Akizungumza katika kipindi cha Sports Extravaganza kinachorushwa na TV47 na kuendeshwa na Tony Kwalanda, Dkt. Gholampour alisema kuwa michezo ni daraja muhimu la kuunganisha mataifa na jamii.
Dk. Pourmarjan, mtetezi kwa bidii wa elimu, alieleza dhamira ya Ubalozi wa Iran Nchini Kenya kuwa ni kutoa ufadhili wa masomo kwa Wanafunzi wanaoishi katika mazingira magumu, kwa lengo la kuwapa fursa bora zaidi kwa maisha yao bora ya baadaye.