11 Februari 2026 - 18:44
Sepah: Njama za Adui Kuangusha Mfumo wa Uongozi wa Kiislamu Zashindwa kwa Busara ya Kiongozi Mkuu wa Iran na Uangalifu wa Wananchi

Jenerali Naeini amesema tangu 13 Juni 2025 adui alilenga kuuangusha mfumo wa Kiislamu wa Iran kwa kusababisha machafuko ya kijamii, lakini kwa busara ya Kiongozi Mkuu Sayyid Ali Khamenei (h.a.) na uangalifu wa wananchi, njama hizo zilivunjika. Pia katika ghasia za 8 Januari 2026 na operesheni ya “Ahadi ya Kweli”, juhudi za adui zilikabiliwa na kushindwa kabisa.

Shirika la Habari la Kimataifa la Ahlul-Bayt (as) -ABNA-  Jenerali Naeini - Msemaji wa Sepah amesema kwamba: Adui tangu tarehe 13 Juni 2025 alikuwa analenga kuunyang’anya mfumo (Uongozi wa Kiislamu wa Iran) uwezo wa kufanya maamuzi, lakini kwa busara na hekima ya Kiongozi Mkuu wa Mapinduzi, Sayyid Ali Khamenei (Allah Amuhifadhi) mipango yao ilivunjwa mmoja baada ya mwingine.

Lengo la adui lilikuwa kusababisha machafuko ndani ya jamii kwa kutumia shinikizo la maisha, lakini nyoyo za watu zimejikita kwa uongozi wa Kiungu, hivyo njama hii pia ilishindwa.

Katika ghasia za tarehe 8 Januari 2026, huduma za kijasusi za zaidi ya nchi 50 ziliingia uwanjani moja kwa moja na kwa njia zisizo za moja kwa moja.

Lengo kuu lilikuwa ni kuuangusha mfumo wa Kiislamu, lakini uangalifu wa wananchi na nguvu ya dola uliifanya miradi hiyo ishindwe kabisa.

Katika operesheni ya “Ahadi ya Kweli (Al_Wa‘d Al_Sadiq)”, zaidi ya ndege 300 katika nchi za eneo zilijaribu kuzuia makombora yetu, na adui licha ya kutumia mamia ya ndege na mifumo ya ulinzi wa anga, alipatwa na mkanganyiko na kushindwa.

Tags

Your Comment

You are replying to: .
captcha