Tanzania
-
Mazoezi ni Afya: Jamiat Al-Mustafa (s) Yaendeleza Michezo kwa Ajili ya Kuimarisha Afya ya Mwili na Akili
Kwa hakika, michezo na mazoezi haya yamekuwa kielelezo cha namna Uislamu unavyopenda mwili wenye nguvu, akili timamu, na mshikamano wa kijamii, ili kumsaidia Muislamu kuwa na uwezo wa kutekeleza majukumu yake ya kidini, kijamii na kiulimwengu.
-
Uwajibikaji na Utawala Bora | Bi.Leila Bhanj Aiwakilisha JMAT-TAIFA Katika Kikao cha Mihimili ya Sheria Dodoma - Tanzania
Ushiriki wa Bi.Leila katika kikao hicho umetajwa kuwa ni uwakilishi mkubwa wa JMAT-TAIFA, ambapo mijadala ilihusu masuala ya utawala bora na uwajibikaji katika mfumo wa sheria.
-
Mkutano wa Mwakilishi wa Kanda wa Al-Mustafa na Wanafunzi kutoka Tanzania, Burundi na Malawi katika Kituo cha Bayan
Katika mkutano huo, Hujjatul-Islam Taqavi alieleza kufurahishwa kwake na kufanyika kwa kikao hicho, na alisisitiza umuhimu wa kunufaika kikamilifu na uwezo mkubwa wa kituo hiki cha elimu. Aliwahimiza wanafunzi kutumia ipasavyo fursa zilizopo katika kituo cha Bayan ili kupata maarifa na stadi muhimu kwa ajili ya maisha na kazi zao za baadaye.
-
Hafla ya 4 ya Mashindano ya Kuhifadhi Qur'an Yaendelea Mubashara Kibaha – Pwani | Sheikh Dr. Alhad Mussa Salum Mgeni Rasmi Katika Hafla Hii
Kauli mbiu ya mashindano haya ni: “Hakika Qur’an ni Muongozo,” ikisisitiza nafasi ya Qur’an katika kuleta maadili, amani, na maendeleo ya kiroho katika jamii.
-
Jamiatul Mustafa (s) Yaandaa Maadhimisho ya Maulid Al-Nabi, Dar-es-Salaam - Tanzania | Fursa ya Kusherehekea Kuzaliwa kwa Mtume Wetu Muhammad(s.a.w.w)
Maulid hii itafanyika Tarehe 07-09-2025, Pweza Beach Road - Kigamboni, Dar-es-salaam.
-
Jamiat Al-Mustafa(s) - Dar-es-Salam | Kikao cha Kielimu: Nafasi ya Imam Hassan Askari(as) katika Kuhifadhi Madhehebu ya Shia Kuendeleza Njia ya Uimamu
Katika hotuba yake, aligusia mazingira ya kisiasa ya wakati huo, mbinu za kitaqiyya (kuficha imani kwa sababu za kiusalama), kulea wafuasi maalum, na juhudi za Imam katika kuimarisha misingi ya aqida ya Kishia.
-
Jamiat Al-Mustafa (s) - Dar-es-salaam | Mtihani wa Kila Wiki: Hatua ya Kuimarisha Uelewa na Maandalizi Bora ya Kielimu na Ufaulu wa Wanafunzi
Kupitia mitihani hii ya wiki, walimu hupata nafasi ya kufuatilia maendeleo ya kielimu kwa kila mwanafunzi, kutambua changamoto zinazojitokeza katika masomo, na kuweka mikakati ya kuboresha ufaulu.
-
Askofu Dkt.Gabriel O.Maasa Aiwakilisha Vyema JMAT-TAIFA -Katika Ushirikiano wa Kijamii na Taasisi za Umma- Katika Kikao Kazi cha Kitaifa Jijini Arusha
Askofu Dkt. Maasa ameendelea kuacha alama ya kumbukumbu isiyofutika katika maisha ya jamii. Juhudi zake ni kielelezo cha dhati cha Falsafa ya JMAT-TAIFA - kuendeleza Maridhiano, Amani, Mshikamano na Ustawi wa Wananchi wote.
-
JMAT TAIFA:
Mdahalo wa Viongozi wa Dini na Siasa: Wito wa Kudumisha Amani na Demokrasia Safi kuelekea Uchaguzi Mkuu
Sheikh Dkt. Al-Hadi Mussa Salum: "Amani na Utulivu nchini ni msingi wa maendeleo ya Taifa na Ustawi wa kila Mtanzania".
-
Miaka 10 ya Uongozi wa Mufti wa Tanzania Dr.Abubakar Zubair: Historia ya Mafanikio na Maboresho Makubwa
Miradi mikubwa yenye thamani ya mabilioni imetekelezwa katika mikoa mbalimbali, huku maboresho ya kiutawala na ya kimuundo yakifanikishwa, ikiwemo kuanzishwa kwa Ofisi ya Mufti, JUWAKITA na JUVIKIBA, pamoja na mabadiliko ya Katiba ya BAKWATA ili kuendana na mahitaji ya sasa.
-
Ridhwan Kikwete: Miongozo ya Kima cha Chini Cha Mshahara Kusainiwa Hivi Karibuni
Serikali imedhamiria kuhakikisha wafanyakazi wa sekta binafsi wananufaika na viwango vipya vya mishahara, hatua inayotarajiwa kuboresha hali ya maisha na kulinda heshima ya kazi nchini.
-
-
Arubaini ya Imam Hussein (a.s):
Taasisi za Kijamii Nchini Tanzania: BEF na Nyota Foundation Zandaa Tukio la Uchangiaji Damu kwa Upendo na Huruma ya Kibinadamu
Tukio hili limeonesha mshikamano wa kijamii na mshikikano wa kiimani kwa kuenzi mfano wa kujitolea na ubinadamu wa Imam Hussein (a.s), na limekuwa ni ishara muhimu ya mshikamano wa Waislamu na Watanzania wote kwa ujumla katika kusaidia wenzao wenye uhitaji wa Damu Mahospitalini.
-
Chuo Kikuu cha al-Mustafa (s) Dar es Salaam - Tanzania Chaandaa Kongamano la Kielimu Kuhusu: "Dakika za Mwisho za Maisha ya Mtume Muhammad (s.a.w.w)"
Mtoa Mada: Sheikh Taqi Zakariya. Tarehe: Jumamosi, 16-08-2025. Muda: Kuanzia Saa 4:00 Ask Asubuhi hadi 6:00 Mchana. Eneo: Muswalla wa Chuo Kikuu cha Al-Mustafa (s) - Dar-es-salaam. Mwaliko huu ni kwa Wote.
-
Mufti wa Tanzania, Sheikh Dkt. Abubakar Zuber, Arejea Nchini Baada ya Kikao cha Kimataifa Nchini Misri
"Tumejadili namna bora ya kumaliza mzozo huo kwa njia ya amani. Na tunawaombea ndugu zetu wa Gaza ili Mwenyezi Mungu awape amani na kumaliza mgogoro huu wa muda mrefu,"
-
Taifa Stars Yaandika Historia, Yaingia Robo Fainali CHAN 2024 Baada ya Kuifunga Madagascar 2–1
Hongereni sana wachezaji, benchi la ufundi, na Watanzania wote kwa mafanikio haya makubwa.
-
Zaidi ya Watu 10,000 Wanufaika na Huduma za Afya za Khoja Shia Ithnasheri Jamaat – Mwenyekiti Dewji Afichua Mafanikio
Khoja Shia Ithnasheri Jamaat Nchini Tanzania imeendeleza Utaratibu wake wa kutoa Huduma za Afya kwa Maelfu. Dewji ametoa Takwimu Kamili juu ya hilo.
-
Zanzibar | Rais Mwinyi Atoa Wito wa Kuendelea Kuliombea Taifa Amani
Alisema: “Kila ninapopata nafasi ya kuzungumza na Wananchi, nitaendelea kusisitiza juu ya umuhimu wa amani na utulivu kwa sababu ndiyo njia pekee ya kuhakikisha tunapata maendeleo.”
-
Mwanamke na Nusu - Mratibu JMAT-TAIFA na Balozi wa Amani Duniani wa Shirika la Amani la (IWPG), Bi.Fatima F.Kikkides Katika Mkutano wa JMAT - Dodoma
Mkutano huu ni katika muktadha wa kudumisha Amani na Utulivu wa Taifa letu la Tanzania na kulitakia Kheri na Baraka Taifa hili kwa ajili ya Maendeleo ya Jamii na Ustawi wa Wananchi.
-
Maneno Muhimu na ya Hekima ya Sheikh Dr.Alhad Mussa Salum - kuhusu: Wanaoitwa Mitume na Manabii Tanzania, Udugu wa Watanzania, na Amani ya Tanzania
Jumuiya ya Maridhiano na Amani Tanzania tutasimama na Serikali Daima katika kulinda na kudumisha Amani na Maridhiano ya nchi yetu kwa ajili ya Ustawi wa nchi yetu.
-
Madrasat Hazrat Zainab (SA) - Kigamboni | Imam Hussein (A.S) ni Mlango wa Rehema Pana ya Mwenyezi Mungu
Imam Hussein (A.S) alikuwa ni mfano wa rehema ya Mwenyezi Mungu duniani. Mapambano na msimamo wake ni darasa kwa Umma. Kwa hiyo: 1_Waislamu waitikie wito wa Imam Hussein (A.S). 2_Waonyeshe huruma kwa wengine. 3_Watubu na wafanye toba kwa kupitia Ahlulbayt ili kupata msamaha wa Mwenyezi Mungu.
-
Wito wa Kwanza | Tamasha la Kitaifa la Ushairi wa Ghadir Kufanyika Katika Chuo Cha Jamiat Al-Mustafa Foundation - Mbezi Beach - Dar-es- Salaam
Washairi wa Kiislamu kutoka sehemu mbalimbali watahudhuria kwa ajili ya kusoma mashairi yanayogusa nyoyo kuhusu: Tukio la Ghadir, Mapenzi kwa Ahlul-Bayt(as), na mafundisho ya Kiislamu.
-
Dkt. Al-Had Mussa Salum - Mwenyekiti wa Jumuiya ya Maridhiano na Amani Tanzania (JMAT-TAIFA) Azungumzia Mambo Matatu Muhimu kwa Mustakbali wa Taifa
JMAT imepanga kuendesha matembezi ya amani kutoka Dar es Salaam hadi Dodoma, Makao Makuu ya Tanzania. Lengo ni kuleta Watanzania pamoja na kuhamasisha Amani na Maridhiano hasa katika kipindi hiki cha kuelekea katika Uchaguzi Mkuu.
-
Wanafunzi wa Madrasatul Hizbullah Al-‘Ilmiyyah Wafanya Mtihani wa Mwisho wa Mwezi - Kazole, Vikindu
Madrasatul Hizbullah Al-‘Ilmiyyah inatoa wito kwa jamii kuendelea kuiunga mkono taasisi hiyo ili iweze kuendelea kutoa elimu bora na kukuza kizazi chenye maarifa, hikma na hofu ya Mwenyezi Mungu.
-
Dar es Salaam, Tanzania - Mei 2025:
BAKWATA Yatangaza Rasmi Tarehe ya Sikukuu ya Eid El-Adh’ha: Jumamosi, Juni 7, 2025
Taarifa hiyo imetolewa na Katibu Mkuu wa BAKWATA, Alhaj Nuhu Jabiri Mruma, ambapo imeelezwa kuwa sherehe za kitaifa za Eid El-Adh’ha mwaka huu zitafanyika jijini Dar es Salaam, katika Msikiti wa Mfalme Mohamed VI uliopo Makao Makuu ya BAKWATA – Kinondoni.
-
Mada ya Ijumaa Masjidul Ghadir Kigogo Post: "Hijjah na Athari Zake Katika Malezi (ya Watoto na Jamii)"
Tarehe: Ijumaa, 30 Mei 2025. Mahali: Masjidul Ghadir, Kigogo Post – Dar-es-Salaam, Tanzania. Khatibu wa Swala ya Ijumaa: Maulana Sheikh Hemed Jalala. Mada ya Khutba ya Ijumaa: "Hijjah na Athari Zake Katika Malezi". Khutba hii iliangazia Nafasi ya Hijjah kama Shule ya Malezi ya kina, ikihimiza wazazi na jamii kwa ujumla kutumia mafundisho ya Hijjah kuwalea watoto katika misingi ya Utii, Ucha Mungu, Uvumilivu, Unyenyekevu na Umoja. Pia, iliweka msisitizo wa umuhimu wa Mwezi wa Dhilhijja katika historia ya Uislamu na fadhila za ibada ndani yake.
-
Mahojiano Maalum ya Firdaus TV na Sheikh Dkt. Alhad Mussa Salum - Mwenyekiti JMAT-TAIFA Yaliyofanyika Katika Uwanja wa Michezo wa Mkwakwani, Tanga
Ni katika Kongamano la Qur'an Tukufu lililofanyiks Jijini Tanga. Tukio hilo liliimarisha misingi ya Amani, Mshikamano, Maridhiano, na Ushirikiano kati ya Watanzania, likiwa ni Jukwaa la kuendeleza Mafundisho ya Qur’an Tukufu yanayohimiza Utulivu na Maelewano ya Kijamii.
-
JMAT Yatoa Wito kwa Viongozi wa Dini Nchini Kenya wa Kushirikiana Katika Kuwaongoza Wananchi wao ili Kuheshimiana na Kutunza Mahusiano ya Amani
Sheikh Dkt. Alhad Mussa Salum: "Wakenya ni ndugu wa Watanzania, na mbali na uhusiano wa kijamii, ni ndugu wa damu. Tunatambua kuwa mizozo hii inahusu zaidi vijana wa Kenya, lakini ni muhimu kuwakumbusha kuwa heshima ni nguzo muhimu katika mahusiano ya mataifa. Tunaamini Kenya ina Viongozi wa Dini na Serikali wanaoweza kusaidia katika hili."
-
Ziara ya Maulana Sheikh Jalala Hospitali ya Mloganzila kumtembelea Sheikh Mbelango Allah aimarishe Afya yake
Tunamuomba Mwenyezi Mungu Mtukufu ampe afueni ya haraka na amuwekee wepesi katika kila jambo. Uwepo wake ni hazina kwa Uislamu na Waislamu.
-
Ripoti ya Mahudhurio ya Wasomaji wa Qur'an wa Programu ya "Mahfali" nchini Tanzania
Katika hafla hii Tukufu ya Qur’an, wasomaji wa Kiirani walioshiriki ni pamoja na Ustadh Shakernejad, Ustadh Abolghasemi, Qari kijana Mohammad Hossein Azimi, na Muhanna Ghanbari – ambaye ni mhifadhi wa Qur’an nzima.