za kisasa za Mawasiliano na Vyombo vya Habari.
-
Utamaduni wa Kisasa wa Mauaji ya Kimbari ya Mawazo na Imani
"Mashambulizi ya Kitamaduni hayako tena katika kiwango cha tahadhari au nadharia; leo hii yamejikita katika kona za fikra za kijana wa Kiiran na kwa utulivu, lakini kwa mfululizo, na yanashambulia imani, utambulisho na mtindo wa maisha ya Kiislamu."
-
"Mkutano wa Tatu wa Kimataifa wa Waandishi wa Habari wa Ahlul Bayt (a.s) umeanza kwa kushirikisha Wanahabari kutoka Bara la Afrika."
Mkutano wa Tatu wa Kimataifa wa Waandishi wa Habari wa Ahlul Bayt (a.s) waanza kwa ushiriki wa wanahabari na wasomi kutoka Iran na Bara la Afrika Mjini Qom
-
Dalili ya wazi na kubwa Kuhusu Kupigana kwa Malaika Pembeni ya Ali (as)
kwa Hakika Amirul-Mu'minin Ali (a.s) hakuwa anarudi kutoka vitani mpaka apate ushindi kwa msaada wa Mwenyezi Mungu. Na ni fadhila iliyo kubwa kiasi gani kuwa Malaika Jibril (as) anapigana upande wa kulia wake, na Mikail (as) upande wa kushoto wake.
-
Makala Fupi Kuhusu Kuzaliwa kwa Sayyidat Fatima Maasoumeh (sa) | Imam Ridha (as) alisema: "Yeyote atakayemzuru Fatima Maasoumeh Qom, atapata Pepo."
Fatima Maasoumeh (sa) alikuwa mashuhuri kwa elimu yake, ibada, na ufasaha. Alifuatilia harakati za kaka yake, Imam Ridha (as), na alikuwa mstari wa mbele katika kutetea haki na kufichua dhulma za watawala wa wakati huo. Katika safari yake ya kuelekea Khurasan kumtembelea kaka yake aliyehamishwa kwa nguvu na Khalifa Ma’mun, Sayyidat Fatima alifika mji wa Qom (Iran ya leo), ambako alipata maradhi mazito na kufariki dunia tarehe 10 Rabi'ul Thani mwaka 201 Hijria. Alizikwa mjini Qom, ambao baadaye ukawa kituo muhimu cha elimu ya Kiislamu.
-
Matendo Mema katika Dua na Swala za Sunna (Sehemu ya 1)
Huu ni mkusanyiko uliokusanya baadhi ya matendo ya kufanya usiku na mchana, swala za Sunnah zilizopokewa, ponyo, kinga, dhikir, dua za ajabu, athari za baadhi ya Aya na ufupisho wa kuwafanyia adabu waliokufa, nimezikusanya ili niziambatanishe kwenye Mafatihul Jinani kisha kitabu kikamilike kwa njia zote na iwe na manufaa kwayo yaliyotimia.
-
Siku ya Wakati Maalum:
Ni ipi Maana ya Kauli ya Mwenyezi Mungu aliposema kumwambia Shetani: "یوم الوقت المعلوم" “Siku ya Wakati Maalum"
katika ufahamu wa Shia (Wafuasi wa Ahlul-Bayt - a.s - ), "یوم الوقت المعلوم" ni Siku ya dhahiri ya Haki na Uadilifu wa Mwenyezi Mungu Duniani, yaani Siku ya Mapinduzi ya Dunia yakiongozwa na Imam Mahdi (a.t.f.s), kabla ya Siku ya Kiyama.
-
Hadithi ya Shetani na Mwanadamu:
"Siri ya Muda wa Shetani Kuishi: Kwa Nini Mwenyezi Mungu Alimpa Shetani Muda Mrefu wa Kuishi?
Tangu wakati huo ambapo Shetani aliasi na kukataa kumsujudia Adam (a.s), mzozo wa kihistoria kati yake na Mwanadamu ulianza; mzozo ambao unaendelea hadi leo hii. Lakini swali muhimu ni hili: Kwa nini Mwenyezi Mungu alimpa adui huyu katili (Shetani) muda mrefu wa kuendelea kuishi na kujaribu na kuwapoteza watoto wa Adam (Wanadamu)?!. Nakuletea Hadithi nzuri na yenye mazingitio ndani yake kuhusu Shetani na Mwanadamu, na utaijua sababu na siri ya Ruhusa ya Mwenyezi Mungu kwa Shetani ili aendelee kuishi kwa muda mrefu.
-
Yemen yaachia kombora la Hipersoniki kulenga kituo cha kijeshi cha Wazayuni katika eneo la Negev
Jeshi la Missili la Jeshi la Silaha la Yemen limetekeleza operesheni ya kijeshi ikilenga Kituo cha Anga cha Nevatim katika eneo la Negev, kusini mwa Palestina iliyokaliwa, kwa kutumia kombora la hipersoniki la balistiki.
-
Waqfu wa Kiongozi wa Mapinduzi 5 / Mtoaji mkubwa wa Waqfu wa Nakala za Maandishi ya Kale katika historia ya Haram Tukufu ya Razavi
Kiongozi Mkuu wa Mapinduzi, pamoja na Waqfu mbalimbali alizotoa kwa Haram Tukufu ya Razavi katika zaidi ya miaka 40 iliyopita, ametoa waqfu wa vitabu vingi vya kale kuliko wakati mwingine wowote katika historia ya Haram Tukufu ya Razavi.
-
Hadithi / Tukio la Kushusha Bendera ya Kuba ya Haram ya Bibi Zainab (a.s)
Imam wa Haram ya Bibi Zainab (a.s) alitangaza sababu ya kushushwa kwa bendera iliyokuwa juu ya Kuba ya Haram hiyo Tukufu.
-
Katika kongamano la Kimataifa la "Sayansi, Dini, na Akili Bandia" lililofanyika Zagreb, Shahriyari:
Akili bandia si dhana bali ni mshirika kwa Binadamu katika kila dakika ya maisha yake
Katibu Mkuu wa Umoja wa Kimataifa wa Kuleta Ukaribu wa Madhehebu ya Kiislamu alisema: Mjadala wa akili bandia ni mpana sana na unahusisha kila nyanja ya maisha ya binadamu, na kila mtu anapaswa kuuhusisha kulingana na wajibu wake mwenyewe.
-
Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Kimataifa ya Umoja wa Madhehebu ya Kiislamu:
Udhalilishaji wa hivi karibuni wa mambo matukufu ya Waislamu wa Kisunni una nyanja tata zaidi
Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Kimataifa ya Kudumisha Umoja wa Madhehebu ya Kiislamu akilaani udhalilishaji wa mambo matukufu ya Waislamu wa Kisunni alisema: Udhalilishaji wa hivi karibuni una nyanja tata zaidi, na inatarajiwa kutoka kwa viongozi wa masuala haya kuchukua hatua za kuzuia kurudiwa kwa maafa kama haya.
-
Serikali ya Muda ya Afghanistan Yatoa Pole kwa Watu wa Iran Kufuatia Mlupuko wa Bandar Abbas
Baada ya mlipuko uliotokea jana katika Bandari ya Shahid Rajaei iliyopo katika Mji wa Bandar Abbas, Serikali ya Muda ya Afghanistan, sambamba na mataifa mengi duniani, imetoa pole kwa watu na Serikali ya Iran.
-
Iran | Kesho ni Siku ya Maombolezo ya Kitaifa Nchini Iran / Idadi ya Waliopoteza Maisha Yafikia 28
Baada ya tukio la kusikitisha katika Bandari ya Shahid Rajaei lililosababisha vifo vya makumi ya raia wapenzi wa Iran, Baraza la Mawaziri limetangaza kuwa kesho kutakuwa na maombolezo ya kitaifa kote nchini.
-
"Hezbollah ya Lebanon imetoa pole kwa Kiongozi wa Mapinduzi na Taifa la Iran kufuatia tukio la Mlipuko wa Bandar Abbas"
Baada ya tukio la kusikitisha katika Bandari ya Shahid Rajaei Bandar Abbas lililosababisha mashahidi na majeruhi kadhaa, Hezbollah ya Lebanon imetoa taarifa ya kuonesha mshikamano na Jamhuri ya Kiislamu ya Iran.
-
Ukabidhi wa Hiari wa Silaha Parachinar; Hatua Muhimu kuelekea Amani Endelevu
Baada ya utekelezaji wa Mkataba wa Amani wa Kohat, Waislamu wa madhehebu ya Shia katika wilaya ya Kurram, eneo la Parachinar nchini Pakistan, wamekabidhi silaha zao kwa hiari kwa wawakilishi wa jeshi na maafisa wa serikali ya Pakistan ili kuonesha nia yao ya kutafuta amani.
-
Mufti na Sheikh Mkuu wa Tanzania, Dr.Abubakar Zubair bin Ally, asisitiza umuhimu wa Elimu ya Dini ya Kiislamu
Elimu ya dini ni muhimu kwa msingi wa maadili mema, lakini haiwezi kuchukua nafasi ya elimu ya dunia katika maendeleo ya kiuchumi na kijamii ya taifa. “Tunapaswa kuwa na masheikh na maimamu, lakini pia tuwe na madaktari, wahandisi na wanasayansi,”.
-
Hawzat Hazrat Zainab (sa) Kigamboni - Dar-es-salaam | Wanawake katika Kuadhimisha Shahadat ya Imam Sadiq (a.s) + Picha
Wanawake katika jamii za Kiislamu wanachukua jukumu muhimu katika kuadhimisha kifo cha Kishahidi cha Imam Sadiq (a.s), ambapo si tu wanahudhuria kimwili katika vikao kama hivi vya Maombolezo, bali pia wanashiriki kikamilifu kwa njia ya vitendo katika kueneza mafundisho ya Imam Sadiq (as) katika nyanja mbalimbali.
-
Dr. Ali Taqavi, Mwakilishi wa Jamiat Al-Mustafa (s)Tanzania, akiambatana na Sheikh Dr. Alhad Mussa Salum watembelea uwanja wa Michezo Zanzibar + Picha
Uislamu umesisitiza Umoja wa Kiislamu, na madhehebu yote ya Kiislamu yanaunganishwa na Umoja wa Kiislamu, na Kibla cha Waislamu wote ni kimoja, na Qur'an ndio Kitabu chao na Muongozo wao.
-
Dr. Ali Taqavi, Mwakilishi wa Jamiat Al-Mustafa (s), Dar-e-Salam, Tanzania, katika ziara muhimu Zanzibar - Tanzania + Picha
"Ni muhimu kwa Wanafunzi kuzingatia elimu na maarifa ya Qur'an Tukufu, na kuwaasa katika kuzidisha juhudi zao kwenye suala muhimu la kusoma na kuhifadhi Qur'an Tukufu, na kuiweka Qur'an Tukufu mbele ya Maisha yao ya kila siku".
-
Tarehe 25 Shawwal Mwaka 148 Hijiria, ulimwengu wa Kiislamu ulipatwa na Huzuni kufuatia kuondokewa na mmoja wa Ahlul-Bayti wa Mtume wa Uislamu (saww)
Licha ya kwamba Ahlul-Bayti wa Mtume (s.a.w.w) walikabiliwa na changamoto tofauti kisiasa na kijamii, lakini walijitahidi kuhakikisha wanainua bendera ya dini ya Kiislamu katika zama zao zote. Dakta Shahid Mutwahhari, mwanafikra mashuhuri wa Iran anaandika kwa kusema: " Ahlul-Bayti (a.s) walikuwa wakichunga maslahi ya Kiislamu na Waislamu kwa ujumla".
-
Je, Mazungumzo Kati ya Mwanamume na Mwanamke Wasiokuwa Mahramu Yamekatazwa kwa namna yoyote ile katika Uislamu?
“Kauli yenye nguvu zaidi ni hii kwamba kusikia (kusikiliza) sauti ya Mwanamke asiyekuwa Mahram, maadamu si kwa ajili ya tamaa, starehe au maslahi, ni jambo linaloruhusiwa (linajuzu). Vivyo hivyo kwa Mwanamke, ikiwa hakuna hofu ya fitina, anaweza kusikika na Wanaume wasio mahram kwake".
-
Kumbukumbu ya Shahada ya Imam Ja’far al-Sadiq (a.s) | Jua la Elimu na Uchaji Mungu Limezimwa
Shahada ya Imam Ja’far al-Sadiq (a.s) haikuwa tu kumpoteza kiongozi wa kiroho, bali ilikuwa ni jaribio la kuangamiza nuru ya elimu na mwongozo wa Ahlul Bayt(a.s). Hata hivyo, athari ya mafundisho yake bado inaishi hadi leo kupitia Maktaba ya Ja’fariyya, ambayo ni msingi wa Madhehebu ya Shia Ithna ‘Ashari.
-
Mkutano wa Mufti wa Burundi na Mwakilishi wa Al-Mustafa (s) Nchini Tanzania + Picha
Mufti wa Burundi akutana na kuzungumza na Hojjatul Islam wal-Muslimin, Dr.Ali Taqavi Katika Ofisi ya Al-Mustafa (s) Dar -es- Salaam - Tanzania.
-
Afrika Katika Ramani ya Utalii wa Vyakula: Tanzania Yaongoza Jitihada
Tanzania inatazamiwa kuwa mwenyeji wa Kongamano la 2 la Umoja wa Mataifa la Elimu ya Utalii kwa Afrika Mwezi Aprili 2025, likileta pamoja wataalamu wa kimataifa ili kuangazia umuhimu wa utalii wa upishi katika kukuza uchumi na kukuza urithi wa vyakula mbalimbali Barani Afrika.
-
Palestina lazima ibaki / Watawala wetu wamepotoka kutoka kwenye Misingi ya Umma wa Kiislamu
Mwenyekiti wa Majlisi ya Umoja wa Waislamu wa Pakistan akisisitiza umuhimu wa kuendelea kuiunga mkono Palestina amesema kuwa, watawala na wanasiasa wa sasa wa nchi hiyo wamejitenga na thamani halisi za Umma wa Kiislamu.