6 Agosti 2025 - 23:17
Kiongozi wa Baraza la Maulamaa wa Kishia Pakistan: Suluhisho la Kashmir ni Sharti la Amani ya Kudumu katika Ukanda huu

Kiongozi wa Baraza la Maulamaa wa Kishia Pakistan ameeleza kuwa: > “Hadi pale ambapo suala la Kashmir halitatatuliwa kwa mujibu wa maazimio ya Umoja wa Mataifa, kufanikisha amani ya kudumu katika ukanda huu kutabaki kuwa ni ndoto ya mchana (serabu) tu.”

Shirika la Habari la Kimataifa la Ahlul-Bayt (as) –ABNA– Kiongozi Mkuu wa Baraza la Maulamaa wa Kishia nchini Pakistan, Ayatollah Sayyid Sajid Ali Naqvi, amesema kuwa kufanikisha amani ya kweli na ya kudumu katika Asia ya Kusini hakutawezekana bila kutatuliwa kwa suala la Kashmir kwa mujibu wa maazimio ya Umoja wa Mataifa.

Katika taarifa yake, Ayatollah Naqvi alibainisha kuwa Kashmir ni sehemu isiyokamilika ya mgawanyo wa kihistoria kati ya India na Pakistan, na kwamba mpaka suala hili litakapotatuliwa, amani ya kweli itaendelea kuwa ndoto isiyofikiwa.

Kashmir ni Mgogoro wa Kimataifa

Kiongozi huyo alisisitiza kuwa eneo la Kashmir ni eneo lenye mgogoro wa kimataifa, na njia pekee ya haki ya kulitatua ni kutekelezwa kwa maazimio ya Umoja wa Mataifa pamoja na kusikiliza matakwa ya watu wa Kashmir.

Ayatollah Naqvi aliongeza kuwa kuingiza Kashmir ndani ya mipaka ya India ni kitendo kilicho kinyume na sheria za kimataifa, Mkataba wa Geneva, na maazimio ya Umoja wa Mataifa, hivyo hakuna uhalali wowote wa hatua hiyo.
India Yenyewe Iliwasilisha Suala Hilo Umoja wa Mataifa

Akikumbusha historia ya suala hilo, alieleza kuwa India yenyewe ndiyo iliyowasilisha suala la Kashmir kwa Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa, na kwa msingi huo, maazimio kadhaa yalipitishwa. Licha ya kupita kwa zaidi ya miaka sabini, maazimio hayo bado yako mezani, jambo linaloonesha kuwa hali ya utata na mzozo bado inaendelea.

Umoja wa Mataifa Ulitaka Kura ya Maoni

Ayatollah Naqvi alifafanua kuwa Umoja wa Mataifa, tangu mwaka 1948, uliamuru kusitishwa kwa mapigano katika eneo la Kashmir na kutaka kura ya maoni ifanyike ili watu wa Kashmir waamue hatima yao. Hata hivyo, alieleza kwa masikitiko kuwa India bado inaendelea na uvamizi wa kijeshi kinyume na sheria.

Kura ya Maoni Ndiyo Suluhisho Pekee

Kwa mujibu wa Ayatollah Naqvi, kura ya maoni kwa mujibu wa maazimio ya Umoja wa Mataifa ndiyo suluhisho la kweli na la kudumu kwa mzozo wa Kashmir. Aliongeza kuwa watu wa Pakistan wanaunga mkono kwa hali zote — kisiasa, kimaadili na kidiplomasia — haki ya watu wa Kashmir kuamua mustakabali wao.

Tags

Your Comment

You are replying to: .
captcha