27 Agosti 2025 - 12:14
Askofu Dkt.Gabriel O.Maasa Aiwakilisha Vyema JMAT-TAIFA -Katika Ushirikiano wa Kijamii na Taasisi za Umma- Katika Kikao Kazi cha Kitaifa Jijini Arusha

Askofu Dkt. Maasa ameendelea kuacha alama ya kumbukumbu isiyofutika katika maisha ya jamii. Juhudi zake ni kielelezo cha dhati cha Falsafa ya JMAT-TAIFA - kuendeleza Maridhiano, Amani, Mshikamano na Ustawi wa Wananchi wote.

Shirika la Habari la Kimataifa la Ahlul-Bayt (as) -ABNA- Arusha, Tanzania – Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Maridhiano na Amani Tanzania (JMAT-TAIFA), Askofu Dkt. Gabriel Ole Maasa, ameshiriki katika Kikao Kazi cha Wenyeviti wa Bodi na Watendaji Wakuu wa Taasisi za Umma kilichofanyika katika Ukumbi wa Kimataifa wa Mikutano wa AICC jijini Arusha.

Askofu Dkt.Gabriel O.Maasa Aiwakilisha Vyema JMAT-TAIFA -Katika Ushirikiano wa Kijamii na Taasisi za Umma- Katika Kikao Kazi cha Kitaifa Jijini Arusha

Ushiriki wa Katibu Mkuu huyu katika kikao hicho umeonesha dhamira ya dhati ya JMAT-TAIFA katika kuimarisha mashirikiano na taasisi za kitaifa na kimataifa, hususan katika kutafuta suluhu za changamoto mbalimbali za kijamii.

Sehemu ya Sifa za Uongozi Wake na Majukumu Yake

Miongoni mwa sifa zinazomtambulisha Askofu Dkt. Maasa - hususan Jijini Arusha - ni jitihada zake za kuhakikisha kuwa mahitaji ya msingi ya binadamu kama maji safi, huduma za afya na dawa yanapatikana kwa urahisi kwa wananchi wa maeneo yenye uhitaji.

Askofu Dkt.Gabriel O.Maasa Aiwakilisha Vyema JMAT-TAIFA -Katika Ushirikiano wa Kijamii na Taasisi za Umma- Katika Kikao Kazi cha Kitaifa Jijini Arusha

Ushirikiano na Mashirika ya Umma na Kimataifa

Kupitia JMAT-TAIFA, Katibu Mkuu ameweza kuikutanisha jumuiya na mashirika kadhaa ya kitaifa na kimataifa, ikiwemo “ALL FOR HIS GLORY” pamoja na mengineyo. Mashirikiano haya yamewezesha utekelezaji wa miradi muhimu ya kijamii kama vile:

  • Uchimbaji wa visima katika vijiji vyenye uhitaji.
  • Ujenzi wa zahanati na vituo vya afya.
  • Uhakika wa upatikanaji wa dawa katika maeneo ya vijijini.

Askofu Dkt.Gabriel O.Maasa Aiwakilisha Vyema JMAT-TAIFA -Katika Ushirikiano wa Kijamii na Taasisi za Umma- Katika Kikao Kazi cha Kitaifa Jijini Arusha

Wito na Baraka kwa Taifa

Kwa kujitoa kwake bila ubinafsi, Askofu Dkt. Maasa ameendelea kuacha alama ya kumbukumbu isiyofutika katika maisha ya jamii. Juhudi hizi ni kielelezo cha dhati cha falsafa ya JMAT-TAIFA – kuendeleza amani, mshikamano na ustawi wa wananchi wote.

Mungu Ibariki Tanzania – Tanzania Yetu, Amani Kwanza.

Tags

Your Comment

You are replying to: .
captcha