Qur ani tukufu
-
Hujjatul-Islam wal-Muslimin Woldan:
Mwezi Mtukufu wa Ramadhani ni fursa ya Kimungu ya kurekebisha mtindo wa maisha
Mkurugenzi Mkuu wa Tablighi za Kiislamu mkoa wa Fars ameeleza kuwa Mwezi Mtukufu wa Ramadhani ni fursa ya Kimungu ya kujenga upya roho na kurekebisha mtindo wa maisha. Amesema kuwa Mwenyezi Mungu ameumba mfumo wa uwepo wa mwanadamu kwa namna ambayo katika kipindi fulani cha mwaka huhitaji mabadiliko katika namna ya kuishi na kula; mabadiliko ambayo hupelekea kuinuka kwa roho na kuimarika kwa irada. Ramadhani ni uwanja wa mazoezi ya ibada na kujijenga nafsi, na kwa tafsiri nyingine ni hundi nyeupe yenye saini ya Kimungu kwa ajili ya msamaha na kuangazwa kwa nyoyo.
-
Kikao cha Qur’an katika Husseiniyyah ya Imam Khomeini kikihudhuriwa na Kiongozi Mkuu wa Iran Siku ya Kwanza ya Ramadhan
Kikao cha Qur’an katika Husseiniyyah ya Imam Khomeini (M.A) Siku ya kwanza ya Ramadhan kilisisitiza umuhimu wa Qur’an katika maisha ya kiroho ya Waislamu na thawabu za usomaji wake.
-
Ayatllah Hosseini Gorgani amesisitiza kuwa:
Fiqh ya Usimamizi Ina Historia Ndefu | Utendaji wa vitendo unaoendana na Qur’an ni muhimu katika utawala na usimamizi wa umma
Mwalimu wa Dars-e-Kharij katika Hawza Ilmiyya ya Qom amesema kuwa kuunda serikali na utawala na manabii wa Mungu si jambo jipya, na Qur’an kwa uwazi inataja mtindo wa utawala wa baadhi ya manabii.
-
Uvumilivu wa Kishujaa wa Imam Jawad (a.s); Mwingiliano na Mke Asiyeelewana
Migogoro ni fundo linaloweza kukalia maisha ya mtu binafsi na ya kijamii; lakini ufunguo wa kulitatua si nguvu, bali ni haki (uadilifu). Mwenendo wa Imam Jawad (a.s) unaonesha kuwa hata katika migongano mikali zaidi, inawezekana kubaki binadamu, kuhifadhi heshima na kufungua njia ya uadilifu.
-
Usijivune kwa Maneno Maneno na Kujiona Mwenye Fadhila | Ibada na Jema lolote bila Unyenyekevu, ni Njia ya kupoteza kila Kheri
Baadhi ya Mabedui walikuwa wakimfanyia Mtume (s.a.w.a) madai ya fadhila kwa kusilimu kwao, kama Qur’ani inavyosema: “Wanakuonea fadhila kwa kusilimu kwao.” Basi Qur’ani ikawafunza adabu kwa kusema: “Sema: Msinionee fadhila kwa Uislamu wenu; bali Allah ndiye anayekuoneeni fadhila kwa kuwaongoza kwenye imani, ikiwa nyinyi ni wakweli.” (Al-Hujurāt: 17).
-
Mamilioni ya Wayemeni Wafurika Barabarani Kuitetea Qur’ani Tukufu Baada ya Kudharauliwa Nchini Marekani
Qur’ani Tukufu ni Kitabu Kitakatifu kisichoguswa, na kitendo chochote cha kuidharau kitapokelewa kwa upinzani na laana kali kutoka kwa Waislamu duniani kote.
-
Rais katika ujumbe wake kwa sherehe ya kumaliza mashindano ya 17 ya Qur’ani ya Medhametan:
''Jukumu la vituo vya misikiti katika kulea na kuandaa kizazi kipya cha vijana watiifu na wa Qur’ani ni la kuthaminiwa sana.”
“Dkt. Pezeshkian katika ujumbe wake kwa sherehe ya kumaliza mashindano ya 17 ya Qur’ani ‘Medhametan (ni jina la tukio / shindano)’, huku akitoa shukrani kwa waandaji wa mashindano haya, alisisitiza: Jukumu la vituo vya misikiti katika kulea na kuandaa kizazi kipya cha vijana watiifu katika nyanja hii ya ujenzi wa kiroho ni la kuthaminiwa sana.”
-
Uzinduzi wa Mfumo wa Kielelezo cha Kujadiliana na Tafsiri za Qur’ani / Ayatollah Makarem:Teknolojia Mpya Iwe Kwenye Huduma ya Qur’ani na AhlulBayt(as)
Ayatollah Makarem Shirazi, mmoja wa maraja’ wa kiislamu, akisisitiza umuhimu wa kueneza habari za mafanikio ya kisayansi, alisema: “Moja ya mahitaji muhimu ya leo ni kuwafahamisha watu. Kuna shughuli nyingi zenye thamani zinafanyika, lakini taarifa zake ni chache. Vyombo vya habari, redio, televisheni na mashirika ya habari vinapaswa kusambaza maendeleo haya ili wananchi waone kiwango cha maendeleo ya teknolojia mpya katika sekta ya elimu ya dini.”
-
Shia wa Ahlul-Bayt (as) Kamwe Hawatukani Masahaba wala Mtu yeyote hata kama ni dhalimu, bali Hufuata Manhaj wa Qur’an Tukufu katika Kukosoa kwa Hekima
Shia na Mtazamo wao kwa Masahaba Shia hawawatusi Masahaba wa Mtume (s.a.w.w), bali hukosoa matendo au maneno ya baadhi yao pale yanapopingana na mafundisho ya Uislamu na Qur’an Tukufu. Kukosoa kwao si kutokana na chuki, bali ni kutokana na ufuasi wa haki na uchambuzi wa kielimu.
-
Ayatollah al-Udhma Javadi Amoli:
Maneno ya Ahlul-Bayt yana uzito sawa na Qur’an / “Tunapaswa kujiakisi kwa kushikamanisha nafsi zetu na viumbe walio hai na walio katika njia ya Haki
“Kile ambacho ni utambulisho wa Ahlul-Bayt (a.s), ni kilekile ambacho ni utambulisho wa Qur’an; ikiwa Qur’an inazungumza kwa ukweli, basi Ahlul-Bayt (a.s) pia wanazungumza kwa kweli, na ikiwa walisitiza kusema kitu fulani, kilikuwa kwa kweli.”
-
Darasa la Qur’an Tukufu katika Madrasat ya Mabanati ya Hazrat Zainab (sa) Laendelea kwa Mafanikio Makubwa
Darsa hili la Qur’an Tukufu linawafundisha zaidi Wanafunzi kuwa Qur'an ni mshirika na muombezi wa yeyote mwenye kushikamana nayo Siku ya Kiyama, hummulikia njia yake hapa duniani, na humuinua katika ngazi za juu Peponi
-
Ndoa ya “Kiutendaji” na “Kimwitikio” katika Mtindo wa Maisha wa Kiislamu
Ndoa ya Kiutendaji (konshi) inajengwa juu ya msingi wa uelewa, upangaji, kuwa na malengo, na maarifa ya kina, ambayo yanaendana na mafundisho ya Qur'ani yanayosisitiza kutafakari na kutumia akili kwa kina. Kinyume chake, ndoa ya Kimwitikio (vakoneshi) hutokana na mashinikizo ya nje, pupa, na hisia za muda mfupi, hali ambayo inakinzana na mafunzo ya Qur'ani yanayohimiza kuepuka pupa na kufanya mashauriano. Kwa hivyo, uchaguzi wa ndoa wa kimakini na wa kuwajibika – yaani ndoa ya kiutendaji – unakubaliana zaidi na mtazamo wa Kiislamu.
-
Hafla ya 4 ya Mashindano ya Kuhifadhi Qur'an Yaendelea Mubashara Kibaha – Pwani | Sheikh Dr. Alhad Mussa Salum Mgeni Rasmi Katika Hafla Hii
Kauli mbiu ya mashindano haya ni: “Hakika Qur’an ni Muongozo,” ikisisitiza nafasi ya Qur’an katika kuleta maadili, amani, na maendeleo ya kiroho katika jamii.
-
Kikao Maalum cha Uchambuzi wa Masomo ya Qur’an Tukufu Chafanyika Madrasa ya Wasichana ya Hazrat Zainab (sa) - Kigamboni, Dar-es-salaam
Katika kikao hicho, walimu mbalimbali walitoa maoni kuhusu mbinu bora za kufundishia na kuhimiza nidhamu ya kielimu, huku wanafunzi nao wakipewa nafasi ya kueleza changamoto wanazokutana nazo.
-
Safari ya Walimu wa Sayansi ya Qur'ani hadi “Erambuyeh” Makaburini mwa “Ali bin Hamzah Kufi Kisai”
Baadhi ya walimu wa taaluma za Qur'ani kutoka Iran wamefanya ziara katika kijiji cha Erambuyeh, kilichoko katika mkoa wa Pakdasht, Tehran, wakiamini kuwa eneo hilo ni mahali alipozikwa Abu al-Hasan Ali bin Hamzah al-Kufi, maarufu kama Kisā’i—mmoja wa wasomaji mashuhuri saba wa Qur’ani (Qurrā’ Sab‘a) na mwanazuoni mkubwa wa sarufi na lugha ya Kiarabu katika karne ya pili Hijria.
-
Maneno Muhimu na ya Hekima ya Sheikh Dr.Alhad Mussa Salum - kuhusu: Wanaoitwa Mitume na Manabii Tanzania, Udugu wa Watanzania, na Amani ya Tanzania
Jumuiya ya Maridhiano na Amani Tanzania tutasimama na Serikali Daima katika kulinda na kudumisha Amani na Maridhiano ya nchi yetu kwa ajili ya Ustawi wa nchi yetu.