25 Mei 2025 - 19:52
Ripoti ya Mahudhurio ya Wasomaji wa Qur'an wa Programu ya "Mahfali" nchini Tanzania

Katika hafla hii Tukufu ya Qur’an, wasomaji wa Kiirani walioshiriki ni pamoja na Ustadh Shakernejad, Ustadh Abolghasemi, Qari kijana Mohammad Hossein Azimi, na Muhanna Ghanbari – ambaye ni mhifadhi wa Qur’an nzima.

Kwa mujibu wa Ripoti ya Shirika la Habari la Kimataifa la Ahlul-Bayt (as) - ABNA- Leo Jumapili, tarehe 25/05/2025, hafla ya kuvutia ilifanyika katika uwanja wa Mnazi Mmoja, Jijini Dar-es-salaam - Tanzania ikihudhuriwa na watazamaji wengi zaidi Elfu Kumi (10) kutoka maeneo mbalimbali ya Jiji la Dar-es-salaam na nje yake, kwa ajili ya kuja kusikiliza wasomaji bingwa na maarufu wa Qur’an Tukufu walioifanya programu hii ya Mahfali ya Qur'an kupendeza kwa visomo vyao vizuri vya Qur'an kwa Njia ya Tajweed.

Ripoti ya Mahudhurio ya Wasomaji wa Qur'an wa Programu ya "Mahfali" nchini Tanzania

Hafla hii iliandaliwa kwa ushirikiano wa Jumuiya ya Al-Mustafa na Ubalozi wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran pamoja na Ofisi ya Ushauri wa kiutamaduni wa Iran nchini Tanzania.

Ripoti ya Mahudhurio ya Wasomaji wa Qur'an wa Programu ya "Mahfali" nchini Tanzania

Miongoni mwa waliohudhuria hafla hiyo ni Balozi wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran, Mshauri wa masuala ya kiutamaduni, na Mwakilishi wa Kikanda wa Jamiat Al-Mustafa (s) nchini Tanzania. 

Ripoti ya Mahudhurio ya Wasomaji wa Qur'an wa Programu ya "Mahfali" nchini Tanzania

Ripoti ya Mahudhurio ya Wasomaji wa Qur'an wa Programu ya "Mahfali" nchini Tanzania

Hafla hii ilifanyika chini ya kauli mbiu ya kuleta umoja isemayo: “Qur’an Inatuunganisha”, na ilipokelewa kwa hamasa kubwa na Wananchi wa Jiji la Dar-es-salaam.

Ripoti ya Mahudhurio ya Wasomaji wa Qur'an wa Programu ya "Mahfali" nchini Tanzania

Wadau mbalimbali wa Qur'an Tukufu wametoa shukrani zao maalumu kwa Iran kwa kuleta wasomaji mahiri wa Qur’an nchini Tanzania, wakilitaja tukio hilo kuwa ni ishara ya uhusiano wa kina wa kitamaduni na kidini kati ya Mataifa haya mawili.

Ripoti ya Mahudhurio ya Wasomaji wa Qur'an wa Programu ya "Mahfali" nchini Tanzania

Ripoti ya Mahudhurio ya Wasomaji wa Qur'an wa Programu ya "Mahfali" nchini Tanzania

Katika hafla hii Tukufu ya Qur’an, wasomaji wa Kiirani walioshiriki ni pamoja na Ustadh Shakernejad, Ustadh Abolghasemi, Qari kijana Mohammad Hossein Azimi, na Muhanna Ghanbari - ambaye ni mhifadhi wa Qur’an nzima. 

Ripoti ya Mahudhurio ya Wasomaji wa Qur'an wa Programu ya "Mahfali" nchini Tanzania

Ripoti ya Mahudhurio ya Wasomaji wa Qur'an wa Programu ya "Mahfali" nchini Tanzania

Wasomaji hawa wa Qur'an Tukufu, walitumbuiza kwa tilawa za kuvutia ambazo zilijaza kumbi za viwanja vya Mnazi Mmoja hali ya furaha ya kiroho. 

Ripoti ya Mahudhurio ya Wasomaji wa Qur'an wa Programu ya "Mahfali" nchini Tanzania

Ripoti ya Mahudhurio ya Wasomaji wa Qur'an wa Programu ya "Mahfali" nchini Tanzania

Aidha, baadhi ya wasomaji wa Kitanzania pia walipata nafasi ya kusoma Qur’an na walipokelewa vyema na hadhira.

Ripoti ya Mahudhurio ya Wasomaji wa Qur'an wa Programu ya "Mahfali" nchini Tanzania

Ripoti ya Mahudhurio ya Wasomaji wa Qur'an wa Programu ya "Mahfali" nchini Tanzania

Tags

Your Comment

You are replying to: .
captcha