Shirika la Habari la Kimataifa la Ahlul-Bayt (as) - ABNA - Mkutano ulifanyika kati ya Mrs. Taqavi, Mkurugenzi (Mudira) wa Shule ya Wasichana ya Hazrat Zahra (sa) na Wanafunzi wa Shule hiyo, ambapo mada kuu zilijumuisha maendeleo ya kielimu, masuala ya utawala wa shule, na njia za kuboresha mazingira ya kujifunzia.
Mkurugenzi alisisitiza umuhimu wa bidii katika masomo, kushirikiana na walimu, na kuwa na nidhamu katika shule.
Wanafunzi walikubaliana kuwa ni muhimu kujizatiti ili kufikia malengo yao ya kitaaluma, na walieleza changamoto wanazokutana nazo katika masomo na maisha ya shule.
Mkutano ulimalizika kwa mipango ya kuboresha huduma za shule na kuimarisha ushirikiano kati ya wanafunzi na walimu.
Your Comment