6 Januari 2026 - 16:09
Rais Samia Afanya Mazungumzo na Viongozi wa Wizara ya Ulinzi na JKT Zanzibar

Mazungumzo hayo yamezingatia masuala mbalimbali ya usalama, ulinzi wa taifa, na maendeleo ya majeshi, huku akisisitiza umuhimu wa ushirikiano kati ya majeshi na wananchi katika kuhakikisha amani na utulivu wa taifa.

Shirika la Habari la Kimataifa la Ahlul-Bayt (as) -ABNA- TUNGUU, ZANZIBAR – Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, leo Januari 06, 2026, amefanya mazungumzo na viongozi wa Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) katika Ikulu Ndogo ya Tunguu, Zanzibar.

Rais Samia Afanya Mazungumzo na Viongozi wa Wizara ya Ulinzi na JKT Zanzibar

Kikao hicho kilihudhuriwa na viongozi wakuu wa wizara na majeshi ikiwa ni pamoja na:

1_Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, Mhe. Dkt. Rhimo Simeon Nyansaho

2_Katibu Mkuu Kiongozi, Mhe. Balozi Dkt. Moses Kusiluka

3_Katibu Mkuu wa Wizara ya Ulinzi na JKT, Dkt. Faraji Mnyepe

4_Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Tanzania, Jenerali Jacob John Mkunda

5_Mkuu wa Jeshi la Kujenga Taifa (JKT), Meja Jenerali Rajabu Mabele.

Rais Samia Afanya Mazungumzo na Viongozi wa Wizara ya Ulinzi na JKT Zanzibar

Mazungumzo hayo yamezingatia masuala mbalimbali ya usalama, ulinzi wa taifa, na maendeleo ya majeshi, huku akisisitiza umuhimu wa ushirikiano kati ya majeshi na wananchi katika kuhakikisha amani na utulivu wa taifa.

Rais Samia pia alisisitiza kuimarisha mafunzo, usalama wa rasilimali, na ufanisi wa Jeshi la Kujenga Taifa.

Rais Samia Afanya Mazungumzo na Viongozi wa Wizara ya Ulinzi na JKT Zanzibar

Tags

Your Comment

You are replying to: .
captcha