Dar es salaam
-
Hafla ya Ugawaji Zawadi kwa Washindi wa Mashindano ya Uandishi wa Muhtasari "Summary Writing" Yafanyika Kigamboni - Dar-es-salaam
Katika hafla iliyofanyika katika shule ya wasichana ya Kigamboni, washindi wa mashindano ya kuandika muhtasari kuhusu “Shahada ya Ayatollah Sayyid Ali Khamenei (ra)” walikabidhiwa zawadi maalum katika mwendelezo wa masomo ya Qur’an chini ya usimamizi wa Bi. Fatma Ma‘suma, ikiwa ni sehemu ya kuhamasisha elimu, ubunifu na ushindani wenye tija kwa wanafunzi.
-
Tanzania Yakamata Pakiti 20 za Skanka Zenye Kilogramu 20 Kwenye Bus la Kimataifa, Temeke - Dar-es-salaam
Mamlaka ya DCEA imekamatwa pakiti 20 za skanka zenye uzito wa kilo 20.03 zilizofichwa kwenye balo la mitumba ndani ya bus la Scania la King Masai Tours, lenye namba za usajili AAM 297 CA, likisafiri kati ya Nampula, Msumbiji na Dar es Salaam. Watuhumiwa waliokamatwa ni Amasha Iddi Mrisho (40) kutoka Dar es Salaam na Seleman Juma Ally (32) raia wa Msumbiji. Uchunguzi na kesi za kiutumishi zinaendelea.
-
Majlis ya Kuhuisha Shahada ya Sayyidat Fatima Al-Zahra (sa) kwa Akina Mama Jijini Dar es Salaam +Picha
Katika khutba yake, Sheikh Ja'far Mwazoa alieleza kwa ufafanuzi wa kina fadhila zake nyingi, akibainisha namna ambavyo Bibi Fatima (sa) ni kigezo bora cha kuigwa na wanawake wote wa Kiislamu, na hata wanaume wa Umma wa Mtume Muhammad (saww), kutokana na uchamungu wake, hekima yake, na msimamo wake thabiti katika kutetea ukweli.
-
Ujumbe wa Kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu kwa Mkutano wa 32 wa Kitaifa wa Sala
Ayatollah Khamenei katika ujumbe wake kwa Mkutano wa 32 wa Kitaifa wa Sala alielezea mambo muhimu yanayohusu mkutano huu pamoja na sifa za sala.
-
Kuzingatia Umuhimu wa Swala ya Ijumaa na Tabia Njema katika Hawzat ya Wasichana ya Hazrat Zainab (s.a) - Tanzania
Hadithi: “إِنَّمَا بُعِثْتُ لِأُتَمِّمَ مَکَارِمَ الأَخْلَاقِ.” “Mimi nimetumwa ili nikamilishe tabia njema.” Aya Tukufu: «قَدْ أَفْلَحَ مَن زَكَّاهَا وَقَدْ خَابَ مَن دَسَّاهَا» (Surat Ash-Shams, Aya 9–10). "Amefaulu yule aliyeitakasa nafsi yake, na ameharibikiwa yule aliyeichafua (aliyeifisidi)".
-
Mazoezi ni Afya: Jamiat Al-Mustafa (s) Yaendeleza Michezo kwa Ajili ya Kuimarisha Afya ya Mwili na Akili
Kwa hakika, michezo na mazoezi haya yamekuwa kielelezo cha namna Uislamu unavyopenda mwili wenye nguvu, akili timamu, na mshikamano wa kijamii, ili kumsaidia Muislamu kuwa na uwezo wa kutekeleza majukumu yake ya kidini, kijamii na kiulimwengu.
-
Jamiatul Mustafa (s) Yaandaa Maadhimisho ya Maulid Al-Nabi, Dar-es-Salaam - Tanzania | Fursa ya Kusherehekea Kuzaliwa kwa Mtume Wetu Muhammad(s.a.w.w)
Maulid hii itafanyika Tarehe 07-09-2025, Pweza Beach Road - Kigamboni, Dar-es-salaam.
-
Jamiat Al-Mustafa (s) - Dar-es-salaam | Mtihani wa Kila Wiki: Hatua ya Kuimarisha Uelewa na Maandalizi Bora ya Kielimu na Ufaulu wa Wanafunzi
Kupitia mitihani hii ya wiki, walimu hupata nafasi ya kufuatilia maendeleo ya kielimu kwa kila mwanafunzi, kutambua changamoto zinazojitokeza katika masomo, na kuweka mikakati ya kuboresha ufaulu.
-
-
Chuo Kikuu cha al-Mustafa (s) Dar es Salaam - Tanzania Chaandaa Kongamano la Kielimu Kuhusu: "Dakika za Mwisho za Maisha ya Mtume Muhammad (s.a.w.w)"
Mtoa Mada: Sheikh Taqi Zakariya. Tarehe: Jumamosi, 16-08-2025. Muda: Kuanzia Saa 4:00 Ask Asubuhi hadi 6:00 Mchana. Eneo: Muswalla wa Chuo Kikuu cha Al-Mustafa (s) - Dar-es-salaam. Mwaliko huu ni kwa Wote.
-
Wanafunzi wa Chuo cha Kimataifa cha Al-Mustafa (s) Foundation wakihuisha Usomaji wa Dua ya Nudba Leo hii Mbezi Beach, Jijini Dar-es-Salaam
Matukio kama haya ya Usomaji wa Dua mbalimbali yanaongeza moyo wa ibada miongoni mwa wanafunzi na hutoa nafasi ya kuungana kiroho katika jamii ya hawza hiyo, huku yakihimiza umuhimu wa dua kama silaha ya waumini katika maisha ya kila siku.
-
Dua ya Nudba Yafanyika Leo hii Ijumaa Katika Hawza ya Mabanati ya Hazrat Zainab (sa), Kigamboni - Dar-es-Salam
Usomaji wa Dua wa namna hii kawaida huvutia ushiriki mkubwa wa Wanafunzi na Wapenzi wa Ibada na Dua, na kuleta hali ya utulivu wa kiibada katika mazingira ya Chuo hiki cha Kiislamu.
-
Sheikh Dr. Alhad Musa Salum Akabidhiwa Tuzo ya Uongozi wa Mfano na JMAT Mkoa wa Dar -es- Salaam
Tukio hilo lilifanyika katika Mkutano Mkuu wa Mkoa wa JMAT kwa Muhula wa Kwanza wa Mwaka 2025, ambapo viongozi mbalimbali wa kidini na kijamii walihudhuria.
-
Madrasa Hazrat Zainab (sa) | Dini na Afya: Dkt. Beshteri Azungumzia Umuhimu wa Lishe Sahihi kwa Muislamu
Dkt. Beshteri alieleza kuhusu adabu za kula chakula kulingana na mafundisho ya Imam Ja’far Sadiq (a.s), akitaja riwaya mbalimbali zinazoelekeza namna bora ya kula kwa mujibu wa maadili ya Kiislamu.
-
Swala ya Ijumaa - Madrasa Hazrat Zainab (sa) - Kigamboni | Changamoto za Kijamii Zinazotokana na Kuachana na Mafundisho ya Dini
Sala ilisaliwa kwa nidhamu kubwa na utulivu wa hali ya kiroho, na iliacha athari kubwa kwa washiriki wote katika ibada hii.
-
Jumuiya ya Waislamu wa Shia Khoja Ithna Ashari Jamiat katika Matembezi ya A'shura
ASHURA ni siku ya kumi ya mwezi mtukufu wa Muharram. Katika siku hii ya Ashura mjukuu wa Mtume yaani Imam Hussain (as) aliuawa katika tambarare za mji wa Karbala baada ya kusimama kidete dhidi ya mtawala dhalimu wa wakati ule, Yazid bin Muawiya, akatoa fundisho la kukataa kumpigia magoti mdhalimu huyo, ndipo akajitolea maisha yake, akauawa ili kunusuru ubinaadamu , utu pamoja na kupigania uislamu.
-
Dkt. Al-Had Mussa Salum - Mwenyekiti wa Jumuiya ya Maridhiano na Amani Tanzania (JMAT-TAIFA) Azungumzia Mambo Matatu Muhimu kwa Mustakbali wa Taifa
JMAT imepanga kuendesha matembezi ya amani kutoka Dar es Salaam hadi Dodoma, Makao Makuu ya Tanzania. Lengo ni kuleta Watanzania pamoja na kuhamasisha Amani na Maridhiano hasa katika kipindi hiki cha kuelekea katika Uchaguzi Mkuu.
-
Dar es Salaam, Tanzania - Mei 2025:
BAKWATA Yatangaza Rasmi Tarehe ya Sikukuu ya Eid El-Adh’ha: Jumamosi, Juni 7, 2025
Taarifa hiyo imetolewa na Katibu Mkuu wa BAKWATA, Alhaj Nuhu Jabiri Mruma, ambapo imeelezwa kuwa sherehe za kitaifa za Eid El-Adh’ha mwaka huu zitafanyika jijini Dar es Salaam, katika Msikiti wa Mfalme Mohamed VI uliopo Makao Makuu ya BAKWATA – Kinondoni.
-
Mada ya Ijumaa Masjidul Ghadir Kigogo Post: "Hijjah na Athari Zake Katika Malezi (ya Watoto na Jamii)"
Tarehe: Ijumaa, 30 Mei 2025. Mahali: Masjidul Ghadir, Kigogo Post – Dar-es-Salaam, Tanzania. Khatibu wa Swala ya Ijumaa: Maulana Sheikh Hemed Jalala. Mada ya Khutba ya Ijumaa: "Hijjah na Athari Zake Katika Malezi". Khutba hii iliangazia Nafasi ya Hijjah kama Shule ya Malezi ya kina, ikihimiza wazazi na jamii kwa ujumla kutumia mafundisho ya Hijjah kuwalea watoto katika misingi ya Utii, Ucha Mungu, Uvumilivu, Unyenyekevu na Umoja. Pia, iliweka msisitizo wa umuhimu wa Mwezi wa Dhilhijja katika historia ya Uislamu na fadhila za ibada ndani yake.
-
Ziara ya Maulana Sheikh Jalala Hospitali ya Mloganzila kumtembelea Sheikh Mbelango Allah aimarishe Afya yake
Tunamuomba Mwenyezi Mungu Mtukufu ampe afueni ya haraka na amuwekee wepesi katika kila jambo. Uwepo wake ni hazina kwa Uislamu na Waislamu.