25 Septemba 2025 - 17:50
"Ushahidi (shahada) ni thawabu ya jitihada za jihadi; iwe katika utetezi wa miaka 8, au katika mapambano ya kishujaa ya siku 12"

Kiongozi Mkuu wa Mapinduzi ya Kiislamu, katika ujumbe wake kwa mnasaba wa Wiki ya Utetezi Mtakatifu, aliitaja shahada kuwa ni thawabu ya juhudi za jihadi, na alisisitiza juu ya umuhimu wa kujitolea huku katika kukuza mataifa. Vilevile, alieleza yakini yake juu ya ushindi wa haki na umuhimu wa kushikamana na majukumu ya kidini.

Kwa Jina la Mwenyezi Mungu Mwingi wa Rehema Mwenye Kurehemu

Mwaka huu, Wiki ya Utetezi Mtakatifu imepata mwonekano na adhama nyingine kwa sababu ya kufa shahidi kwa kundi la Mashujaa wakuu wa njia ya Muqawama (Mapambano ya Kiislamu) na vijana jasiri katika maeneo mbalimbali.

Shahada ni thawabu ya juhudi za jihadi - iwe ni katika utetezi wa miaka 8, au katika mapambano ya kishujaa ya siku 12, au huko Lebanon, Gaza, na Palestina. Mataifa hukua kwa juhudi hizi za kujitolea, na hupata Mwangaza na uzuri kwa sababu ya Mashahidi hawa.

Kilicho muhimu ni kuwa na yakini juu ya ahadi ya Mwenyezi Mungu kuhusu ushindi wa haki na kuangamia kwa batili (udhalimu), na kudumu katika kutekeleza wajibu wetu wa kunusuru dini ya Mwenyezi Mungu.

Sayyid Ali Khamenei
24 Septemba, 2025.

Tags

Your Comment

You are replying to: .
captcha