uongozi
-
Ayatullah A‘rafi: Hatua Zote Kuhusu Wahamiaji Zinapaswa Kuchukuliwa kwa Mtazamo wa Maadili na Uislamu
Ayatollah A'rafi aliashiria juu ya umuhimu wa uongozi maalumu katika masuala ya wahamiaji, akitaja mji wa Qom kuwa ni eneo lenye umuhimu mkubwa linalohitaji mpango thabiti wa kiutamaduni, usimamizi wa karibu, na juhudi za kudumisha utambulisho wa kidini na kijamii wa wahamiaji.
-
Afisa wa Kijeshi wa Iraq: Kamwe Haitatokea kusahau msaada wa Iran
Rais wa Chuo cha Ulinzi wa Iran: “Tunafurahia sana kwamba maafisa wa Iraq wanasoma katika Chuo cha Uongozi na Makao Makuu ya Jeshi la Iran. Ingawa kuna uwezekano wa kusoma katika nchi nyingine, tunapendelea maafisa wetu wapate elimu yao hapa Iran, kwa kuwa tunajua wanapata mafunzo bora chini ya wakufunzi wenye kiwango cha juu cha kielimu na kitaaluma.”
-
Sharm el-Sheikh: Dunia Iliyo Pinduliwa na Mashujaa wa Uongo / Maonyesho ya Amani kwa Ajili ya Kukwepa Haki
Mkutano wa Sharm el-Sheikh umehudhuriwa na watu kama Donald Trump, Emmanuel Macron, na viongozi wengine wa Magharibi ambao kwa hakika ni washirika wa mauaji ya halaiki ya Gaza.
-
Ayatullah Malakooti:
"ABNA Ina Wajibu wa Kutambulisha Madhehebu ya Ahlul-Bayt (A.S) Ulimwenguni / Baba Marehemu alikuwa wa Awali Kusaini kuondolewa kwa Shah"
Akizungumza na Shirika la Habari la Kimataifa la Ahlul-Bayt (ABNA) Jumapili, 20 Mehr 1404 (2025), Ayatullah Malakooti alisisitiza umuhimu wa kueleza Ushia kwa usahihi mbele ya upotoshaji. Alieleza kuwa kabla ya Mapinduzi ya Kiislamu, dunia haikuufahamu Ushia kama ilivyostahili; taarifa nyingi zilizokuwepo zilitokana na maandiko ya Ahlus-Sunnah yaliyo na taarifa zisizokamilika au kwa makusudi kutoeleza Ushia kwa usahihi, na hivyo Ushia / Mashia walichukuliwa kama kundi dogo au la upande mmoja.
-
Bi Mujtahida Saffati: Vyuo vya kidini vya wanawake vinapaswa kuchukua uongozi wa kielimu wa wanawake katika ulimwengu wa Kiislamu
Profesa mashuhuri wa vyuo vya kidini vya wanawake, katika hafla ya uzinduzi wa mwaka mpya wa masomo, alivitaja “ikhlasi na uchamungu (taqwa)”, “kuungana na uongozi wa Kiislamu (wilaya)”, na “kuzingatia haki za wengine” kuwa ni nguzo tatu muhimu za mafanikio kwa wanafunzi wa fani za dini. Akaeleza kwa msisitizo kuwa: Taasisi za kielimu za wanawake zinapaswa kuchukua uongozi wa kielimu kwa wanawake wa ulimwengu wa Kiislamu, na kutumia uwezo huo kwa ajili ya kusambaza maarifa ya Kiislamu katika ulimwengu mzima wa Kiislamu.
-
Kumbukumbu ya Shahada ya Imam Hasan al-Askari (AS)
Mojawapo ya malengo ya Mitume na Maimam (amani iwe juu yao), ni kusimamisha uadilifu na usawa katika jamii. Kwa mujibu wa Qur'an na hadithi za Maimamu, jamii haiwezi kusimama bila ya uongozi wa Imam Mwadilifu atakayeongoza masuala ya kidini na kijamii. Imam ni mlinzi wa sheria na mwongoza watu kuelekea haki na mafanikio.
-
Sheikh Dr. Alhad Musa Salum Akabidhiwa Tuzo ya Uongozi wa Mfano na JMAT Mkoa wa Dar -es- Salaam
Tukio hilo lilifanyika katika Mkutano Mkuu wa Mkoa wa JMAT kwa Muhula wa Kwanza wa Mwaka 2025, ambapo viongozi mbalimbali wa kidini na kijamii walihudhuria.
-
Maana ya Ghadir Khum na Umuhimu wa Siku ya Ghadir Khum katika Uislamu
Ghadir Khum ni tukio la kihistoria lenye uzito mkubwa kwa Waislamu, hasa kwa wale wanaotilia mkazo nafasi ya Ahlul Bayt (a.s) katika uongozi wa umma. Ni siku ya kutafakari juu ya uongozi wa haki, kutambua mafundisho ya Mtume (s.a.w.w), na kuhuisha uhusiano wa kidini kwa msingi wa upendo, uadilifu, na utiifu kwa uongozi wa kweli wa Kiislamu.
-
Kufanyika kwa Vikao vya Kitaaluma Vinavyohusiana na Kongamano la Mfano wa Uongozi wa Shahid Raisi Katika Nchi 6; Kuanzia Iran hadi Malaysia na Iraq
Katibu wa Kwanza wa Kongamano la Kimataifa la Mfano wa Uongozi wa Shahid Ayatollah Dkt. Sayyid Ebrahim Raisi: Kongamano Limekuwa Jukwaa la Kimataifa kwa Ufafanuzi wa Uongozi wa Kiislamu Katibu wa kongamano la kwanza la kimataifa kuhusu mfano wa uongozi wa Shahid Ayatollah Dkt. Sayyid Ebrahim Raisi amesema kuwa, kongamano hili limekuwa jukwaa la kimataifa kwa ajili ya kufafanua dhana ya uongozi wa Kiislamu, kupitia vikao mbalimbali vilivyofanyika katika nchi sita — ambazo ni India, Pakistan, Indonesia, Malaysia, Iraq na Iran.
-
Tamasha la 30 la Kimataifa la Al-Mustafa la Qur'an na Hadithi - Zanzibar, Tanzania limefanyika kwa mafanikio makubwa
Tamasha hili la Mashindano ya Qur'an Tukufu, ni katika kuhuisha utajo wa Quran Tukufu, na hii ni harakati muhimu ya kuthamini na kuenzi Qur'an Tukufu inayoendelea nchini Tanzania, chini ya Usimamizi na Uongozi bora wa Hojjat Al-Islam Dr. Ali Taqavi (Mwenyezi Mungu Amuhifadhi) kwa kazi nzuri anayoendelea kuifanya katika uwanja Tablighi na khidma kwa Qur'an Tukufu, kwa hakika anajituma na kuhakikisha kuwa nuru ya elimu na maarifa ya Quran na ahlulbayt (as) vinazidi kuwaangazia watu wa jamii mbalimbali nchini Tanzania.
-
Ayatollah Ramezani: Kutokushindwa ndio msingi wa utawala wa Alawi; Imam Ali (amani iwe juu yake) ni kielelezo cha Ulimwengu wa Mwanadamu
Katibu Mkuu wa Baraza la Kidunia la Ahlul-Bayt (a.s.) katika hafla ya kuhuisha Usiku wa 21 wa Ramadhani, akiashiria kwamba kutokukubali ndio msingi wa utawala wa Alawi, alisema: Imam Ali (a.s) ni kielelezo cha ulimwengu wa Wanadamu.