Wakisambaza ujumbe wao kwa sauti na maandamano, wananchi hao wamesisitiza kuwa Hizbullah si tu harakati ya kijeshi, bali pia ni nguzo muhimu ya taifa katika ulinzi wa mipaka na heshima ya Lebanon. Kwao, wazo la kuondoa silaha za harakati hiyo ni sawa na kuiweka Lebanon mikononi mwa maadui wake.
Baadhi ya viongozi wa kisiasa wa Uingereza, wakiwemo Waziri Mkuu wa nchi hiyo, wametuma salamu za pongezi kwa Waislamu wa Uingereza na ulimwenguni kote kwa mnasaba wa Sikukuu ya Eid al-Adha.