Umoja wa mataifa
-
Balozi wa Iran katika Umoja wa Mataifa Aitaka Baraza la Usalama Kuepuka Hatua za Uchochezi
Mwakilishi wa Kudumu wa Iran katika Umoja wa Mataifa, Amir Saeid Iravani, amesema Baraza la Usalama linapaswa kuunga mkono diplomasia na kuepuka hatua zinazoweza kuchochea mvutano au kudhoofisha mazungumzo yanayoendelea.
-
Balozi wa Iran katika Umoja wa Mataifa: Hatutawahi Kusalimu Amri kwa Vitisho wala Mashinikizo
Balozi wa Kudumu wa Iran katika Umoja wa Mataifa amesema Jamhuri ya Kiislamu ya Iran haitawahi kusalimu amri mbele ya vitisho, mashinikizo au vitendo vya kutisha kutoka nje, akisisitiza kuwa taifa hilo litaendelea kulinda uhuru na haki zake kwa uthabiti.
-
Iran: Mfumo wa Sasa wa Utawala wa Dunia Unakabiliwa na Mgogoro wa Imani na Uhalali
Balozi wa Iran katika Umoja wa Mataifa amesema jamii ya kimataifa inashuhudia kuongezeka kwa migogoro, ukosefu wa usawa na kudhoofika kwa diplomasia, huku akisisitiza umuhimu wa kuheshimu sheria za kimataifa na kuimarisha ushirikiano wa kweli wa kimataifa.
-
Somalia Yasisitiza Umoja wa Kitaifa na kwamba Ukamilifu wa Ardhi na Mamlaka ya Taifa Lake Haviwezi Kugawanyika
Balozi wa Somalia katika Umoja wa Mataifa amesisitiza kuwa ukamilifu wa ardhi na mamlaka ya taifa la Somalia hauwezi kugawanywa, akieleza vipaumbele vya urais wa Somalia wa Baraza la Usalama Januari 2026 na kukataa vikali hatua zozote zinazolenga kudhoofisha umoja wa nchi hiyo.
-
Kinyume na madai ya Taliban; Umoja wa Mataifa waripoti kuongezeka kwa shughuli za ISIS nchini Afghanistan
Umoja wa Mataifa katika tathmini yake ya hivi karibuni ya kiusalama umetangaza kuwa ISIS Khorasan, kinyume na madai ya Taliban, si tu kwamba haijadhibitiwa, bali kwa kubadili mbinu na kuvutia wapiganaji wapya, imepanua shughuli zake hadi katika miji mikubwa ya Afghanistan.
-
Malta Yaitambua Rasmi Palestina
Malta imetangaza kuwa leo itaikubali rasmi Palestina kama taifa huru.
-
Zaidi ya Wanawake na Wasichana 1,000 Wafariki Katika Tetemeko la Ardhi Mashariki mwa Afghanistan
UN: Wanawake na Wasichana 1,025 Wamefariki Katika Tetemeko la Ardhi Mashariki mwa Afghanistan. Ofisi ya Kuratibu Misaada ya Kibinadamu ya Umoja wa Mataifa (OCHA) nchini Afghanistan imetangaza kuwa: Jumla ya wanawake na wasichana 1,025 wamepoteza maisha kutokana na tetemeko la ardhi lililotokea katika maeneo ya mashariki mwa Afghanistan. Taarifa hiyo inasisitiza ukubwa wa athari za kibinadamu, hasa kwa wanawake na watoto, katika tukio hili la maafa ya asili.
-
Macron: Kuzuia Palestina Kushiriki Mkutano wa Umoja wa Mataifa ni Kitendo Kisichokubalika
Rais wa Ufaransa, Emmanuel Macron, amelaani uamuzi wa Marekani wa kutowapa viza maafisa wa Palestina kwa ajili ya kushiriki katika mikutano ijayo ya Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa, akisema kuwa kitendo hicho hakikubaliki kabisa.
-
Kiongozi wa Baraza la Maulamaa wa Kishia Pakistan: Suluhisho la Kashmir ni Sharti la Amani ya Kudumu katika Ukanda huu
Kiongozi wa Baraza la Maulamaa wa Kishia Pakistan ameeleza kuwa: > “Hadi pale ambapo suala la Kashmir halitatatuliwa kwa mujibu wa maazimio ya Umoja wa Mataifa, kufanikisha amani ya kudumu katika ukanda huu kutabaki kuwa ni ndoto ya mchana (serabu) tu.”