Ayatollah Khamenei
-
Kiongozi wa Iran: Ukiukaji wa Marekani unathibitisha saini yake haina thamani; Iran ina masomo yasiyosahaulika kwa adui
Katika ujumbe kuhusu kuaga kwa kishujaa kwa Kiongozi shahidi wa Iran, Kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu Ayatollah Sayyid Mojtaba Khameni amesema kuwa ukiukaji wa mara kwa mara wa Marekani wa makubaliano yaliyosainiwa kati ya marais wa Iran na Marekani umeonyesha tena kuwa saini ya rais wa Marekani haina thamani. Amesema pia kuwa Iran na mhimili wa muqawama wana masomo yasiyosahaulika kwa adui, kama ilivyoonekana kupitia ujasiri wa wapiganaji na uhodari wa wananchi wa maeneo ya kusini.
-
Naibu Mwenyekiti wa Baraza Kuu la Kiislamu la Washia Lebanon: Iran Inaingia Katika Kipindi Kipya cha Nguvu
Sheikh Ali Al-Khatib amesema kuwa baada ya kuuawa shahidi kwa Kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu, Ayatollah Sayyid Ali Khamenei, Iran imeingia katika hatua mpya ya nguvu, akisisitiza kuwa misingi ya fikra, dini na maadili ya uongozi wake imejikita kwa kina miongoni mwa Wairani, Waislamu na watu huru duniani.
-
Iraq Yaandaa Mazishi ya Kihistoria ya Kiongozi Shahidi wa Mapinduzi ya Kiislamu Ayatollah Sayyid Ali Khamenei (ra)
Marasimu ya kihistoria ya mazishi ya mwili mtukufu wa Kiongozi Shahidi wa Mapinduzi ya Kiislamu, Ayatullah Sayyid Ali Hussein Khamenei, pamoja na mashahidi wa familia yake, yanafanyika leo nchini Iraq kwa ushiriki wa maelfu ya waombolezaji.
-
Rais wa Iran Masoud Pezeshkian Awasili Najaf Kushiriki Mazishi ya Kiongozi Shahidi Ayatullah Sayyid Ali Khamenei
Rais wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran, Dkt. Masoud Pezeshkian, amewasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Najaf nchini Iraq kwa ajili ya kushiriki katika mazishi ya Kiongozi Shahidi Ayatullah Sayyid Ali Khamenei, ambapo alipokelewa na Waziri Mkuu wa Iraq pamoja na viongozi wengine waandamizi wa nchi hiyo.
-
Mwanaharakati wa Vyombo vya Habari wa Urusi: Sijawahi Kushuhudia Jambo Kama Hili Maishani Mwangu
Mwanaharakati wa vyombo vya habari kutoka Urusi amesema umati mkubwa wa wananchi waliojitokeza kumuaga kiongozi wao umeandika historia, akisisitiza kuwa mshikamano wa Wairani umeonyesha mapenzi ya dhati kwa taifa na uongozi wao.
-
Mkuu wa Mhimili wa Mahakama Awashukuru Waombolezaji wa Mazishi ya Kiongozi Shahidi Ayatollah Sayyid Ali Khamenei
Mkuu wa Mhimili wa Mahakama wa Iran amesema mahudhurio ya mamilioni ya wananchi katika mazishi ya Kiongozi Shahidi Ayatollah Sayyid Ali Khamenei yameandika ukurasa mpya wa historia ya mshikamano, heshima na uimara wa taifa la Iran.
-
Washington post: Familia Nyingi Zilishiriki Katika Mazishi ya Kiongozi Shahidi wa Iran
Gazeti la Washington Post limesema kuwa Mazishi ya Kiongozi Shahidi wa Iran yalishuhudia ushiriki mkubwa wa wananchi, wakiwemo familia zilizofika na watoto wao, huku yakieleza kuwa tukio hilo lilidhihirisha mshikamano wa kitaifa na uthabiti wa wananchi.
-
Sheikh Isa Qassim: Kiongozi Shahidi alisimama kwa ajili ya Uislamu, Umma na ubinadamu
Mwanazuoni mashuhuri wa Bahrain, Ayatullah Sheikh Isa Ahmad Qassim, amesema kuwa Kiongozi Shahidi Ayatullah Sayyid Ali Khamenei alijitolea maisha yake kwa ajili ya Uislamu, Umma wa Kiislamu na ubinadamu, huku akieleza kuwa urithi wake utaendelea kuongoza njia ya Muqawama na umoja wa Waislamu.
-
Ayatullah Makarim Shirazi: Wauaji wa Kiongozi Shahidi hawataepuka adhabu ya Mwenyezi Mungu
Ayatullah al-Udhma Sheikh Nasir Makarim Shirazi amesema kuwa waliohusika na mauaji ya Kiongozi Shahidi wa Mapinduzi ya Kiislamu, pamoja na viongozi, raia wasio na hatia na watoto waliouawa, hawataokoka adhabu ya Mwenyezi Mungu na kwamba damu za mashahidi hao hazitasahaulika kamwe.
-
kamanda wa jeshi la majini la Iran: muqawama haujafungwa tena na mipaka ya kijiografia
Kamanda wa Jeshi la Majini la Iran, Admiral Shahram Irani, amesema kuwa Muqawama sasa umevuka mipaka ya kijiografia, akisisitiza kuwa mataifa na vikosi vya Muqawama vinaendelea kuimarisha umoja na mshikamano katika kukabiliana na changamoto.
-
Ayatollah Makarim Shirazi: Waliomuua Kiongozi Shahidi Hawataepuka Adhabu ya Mwenyezi Mungu
Ayatollah Nasser Makarim Shirazi amesema wahusika na wapangaji wa mauaji ya Kiongozi Shahidi wa Mapinduzi ya Kiislamu, pamoja na waliohusika na umwagaji damu wa viongozi, raia wasio na hatia na watoto, hawataokoka adhabu ya Mwenyezi Mungu, huku akisisitiza kuwa damu zao takatifu haitasahaulika kamwe.
-
“Diplomasia ya Aya”: Aya za Qur'ani zilizosomwa katika marasimu ya mazishi ya Kiongozi Shahidi Imam Sayyid Ali Khamenei zavutia hisia za wengi
Katika marasimu ya kuuaga mwili wa Kiongozi Shahidi wa Mapinduzi ya Kiislamu, Imam Sayyid Ali Khamenei (Quds Sirruh), uteuzi wa Aya za Qur'ani Tukufu zilizosomwa kwa kila ujumbe wa wageni waliotoa salamu za rambirambi ulivutia hisia za wengi, huku kila Aya ikionekana kubeba ujumbe maalumu wa kisiasa, kiitikadi na kiroho.
-
Mazingira ya Mazishi ya Imam Shahidi (r.a) Kufanyika kwa Maelekezo ya Kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu
Katibu wa Kamati ya Kitaifa ya Kuaga na Kusimamia Mazishi ya Imam Shahidi (r.a) amesema kuwa maandalizi ya mazishi hayo yanafanyika kwa uongozi na maelekezo ya Kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu, Ayatullah Sayyid Mujtaba Husseini Khamenei, huku akizitaka vyombo vya habari kuhifadhi tukio hilo la kihistoria kwa ajili ya vizazi vijavyo.
-
Serikali ya Iran Yatangaza Mali Zilizoachwa na Kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu Ayatollah Sayyid Ali Khamenei (r.a)
Serikali ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran imesema uchunguzi wa mali za Ayatullah Sayyid Ali Khamenei (r.a.) umebaini kuwa aliacha mali chache sana, jambo linalotajwa kuakisi maisha yake ya ucha-Mungu na kujiepusha na anasa.
-
Aref: Hafla za Kuaga na Mazishi ya Imam Shahidi Zitafanyika kwa Hadhi Inayolingana na Nafasi Yake ya Kihistoria na Kimataifa
Makamu wa Kwanza wa Rais wa Iran, Mohammad Reza Aref, amesema maandalizi yanaendelea kuhakikisha hafla za kuaga na mazishi ya Imam Shahidi zinafanyika kwa ushiriki mkubwa wa wananchi na kwa hadhi inayostahili nafasi yake ya kihistoria na kimataifa.
-
Mwitikio wa Kuunga Mkono Wanaodhulumiwa; Kuongezeka kwa Kuonesha Mapenzi kwa Ayatollah Sayyid Ali Khamenei nchini Pakistan
Kuongezeka kwa kuonesha mapenzi kwa Ayatollah Sayyid Ali Khamenei nchini Pakistan, ikiwemo kuonekana kwa picha au kauli mbiu katika mabasi ya mji wa Islamabad, kunaelezwa kuwa ni ishara ya uungwaji mkono kwa viongozi wanaotetea wanyonge na kupinga dhulma.
-
-
Sepah: Njama za Adui Kuangusha Mfumo wa Uongozi wa Kiislamu Zashindwa kwa Busara ya Kiongozi Mkuu wa Iran na Uangalifu wa Wananchi
Jenerali Naeini amesema tangu 13 Juni 2025 adui alilenga kuuangusha mfumo wa Kiislamu wa Iran kwa kusababisha machafuko ya kijamii, lakini kwa busara ya Kiongozi Mkuu Sayyid Ali Khamenei (h.a.) na uangalifu wa wananchi, njama hizo zilivunjika. Pia katika ghasia za 8 Januari 2026 na operesheni ya “Ahadi ya Kweli”, juhudi za adui zilikabiliwa na kushindwa kabisa.
-
Israel Leo Iko Dhaifu, Iran Imebaki Imara – Sheikh Naeem Qasim
Sheikh Naeem Qasim na Katibu Mkuu wa Hezbollah wanasema kuwa Israel leo iko dhaifu kuliko hapo awali, huku Iran chini ya uongozi wa Imam Khamenei ikibaki imara, huru na thabiti. Mapinduzi ya Iran yameendeleza upinzani katika eneo kwa miaka 47 bila kutegemea Mashariki au Magharibi, na Jamhuri ya Kiislamu imefanikiwa katika mapambano yake, hasa dhidi ya uvamizi wa Israel.
-
Jumuiya ya Wanazuoni wa Ahlul-Bayt (a.s) Uturuki Yaionya Marekani: Imam Khamenei ni Mstari wetu Mwekundu
Jumuiya ya Wanazuoni wa Ahlul-Bayt (a.s) nchini Uturuki, katika tamko lake, imetangaza kuwa jaribio lolote la kumvunjia heshima au kumdhuru Kiongozi Mkuu wa Mapinduzi ya Kiislamu ni mstari mwekundu wa ulimwengu wa Kiislamu.
-
Ujumbe wa rambirambi wa Kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu kufuatia kifo cha A'lim Mwanajihad na Mtumishi Hujjatul-Islam Shahcheraghi
Kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu kupitia ujumbe wake ametoa rambirambi kufuatia kifo cha A'lim (mjuzi) Mwanajihadi na Mtumishi, Hujjatul-Islam Sayyid Mohammad Shahcheraghi.
-
Umoja wa Waislamu na kuunga mkono Iran kama mstari wa mbele wa kulinda Quds ni jambo la lazima
Mwanafikra mashuhuri wa Algeria amesisitiza kuwa umoja wa Waislamu, kuacha misimamo ya chuki za kimadhehebu na kuunga mkono Iran kama ngome ya mbele ya kulinda Quds (Msikiti wa Al-Aqsa) na Umma wa Kiislamu ni jambo la lazima, na kwamba mataifa pamoja na wanazuoni wa Kiislamu wanapaswa kusimama bega kwa bega na Jamhuri ya Kiislamu ya Iran katika nyanja za vyombo vya habari, siasa, utamaduni na usalama.
-
Irani Dhidi ya Magharibi: Kutoka Uzoefu wa Kihistoria Hadi Mapambano ya Kistaarabu ya Leo
Mkutano “Sisi na Magharibi katika Mitazamo na Fikra za Ayatullah Al-Udhma Sayyid Ali Khamenei” wafanyika Tehran.
-
Ayatollah Khamenei: Makubaliano ya Mabavu si Makubaliano, Bali ni Kulazimishwa — Iran Haitakubali Kulazimishwa
"Rais wa Marekani anasema anataka kufanya makubaliano na Iran; makubaliano ambayo matokeo yake yamepangwa tayari kwa njia ya vitisho na mabavu siyo makubaliano-bali ni kulazimishwa, na taifa la Iran halitakubali kulazimishwa.”
-
Ayatollah Khamenei Asifu Uwezo wa Makombora ya Iran, Asema Yameharibu Vituo Muhimu vya Utawala wa Kizayuni
Ayatollah Khamenei pia aliongeza kuwa utawala wa Kizayuni (Israel), ambao kwa muda mrefu umekuwa ukifanya vitisho na mashambulizi dhidi ya eneo hili la kikanda, sasa “umepokea funzo ambalo litabaki kwenye kumbukumbu zake,” akisisitiza kuwa taifa la Iran halitasita kujibu hatua yoyote ya uchokozi
-
Mwitikio Mkubwa wa Kauli za Kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu Duniani: “Kiongozi wa Iran amwambia Trump: Endelea Kuota!”
Ayatollah Khamenei, akimjibu Trump, amesema: “Uliota kuwa umeangamiza nguvu za nyuklia za Iran - basi endelea kuota!”
-
Kamanda Mkuu wa Majeshi ya Iran, Meja Jenerali Abdolrahim Mousavi:
“Vikosi vya Ulinzi vya Iran vimewapiga maadui zao Kofi lisilosahaulika”
Jenerali Mousavi alisema kuwa kipindi cha masomo ya kijeshi kwa wanafunzi hao kilitokea katika wakati wa kipekee - wakati ambao muqawama ulithibitisha ushindi wa imani juu ya dhulma na ubabe wa kimataifa.
-
Kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu amwambia Rais wa Marekani:
“Wewe ni nani hasa?”
Khamenei: "Rais wa Marekani alisafiri hadi Palestina iliyokaliwa kwa mabavu na kutoa maneno matupu yenye kejeli ili kuwatia moyo Wazayuni waliokata tamaa."
-
Ujumbe wa Kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu kwa Mkutano wa 32 wa Kitaifa wa Sala
Ayatollah Khamenei katika ujumbe wake kwa Mkutano wa 32 wa Kitaifa wa Sala alielezea mambo muhimu yanayohusu mkutano huu pamoja na sifa za sala.
-
Ayatollah Sayyid Yasin Musawi, Imamu wa Ijumaa Baghdad:
Jeshi la Muqawama chini ya Bendera ya Wilayat litaendeleza njia ya Shahidi Nasrallah | Umoja na utiifu kwa Kiongozi wa Kiislamu ni sharti la ushindi
Ayatollah Musawi alisisitiza kuwa jina “Nasrallah” lina mizizi katika nusra ya Mwenyezi Mungu, na historia ya mapambano imethibitisha kuwa licha ya gharama kubwa, irada ya umma kuendeleza njia ya mashahidi na kufikia ushindi haitadhoofika kamwe.