Katika hafla hii Tukufu ya Qur’an, wasomaji wa Kiirani walioshiriki ni pamoja na Ustadh Shakernejad, Ustadh Abolghasemi, Qari kijana Mohammad Hossein Azimi, na Muhanna Ghanbari – ambaye ni mhifadhi wa Qur’an nzima.
Kila Aya katika Aya za Qur’an ni chimbuko la mwangaza, muongozo na rahma, kwa hiyo mwenye kutaka mafanikio ya milele na kuokoka katika dunia yake, basi ni juu yake kushikamana na kitabu cha Mwenyeezi Mungu (s.w) usiku na mchana na kuzifanya Aya za Qur’an Tukufu kuwa mfano katika kumbukumbu zake na kituo cha fikra zake ili awe katika mwangaza wa Mwenyeezi Mungu (s.w).