Kiongozi
-
Kiongozi wa Iran: Wageni wa Kigeni Wanaofanya Uvamizi Ghuba ya Uajemi Hawana Mahali Isipokuwa Chini ya Maji Yake
Kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu amesema kuwa wageni kutoka maelfu ya kilomita mbali wanaoingilia na kufanya vitendo vya uchokozi katika Ghuba ya Uajemi hawana nafasi katika eneo hilo, isipokuwa chini ya maji yake. Kauli hiyo ilitolewa katika ujumbe wake wa kuadhimisha Siku ya Kitaifa ya Ghuba ya Uajemi.
-
Wizara ya Ulinzi Iran: Tutaendelea kwa nguvu na njia ya Kiongozi Shahidi katika kujenga uwezo wa ulinzi wa taifa
Wizara ya Ulinzi ya Iran imesisitiza kuendelea kuimarisha uwezo wa ulinzi wa nchi, kwa kuendeleza njia iliyowekwa na Kiongozi Shahidi wa Mapinduzi ya Kiislamu, huku ikisisitiza kujitegemea na kutumia uwezo wa vijana, wanasayansi na wataalamu wa Iran.
-
Balozi wa Iran: Fidel Castro ni ishara ya utashi wa taifa lililochagua kuishi kwa uhuru na kujitegemea
Balozi wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran nchini Mexico, Abolfazl Besandideh, amesema Fidel Castro hakuwa tu kiongozi wa kisiasa wa Cuba, bali aligeuka kuwa alama ya kimataifa ya mapambano ya watu wanaotetea uhuru, mamlaka ya kitaifa na kujitawala bila kuingiliwa na nguvu za nje.
-
Nablus Yapokea Kongamano na Kikao cha Kumuenzi Kiongozi wa Iran
Kongamano na kikao cha kumbukumbu kilifanyika katika mji wa Nablus, Ukingo wa Magharibi, kwa ushiriki wa wanaharakati wa utamaduni na vyombo vya habari, ambapo washiriki walijadili mchango wa Kiongozi wa Iran katika siasa za kikanda na msimamo kuhusu Palestina.
-
Kiongozi wa Yemen: Kulengwa kwa Meli ya Saudi Kumeimarisha Mlingano wa "Mzingiro kwa Mzingiro"
Mjumbe wa Baraza Kuu la Kisiasa la Yemen, Abdulaziz bin Habtour, amesema operesheni ya vikosi vya Yemen dhidi ya meli ya Saudi Arabia imethibitisha kuwa njia mbadala za kukwepa hatua zilizotangazwa na Yemen hazina usalama tena.
-
Waziri wa Sayansi wa Iran Aagiza Kuandaliwa Mikutano ya Kisayansi Kuhusu Fikra za Kiongozi Shahidi wa Mapinduzi ya Kiislamu
Waziri wa Sayansi, Utafiti na Teknolojia wa Iran amesisitiza umuhimu wa kuandaa makongamano ya kisayansi ya kitaifa na kimataifa kuhusu fikra za Kiongozi Shahidi wa Mapinduzi ya Kiislamu, sambamba na kuendeleza sera za sayansi na teknolojia nchini.
-
Hezbollah Yatuma Ujumbe wa Utii na Uungaji Mkono kwa Kiongozi Mkuu wa Iran
Hezbollah - Muqawama wa Kiislamu nchini Lebanon — imemtumia ujumbe Ayatullah Sayyid Mojtaba Khamenei, ikimpongeza kwa kuuawa shahidi kwa baba yake, Ayatullah Sayyid Ali Khamenei, na kutangaza kumpa kiapo cha utii pamoja na kuahidi kuendelea na njia ya muqawama, jihadi na kujitolea chini ya uongozi wake.
-
Mohammad Mokhber: Trump anapozidisha makelele na kelele, hiyo ni dalili ya kushindwa kwake
Mohammad Mokhber, Mshauri wa Kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu, amesema kuwa vitisho vya Donald Trump vinatokana na kipigo alichopokea kutoka kwa Iran, akisisitiza kuwa wapiganaji wa Iran, kwa kutegemea uungaji mkono wa wananchi, watampiga Trump pigo la mwisho na kumweka katika mipaka yake.
-
Kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu: Kumuaga Shahidi Mkuu wa Iran Kulikuwa Tukio la Kihistoria na Mwamko Mkubwa Usio na Mfano
Kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu amepongeza wananchi wa Iran kwa kuandaa tukio kubwa la kihistoria la kumuaga shahidi mkuu wa Iran, akisema kuwa ushiriki wa makumi ya mamilioni ya wananchi umeonesha kiwango kipya cha utambulisho wa Kiislamu na Kiirani, uaminifu, uelewa na upendo mkubwa kwa kiongozi wa Umma wa Kiislamu na kiongozi shahidi wa Mapinduzi.
-
Bayani / Taarifa ya Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Kimataifa ya Ahlul-Bayt (as):
Kuuawa Shahidi kwa Kiongozi Mkuu wa Waislamu kulikuwa Mwanzo wa Biitha Mpya ya watu wa Iran na Umma wa Kiislamu
Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Kimataifa ya Ahlul-Bayt (as), akitoa taarifa kwa mnasaba wa kuuawa na kuzikwa kwa Kiongozi Shahidi wa Mapinduzi ya Kiislamu, amelitaja tukio hilo kuwa ni msiba usioweza kurekebishwa kwa Uislamu, Taifa la Iran na Umma wa Kiislamu, na ameielezea safari ya kihistoria ya kuaga ya makumi ya mamilioni ya watu katika miji mitano ya nchi mbili kuwa ni ishara ya “Biitha mpya ya umma” na azma ya Waislamu ya kuendeleza mapambano dhidi ya ubeberu na utawala wa Kizayuni chini ya uongozi wa mrithi mwema wa Kiongozi huyo.
-
Meya wa Tehran: Trump hatakuwa salama popote duniani baada ya mauaji ya Kiongozi wa Iran
Meya wa Tehran, Alireza Zakani, amesema kuwa wale wanaohusika na kuuawa kwa Kiongozi Mkuu wa Iran, Ayatullah Sayyid Ali Khamenei, watakabiliwa na hatua za kulipiza kisasi, akisema kuwa Rais wa Marekani Donald Trump "hatakuwa salama popote duniani."
-
Kumbukumbu ya Shahidi Sayyid Ali Khamenei | Ikhlasi kwa Mwenyezi Mungu Ndiyo Siri ya Athari ya Kudumu
Ujumbe huu unaotolewa katika mnasaba wa kumbukumbu ya Shahidi Ali Khamenei unasema hivi kuwa "Ikhlasi kwa Mwenyezi Mungu ndiyo msingi wa kudumu kwa matendo mema", huku ukisisitiza kwamba athari ya kweli huzaliwa na nia safi ya kumtumikia Allah (swt).
-
Ayatullah Mujtaba al-Husseini Khamenei: Shahidi Aliishi na Kupigania Njia ya Imam Hussein (AS)
Ayatullah Sayyid Mujtaba al-Husseini Khamenei amesema kuwa kiongozi shahidi aliishi, akafikiri, akapambana na hatimaye akapata shahada kwa kufuata kwa dhati njia na mafundisho ya Imam Hussein (AS).
-
Balozi Mdogo wa Iraq nchini Iran: Kuuawa Shahidi kwa Ayatullah Khamenei ni Msiba Unaouhuzunisha Ulimwengu wa Kiislamu
Balozi Mdogo wa Iraq nchini Iran, Athir Al-Abadi, amesema kuuawa shahidi kwa Ayatullah al-Udhma Sayyid Ali Khamenei ni pigo kubwa kwa Umma wa Kiislamu, akimtaja kuwa kiongozi aliyelitumikia dini ya Uislamu kwa kujitolea na kutetea maadili na misingi ya haki.
-
Kiongozi wa Mapinduzi: Kulipiza kisasi hakutategemea uwepo wangu au wa viongozi wengine
Kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu amesema kuwa kuwawajibisha waliohusika na mauaji ya Kiongozi Shahidi ni jambo ambalo litaendelea bila kutegemea uwepo wake binafsi au wa viongozi wengine, akisisitiza kuwa watu huru duniani watatekeleza wajibu wao kwa wakati wake.
-
Ayatollah Araki Akihutubia Vijana Duniani:
“Kumwaga damu ya Trump, Netanyahu na washirika wao ni ‘wajibu’; vijana wenye ari duniani kote watekeleze hukumu ya Mwenyezi Mungu”
Ayatollah Araki amesisitiza kwamba: “Ujumbe wa Kiongozi Mkuu na mpendwa kuhusu kulipiza damu ya Imam shahidi na mashahidi wote ni amri ya ‘wajibu wa kutii’. Na kwa wale wote wanaoweza kwa namna yoyote kuchangia katika kutekelezwa kwa jambo hilo, ni wajibu kuchukua hatua zinazohitajika haraka.”
-
Ayatollah Khatami: Trump na Netanyahu Hawatakuwa na Usingizi wa Amani
Mwanachama wa Jumuiya ya Walimu wa Hawza ya Elimu ya Kiislamu ya Qom amesema kuwa ibada za mazishi ya Kiongozi aliyefariki akiwa shahidi katika maeneo mbalimbali ya nchi zimegeuka kuwa jukwaa la umoja, mshikamano na kuhuisha ahadi ya utii kwa Mapinduzi ya Kiislamu. Amesisitiza kwamba: “Trump na Netanyahu hawatakuwa na usingizi wa amani.”
-
Chuo cha Al-Mustafa (s) Tanzania Kuaandaa Kongamano la Kielimu Kumuenzi Imam Shahidi Sayyid Ali Khamenei(ra)
Kitengo cha Utafiti wa Kisayansi cha Chuo Kikuu cha Al-Mustafa (s) Tawi la Dar es Salaam - Tanzania kitaandaa Kongamano la Kielimu lenye anuani "Imam Khamenei: Kutoka Jihadi hadi Ushahidi," likiwa na lengo la kuchambua kwa ufupi Maisha ya Kiongozi huyo wa Mapinduzi ya Kiislamu, na hatimaye kukuachia msikilizaji na mfuatiliaji Nafasi ya kupata mazingitio na masomo mbalimbali ya kimaisha kutoka katika kumbukumbu ya Maisha yake Matukufu, katika muktadha ule ule wa Maelekezo ya Qur'an Tukufu aliposema Mwenyezi Mungu: Hakika kuna mazingatio ndani ya visa vyao (Historia Yao) kwa watu wenye Akili"
-
Makamu wa Kwanza wa Rais wa Iran: Tumeanza Enzi Mpya Chini ya Uongozi wa Ayatollah Sayyid Mojtaba Khamenei
Makamu wa Kwanza wa Rais wa Iran, Mohammad Reza Aref, amesema Jamhuri ya Kiislamu imeanza enzi mpya chini ya uongozi wa Ayatullah Sayyid Mojtaba Khamenei, akitoa shukrani kwa mahudhurio makubwa ya wananchi wa Iran na Umma wa Kiislamu katika mazishi ya Kiongozi Shahidi.
-
Rais Pezeshkian Aishukuru Iraq kwa Kuandaa Mazishi ya Kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu Sayyid Ali Khamenei (ra)
Rais wa Iran, Masoud Pezeshkian, ameishukuru serikali na wananchi wa Iraq kwa mapokezi na ushirikiano walioutoa wakati wa shughuli za kuaga na kusafirisha mwili wa Kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu, Ayatullah Sayyid Ali Khamenei, akisema taifa la Iran halitasahau kamwe mshikamano huo.
-
Kisa cha Kihistoria:Jinsi na Kwa Nini Shahidi Hujjatul Islam Sayyid Abdul Karim Hashimi Nejad Aliuawa na Shirika la Kigaidi la Mujahideen-e Khalq /MEK
Kwa mujibu wa simulizi za kihistoria, kuuawa kwa Shahidi Hujjatul Islam Sayyid Abdul Karim Hashimi Nejad mnamo mwaka 1981 kulikuwa sehemu ya mfululizo wa mauaji yaliyotekelezwa na Shirika la Kigaidi la Mujahideen-e Khalq (MEK), likiwa na lengo la kuwaondoa viongozi waliokuwa na mchango mkubwa katika kuimarisha Mapinduzi ya Kiislamu nchini Iran.
-
Makao Makuu ya Khatam al-Anbiya: Iran Haitaruhusu Uingiliaji wa Usimamizi wa Mlango wa Bahari wa Hormuz
Makao Makuu ya Khatam al-Anbiya (s) yametangaza kuwa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran haitaruhusu kwa hali yoyote uingiliaji wa mamlaka yoyote katika usimamizi wa Mlango wa Bahari wa Hormuz, huku yakiahidi kutoa jibu kali dhidi ya kile ilichokitaja kuwa uchokozi wa Marekani.
-
Msanii wa Iran: Shahidi Sayyid Ali Khamenei alitupanda ndani yetu mapenzi ya sanaa na ukweli
Msanii wa Iran Hussein Esmati amesema kuwa kufariki shahidi kwa Sayyid Ali Khamenei kumewaathiri kwa kina wasanii wa Iran, jambo lililoonekana katika kazi nyingi za kisanii zinazoakisi maombolezo, mapenzi na maadili aliyoyasimamia.
-
Mwanaharakati wa Vyombo vya Habari wa Urusi: Sijawahi Kushuhudia Jambo Kama Hili Maishani Mwangu
Mwanaharakati wa vyombo vya habari kutoka Urusi amesema umati mkubwa wa wananchi waliojitokeza kumuaga kiongozi wao umeandika historia, akisisitiza kuwa mshikamano wa Wairani umeonyesha mapenzi ya dhati kwa taifa na uongozi wao.
-
Washington post: Familia Nyingi Zilishiriki Katika Mazishi ya Kiongozi Shahidi wa Iran
Gazeti la Washington Post limesema kuwa Mazishi ya Kiongozi Shahidi wa Iran yalishuhudia ushiriki mkubwa wa wananchi, wakiwemo familia zilizofika na watoto wao, huku yakieleza kuwa tukio hilo lilidhihirisha mshikamano wa kitaifa na uthabiti wa wananchi.
-
Qalibaf: Amani ya kweli nchini Lebanon haiwezi kupatikana bila mchango wa Iran
Spika wa Bunge la Jamhuri ya Kiislamu ya Iran, Mohammad Baqer Qalibaf, amesema kuwa amani ya kudumu nchini Lebanon inaweza kupatikana kupitia nafasi ya Iran, huku akisisitiza kuendelea kuunga mkono washirika wa Jamhuri ya Kiislamu katika Muqawama.
-
kamanda wa jeshi la majini la Iran: muqawama haujafungwa tena na mipaka ya kijiografia
Kamanda wa Jeshi la Majini la Iran, Admiral Shahram Irani, amesema kuwa Muqawama sasa umevuka mipaka ya kijiografia, akisisitiza kuwa mataifa na vikosi vya Muqawama vinaendelea kuimarisha umoja na mshikamano katika kukabiliana na changamoto.
-
Ayatollah Makarim Shirazi: Waliomuua Kiongozi Shahidi Hawataepuka Adhabu ya Mwenyezi Mungu
Ayatollah Nasser Makarim Shirazi amesema wahusika na wapangaji wa mauaji ya Kiongozi Shahidi wa Mapinduzi ya Kiislamu, pamoja na waliohusika na umwagaji damu wa viongozi, raia wasio na hatia na watoto, hawataokoka adhabu ya Mwenyezi Mungu, huku akisisitiza kuwa damu zao takatifu haitasahaulika kamwe.
-
Panahian: Iran Itasimama Imara Kulipiza Kisasi cha Kiongozi Shahidi Sayyid Ali Khamenei
Mwanazuoni wa Kiislamu wa Iran, Alireza Panahian, amesema wakati wa mazishi ya Kiongozi Shahidi Sayyid Ali Khamenei kwamba Iran iko tayari kujitolea kwa gharama kubwa ili kuhakikisha kisasi kwa kuuawa kwa kiongozi huyo, akisisitiza kuwa jambo hilo halitaachwa bila majibu.
-
Hilali Nyekundu: Hakuna Majeruhi Walioripotiwa Katika Hafla ya Kuaga Kiongozi Shahidi Licha ya Mamilioni ya Waombolezaji Kushiriki
Shirika la Hilali Nyekundu limetangaza kuwa hadi sasa hakuna majeruhi walioripotiwa katika hafla ya kuaga Kiongozi Shahidi Ayatullah Sayyid Ali Khamenei, licha ya mamilioni ya waombolezaji kushiriki. Shirika hilo limeeleza kuwa mafanikio hayo yametokana na usimamizi mzuri wa tukio hilo pamoja na ushirikiano wa wananchi.