Mnasaba
-
Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran: Njia ya Kiongozi Shahidi wa Mapinduzi ya Kiislamu itaendelea kwa nguvu
Wizara ya Mambo ya Nje ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran imesisitiza kuwa kuuawa shahidi kwa Kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu, Imam Sayyid Ali Khamenei (Quds Sirruh), si mwisho wa safari, bali ni mwanzo wa hatua mpya ya kuendeleza hadhi ya Uislamu na Iran, huku njia na misingi yake ikiendelea kwa nguvu na uthabiti.
-
Kiongozi Mkuu wa Mapinduzi ya Kiislamu ya Iran: Bunge la Kiislamu Ni Nguzo Kuu ya Utashi wa Wananchi na Sheria
Kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu ya Iran amesisitiza kuwa Majlisi ya Shura ya Kiislamu ni kiini cha wananchi na nguzo muhimu ya sheria na utungaji wa sheria, akieleza kuwa taasisi hiyo ina jukumu la msingi katika kutekeleza matakwa ya wananchi ndani ya mfumo wa Jamhuri ya Kiislamu.
-
Mkurugenzi wa Ofisi ya Jumuiya ya Kiislamu ya Ahlul-Bayt (a.s) nchini Lebanon akutana na Sheikh Ahmad Qablan
Mkutano huo uliandaliwa kwa mnasaba wa kuzaliwa kwa Bibi Zainab (a.s), ambapo Nakhai alitoa taarifa kuhusu maendeleo na utekelezaji wa programu mbalimbali za Jumuiya hiyo nchini Lebanon.
-
Waziri wa Mambo ya Nje:
Ulinzi Usio wa Kijeshi lazima uwe makini na wenye umakini wa hali ya juu
Kauli hiyo imetolewa katika ujumbe wake maalum kwa mnasaba wa Wiki ya Kuheshimu Ulinzi Usio wa Kijeshi, ambapo amesema kuwa kipindi hiki ni fursa muhimu ya kueleza umuhimu wa mikakati na mipango ya kuongeza usalama, uimara, na kinga ya miundombinu ya taifa dhidi ya kila aina ya vitisho vya maadui.
-
Ujumbe wa Kiongozi wa Mapinduzi kwa mnasaba wa Wiki ya Utetezi Mtakatifu:
"Ushahidi (shahada) ni thawabu ya jitihada za jihadi; iwe katika utetezi wa miaka 8, au katika mapambano ya kishujaa ya siku 12"
Kiongozi Mkuu wa Mapinduzi ya Kiislamu, katika ujumbe wake kwa mnasaba wa Wiki ya Utetezi Mtakatifu, aliitaja shahada kuwa ni thawabu ya juhudi za jihadi, na alisisitiza juu ya umuhimu wa kujitolea huku katika kukuza mataifa. Vilevile, alieleza yakini yake juu ya ushindi wa haki na umuhimu wa kushikamana na majukumu ya kidini.
-
Mawakibu (1,800) za waombolezaji yalifurika katika Haram Tukufu ya Imam Ali (a.s) kwa Mnasaba wa kumbukumbu ya kufariki kwa Mtukufu Mtume Muhammad (s)
Haram Tukufu ya Imam Ali (a.s) Yapokea Makundi 1800 ya Waombolezaji Kutoka Ndani na Nje ya Iraq kwa Kumbukumbu ya Kifo cha Mtume Muhammad (s.a.w.w).
-
Maelfu waandamana Beirut kuunga mkono Hizbullah dhidi ya shinikizo la kuondolewa silaha
Wakisambaza ujumbe wao kwa sauti na maandamano, wananchi hao wamesisitiza kuwa Hizbullah si tu harakati ya kijeshi, bali pia ni nguzo muhimu ya taifa katika ulinzi wa mipaka na heshima ya Lebanon. Kwao, wazo la kuondoa silaha za harakati hiyo ni sawa na kuiweka Lebanon mikononi mwa maadui wake.