Ayatollah Khamenei
-
"Watu wenye busara wanaoijua Iran,watu wake na historia yake,hawazungumzi na taifa hili kwa lugha ya vitisho,kwa sababu taifa la Iran halisalimu amri"
"Wamarekani wanapaswa kufahamu kuwa aina yoyote ya uvamizi wa kijeshi kutoka kwao hakika itasababisha madhara yasiyoweza kufidiwa.”
-
Mikakati ya Imam Hadi (a.s) katika Kueneza Mtandao wa Shi'a na Kuimarisha Harakati za Kijamii
Shughuli za Imam Hadi (a.s) zilikuwa na nafasi muhimu katika kuhifadhi utambulisho wa kiakili na imani wa Waislamu wafuasi wa Madhehebu ya Shi'a Ithna Ashari. Uongozi wake wa kiroho na wa fikra kwa Shi'a waliokuwa Samarra, kuimarisha mtandao wa mawasiliano kati ya wafuasi wa Ahlul Bayt(as), na kusimama imara dhidi ya shinikizo la wa Abbasi, ni miongoni mwa huduma muhimu za Imamu Hadi katika maandalizi ya Shi'a kwa zama za Ghaibat Kubwa (Kutoonekana kwa Muda Mrefu).
-
Ujumbe wa Kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu kwa Mahujaji: "Ulimwengu wa Kiislamu wahitaji kutekeleza mafundisho ya Hija ili kusitisha maafa ya Gaza"
Ayatullah Ali Khamenei amesema kuwa Ulimwengu wa Kiislamu kwa sasa unayahitaji zaidi kuliko wakati mwingine wowote mafundisho ya Hija, na akibainisha kuwa Hija ya mwaka huu ni msimu wa pili unaofanyika sambamba na jinai za utawala wa Kizayuni huko Gaza, ameuliza swali lifuatalo:“Ni nani anapaswa kusimama dhidi ya janga hili la kibinadamu?” Kisha ameongeza kwa kusisitiza: “Bila shaka yoyote, serikali za Kiislamu ndizo zinazobeba wajibu wa kwanza wa jukumu hili, na mataifa ya Kiislamu yana haki ya kudai utekelezaji wa wajibu huo kutoka kwa serikali zao.”
-
Katika mkutano na maelfu ya wafanyakazi kutoka kote nchini:
Kiongozi wa Mapinduzi ametoa uungaji mkono kamili kwa jamii ya wafanyakazi / Fikira zisikengeushwe kutoka kwenye suala la Palestina
Ayatollah Khamenei pia alisisitiza kuwa, pamoja na kuendelea kwa jinai na mauaji ya kikatili dhidi ya watu wa Gaza na Palestina yanayofanywa na utawala wa Kizayuni kwa msaada wa Marekani na Uingereza, mataifa yanapaswa kusimama dhidi ya utawala wa Kizayuni na wafuasi wake, na wasiruhusu masuala yanayohusu Palestina kusahaulika.
-
Ujumbe wa Kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu kufuatia tukio la moto katika Bandari ya Shahid Rajaei, Bandar Abbas
Ayatollah Khamenei amewaombea Marehemu rehma na msamaha kutoka kwa Mwenyezi Mungu, na amewatakia familia za wahanga subira na utulivu wa moyo. Vilevile, amewaombea majeruhi wapate uponyaji wa haraka.
-
Waqfu wa Kiongozi wa Mapinduzi 5 / Mtoaji mkubwa wa Waqfu wa Nakala za Maandishi ya Kale katika historia ya Haram Tukufu ya Razavi
Kiongozi Mkuu wa Mapinduzi, pamoja na Waqfu mbalimbali alizotoa kwa Haram Tukufu ya Razavi katika zaidi ya miaka 40 iliyopita, ametoa waqfu wa vitabu vingi vya kale kuliko wakati mwingine wowote katika historia ya Haram Tukufu ya Razavi.
-
Kiongozi wa Mapinduzi: Uhusiano kati ya Iran na Saudi Arabia utakuwa wa manufaa kwa nchi zote mbili / Kupanua uhusiano kati ya nchi hizi 2 kuna maadui
Katika kikao hicho Ayatollah Khamenei akiashiria baadhi ya maendeleo ya Iran amesema: Jamhuri ya Kiislamu iko tayari kuisaidia Saudi Arabia katika maeneo hayo.
-
Adui amechanganyikiwa na ana hofu kuhusu maendeleo ya Jamhuri ya Kiislamu / Kudumisha utayari wa hali ya juu na uboreshaji wa maunzi na programu
Ayatullah Khamenei amehusisha hasira za watu wasio na mapenzi mema (wenye nia mbaya) na mabishano yao kwenye vyombo vyao vya habari kuwa ni kuzidisha maendeleo ya Iran na kusema: "Wanabainisha mambo (matakwa) ambayo ni sehemu ya matamanio yao kwa anuani kuwa ni habari na uhakika, na ni lazima kubuni njia za kukabiliana na dhana na propaganda hizi."
-
Kielezo cha Maandishi cha Hotuba ya Kiongozi wa Mapinduzi katika Khutba zake mbili za Sala ya Eid al-Fitr
Kiongozi Muadhamu alieleza msimamo wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran kuhusiana na vitisho vya maadui katika Khutba za Sala ya Eid al-Fitr.
-
Kiongozi wa Mapinduzi: Ikiwa Amerika itafanya jambo lolote ovu, litajibiwa vikali
Ayatollah Khamenei amesema kuhusu misimamo ya vitisho ya hivi karibuni ya Marekani: Kwanza, iwapo uovu utafanywa kutoka nje, jambo ambalo bila shaka halina uwezekano mkubwa, kwa hakika watajibiwa kwa kupigwa kwa pigo kali , na pili, ikiwa adui anafikiria kuzusha mpasuko (fitna) kwa ndani, kama ilivyokuwa katika baadhi ya miaka ya nyuma, Taifa litatoa jibu kali kwa waasi (wapenzi wa fitna) kama ilivyokuwa kwa miaka hiyo.
-
Kiongozi wa Mapinduzi: Maandamano ya Mwaka huu yatakuwa miongoni mwa Maandamano yenye Heshima Kubwa katika Siku ya Quds
Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu amesema: Mwenyezi Mungu akipenda (Insha Allah), Matembezi (Maandamano) ya Mwaka huu yatakuwa miongoni mwa Matembezi bora zaidi, Matukufu na yenye Heshima Kubwa katika Siku ya Quds.
-
Iran imeapa kutoa jibu "kali" ikiwa itawekewa tena vikwazo vya Magharibi kupitia Umoja wa Mataifa
Msemaji wa Shirika la Nishati ya Atomiki la Iran (AEOI) Behrouz Kamalvandi anasema kuhusu nchi za Magharibi: Iran imezionya nchi za Magharibi dhidi ya kichochezi cha "kidhalimu" cha "kuwekea kwa mara nyingine tena" vikwazo dhidi ya Jamhuri ya Kiislamu katika Umoja wa Mataifa, akisema kwamba Iran itatoa jibu kali la kutisha.
-
Wamarekani wanapaswa kujua: Vitisho havipeleki popote; Kofi kali la usoni ni jibu la uovu wowote
Ayatollah Khamenei amesisitiza kuwa, Wamarekani wanapaswa kujua kwamba kamwe hawatafika popote kwa vitisho dhidi ya Iran na akasema: Wao na wengine wanapaswa kujua kwamba iwapo watafanya jambo lolote ovu kwa Taifa la Iran, watapigwa kofi kali.
-
Ujumbe wa Nowruz wa Kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu kwa Mnasaba wa Mwaka Mpya
Mwaka 1404, ni Mwaka wa "Uwekezaji kwa ajili ya Uzalishaji"
Katika ujumbe wake kwa mnasaba wa mwanzo wa mwaka mpya wa 1404 Hijria Shamsia, Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu ameutaja mwaka mpya kuwa ni mwaka wa "Uwekezaji kwa ajili ya Uzalishaji".