Kiongozi
-
Tarehe 13 Rajab: Maadhimisho ya Kuzaliwa kwa Kiongozi Mkuu wa Umma, Imam Ali (a.s)
Tarehe 13 ya mwezi wa Rajab ni siku ya kuzaliwa kwa Imam Ali (a.s), kiongozi mkuu baada ya Mtume Muhammad (s.a.w.w), ambaye ni mtu pekee aliyezaliwa ndani ya Al-Kaaba Tukufu na anayetambuliwa kwa elimu, uadilifu, ujasiri na maadili mema kwa wanadamu wote.
-
Marekani na Israel Baada ya Kushindwa katika Vita vya Siku 12; Wanajaribu Kuchochea Ghasia Nchini Iran / Vyombo vya Habari Vihangaike Kutoa Ukweli
Baada ya kushindwa katika vita vya siku 12, Marekani na Israel wanajaribu kuhamishia shinikizo ndani ya Iran kwa kuchochea ghasia za kiuchumi na kijamii; wachambuzi wakisisitiza umuhimu wa vyombo vya habari kusambaza ukweli na kutofautisha kati ya madai halali na machafuko.
-
Vitisho vya Trump dhidi ya Iran Vinatokana na Kukata Tamaa: IRGC
IRGC imesema vitisho vya Rais wa Marekani Donald Trump dhidi ya Iran vinatokana na kukata tamaa baada ya kushindwa kuishinikiza Iran, ikisisitiza utii wake kwa Kiongozi wa Mapinduzi Ayatollah Ali Khamenei na kuendelea kulinda taifa la Iran na kuimarisha njia ya Shahidi Qassem Soleimani katika Mhimili wa Upinzani.
-
Kiongozi Mkuu wa Wahouthi: Hatutakubali Israel kutumia ardhi ya Somalia kama kambi ya kijeshi
Ikumbukwe kuwa, moja ya sababu kuu zinazotajwa katika hatua ya Israel kuitambua Somaliland ni nafasi ya kijiografia ya eneo hilo, ambayo inaonekana kuwa na umuhimu wa kimkakati kwa Israel katika kuendesha mashambulizi dhidi ya Wahouthi wa Yemen.
-
Burkina Faso, Mali na Niger Zazindua Operesheni ya Pamoja ya Kijeshi Dhidi ya Makundi ya Kijihadi
Kiongozi wa mpito wa Burkina Faso, Ibrahim Traoré, ametangaza kuanza kwa hatua mpya za kijeshi katika eneo la Sahel baada ya nchi yake, kwa kushirikiana na Mali na Niger, kuzindua operesheni ya pamoja inayolenga kukabiliana na makundi ya kijihadi yanayohusishwa na Al-Qaeda na ISIS. Hatua hiyo inakuja katika muktadha wa kuimarishwa kwa muungano wa kijeshi wa nchi hizo tatu, huku zikisisitiza mshikamano wa kiusalama na mwelekeo mpya wa ushirikiano wa kikanda kufuatia kujiondoa kwao katika ECOWAS na kuvunja ushirikiano wa awali na Ufaransa na Marekani.
-
Sayyid Sajid Ali Naqvi: Ni kwa kutekeleza fikra za “Qaid-e-Azam” pekee ndipo mustakabali wa Pakistan unaweza kuwa salama
“Muhammad Ali Jinnah alipigania kwa juhudi zisizochoka, uaminifu na busara ya kisiasa ili kuanzisha nchi huru, inayojitegemea na yenye misingi ya kiitikadi; na leo jukumu la kulinda usalama, uthabiti na uhai wa nchi hii halipo tu juu ya serikali, bali pia juu ya kila raia.”
-
Habari Kuhusu Makubaliano ya “Mfumo wa Uratibu wa Vyama vya Kishia Iraq” Juu ya Mgombea wa Uwaziri Mkuu
Vyanzo vya kisiasa vya Iraq vimeripoti kuwepo kwa makubaliano ya awali miongoni mwa vyama vinavyounda muungano wa “Mfumo wa Uratibu wa Vyama vya Kishia Iraq” kuhusu uteuzi wa mgombea wa kuongoza serikali ijayo ya nchi hiyo.
-
Tamko la Mkurugenzi Mkuu wa Hawza za Kiislamu Kufuatia Mauaji ya Kinyama Dhidi ya Watu Wanyonge wa Sudan
Jumuiya za Kimataifa na Mashirika ya Haki za Binadamu Waitikie Kilio cha Watu Wanaodhulumiwa Sudan
-
Mwakilishi wa Waliyyul-Faqih katika Jeshi la Kikomando la Sepah:
"Vitisho vimegeuzwa kuwa fursa ya kuimarisha mamlaka ya mfumo”
Mwakilishi wa Kaimu wa Kiongozi wa Mapokeo katika Jeshi la Kikomando alisema kuwa Mungu hubadilisha vitisho kuwa fursa ya kuimarisha mamlaka ya mfumo. Aliongeza kuwa: “Dushmani katika vita vya siku 12, licha ya kuwa na rasilimali nyingi, ilipigwa na hatimaye ilishindwa na kuomba kurudi nyuma; lakini katika vita vya kiakili bado haijatangaza mapumziko ya silaha.”
-
Tone kutoka Nahjul-Balagha 27 | Kuheshimu Hadhi ya Imamu ni Nini?
Matokeo ya utiifu ni nini?. Amirul-Mu’minin Ali bin Abi Talib (AS) katika khutba ya 156 anasema: «إِنْ أَطَعْتُمُونِی فَإِنِّی حَامِلُکُمْ إِنْ شَاءَ اللَّهُ عَلَی سَبِیلِ الْجَنَّةِ» Yaani: “Mkinitii mimi – mimi kama Imamu– bila shaka nitawaongoza katika njia ya Peponi"
-
Shukrani za Ayatollah Nouri Hamadani kwa jitihada za Ofisi ya Vikundi vya Misikiti katika shughuli za Qur’an / Ihitaji uwepo mkubwa zaidi wa vijana katika Misikiti.
Kiongozi wa kiitikadi wa Mashia alisema kuwa: ‘Msikiti usio na vijana hauwezi kustawi, na uwepo wa vijana katika misikiti ni wa thamani sana.’ Alisisitiza: ‘Ninashukuru na kupongeza jitihada za Vikundi vya Utamaduni na Sanaa vya Misikiti katika shughuli za Qur’an na uhai wa misikiti, na nina matumaini uwepo wa vijana katika misikiti utakuwa mkubwa zaidi.
-
Kiongozi wa Harakati ya Hamas: Ghaza imejeruhiwa lakini imebaki yenye nguvu; Ummah wa Kiarabu unapaswa kuimarisha uwezo wake wa upinzani
Kiongozi wa Harakati ya Hamas, katika Ukanda wa Ghaza, katika Kongresi ya 34 ya Taifa ya Kiarabu huko Beirut, alieleza kuwa Operesheni “Tofaan Al-Aqsa / Kimbunga cha Al-Aqsa” ilikuwa jibu kwa juhudi za kuondoa suala la Palestina na kubuni Mashariki ya Kati mpya, na alisisitiza uhitaji wa kuimarisha uwezo wa upinzani.
-
Imam Khamenei: Uhasama kati ya Iran na Marekani ni wa asili, ni mgongano wa maslahi kati ya mitindo miwili
Hivi karibuni kabla ya tarehe 4 Novemba, inayojulikana kama “Siku ya Wanafunzi na Siku ya Kitaifa ya Kupambana na Ukorofi wa Kidunia”, Imam Khamenei, Kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu, alikutana na wanafunzi wa rika zote, wakiwemo wanafunzi wa vyuo vikuu, pamoja na familia za mashahidi wa Vita vya Siku 12 Vilivyowekezwa"
-
Ayatullah Javadi Amoli alisema:
“Iwapo kitovu cha mgawanyiko kitaundwa kati ya taifa na serikali, msingi wa mfumo utadhurika”
Mmoja wa maraji wa juu wa Washia alisema: “Iwapo kitovu cha mgawanyiko kitaibuka kati ya serikali na taifa, msingi wa mfumo utadhurika. Iwapo kiongozi atakuwa na wavurugiko kati ya matakwa yake ya kimaakili na tamaa za nafsi, ataondoka mbali na haki.”
-
Israeli imeshindwa katika vita vya Gaza - Kiongozi wa Shia Pakistan
Mmoja wa viongozi wakuu wa Majlis-e Wahdat-e Muslimeen (Bodi ya Muungano wa Waislamu) wa Pakistan, amesema kuwa Israeli imepoteza vita hii na kwamba wanamaji (mujahideen) wa Gaza na Palestina wameifungisha vita kwa ushindi. Aliongeza kwamba hatimaye Israeli italazimika kuondoa ukoloni wake wa dhulma wa Palestina.
-
Kulaaniwa Vikali Shambulio Dhidi ya Katibu Mkuu wa Baraza la Wanazuoni wa Kiislamu wa India katika Mkutano wa Maandamano Mjini Lucknow
Hujjatul-Islam Muhammad Miyan Abidi Qummi: "Lengo kuu la mashambulio kama haya,” alisema, “ni kudhoofisha harakati ya ulinzi wa wakfu na kunyamazisha sauti ya wanaotetea haki.”
-
Mwitikio Mkubwa wa Kauli za Kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu Duniani: “Kiongozi wa Iran amwambia Trump: Endelea Kuota!”
Ayatollah Khamenei, akimjibu Trump, amesema: “Uliota kuwa umeangamiza nguvu za nyuklia za Iran - basi endelea kuota!”
-
Kiongozi Mkuu wa Mapinduzi ya Kiislamu:“Wazayuni hawakutarajia nguvu ya makombora ya Iran / Marekani haina haki kujihusisha na teknolojia ya Iran"
Ayatollah Sayyid Ali Khamenei amebainisha kwamba: Marekani haina haki kujihusisha na suala la teknolojia ya nyuklia ya Iran - na akahoji kuhusiana na Trump akisema: Wewe ni nani hasa?”.
-
Kenya yaomboleza kifo cha Waziri Mkuu wa zamani Raila Odinga | Aagwa kwa Heshima Bungeni
Kifo cha Raila kimeacha pengo kubwa katika historia ya kisiasa ya Kenya, na atakumbukwa kama shujaa wa mageuzi na demokrasia nchini humo.
-
Chuo cha Al-Mustafa (s) - Tanzania Kimeandaa Kongamano la Kielimu Kuhusu Ustaarabu wa Magharibi na Mikakati yake ya Kikoloni
Ustaarabu wa Magharibi na misingi ya kuuelewa ipasavyo.
-
Maoni ya Velayati Kuhusu Kusitisha Mapigano (Vita) Huko Ghaza
Mshauri wa Kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu ameandika akirejea kusitishwa kwa mapigano huko Ghaza kwamba: “Kuanza kwa kusitishwa mapigano huko Ghaza kunaweza kuwa nyuma ya pazia la kumalizika kwa kusitishwa mapigano mahali pengine.”
-
Ayatollah Sayyid Yasin Musawi, Imamu wa Ijumaa Baghdad:
Jeshi la Muqawama chini ya Bendera ya Wilayat litaendeleza njia ya Shahidi Nasrallah | Umoja na utiifu kwa Kiongozi wa Kiislamu ni sharti la ushindi
Ayatollah Musawi alisisitiza kuwa jina “Nasrallah” lina mizizi katika nusra ya Mwenyezi Mungu, na historia ya mapambano imethibitisha kuwa licha ya gharama kubwa, irada ya umma kuendeleza njia ya mashahidi na kufikia ushindi haitadhoofika kamwe.
-
Kiongozi wa kidini wa Waislamu wa Sunni nchini Afghanistan;
Amekosoa sera za Taliban dhidi ya wanawake, akisema: «Mwanamke ni shujaa na ndiye anayezalisha mashujaa wengine»
Hali ilivyo sasa ambapo Taliban nchini Afghanistan wamepunguza haki za wanawake na wasichana kuhusiana na elimu, kazi, na ushiriki katika jamii, kiongozi mmoja wa dini wa Sunni amekosoa waziwazi sera za kutozingatia wanawake za Taliban katika hotuba yake ya umma.
-
Ujumbe wa Kiongozi wa Mapinduzi kwa mnasaba wa Wiki ya Utetezi Mtakatifu:
"Ushahidi (shahada) ni thawabu ya jitihada za jihadi; iwe katika utetezi wa miaka 8, au katika mapambano ya kishujaa ya siku 12"
Kiongozi Mkuu wa Mapinduzi ya Kiislamu, katika ujumbe wake kwa mnasaba wa Wiki ya Utetezi Mtakatifu, aliitaja shahada kuwa ni thawabu ya juhudi za jihadi, na alisisitiza juu ya umuhimu wa kujitolea huku katika kukuza mataifa. Vilevile, alieleza yakini yake juu ya ushindi wa haki na umuhimu wa kushikamana na majukumu ya kidini.
-
Hekalu la Chini ya Ardhi’ limechapishwa kwa Kiarabu
Katika Muktadha wa Wiki ya Utetezi Mtakatifu (Sacred Defence), tafsiri ya Kiarabu ya kitabu “Hekalu ya Chini ya Ardhi” kilichoandikwa na Ma‘sumeh Mirabutalebi, ambacho kimepambwa na (maoni ya kupongeza) ya Kiongozi Mkuu wa Mapinduzi ya Kiislamu (Ayatollah Khamenei), kimechapishwa na Dar Tamkin nchini Iraq.
-
Kiongozi wa Mapinduzi atazungumza na wananchi usiku wa leo
Sambamba na Wiki Takatifu ya Ulinzi (au Wiki ya Utetezi Mtukufu - Sacred Defence), Ayatollah Khamenei atazungumza na Wananchi wa Iran na Ulimwengu mzima Usiku wa leo akidadavua masuala mbalimbali ya kitaifa na kimataifa.
-
Kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu ameipongeza timu ya taifa ya Iran ya mieleka ya Greco-Roman kwa ushindi wao wa ubingwa wa dunia
Hii ni mara ya kwanza katika historia ya michezo ya nchi yetu ambapo Timu ya Taifa ya mieleka ya “freestyle” na “Greco-Roman” zimefanikiwa kwa pamoja kutwaa ubingwa wa dunia katika mashindano moja.
-
Hasira ya Viongozi wa Kizayuni Kufuatia Hatua ya Uingereza, Australia na Canada Kutambua Nchi ya Palestina
Hatua ya nchi tatu — Uingereza, Australia na Canada — kutambua rasmi nchi huru ya Palestina, imeibua hasira na ghadhabu kubwa miongoni mwa viongozi wa utawala wa Kizayuni.
-
Uteuzi wa Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Kimataifa ya Ahlul-Bayt(a.s) kwa amri ya Kiongozi Mkuu wa Mapinduzi
Kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu Ayatollah Khamenei; Amemteua Hujjatul-Islam wal-Muslimin Ramezani kuwa Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Kimataifa ya Ahlul-Bayt(as) kwa muhula mwingine tena.
-
Msingi wa Imam Mahdi (AF) Mkoa wa Qom Watangaza Mpango wa Kipekee kwa Maadhimisho ya Kuanza kwa Uimamu wa Imam Mahdi (AF)
Hii ni miaka 1187 tangu Imam Mahdi (AF) aingie katika kipindi cha Ghaiba Kubwa. Tukio hili ni fursa ya kuhuisha upendo wetu kwake, na kuonyesha kuwa taifa la Iran, hasa Qom, linasimama imara katika njia ya Imam wa Zama."