Nuru

  • Andiko Kamili la Khutba ya Fadak ya Bibi Fātima Zahra (a.s) pamoja na tarjama yake

    Andiko Kamili la Khutba ya Fadak ya Bibi Fātima Zahra (a.s) pamoja na tarjama yake

    1. Mwanzo wa Khutba – Malalamiko kuhusu dhulma na msimamo wa watu Kisha hamkungoja hata kidogo ili moyo uliokuwa umejeruhiwa utulie, na hali ile ngumu iwe nyepesi. Bali mliongeza kuni kwenye moto, mkaufukuzia upepo ili uongezeke kuwaka. Mlikuwa tayari kuitikia mwito wa Shetani, mkijiandaa kuzima nuru angavu ya dini ya Mwenyezi Mungu, na kuondoa Sunna za Mtume Muhammad (s.a.w.w) aliyechaguliwa. Kwa kisingizio cha maslahi, mlikuwa mkila kijuujuu na kuficha nia zenu. Mlikuwa mkifanya njama nyuma ya vilima na miti dhidi ya familia yake na watoto wake. Na sisi tulipaswa kustahimili mambo haya yenye uchungu kama kisu chenye makali makali, au mkuki unaopenya tumboni.

  • Ripoti ya Mahudhurio ya Wasomaji wa Qur'an wa Programu ya "Mahfali" nchini Tanzania

    Ripoti ya Mahudhurio ya Wasomaji wa Qur'an wa Programu ya "Mahfali" nchini Tanzania

    Katika hafla hii Tukufu ya Qur’an, wasomaji wa Kiirani walioshiriki ni pamoja na Ustadh Shakernejad, Ustadh Abolghasemi, Qari kijana Mohammad Hossein Azimi, na Muhanna Ghanbari – ambaye ni mhifadhi wa Qur’an nzima.

  • Umuhimu wa Qur'an Tukufu katika Maisha yetu kama Wanadamu

    Umuhimu wa Qur'an Tukufu katika Maisha yetu kama Wanadamu

    Kila Aya katika Aya za Qur’an ni chimbuko la mwangaza, muongozo na rahma, kwa hiyo mwenye kutaka mafanikio ya milele na kuokoka katika dunia yake, basi ni juu yake kushikamana na kitabu cha Mwenyeezi Mungu (s.w) usiku na mchana na kuzifanya Aya za Qur’an Tukufu kuwa mfano katika kumbukumbu zake na kituo cha fikra zake ili awe katika mwangaza wa Mwenyeezi Mungu (s.w).