Shirika la Habari la Kimataifa la Ahlul-Bayt (as) - ABNA - Dr. Ali Taqavi, Mwakilishi wa Jamiat Al-Mustafa (s) - Dare-salam, Tanzania, alifanya ziara muhimu Zanzibar - Tanzania na kutembelea Chuo cha Qur'an Tukufu ndani ya Zanzibar, klilichopo chini ya Jamiat Al-Mustafa (s) - Dar- es Salam - Tanzania. Katika ziara hii alizungumza na wanafunzi wa chuo hiki na kuwahamasisha kuzingatia elimu na maarifa ya Qur'an Tukufu, na kuwaasa katika kuzidisha juhudi zao kwenye suala muhimu la kusoma na kuhifadhi Qur'an Tukufu, na kuiweka Qur'an Tukufu mbele ya Maisha yao ya kila siku.
Hojjat Al-Islam wal Muslimin, Dr. Ali Taqavi akizungumza na wanafunzi wa chuo cha Qur'an Tukufu, Zanzibar - Tanzania.
Your Comment