Tanzania
-
Kamishna wa Polisi Jamii CP Alex Mkama Apokelewa Katika Makao Makuu ya JMAT-TAIFA
Kamishna wa Polisi Jamii CP Alex Mkama amepokelewa katika Makao Makuu ya JMAT-TAIFA na Mwenyekiti wake Sheikh Profesa Alhad Mussa Salum, ambapo wamejadili umuhimu wa ushirikiano katika kuimarisha amani, maridhiano na mshikamano wa kitaifa.
-
Baraza la Ulamaa BAKWATA Lamsimamisha Sheikh wa Mkoa wa Dar es Salaam, Lateua Kaimu Katika Nafasi Hiyo
Baraza la Ulamaa la BAKWATA, katika kikao chake cha dharura kilichoongozwa na Kaimu Mufti wa Tanzania, Sheikh Ali Khamis Ngeruko, limeazimia kumsimamisha Sheikh wa Mkoa wa Dar es Salaam na kumteua Sheikh Abbas Ramadhani kukaimu nafasi hiyo.
-
Kituo cha Imam Sajjad (as) Kigoma kinaendelea kuelimisha vijana na kueneza mafundisho ya Ahlul-Bayt (as)
Chini ya usimamizi wa Mkurugenzi Mkuu, Sheikh Hussein Moshi Abdallah, Kituo cha Imam Sajjad (as) kilichopo Kasuko, mkoani Kigoma, kinaendelea kutoa elimu ya dini kwa vijana na kuinua bendera ya Ahlul-Bayt (as) nchini Tanzania.
-
Sheikh Pro.Alhad Mussa Salum: Serikali Hupambana na Kuchukua Hatua dhidi ya Wanaotishia Maslahi Yake, Sio kwa Msingi wa Dini
Sheikh Prof.Alhad Mussa Salum: "Nchi ya Tanzania ni nchi ya Amani na sisi sote ni Watanzania, tunaishi kwa Upendo na Amani na watu wote. Uislamu ni Amani na unatufundisha kuishi kwa wema na watu wote."
-
ABNA Yampongeza Sheikh Prof. Alhad Mussa Salum kwa Uongozi Wake wa Kuimarisha Amani na Maridhiano Nchini Tanzania
Shirika la Habari la Kimataifa la Ahlul-Bayt News Agency (ABNA) limetoa pongezi kwa Sheikh Prof. Alhad Mussa Salum kwa mchango wake katika kukuza maridhiano ya kijamii, kuimarisha umoja wa kitaifa na kudumisha amani, akiwa kielelezo cha uongozi wenye hekima na busara, katika siku muhimu ya kuzaliwa kwake.
-
Hafla ya Ugawaji Zawadi kwa Washindi wa Mashindano ya Uandishi wa Muhtasari "Summary Writing" Yafanyika Kigamboni - Dar-es-salaam
Katika hafla iliyofanyika katika shule ya wasichana ya Kigamboni, washindi wa mashindano ya kuandika muhtasari kuhusu “Shahada ya Ayatollah Sayyid Ali Khamenei (ra)” walikabidhiwa zawadi maalum katika mwendelezo wa masomo ya Qur’an chini ya usimamizi wa Bi. Fatma Ma‘suma, ikiwa ni sehemu ya kuhamasisha elimu, ubunifu na ushindani wenye tija kwa wanafunzi.
-
Tanzania Yakamata Pakiti 20 za Skanka Zenye Kilogramu 20 Kwenye Bus la Kimataifa, Temeke - Dar-es-salaam
Mamlaka ya DCEA imekamatwa pakiti 20 za skanka zenye uzito wa kilo 20.03 zilizofichwa kwenye balo la mitumba ndani ya bus la Scania la King Masai Tours, lenye namba za usajili AAM 297 CA, likisafiri kati ya Nampula, Msumbiji na Dar es Salaam. Watuhumiwa waliokamatwa ni Amasha Iddi Mrisho (40) kutoka Dar es Salaam na Seleman Juma Ally (32) raia wa Msumbiji. Uchunguzi na kesi za kiutumishi zinaendelea.
-
Waziri Mkuu Dkt.Mwigulu Nchemba Afungua Skuli ya Sekondari Chukwani Zanzibar Katika Maadhimisho ya Miaka 62 ya Mapinduzi +Picha
Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mwigulu Nchemba, amefungua rasmi Skuli ya Sekondari Chukwani Zanzibar iliyogharimu shilingi bilioni 6.1, katika maadhimisho ya miaka 62 ya Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar, akisisitiza umuhimu wa uwekezaji katika elimu kwa maendeleo ya taifa.
-
Mufti Mkuu wa Tanzania:
"Qur’an Tukufu Inahimiza Amani Kama Msingi wa Maisha ya Mwanadamu | Tunajifunza Amani Kutoka Katika Kisa cha Nabii Ibrahim (as)
Katika kufafanua hoja yake, Mufti Mkuu wa Tanzania ametaja kisa cha wageni wa Nabii Ibrahim (as) kama kinavyosimuliwa ndani ya Qur’an Tukufu. Amesema kuwa wageni hao walipoingia nyumbani kwa Nabii Ibrahim (as), walimpa maamkizi ya amani, naye akajibu kwa maamkizi yale yale ya amani.
-
Balozi Matinyi Auvunja Msimamo wa Kibeberu: Tanzania Si Taifa la Huruma, Bali Nguvu Inayoinuka Kiuchumi
Katika ujumbe wake mzito kwa jumuiya ya kimataifa, Balozi Matinyi alisisitiza kuwa Tanzania ya sasa inatafuta wafanyabiashara na wawekezaji, si wafadhili. Taifa linaendelea kutekeleza miradi mikubwa ya kimkakati ikiwemo Reli ya Kisasa (SGR), pamoja na mradi wa gesi asilia unaokadiriwa kugharimu dola bilioni 42, miradi inayolenga kuimarisha uchumi wa taifa na nafasi yake katika uchumi wa kikanda na kimataifa.
-
Mwenyekiti wa JMAT–TAIFA: Tukipendana na Kusaidiana Tutajenga Amani ya Taifa Letu
Akizungumza kuhusu msingi wa amani, Mwenyekiti wa Jumuiya ya Maridhiano na Amani Tanzania alibainisha kuwa amani ya kweli huanzia katika mahusiano mema yanayojengwa kwa kujali, kuthaminiana na kusaidiana. Alieleza kuwa kitendo cha kusaidiana huondoa chuki na uhasama, kwani mtu anaposaidiwa huhisi kukubalika na kuheshimiwa, hali inayojenga imani na kuimarisha mshikamano wa kijamii.
-
Tanga | Sheikh Mkuu wa T.I.C Sheikh H. Jalala Mwakindenge Aongoza Hafla ya Ndoa za Vijana 100 Katika Maadhimisho ya Mazazi ya Bibi Fatima Zahra (a.s)
Hafla hii imeendelea kuwa ishara ya umoja, upendo na kuenzi Sunna ya ndoa katika Uislamu, sambamba na kuadhimisha tukio tukufu la mazazi ya Bibi Fatima Zahra (s.a).
-
Kauli ya Mwenyekiti wa Jumuiya ya Maridhiano na Amani Tanzania - Sheikh Dkt.Alhad Mussa Salum katika Kumbukizi ya Miaka 64 ya Uhuru wa Tanganyika
Tanganyika ilipata Uhuru kwa njia ya Amani; na sisi leo hii tunalo jukumu la kuuimarisha na kuurithisha kwa vizazi vijavyo. Kwa niaba ya Jumuiya ya Maridhiano na Amani Tanzania, Nawatakia Kumbukumbu Njema ya Miaka 64 ya Uhuru wa Tanganyika. Hongera Tanganyika, Hongera Tanzania! Amani na Maridhiano Daima.
-
Rais Samia na Marekani Wathibitisha Ushirikiano wa Kimkakati kwenye Miradi Mikubwa ya Uwekezaji
Kwa upande wake, Balozi Lentz alieleza kuwa ushirikiano wa Tanzania na Marekani umejengwa katika misingi ya ustawi wa pamoja, si utegemezi wa misaada, na kupongeza juhudi za Tanzania chini ya falsafa ya 4R na Dira ya Maendeleo ya 2050. Takribani makampuni 400 ya Marekani yanafanya kazi nchini, jambo linaloonesha kuimarika kwa mazingira ya uwekezaji.
-
Rais Mstaafu Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete Aendelea Kuitangaza Tanzania Katika Ajenda ya Elimu Duniani Kupitia Global Partnership for Education
Ushiriki wa Rais Mstaafu Dkt. Jakaya Kikwete katika majukwaa haya ya kimataifa unaonesha kwa vitendo dhamira yake endelevu ya kuitetea elimu kama nguzo kuu ya maendeleo ya binadamu, sambamba na kuendeleza diplomasia ya elimu kwa manufaa ya mataifa duniani, hususan Afrika.
-
Mufti wa Tanzania Atoa Wito wa Kulinda Amani na Kuepuka Uchochezi wa Kidini na Maandamano Yanayopangwa Kufanyika 9 Disemba
"Tuepuke upepo mbaya unaosambazwa kwa chuki za kidini. Sisi Waislamu hatukatazwi kuishi kwa wema na wasiokuwa Waislamu. Maisha ya watu lazima yalindwe,” alisema Mufti.
-
Ustadhi Rajai Ayoub na Wasomi wa Qur'an kutoka Tanzania Wawasili Salama Bangladesh kwa Ajili ya Mahfali Makubwa ya Kimataifa ya Qur'an +Picha
Mahfali hayo ya kimataifa yanakusudiwa kuwa jukwaa muhimu la kiroho na kielimu, ambapo wasomaji bingwa na mahiri wa Qur'an Tukufu kutoka Tanzania watapata fursa ya kuonesha vipaji vyao katika kusoma Aya Tukufu za Mwenyezi Mungu (SWT), kwa mapito na mitindo mbalimbali ya usomaji wa Qur'an (Qira’at).
-
Waziri Mkuu wa Tanzania Dkt. Mwigulu Atoa Maagizo Mazito: Wajawazito Kuhudumiwa Kwa Haraka na Dawa Kupatikana Hospitalini
Waziri Mkuu amewahakikishia wananchi kuwa Serikali imewekeza fedha nyingi kupitia Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa ajili ya: a) Vifaa tiba, b) Dawa, c) Na maboresho ya miundombinu ya afya.
-
Onyo la jarida la The National Interest kuhusu kuibuka kwa “Hezbollah Mpya” Katika Eneo
Jarida la Marekani “The National Interest” katika makala yake ya uchambuzi limeonesha shaka kuhusu mafanikio ya mpango wa Donald Trump wa kuleta uthabiti wa kudumu katika Ukanda wa Gaza, na limeonya kuwa mpango huo unaweza kuchangia kuibuka kwa taasisi au kundi jipya linalofanana na Hezbollah katika eneo hilo.
-
Mazoezi ni Afya: Jamiat Al-Mustafa (s) Yaendeleza Michezo kwa Ajili ya Kuimarisha Afya ya Mwili na Akili
Kwa hakika, michezo na mazoezi haya yamekuwa kielelezo cha namna Uislamu unavyopenda mwili wenye nguvu, akili timamu, na mshikamano wa kijamii, ili kumsaidia Muislamu kuwa na uwezo wa kutekeleza majukumu yake ya kidini, kijamii na kiulimwengu.
-
Uwajibikaji na Utawala Bora | Bi.Leila Bhanj Aiwakilisha JMAT-TAIFA Katika Kikao cha Mihimili ya Sheria Dodoma - Tanzania
Ushiriki wa Bi.Leila katika kikao hicho umetajwa kuwa ni uwakilishi mkubwa wa JMAT-TAIFA, ambapo mijadala ilihusu masuala ya utawala bora na uwajibikaji katika mfumo wa sheria.
-
Mkutano wa Mwakilishi wa Kanda wa Al-Mustafa na Wanafunzi kutoka Tanzania, Burundi na Malawi katika Kituo cha Bayan
Katika mkutano huo, Hujjatul-Islam Taqavi alieleza kufurahishwa kwake na kufanyika kwa kikao hicho, na alisisitiza umuhimu wa kunufaika kikamilifu na uwezo mkubwa wa kituo hiki cha elimu. Aliwahimiza wanafunzi kutumia ipasavyo fursa zilizopo katika kituo cha Bayan ili kupata maarifa na stadi muhimu kwa ajili ya maisha na kazi zao za baadaye.
-
Hafla ya 4 ya Mashindano ya Kuhifadhi Qur'an Yaendelea Mubashara Kibaha – Pwani | Sheikh Dr. Alhad Mussa Salum Mgeni Rasmi Katika Hafla Hii
Kauli mbiu ya mashindano haya ni: “Hakika Qur’an ni Muongozo,” ikisisitiza nafasi ya Qur’an katika kuleta maadili, amani, na maendeleo ya kiroho katika jamii.
-
Jamiatul Mustafa (s) Yaandaa Maadhimisho ya Maulid Al-Nabi, Dar-es-Salaam - Tanzania | Fursa ya Kusherehekea Kuzaliwa kwa Mtume Wetu Muhammad(s.a.w.w)
Maulid hii itafanyika Tarehe 07-09-2025, Pweza Beach Road - Kigamboni, Dar-es-salaam.
-
Jamiat Al-Mustafa(s) - Dar-es-Salam | Kikao cha Kielimu: Nafasi ya Imam Hassan Askari(as) katika Kuhifadhi Madhehebu ya Shia Kuendeleza Njia ya Uimamu
Katika hotuba yake, aligusia mazingira ya kisiasa ya wakati huo, mbinu za kitaqiyya (kuficha imani kwa sababu za kiusalama), kulea wafuasi maalum, na juhudi za Imam katika kuimarisha misingi ya aqida ya Kishia.
-
Jamiat Al-Mustafa (s) - Dar-es-salaam | Mtihani wa Kila Wiki: Hatua ya Kuimarisha Uelewa na Maandalizi Bora ya Kielimu na Ufaulu wa Wanafunzi
Kupitia mitihani hii ya wiki, walimu hupata nafasi ya kufuatilia maendeleo ya kielimu kwa kila mwanafunzi, kutambua changamoto zinazojitokeza katika masomo, na kuweka mikakati ya kuboresha ufaulu.
-
Askofu Dkt.Gabriel O.Maasa Aiwakilisha Vyema JMAT-TAIFA -Katika Ushirikiano wa Kijamii na Taasisi za Umma- Katika Kikao Kazi cha Kitaifa Jijini Arusha
Askofu Dkt. Maasa ameendelea kuacha alama ya kumbukumbu isiyofutika katika maisha ya jamii. Juhudi zake ni kielelezo cha dhati cha Falsafa ya JMAT-TAIFA - kuendeleza Maridhiano, Amani, Mshikamano na Ustawi wa Wananchi wote.
-
JMAT TAIFA:
Mdahalo wa Viongozi wa Dini na Siasa: Wito wa Kudumisha Amani na Demokrasia Safi kuelekea Uchaguzi Mkuu
Sheikh Dkt. Al-Hadi Mussa Salum: "Amani na Utulivu nchini ni msingi wa maendeleo ya Taifa na Ustawi wa kila Mtanzania".
-
Miaka 10 ya Uongozi wa Mufti wa Tanzania Dr.Abubakar Zubair: Historia ya Mafanikio na Maboresho Makubwa
Miradi mikubwa yenye thamani ya mabilioni imetekelezwa katika mikoa mbalimbali, huku maboresho ya kiutawala na ya kimuundo yakifanikishwa, ikiwemo kuanzishwa kwa Ofisi ya Mufti, JUWAKITA na JUVIKIBA, pamoja na mabadiliko ya Katiba ya BAKWATA ili kuendana na mahitaji ya sasa.
-
Ridhwan Kikwete: Miongozo ya Kima cha Chini Cha Mshahara Kusainiwa Hivi Karibuni
Serikali imedhamiria kuhakikisha wafanyakazi wa sekta binafsi wananufaika na viwango vipya vya mishahara, hatua inayotarajiwa kuboresha hali ya maisha na kulinda heshima ya kazi nchini.