Shirika la Habari la Kimataifa la Ahlul-Bayt (as) -ABNA- limeripoti kuwa mamlaka za DCEA (Drug Control and Enforcement Authority) zimefanikiwa kukamata pakiti 20 za dawa za kulevya aina ya skanka, zenye uzito wa kilogramu 20.03, zilizokuwa zimefichwa ndani ya balo la mitumba.

Dawa hizo ziligundulika kufichwa kwenye bus aina ya Scania lenye namba za usajili AAM 297 CA, kutoka Kampuni ya King Masai Tours. Bus hilo linafanya safari zake kati ya Nampula, Msumbiji, na Dar es Salaam, Tanzania.

Mamlaka za DCEA zimetangaza kuwa watuhumiwa wawili wamekamatwa kutokana na tukio hili:
1_Amasha Iddi Mrisho (40), mkazi wa Buza, Dar es Salaam
2_Seleman Juma Ally (32), raia wa Msumbiji.
Hali ya watuhumiwa hao na uchunguzi wa kina unaendelea, huku mamlaka zikitoa wito kwa wananchi kuwa makini na shughuli zinazohusiana na usafirishaji wa mizigo ya hatari.
Mamlaka za DCEA zinaendelea kuimarisha operesheni za kudhibiti dawa za kulevya katika mipaka na maeneo makuu ya miji nchini, kwa lengo la kupunguza uenezaji wa dawa hatari na kulinda usalama wa wananchi.

Your Comment