25 Machi 2025 - 20:48
Iran imeapa kutoa jibu "kali" ikiwa itawekewa tena vikwazo vya Magharibi kupitia Umoja wa Mataifa

Msemaji wa Shirika la Nishati ya Atomiki la Iran (AEOI) Behrouz Kamalvandi anasema kuhusu nchi za Magharibi: Iran imezionya nchi za Magharibi dhidi ya kichochezi cha "kidhalimu" cha "kuwekea kwa mara nyingine tena" vikwazo dhidi ya Jamhuri ya Kiislamu katika Umoja wa Mataifa, akisema kwamba Iran itatoa jibu kali la kutisha.

Kwa mujibu wa Shirika la Habari la Kimataifa la Ahlul-Bayt (a.s) - ABNA-; Msemaji wa Shirika la Nishati ya Atomiki la Iran (AEOI) Behrouz Kamalvandi anasema kuhusu nchi za Magharibi: Iran imezionya nchi za Magharibi dhidi ya kichochezi cha "kidhalimu" cha "kuwekea kwa mara nyingine tena" vikwazo dhidi ya Jamhuri ya Kiislamu katika Umoja wa Mataifa, akisema kwamba Iran itatoa jibu kali la kutisha.

Onyo hilo la msemaji wa Shirika la Nishati ya Atomiki la Iran, Behrouz Kamalvandi la siku ya Jumanne limetolewa baada ya kuwepo kwa kauli za vitisho vya nchi za Magharibi kutaka kuamsha mfumo huo chini ya mapatano ya nyuklia ya mwaka 2015, yanayojulikana pia kama Mpango Kamili wa Utekelezaji wa Pamoja wa (JCPOA).

"Matumizi yasiyo ya haki ya "kichochezi" ikiwa yatafanyika, basi yatafuatiwa na jibu sahihi na kali kutoka kwa Iran," Kamalvani alisema.

Afisa huyo alisema kurejeshwa upya kwa vikwazo vya Umoja wa Mataifa kwa Iran kupitia utaratibu wa "kurudi kwa ghafla vikwazo hivyo" ni sehemu ya shinikizo la nchi za Magharibi kwa Iran kuhusu mpango wake wa amani wa nyuklia.

"Moja ya njia za shinikizo ambazo nchi za Magharibi zinazungumza siku hizi ni matumizi ya njia ya kufyatua kitufe cha kichochezi. Ni ujinga wa kweli kwamba wanataka kuiadhibu Iran kwa ukiukaji ambao ulifanywa na wengine," alisema.

Kujiondoa kwa Washington katika JCPOA mwaka 2018 na kushindwa kwa Wazungu kama washiriki wa makubaliano ya kuilinda Iran dhidi ya vikwazo vya upande mmoja vya Marekani kulipuuza ahadi ya mapatano hayo ya kuhalalisha fedha kwa ajili ya Iran, na kuleta madhara makubwa kwa uchumi wake na watu wake.

Kutokana na hali hiyo, Tehran ilianza kupunguza ahadi zake chini ya JCPOA katika mfululizo wa hatua zilizotangazwa kabla na za wazi baada ya mwaka mmoja wa kusubiri watia saini wengine wa mapatano hayo kuilipa Iran fidia.

"Kama wangetekeleza ahadi zao na vikwazo vingeondolewa, na kama Marekani isingejitoa katika JCPOA, kwa kawaida Iran ingetekeleza ahadi zake," Kamalvandi alisema.

"Ikiwa Iran imesimamisha ahadi zake, ni kwa sababu imeona hainufaiki na kanuni ya jumla ya makubaliano."  

Kamalvani alipuuzilia mbali "urudishaji wa ghafla" wa vikwazo vya Umoja wa Mataifa kwa Iran na kuvitaja kuwa ni "tishio hewa na tupu".

"Jamhuri ya Kiislamu ya Iran inauchukulia mfumo wa kichochezi kama chombo cha mashinikizo kama vile vitisho vingine vya kiuchumi na kijeshi na bila shaka Iran itasimama kidete dhidi yao na kutetea haki za nchi," alisema.

Iran imeapa kutoa jibu "kali" ikiwa itawekewa tena vikwazo vya Magharibi kupitia Umoja wa Mataifa

Iran yaionya E3 dhidi ya matumizi mabaya ya mfumo wa "snapback" wa JCPOA
Iran imetahadharisha kuwa, kitendo kinachoitwa upuuzaji wa wanachama watatu wa Ulaya katika Mpango Kamili wa Utekelezaji wa Pamoja wa JCPOA, kutapatiwa majibu madhubuti na sawia.

Iran, Kamalvandi alisema, daima iko tayari kwa ushirikiano, lakini haikubali shinikizo kwa hali yoyote.

"Sera za jumla za nchi yetu zimeainishwa na Kiongozi Mkuu wa Mapinduzi, na kwa kawaida, tunafuata masilahi ya nchi ndani ya mfumo wa sera hizo," aliongeza.

Kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu Ayatollah Sayyid Ali Khamenei siku ya Ijumaa alisema vitisho vya nchi za Magharibi "havitavifikisha popote," akionya juu ya kutoa hatua za kuafikiana sawia na vitendo vyao "ikiwa watafanya jambo lolote baya" dhidi ya Iran.

Tags

Your Comment

You are replying to: .
captcha