13 Aprili 2025 - 20:03
Tamasha la 30 la Kimataifa la Al-Mustafa la Qur'an na Hadithi - Zanzibar, Tanzania limefanyika kwa mafanikio makubwa

Tamasha hili la Mashindano ya Qur'an Tukufu, ni katika kuhuisha utajo wa Quran Tukufu, na hii ni harakati muhimu ya kuthamini na kuenzi Qur'an Tukufu inayoendelea nchini Tanzania, chini ya Usimamizi na Uongozi bora wa Hojjat Al-Islam Dr. Ali Taqavi (Mwenyezi Mungu Amuhifadhi) kwa kazi nzuri anayoendelea kuifanya katika uwanja Tablighi na khidma kwa Qur'an Tukufu, kwa hakika anajituma na kuhakikisha kuwa nuru ya elimu na maarifa ya Quran na ahlulbayt (as) vinazidi kuwaangazia  watu wa jamii mbalimbali nchini Tanzania.

Shirika la Habari la Kimataifa la Ahlul-Bayt (a.s) - ABNA - Tamasha la 30 la Kimataifa la Al-Mustafa la Quran na Hadithi - Zanzibar, limefanyika kwa mafanikio makubwa chini ya uongozi na usimamizi wa Mwakilishi wa Jamiat Al-Mustafa, Tanzania - Dr. Ali Taqavi. Wanafunzi wa Jamiatul-Mustafa - Tanzania na vyuo vingine wameshiriki katika Mashindano haya ya Hifdhi ya Quran Tukufu na Hadithi. Hii ni katika kuhuisha utajo wa Qur'an Tukufu, na Harakati muhimu ya kuthamini na kuenzi Qur'an Tukufu inayoendelea nchini Tanzania, chini ya Uongozi bora wa Hojjat Al-Islam Dr. Ali Taqavi (Mwenyezi Mungu amuhifadhi) kwa kazi nzuri anayoendelea kuifanya katika uwanja wa Tablighi, kwa kujituma kwa kila jambo ili kuhakikisha kuwa nuru ya elimu na maarifa ya Qur'an na Ahlulbayt (a.) vinazidi kuwaangazia  watu wa jamii mbalimbali nchini Tanzania.

Tamasha la 30 la Kimataifa la Al-Mustafa la Qur'an na Hadithi - Zanzibar, Tanzania limefanyika kwa mafanikio makubwa

Katika Mashindano haya ya Qur'an Tukufu, Wanafunzi wanashinda katika kuhifadhi Qur'an Tukufu kaanzia Juzuu 3, 5, 7, ... mpaka Juzuu 30. Na washindi katika kila kipengele wanajipatia zawadi nono zenye lengo adhimu la kuzidi kuwahamasisha na kuwashajiisha wazidi kuiweka Qur'an Tukufu katika vifua vyao, na katika Maisha yao ya kila siku, na wahakikishe kuwa wanaishi daima kwa mujibu wa muongozo wa Qur'an Tukufu, kwa hakika Qur'an ni uhai wa nyonyo.

Tamasha la 30 la Kimataifa la Al-Mustafa la Qur'an na Hadithi - Zanzibar, Tanzania limefanyika kwa mafanikio makubwa

Tags

Your Comment

You are replying to: .
captcha