Qur ani tukufu
-
Ayatollah Ramezani: "Umoja wa Umma wa Kiislamu Ndiyo Njia ya Kukabiliana na Uonevu wa Kimataifa"
Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Ulimwengu wa Ahlulbayt (a.s) katika kongamano la "Wanafikra wa Dini; Kubadilishana Uzoefu na Teknolojia Mpya" alisisitiza umuhimu wa umoja wa Kiislamu, uenezi wa pamoja wa mafundisho ya Qur'an na Ahlulbayt (a.s), na utambuzi wa uwezo wa ndani.
-
Mada | Dua Unapotengana na Umpendae – Mafunzo ya Kiimani na Faraja ya Kiislamu
Tunafundishwa Dua hii: اللَّهُمَّ اجْبُرْ كَسْرَ قَلْبِي، وَصَبِّرْنِي عَلَى مَا فَاتَنِي... "Ewe Mwenyezi Mungu! Tibu moyo wangu uliovunjika, nivumilishe juu ya kilichonipita..." Kwa Dua hii unajielekeza kwa Allah (SWT) kama Mponyaji wa nyoyo zilizovunjika na Mtulizaji wa roho zilizochoka. Inafundisha kumkabidhi Allah maumivu ya moyo, kukubali kuwa si kila tulichokitaka ni chema kwetu, na kumuomba Atuchagulie kilicho bora.
-
Ripoti ya Mahudhurio ya Wasomaji wa Qur'an wa Programu ya "Mahfali" nchini Tanzania
Katika hafla hii Tukufu ya Qur’an, wasomaji wa Kiirani walioshiriki ni pamoja na Ustadh Shakernejad, Ustadh Abolghasemi, Qari kijana Mohammad Hossein Azimi, na Muhanna Ghanbari – ambaye ni mhifadhi wa Qur’an nzima.
-
Heshima ya Mwanamke wa Kiislamu Katika Muonekano wa Vazi la Hijabu: Mfano wa Mabinti wa Hawzat Hazrat Zainab (sa), Dar es Salaam – Tanzania
Leo hii katika viwanja vya Mnazi Mmoja, jijini Dar es Salaam - Tanzania, palifanyika Kongamano Tukufu la Qur’an ambapo wanafunzi wa kike kutoka Hawzat Hazrat Zainab (sa) walishiriki kwa umahiri na adabu kubwa. Walikuwa mfano halisi wa utekelezaji wa mafundisho bora ya Kiislamu kuhusu namna ya kujisitiri, kuishi, na kuwasilisha ujumbe wa dini kwa vitendo.
-
Sheikh Zakzaky amekutana na wanafunzi wa programu ya Hifdhi ya Qur’an wa Fudiyyah kabla ya sherehe za kuhitimu
Kiongozi wa Harakati ya Kiislamu nchini Nigeria, Sayed Ibraheem Zakzaky, amekutana na wanafunzi wa Fudiyyah waliokamilisha Hifdhi ya Qur’an kabla ya sherehe za kuhitimu
-
Sheikh Dr.Alhad Mussa Salum awaalima watu wote katika Maonyesho ya Qur'an | Dar-es-salaam na Tanga
Qur'an Tukufu ni: Shifa (ponyo) kwa magonjwa ya kiroho na ya moyo kama vile wasiwasi, huzuni, mashaka, ujinga, na upotevu. Na ni Mwongozo wa maisha kwa binadamu wote—kwa mambo ya kidini na ya kila siku.
-
Kwa nini Qur'an inahitaji Tafsiri? | Sehemu ya Kwanza
Ili kuelewa Aya za Mutashabihat, tunahitaji wataalamu (wajuzi) wa Tafsiri ambao wanaweza kufafanua kwa kutumia Aya nyingine au zingine na elimu ya dini.
-
Sheikh Dkt. Abdul- Razak Amiri Atoa Kisa Halisi Cha Mwanamke wa Kiislamu aliyedai Talaka kisa Mume Wake Kaoa Mke wa 2, Hatimaye naye akawa Mke wa Pili
Ndoa ni heshima, ndoa ni stara ya kijamii, na ndio maana Qur'an Tukufu ikasema: «هُنَّ لِبَاسٌ لَّكُمْ وَأَنتُمْ لِبَاسٌ لَّهُنَّ» kwamba "Mwanamke ni vazi kwa Mwanaume, na Mwanaume ni vazi kwa Mwanamke". Katika kazi za vazi (nguo) ni heshima, kupendeza, kuheshimika, vazi kawaida yake linaleta heshima katika jamii, na Ndoa vile vile inaleta heshima katika Jamii.
-
Hujjat-ul-Islam Aali: Msaada kwa wengine unarudishwa (unafidiwa) mara nyingi zaidi na Mwenyezi Mungu
Mwalimu wa chuo kikuu na shule ya kidini alieleza kuwa kusaidia na kutatua matatizo ya wengine ni chanzo cha kupata malipo mengi kutoka kwa Mwenyezi Mungu. Alisisitiza kwamba sehemu ya kila mtu katika neema ya Mwenyezi Mungu inategemea uwezo wake wa kupokea, na ili kufaidika zaidi, ni lazima kuongeza uwezo huu.
-
Dr. Ali Taqavi, Mwakilishi wa Jamiat Al-Mustafa (s)Tanzania, akiambatana na Sheikh Dr. Alhad Mussa Salum watembelea uwanja wa Michezo Zanzibar + Picha
Uislamu umesisitiza Umoja wa Kiislamu, na madhehebu yote ya Kiislamu yanaunganishwa na Umoja wa Kiislamu, na Kibla cha Waislamu wote ni kimoja, na Qur'an ndio Kitabu chao na Muongozo wao.
-
Dr. Ali Taqavi, Mwakilishi wa Jamiat Al-Mustafa (s), Dar-e-Salam, Tanzania, katika ziara muhimu Zanzibar - Tanzania + Picha
"Ni muhimu kwa Wanafunzi kuzingatia elimu na maarifa ya Qur'an Tukufu, na kuwaasa katika kuzidisha juhudi zao kwenye suala muhimu la kusoma na kuhifadhi Qur'an Tukufu, na kuiweka Qur'an Tukufu mbele ya Maisha yao ya kila siku".
-
Kumbukumbu ya Shahada ya Imam Ja’far al-Sadiq (a.s) | Jua la Elimu na Uchaji Mungu Limezimwa
Shahada ya Imam Ja’far al-Sadiq (a.s) haikuwa tu kumpoteza kiongozi wa kiroho, bali ilikuwa ni jaribio la kuangamiza nuru ya elimu na mwongozo wa Ahlul Bayt(a.s). Hata hivyo, athari ya mafundisho yake bado inaishi hadi leo kupitia Maktaba ya Ja’fariyya, ambayo ni msingi wa Madhehebu ya Shia Ithna ‘Ashari.
-
Ufafanuzi kwa ufupi kuhusiana na hatua za mashindano ya Qur'an Tukufu na Hadithi - Jamiat Al-Mustafa (s), Dar-es-Salam - Tanzania, 2025
Tangazo la Matokeo ya mwisho litatolewa kuanzia Tarehe 01 - 05 - 2025 mpaka tarehe 05 - 05 - 2025. Na ratiba ya hafla ya fainali ya mashindano haya pamoja na ugawaji wa zawadi kwa washindi na washiriki utakuwa tarehe 17 - 05 - 2025 katika Ukumbi wa Mikutano ya Kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere - Jijini Dar-es-Salam - Tanzania.
-
Al_Itarah Foundation | Inatambua thamani na uzito wa Elimu na Maarifa ya Qur'an Tukufu,na umuhimu wa Umoja na Mshikamano wa Kiislamu baina ya Waislamu
Zawadi ya Kiroho na muhimu katika fremu ya kutambua thamani na uzito wa Elimu na Maarifa ya Qur'an Tukufu, na umuhimu wa kuendeleza Umoja na Mshikamano wa Kiislamu baina ya Waislamu.
-
Dr. Ali Taqavi, Mwakilishi wa Jamiat Al-Mustafa (S) - Dare-es-Salam, Tanzania, katika Mkutano muhimu na Mh.Mufti wa Zanzibar, Sheikh Saleh Kaabi
Kufanyika kwa Hafla ya Qur'an Tukufu ndani ya Zanzibar kwa ushirikiano baina ya Jamiat Al-Mustafa - Dares-Salam - Tanzania na BAKWATA
-
Tamasha la 30 la Kimataifa la Al-Mustafa la Qur'an na Hadithi - Zanzibar, Tanzania limefanyika kwa mafanikio makubwa
Tamasha hili la Mashindano ya Qur'an Tukufu, ni katika kuhuisha utajo wa Quran Tukufu, na hii ni harakati muhimu ya kuthamini na kuenzi Qur'an Tukufu inayoendelea nchini Tanzania, chini ya Usimamizi na Uongozi bora wa Hojjat Al-Islam Dr. Ali Taqavi (Mwenyezi Mungu Amuhifadhi) kwa kazi nzuri anayoendelea kuifanya katika uwanja Tablighi na khidma kwa Qur'an Tukufu, kwa hakika anajituma na kuhakikisha kuwa nuru ya elimu na maarifa ya Quran na ahlulbayt (as) vinazidi kuwaangazia watu wa jamii mbalimbali nchini Tanzania.
-
Ugumu uliopo katika kuwatangaza Kizazi Kitukufu cha Mtume Muhammad (saww) ambao ni Mawalii wa Mwenyezi Mungu (s.w.t) | Watu hawawajui Ahlu-Bayt (as)!
Leo hii, jambo la kuwatangaza Ahlul-Bayt (a.s) ambao ndio tumeusiwa na Mtume wetu Muhammad (s.a.w.w) tushikamane nao baada yake na kuwafuata wakiwa wakiwa kama Kizito cha Pili baada ya Qur'an Tukufu, ni jambo gumu kulingana na jamii ya watu tunayokabiliana nayo.
-
Al_Itrah Foundation, Dar-es-salaam - Tanzania yampa zawadi ya Tafsiri ya Kiswahili ya Qur'an Tukufu Mwenyekiti wa JMAT - TAIFA Sh.Dr Alhad Mussa Salum
"Kitabu Hicho Hakina Shaka ndani yake, ni Muongozo kwa Wacha Mungu".
-
Umuhimu wa Hijab kwa Mwanamke: Ni kwa nini Hijab ni Wajibu kwa Mwanamke wa Kiislamu?
Katika zama hizi, Hijabu imelinganishwa na kutoendelea kwa jamii na inafikiriwa kuwa ni ishara ya kifungo cha wanawake. Wahubiri wengi wanafikiria kuwa ni bora kutolizungumzia jambo hili katika majlisi zao. Lakini Mtukufu Mtume (s.a.w.w.) amesema: “Inapotokea Bid’ah na Mwanachuoni asikiseme kile akijuacho (dhidi ya Bid’ah hiyo), basi (Mwanachuoni huyo) hulaaniwa na Mwenyezi Mungu, Malaika na Wanadamu.”
-
Kuchapishwa kwa kitabu cha kwanza kuhusu Shahidi Sayyid Hassan Nasrallah kwa ajili ya Watoto
Kitabu cha kwanza cha Watoto na Vijana kuhusu Shahidi Sayyid Hassan Nasrallah, kilichoitwa "Baba Hadi" kilichoandikwa na: Elaheh Akherati, kimechapishwa na sasa kinapatikana kwa wale wanaotaka.
-
Maisha Mazuri:
Maisha kwa mtindo wa Wahyi: Je! Qur'an Inatuonyeshaje Njia ya Maisha ya Furaha (Saada)?
Kuelewa mtindo wa maisha katika zama za sasa, ambazo ni zama za Ghaiba, ni swali muhimu. Kwa sababu kazi muhimu ni kuelimisha kizazi kinacholingana na zama za wahyi ili kumsaidia Imamu wa Zama (Mwenyezi Mungu aharakishe kudhihiri kwake na faraja yake). Kwa kuzichunguza kwa makini Aya na riwaya, kudhihiri na kuonekana kwa maisha mazuri na hatimaye kufikia maisha sahihi katika kipindi cha kudhihiri, kutadhihirika katika mwanga au kivuli cha elimu na marifa juu ya Hojja wa Mwenyezi Mungu.
-
Umuhimu wa Qur'an Tukufu katika Maisha yetu kama Wanadamu
Kila Aya katika Aya za Qur’an ni chimbuko la mwangaza, muongozo na rahma, kwa hiyo mwenye kutaka mafanikio ya milele na kuokoka katika dunia yake, basi ni juu yake kushikamana na kitabu cha Mwenyeezi Mungu (s.w) usiku na mchana na kuzifanya Aya za Qur’an Tukufu kuwa mfano katika kumbukumbu zake na kituo cha fikra zake ili awe katika mwangaza wa Mwenyeezi Mungu (s.w).
-
Qur'an ni Msingi wa Maisha yetu, na ni Kitabu cha kweli, chenye kudumu milele
Muislamu mwenye kuhifadhi Qur'an Tukufu na mwenye Elimu juu ya Qur'an Tukufu, huyo atakuwa ni mwenye kuangaziwa na Nuru ya Qur'an kaburini mwake, na Mtume Muhammad (s.a.w.w) atakuwa Shahidi wake kesho Siku ya Kiyama.
-
Kufunga (Saumu) Kabla ya Uislamu:
Saumu kabla ya Uislamu inasemekana kuwa ilidumu kwa zaidi ya Mwezi mmoja. Ilikuwa ni Miezi mingapi na kwa nini ilikuwa ndefu?
Tunawaona Mayahudi na Wakristo wakifunga kwa namna mbali mbali hadi zama za sasa, ima kwa kujizuia kula nyama au maziwa au kula na kunywa kabisa kwa mujibu wa Hadithi, kufunga (Saumu) katika Mwezi wa Ramadhani haikuwa wajibu kwa nyumati zilizopita, bali waliokuwa wakifunga Saumu ni Mitume (Manabii) wao pekee (a.s), hao ndio waliokuwa wakifunga Mwezi wa Ramadhani.
-
Ufafanuzi wa Dua ya kabla ya Alfajiri 3 | Maimamu (a.s) ni "Neno Kamili" la Mwenyezi Mungu
Dua ya kabla ya alfajiri ikiwa kama dua maarufu zaidi ya kabla ya asubuhi kuingia katika Mwezi Mtukufu wa Ramadhani imepokelewa kutoka kwa Imam Baqir (AS). Uhusiano kati ya dhana ya juu ya Dua hii na nafasi ya Uimamu ni moja ya mada muhimu katika maelezo ya Dua hii.
-
Imani na matendo mema ni funguo za furaha ya Mwanadamu kwa mtazamo wa Qur'an
Hojjat-ul-Islam Madani, katika hafla ya kuhuisha usiku wa 19 wa Mwezi Mtukufu wa Ramadhani huko Mahdiyeh, Rasht, alisisitiza juu ya umuhimu wa kufikiri kabla ya dhikri katika Usiku wa Lailatul - Qadri, na kuanzisha mambo kama vile imani kwa Mwenyezi Mungu na matendo ya haki kama nguzo mbili za msingi za furaha na ustawi wa Binadamu kwa mtazamo wa Qur'an Tukufu
-
Vi[indi vya Tafsiri ya Qur’an Tukufu:
Tafsiri ya Aya ya Kwanza ya Surat Al-Maidah
Kwa kuwa "Hakika ya Waumini ni ndugu", basi Muislamu anatakiwa kuhakikisha kuwa anatimiza Haki ya ndugu yake Muislamu, na anatetea Haki yake kama Muislamu na kama ndugu yake.
-
Hafla ya Ufunguzi wa Husseiniyyah Mpya Jijini Arusha - Tanzania, kwa jina la Imam Ridha (a.s)
Wasomaji wa Kitaifa na Kimataifa wa Qur'an Tukufu wa Tanzania pamoja na Masheikh waliotoka maeneo mbalimbali ya nchi, ni miongoni mwa waliodhuhuria katika Hafla hiyo adhimu.
-
Dk. Pezeshkian: Ikiwa mwongozo wa Qur'an hauonekani katika matendo na maisha yetu, basi tunapaswa kufikiria upya tabia zetu.
Akisisitiza umuhimu wa kuunganisha maarifa ya Qur'an na matendo ya kijamii, Rais wa Iran amesema: Tatizo kubwa ni pengo kati ya kuijua na kuitekeleza Qur'an. Tunadai kuwa Qur’an inatuonyesha njia ya uongofu na inamfikisha Mwanadamu katika kilele cha juu zaidi, lakini ikiwa kivitendo hakuna dalili ya mwongozo huu inayoweza kuonekana katika maisha yetu ya kibinafsi na ya kijamii, basi kwa hakika tunapaswa kuangalia upya tabia zetu.
-
Uzinduzi wa Kituo cha Qur'an - Arusha, Tanzania:
"Hakika Qur'an hii inaongoza katika yaliyonyooka kabisa"
Sheikh Maulid Hussein Kundya amesisitiza juu ya umuhimu wa kuisoma na kuifahamu Qur'an Tukufu, na kuwakumbusha Waumini kuizingatia kauli ya Mwenyezi Mungu ambapo amesema: "Hakika Qur'an hii inaongoza katika yaliyonyooka kabisa, na inawabashiria Waumini wanaotenda mema kwamba watapata ujira mkubwa".