Tanzania
-
Wito wa Kwanza | Tamasha la Kitaifa la Ushairi wa Ghadir Kufanyika Katika Chuo Cha Jamiat Al-Mustafa Foundation - Mbezi Beach - Dar-es- Salaam
Washairi wa Kiislamu kutoka sehemu mbalimbali watahudhuria kwa ajili ya kusoma mashairi yanayogusa nyoyo kuhusu: Tukio la Ghadir, Mapenzi kwa Ahlul-Bayt(as), na mafundisho ya Kiislamu.
-
Dkt. Al-Had Mussa Salum - Mwenyekiti wa Jumuiya ya Maridhiano na Amani Tanzania (JMAT-TAIFA) Azungumzia Mambo Matatu Muhimu kwa Mustakbali wa Taifa
JMAT imepanga kuendesha matembezi ya amani kutoka Dar es Salaam hadi Dodoma, Makao Makuu ya Tanzania. Lengo ni kuleta Watanzania pamoja na kuhamasisha Amani na Maridhiano hasa katika kipindi hiki cha kuelekea katika Uchaguzi Mkuu.
-
Wanafunzi wa Madrasatul Hizbullah Al-‘Ilmiyyah Wafanya Mtihani wa Mwisho wa Mwezi - Kazole, Vikindu
Madrasatul Hizbullah Al-‘Ilmiyyah inatoa wito kwa jamii kuendelea kuiunga mkono taasisi hiyo ili iweze kuendelea kutoa elimu bora na kukuza kizazi chenye maarifa, hikma na hofu ya Mwenyezi Mungu.
-
Dar es Salaam, Tanzania - Mei 2025:
BAKWATA Yatangaza Rasmi Tarehe ya Sikukuu ya Eid El-Adh’ha: Jumamosi, Juni 7, 2025
Taarifa hiyo imetolewa na Katibu Mkuu wa BAKWATA, Alhaj Nuhu Jabiri Mruma, ambapo imeelezwa kuwa sherehe za kitaifa za Eid El-Adh’ha mwaka huu zitafanyika jijini Dar es Salaam, katika Msikiti wa Mfalme Mohamed VI uliopo Makao Makuu ya BAKWATA – Kinondoni.
-
Mada ya Ijumaa Masjidul Ghadir Kigogo Post: "Hijjah na Athari Zake Katika Malezi (ya Watoto na Jamii)"
Tarehe: Ijumaa, 30 Mei 2025. Mahali: Masjidul Ghadir, Kigogo Post – Dar-es-Salaam, Tanzania. Khatibu wa Swala ya Ijumaa: Maulana Sheikh Hemed Jalala. Mada ya Khutba ya Ijumaa: "Hijjah na Athari Zake Katika Malezi". Khutba hii iliangazia Nafasi ya Hijjah kama Shule ya Malezi ya kina, ikihimiza wazazi na jamii kwa ujumla kutumia mafundisho ya Hijjah kuwalea watoto katika misingi ya Utii, Ucha Mungu, Uvumilivu, Unyenyekevu na Umoja. Pia, iliweka msisitizo wa umuhimu wa Mwezi wa Dhilhijja katika historia ya Uislamu na fadhila za ibada ndani yake.
-
Mahojiano Maalum ya Firdaus TV na Sheikh Dkt. Alhad Mussa Salum - Mwenyekiti JMAT-TAIFA Yaliyofanyika Katika Uwanja wa Michezo wa Mkwakwani, Tanga
Ni katika Kongamano la Qur'an Tukufu lililofanyiks Jijini Tanga. Tukio hilo liliimarisha misingi ya Amani, Mshikamano, Maridhiano, na Ushirikiano kati ya Watanzania, likiwa ni Jukwaa la kuendeleza Mafundisho ya Qur’an Tukufu yanayohimiza Utulivu na Maelewano ya Kijamii.
-
JMAT Yatoa Wito kwa Viongozi wa Dini Nchini Kenya wa Kushirikiana Katika Kuwaongoza Wananchi wao ili Kuheshimiana na Kutunza Mahusiano ya Amani
Sheikh Dkt. Alhad Mussa Salum: "Wakenya ni ndugu wa Watanzania, na mbali na uhusiano wa kijamii, ni ndugu wa damu. Tunatambua kuwa mizozo hii inahusu zaidi vijana wa Kenya, lakini ni muhimu kuwakumbusha kuwa heshima ni nguzo muhimu katika mahusiano ya mataifa. Tunaamini Kenya ina Viongozi wa Dini na Serikali wanaoweza kusaidia katika hili."
-
Ziara ya Maulana Sheikh Jalala Hospitali ya Mloganzila kumtembelea Sheikh Mbelango Allah aimarishe Afya yake
Tunamuomba Mwenyezi Mungu Mtukufu ampe afueni ya haraka na amuwekee wepesi katika kila jambo. Uwepo wake ni hazina kwa Uislamu na Waislamu.
-
Ripoti ya Mahudhurio ya Wasomaji wa Qur'an wa Programu ya "Mahfali" nchini Tanzania
Katika hafla hii Tukufu ya Qur’an, wasomaji wa Kiirani walioshiriki ni pamoja na Ustadh Shakernejad, Ustadh Abolghasemi, Qari kijana Mohammad Hossein Azimi, na Muhanna Ghanbari – ambaye ni mhifadhi wa Qur’an nzima.
-
Heshima ya Mwanamke wa Kiislamu Katika Muonekano wa Vazi la Hijabu: Mfano wa Mabinti wa Hawzat Hazrat Zainab (sa), Dar es Salaam – Tanzania
Leo hii katika viwanja vya Mnazi Mmoja, jijini Dar es Salaam - Tanzania, palifanyika Kongamano Tukufu la Qur’an ambapo wanafunzi wa kike kutoka Hawzat Hazrat Zainab (sa) walishiriki kwa umahiri na adabu kubwa. Walikuwa mfano halisi wa utekelezaji wa mafundisho bora ya Kiislamu kuhusu namna ya kujisitiri, kuishi, na kuwasilisha ujumbe wa dini kwa vitendo.
-
Sheikh Hemed Jalala | Khutba ya Ijumaa (Malezi ya Watoto) - Masjidul Ghadir, Kigogo Post, Dar-es-Salaam
Sheikh Hemed Jalala alisisitiza umuhimu wa malezi bora ya watoto kwa kufuata misingi thabiti ya Kiislamu. Alibainisha kuwa familia ni msingi wa jamii, na hivyo malezi ya mtoto yanapaswa kuakisi maadili na mafundisho ya dini.
-
Kisomo cha Dua ya Kumail katika Hawza ya Hazrat Zainab (sa) – Kigamboni, Dar-es-Salaam
Hawza ya Hazrat Zainab (sa) iliyoko Kigamboni, Dar-es-Salaam, ni chuo makhsusi kwa ajili ya kuwalea mabinti wa Kiislamu kielimu na kimaadili. Chuo hiki kipo chini ya usimamizi wa Jamiat Al-Mustafa (s) – Tanzania, na mbali na masomo ya kielimu yanayotolewa humo, wanafunzi pia hupatiwa malezi ya kiroho kwa kupitia mafundisho ya dua na ibada.
-
Sheikh Dr.Alhad Mussa Salum awaalima watu wote katika Maonyesho ya Qur'an | Dar-es-salaam na Tanga
Qur'an Tukufu ni: Shifa (ponyo) kwa magonjwa ya kiroho na ya moyo kama vile wasiwasi, huzuni, mashaka, ujinga, na upotevu. Na ni Mwongozo wa maisha kwa binadamu wote—kwa mambo ya kidini na ya kila siku.
-
Mkutano wa Mrs.Taqavi, Mudira wa Hawzat ya Wasichana ya Hazrat Zahra (s.a) na Wanafunzi wa Hawzat hiyo
Mkutano ulimalizika kwa mipango ya kuimarisha ushirikiano kati ya Wanafunzi na Walimu.
-
Hawzat Hazrat Zainab (sa) Kigamboni - Dar-es-salaam | Wanawake katika Kuadhimisha Shahadat ya Imam Sadiq (a.s) + Picha
Wanawake katika jamii za Kiislamu wanachukua jukumu muhimu katika kuadhimisha kifo cha Kishahidi cha Imam Sadiq (a.s), ambapo si tu wanahudhuria kimwili katika vikao kama hivi vya Maombolezo, bali pia wanashiriki kikamilifu kwa njia ya vitendo katika kueneza mafundisho ya Imam Sadiq (as) katika nyanja mbalimbali.
-
Dr. Ali Taqavi, Mwakilishi wa Jamiat Al-Mustafa (s)Tanzania, akiambatana na Sheikh Dr. Alhad Mussa Salum watembelea uwanja wa Michezo Zanzibar + Picha
Uislamu umesisitiza Umoja wa Kiislamu, na madhehebu yote ya Kiislamu yanaunganishwa na Umoja wa Kiislamu, na Kibla cha Waislamu wote ni kimoja, na Qur'an ndio Kitabu chao na Muongozo wao.
-
Dr. Ali Taqavi, Mwakilishi wa Jamiat Al-Mustafa (s), Dar-e-Salam, Tanzania, katika ziara muhimu Zanzibar - Tanzania + Picha
"Ni muhimu kwa Wanafunzi kuzingatia elimu na maarifa ya Qur'an Tukufu, na kuwaasa katika kuzidisha juhudi zao kwenye suala muhimu la kusoma na kuhifadhi Qur'an Tukufu, na kuiweka Qur'an Tukufu mbele ya Maisha yao ya kila siku".
-
Afrika Katika Ramani ya Utalii wa Vyakula: Tanzania Yaongoza Jitihada
Tanzania inatazamiwa kuwa mwenyeji wa Kongamano la 2 la Umoja wa Mataifa la Elimu ya Utalii kwa Afrika Mwezi Aprili 2025, likileta pamoja wataalamu wa kimataifa ili kuangazia umuhimu wa utalii wa upishi katika kukuza uchumi na kukuza urithi wa vyakula mbalimbali Barani Afrika.
-
Ufafanuzi kwa ufupi kuhusiana na hatua za mashindano ya Qur'an Tukufu na Hadithi - Jamiat Al-Mustafa (s), Dar-es-Salam - Tanzania, 2025
Tangazo la Matokeo ya mwisho litatolewa kuanzia Tarehe 01 - 05 - 2025 mpaka tarehe 05 - 05 - 2025. Na ratiba ya hafla ya fainali ya mashindano haya pamoja na ugawaji wa zawadi kwa washindi na washiriki utakuwa tarehe 17 - 05 - 2025 katika Ukumbi wa Mikutano ya Kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere - Jijini Dar-es-Salam - Tanzania.
-
Chuo Kikuu cha Jamiatul Mustafa - Dar-es-salaam - Tanzania kimeandaa Kongamano la Kisayansi kuhusu Maendeleo katika Ulimwengu wa Kiislamu
Kongamano hili litajadili juu ya Maendeleo katika Ulimwengu wa Kiislamu kati ya changamoto na mkakati. Mhadhiri: Samahat Sheikh Mulaba Saleh. Siku ya: Jumamosi; 19/04/2025. Kuanzia: 10 - 12:00 AM. Katika Ukumbi wa Sala wa Chuo cha Jamiat Al- Mustafa. Watu wote mnakaribishwa kuhudhuria katika nad'wa hii ya Kisayansi.
-
Mufti wa Tanzania atangaza Dua ya Kuiombea Nchini na Wazee waliotangulia mbele ya Haki | Rais Samia Hassan na Rais Mwingi Kushiriki
Dua ya Kuiombea Taifa la Tanzania na kuwarehemu Wazee wetu waliotangulia mbele ya Haki itaongozwa na Mheshimiwa Mufti wa Tanzania.
-
Dr. Ali Taqavi, Mwakilishi wa Jamiat Al-Mustafa (S) - Dare-es-Salam, Tanzania, katika Mkutano muhimu na Mh.Mufti wa Zanzibar, Sheikh Saleh Kaabi
Kufanyika kwa Hafla ya Qur'an Tukufu ndani ya Zanzibar kwa ushirikiano baina ya Jamiat Al-Mustafa - Dares-Salam - Tanzania na BAKWATA
-
Siri na Falsafa ya Ratiba ya Darsa ya "Subhi ya Kimaanawi" kwa Wanafunzi wa Jamiat Al-Mustafa, Dar-es-Salam, Tanzania + Picha
Maulamaa wakubwa katika historia zao, walikuwa wakitafuta Adabu (Maadili) kwanza, kisha ndio wanaitafuta elimu. Wengine walikuwa wakiitafuta adabu kwa muda wa miaka 30, na elimu wanaitafuta kwa muda wa miaka 20.
-
Kozi ya Kompyuta kwa Vitendo ya ICDL kwa Wanafunzi wa Hawzat Sayyidat Zainab (s.a) - Jamiat Al-Mustafa, Dar -es- Salaam - Tanzania
ICDL inawakilisha Leseni ya Kimataifa ya Fani ya (Computer) Kompyuta. Na hiyo ndio maana ya Kozi hii ya ICDL - Yaani: International Computer Driving License. Hii ni Kozi muhimu katika Kozi za Kompyuta ambazo zinauwezo wa kumsaidia na kumsapoti mtu yeyote kujikwamua Kiuchumi.
-
Mubahatha [Kudurusu kwa Pamoja] - Kwa wanafunzi na watafutaji elimu wote!
Ufahamu huwa na viwango tofauti tofauti, kwa malezi au asili. Wewe ambae ni Mwanafunzi katu usipuuze hichi kipengele cha majadiliano ya kielimu baada ya kupokea maarifa ya mada fulani kutoka kwa Mwalimu.
-
Ugumu uliopo katika kuwatangaza Kizazi Kitukufu cha Mtume Muhammad (saww) ambao ni Mawalii wa Mwenyezi Mungu (s.w.t) | Watu hawawajui Ahlu-Bayt (as)!
Leo hii, jambo la kuwatangaza Ahlul-Bayt (a.s) ambao ndio tumeusiwa na Mtume wetu Muhammad (s.a.w.w) tushikamane nao baada yake na kuwafuata wakiwa wakiwa kama Kizito cha Pili baada ya Qur'an Tukufu, ni jambo gumu kulingana na jamii ya watu tunayokabiliana nayo.
-
Al_Itrah Foundation, Dar-es-salaam - Tanzania yampa zawadi ya Tafsiri ya Kiswahili ya Qur'an Tukufu Mwenyekiti wa JMAT - TAIFA Sh.Dr Alhad Mussa Salum
"Kitabu Hicho Hakina Shaka ndani yake, ni Muongozo kwa Wacha Mungu".
-
Uwezo wa kuthamini na kuheshimu vipengele viwili vya Imani na Utamaduni / Jinsi jamii ya Wairani nchini Tanzania inavyo balansi Imani na Utamaduni
Nyakati kama hizo hutoa somo muhimu katika kuishi pamoja Kitamaduni na kwa utangamano wa Kidini, na hili sio kwa Wairan tu, bali ni kwa Jamii ya Kimataifa.
-
Tunajifunza nini baada ya Mwezi Mtukufu wa Ramadhan?
Aliyekuwa akifanya Ibada za Usiku ndani ya Ramadhani na mwendo wake ukabadilika na tabia zake kuwa nzuri ndani ya Ramadhan, basi aendelee kuwa na tabia nzuri hivyo hivyo hata baada ya Ramadhan. Na hii ni sehemu ya wito na funzo zuri toka kwa Mtume wetu Muhammad (s.a.w.w).
-
Taasisi ya SHIDO - Bukoba, Kagera, Tanzania yafanya mafunzo ya ufundishaji kwa kutumia Syllabus kwa Walimu
Twende pamoja mkono kwa mkono katika Harakati za Tabligh za kueneza Mafunzo na Maarifa Safi ya Ahlul-Bayt(a.s).