Kigamboni
-
Kuzingatia Umuhimu wa Swala ya Ijumaa na Tabia Njema katika Hawzat ya Wasichana ya Hazrat Zainab (s.a) - Tanzania
Hadithi: “إِنَّمَا بُعِثْتُ لِأُتَمِّمَ مَکَارِمَ الأَخْلَاقِ.” “Mimi nimetumwa ili nikamilishe tabia njema.” Aya Tukufu: «قَدْ أَفْلَحَ مَن زَكَّاهَا وَقَدْ خَابَ مَن دَسَّاهَا» (Surat Ash-Shams, Aya 9–10). "Amefaulu yule aliyeitakasa nafsi yake, na ameharibikiwa yule aliyeichafua (aliyeifisidi)".
-
Mazoezi ni Afya: Jamiat Al-Mustafa (s) Yaendeleza Michezo kwa Ajili ya Kuimarisha Afya ya Mwili na Akili
Kwa hakika, michezo na mazoezi haya yamekuwa kielelezo cha namna Uislamu unavyopenda mwili wenye nguvu, akili timamu, na mshikamano wa kijamii, ili kumsaidia Muislamu kuwa na uwezo wa kutekeleza majukumu yake ya kidini, kijamii na kiulimwengu.
-
Jamiatul Mustafa (s) Yaandaa Maadhimisho ya Maulid Al-Nabi, Dar-es-Salaam - Tanzania | Fursa ya Kusherehekea Kuzaliwa kwa Mtume Wetu Muhammad(s.a.w.w)
Maulid hii itafanyika Tarehe 07-09-2025, Pweza Beach Road - Kigamboni, Dar-es-salaam.
-
Madrasa ya Wasichana ya Hazrat Zainab (sa) Kigamboni - Yaadhimisha Arubaini ya Imam Hussein (a.s) kwa Majlisi Maalum ya Maombolezo
Kikao hicho kilipambwa kwa kisomo cha Qur’an Tukufu na mashairi ya maombolezo (marsiya), ambapo walimu na wanafunzi walishiriki kwa unyenyekevu na hisia za heshima kwa mashahidi wa Karbala.
-
Kikao Maalum cha Uchambuzi wa Masomo ya Qur’an Tukufu Chafanyika Madrasa ya Wasichana ya Hazrat Zainab (sa) - Kigamboni, Dar-es-salaam
Katika kikao hicho, walimu mbalimbali walitoa maoni kuhusu mbinu bora za kufundishia na kuhimiza nidhamu ya kielimu, huku wanafunzi nao wakipewa nafasi ya kueleza changamoto wanazokutana nazo.
-
Arubaini ya Imam Hussein (a.s):
Taasisi za Kijamii Nchini Tanzania: BEF na Nyota Foundation Zandaa Tukio la Uchangiaji Damu kwa Upendo na Huruma ya Kibinadamu
Tukio hili limeonesha mshikamano wa kijamii na mshikikano wa kiimani kwa kuenzi mfano wa kujitolea na ubinadamu wa Imam Hussein (a.s), na limekuwa ni ishara muhimu ya mshikamano wa Waislamu na Watanzania wote kwa ujumla katika kusaidia wenzao wenye uhitaji wa Damu Mahospitalini.
-
Dua ya Nudba Yafanyika Leo hii Ijumaa Katika Hawza ya Mabanati ya Hazrat Zainab (sa), Kigamboni - Dar-es-Salam
Usomaji wa Dua wa namna hii kawaida huvutia ushiriki mkubwa wa Wanafunzi na Wapenzi wa Ibada na Dua, na kuleta hali ya utulivu wa kiibada katika mazingira ya Chuo hiki cha Kiislamu.
-
Madrasa Hazrat Zainab (sa) | Dini na Afya: Dkt. Beshteri Azungumzia Umuhimu wa Lishe Sahihi kwa Muislamu
Dkt. Beshteri alieleza kuhusu adabu za kula chakula kulingana na mafundisho ya Imam Ja’far Sadiq (a.s), akitaja riwaya mbalimbali zinazoelekeza namna bora ya kula kwa mujibu wa maadili ya Kiislamu.
-
Swala ya Ijumaa - Madrasa Hazrat Zainab (sa) - Kigamboni | Changamoto za Kijamii Zinazotokana na Kuachana na Mafundisho ya Dini
Sala ilisaliwa kwa nidhamu kubwa na utulivu wa hali ya kiroho, na iliacha athari kubwa kwa washiriki wote katika ibada hii.
-
Dua ya Nudba Yasomwa kwa Hisia Kuu na Mabinti wa Madrasa ya Hazrat Zainab (SA) Kigamboni – Wakiadhimisha Mapenzi kwa Imam wa Zama (a.t.f.s)
"Dua ya Nudba ni kilio cha roho inayotamani haki irejee. Ni kilio cha wale waliomsubiri Imam wao wa Zama kwa subira na msimamo."
-
Mabanati wa Madrasa ya Hazrat Zainab (sa) - Kigamboni, Dar-es-salaam, Wapatiwa Vyeti vya (ICDL) Baada ya Kukamilisha Kozi hiyo ya Mafunzo ya Kompyuta
Tunawapongeza waalimu waliowafundisha wasichana hawa wa Kiislamu kwa bidii na uaminifu, na pia Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Kimataifa ya Jamiatul Mustafa (s) - Tanzania, Hojjatul Wal Muslimin, Dr.Ali Taqavi aliyekuja na wazo hili muhimu na kulisimamia kwa hekima na juhudi kubwa.
-
Kisomo cha Dua ya Kumail katika Hawza ya Hazrat Zainab (sa) – Kigamboni, Dar-es-Salaam
Hawza ya Hazrat Zainab (sa) iliyoko Kigamboni, Dar-es-Salaam, ni chuo makhsusi kwa ajili ya kuwalea mabinti wa Kiislamu kielimu na kimaadili. Chuo hiki kipo chini ya usimamizi wa Jamiat Al-Mustafa (s) – Tanzania, na mbali na masomo ya kielimu yanayotolewa humo, wanafunzi pia hupatiwa malezi ya kiroho kwa kupitia mafundisho ya dua na ibada.
-
Mkutano wa Mrs.Taqavi, Mudira wa Hawzat ya Wasichana ya Hazrat Zahra (s.a) na Wanafunzi wa Hawzat hiyo
Mkutano ulimalizika kwa mipango ya kuimarisha ushirikiano kati ya Wanafunzi na Walimu.
-
Hawzat Hazrat Zainab (sa) Kigamboni - Dar-es-salaam | Wanawake katika Kuadhimisha Shahadat ya Imam Sadiq (a.s) + Picha
Wanawake katika jamii za Kiislamu wanachukua jukumu muhimu katika kuadhimisha kifo cha Kishahidi cha Imam Sadiq (a.s), ambapo si tu wanahudhuria kimwili katika vikao kama hivi vya Maombolezo, bali pia wanashiriki kikamilifu kwa njia ya vitendo katika kueneza mafundisho ya Imam Sadiq (as) katika nyanja mbalimbali.