Usalama
-
Hashd al-Shaabi na Jeshi la Iraq washambulia maficho ya Daesh huko Rawah
Operesheni ya vikosi vya Hashd al-Shaabi kwa kushirikiana na Jeshi la Iraq dhidi ya mabaki ya kundi la Daesh katika eneo la Sahul, wilayani Rawah, magharibi mwa Anbar, imekumbwa na mlipuko wa bomu lililokuwa limetegwa na magaidi, ambapo mpiganaji mmoja wa Hashd al-Shaabi amejeruhiwa vibaya.
-
Baghaei: Kupelekwa kwa faili ya nyuklia ya Iran Baraza la Usalama hakuna msingi wa kimantiki
Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran, Ismail Baghaei, amesema hakuna msingi wa kupeleka suala la nyuklia la Iran katika Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa, akisisitiza kuwa Iran haijakiuka majukumu yake yoyote.
-
Iran na Iraq Zaongeza Ushirikiano katika Masuala ya Kisheria na Kimahakama
Mkuu wa Baraza la Juu la Mahakama nchini Iraq, Jaji Faiq Zidan, amezungumzia na Balozi wa Iraq nchini Iran, Yasser Abdul-Zahra Al-Hajjaj, matokeo ya ziara yake ya hivi karibuni mjini Tehran na juhudi za kuimarisha ushirikiano wa kimahakama na kisheria kati ya nchi hizo mbili.
-
IRGC: Hatutaruhusu adui kufanya harakati za ardhini nchini Iran
Kamanda wa Kambi ya Hamza Sayyid al-Shuhada ya Kikosi cha Ardhini cha IRGC amesema adui alijaribu kutumia vita vya tatu vilivyolazimishwa kuleta mpasuko miongoni mwa wananchi, kuchochea ukosefu wa usalama na kulenga mshikamano wa kijamii, lakini vikosi vya Iran havikuruhusu kupenya wala harakati za ardhini za adui.
-
Mohsen Rezaei: Marekani ikichukua hatua ya uhasama dhidi ya Iran, tutalenga maslahi yake kwa namna itakayorekodiwa katika historia
Katibu wa Baraza Kuu la Usalama wa Taifa la Iran, Meja Jenerali Mohsen Rezaei, ameonya kuwa iwapo Marekani itachukua hatua yoyote ya uhasama dhidi ya Iran, Tehran itachukua hatua dhidi ya maslahi yake ya kijeshi na kiuchumi kwa namna itakayorekodiwa katika historia.
-
Wito wa maombi watolewa kwa ajili ya usalama wa mtoto wa Trump
Baadhi ya vyombo vya habari na mitandao ya habari nchini Marekani, ikiwemo CBN News, wametoa wito wa watu kumuombea usalama Donald Trump na familia yake, kufuatia kusambaa kwa video yenye maudhui ya vitisho dhidi ya mtoto wake, Barron Trump.
-
Mohsen Rezaei: Nchi yoyote itakayounga mkono vita vya kiuchumi dhidi ya Iran tutachukulia hatua hiyo kuwa kitendo cha kivita
Katibu wa Baraza Kuu la Usalama wa Taifa la Iran, Meja Jenerali Mohsen Rezaei, ameonya kuwa Iran itachukulia ushiriki au uungaji mkono wa nchi yoyote katika kile alichokiita vita vya kiuchumi vya Marekani dhidi ya wananchi wa Iran kuwa “kitendo cha kivita.”
-
Mtaalamu wa Kisiasa: Kulipiza Kisasi cha Kiongozi Shahidi Lazima Kugeuke Kuwa Mkakati wa Kisiasa
Profesa Fouad Izadi amesema suala la kulipiza kisasi cha kiongozi shahidi halipaswi kubaki katika kiwango cha kauli na misemo, bali linapaswa kufuatiliwa kwa njia za kisheria na kisiasa. Ameonya pia kwamba Marekani inaweza kuwa inarudia mbinu ya kutumia mazungumzo na ahadi za makubaliano kama njia ya kudhibiti mwenendo wa Iran na kuandaa mazingira ya hatua nyingine.
-
Iran: Vita vya siku 40 vimebadilisha mlinganyo wa usalama wa kikanda, vituo vya kijeshi vya kigeni vimekuwa chanzo cha kuyumbisha usalama
Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran, Abbas Araqchi, amesema vita vya siku 40 vimebadilisha mtazamo wa nchi za eneo kuhusu mfumo wa usalama wa kikanda. Amesema uwepo wa majeshi na vituo vya kijeshi vya kigeni haukuweza kuleta usalama, bali umegeuka kuwa sababu ya kuyumbisha usalama katika eneo.
-
Wizara ya Usalama ya Iran: Ufaransa Ichukue Wajibu kwa Uingiliaji wa Wanadiplomasia Wake
Wizara ya Usalama ya Iran imeionya serikali ya Ufaransa kuacha kuingilia masuala ya ndani ya Iran, ikisema endapo vitendo hivyo vitajirudia, wahusika watachukuliwa hatua zinazofaa.
-
Iran: Seli mbili za makundi ya kigaidi zakamatwa kusini mashariki mwa nchi
Wizara ya Usalama ya Iran imetangaza kukamatwa kwa watu wanne wanaodaiwa kuwa wanachama wa makundi ya kigaidi na kuuawa kwa wengine wawili wakati wa mapambano na vikosi vya usalama katika mji wa Khash, mkoani Sistan na Baluchestan.
-
Trump: Tulikabili Hatari Kubwa, Ikiwemo Uwezekano wa Kuuawa, Wakati wa Kuondoka Uturuki
Donald Trump alidai kuwa Marekani “inadhibiti kikamilifu” Mlango wa Hormuz, akisema: “Siitambui Iran kama nchi ya kuaminika, na tunadhibiti kikamilifu Mlango wa Hormuz.”
-
Waziri wa Mambo ya Ndani Pakistan: Uhusiano Imara wa Tehran na Islamabad Ugeuzwe Kuwa Matokeo ya Kivitendo
Mohsin Naqvi amesema uhusiano wa kina kati ya wananchi wa Iran na Pakistan unapaswa kuzaa ushirikiano zaidi na matokeo ya kivitendo, akisisitiza umuhimu wa kuongeza juhudi za pamoja katika kufikia malengo ya nchi hizo mbili.
-
Pakistan: Ziara ya Waziri wa Mambo ya Ndani Tehran Kulenga Kuimarisha Amani na Usalama wa Kikanda
Pakistan imesema ziara ya Waziri wa Mambo ya Ndani, Mohsin Naqvi, nchini Iran inalenga kuendeleza mashauriano na Tehran kuhusu kuimarisha uhusiano wa pande mbili, ushirikiano wa kiusalama na juhudi za kuimarisha amani na utulivu katika eneo.
-
Moscow na Tehran Zafanya Mashauriano ya Kuimarisha Ushirikiano katika Usalama wa Kimataifa
Iran na Urusi zimefanya mashauriano mjini Moscow kuhusu kuimarisha ushirikiano katika masuala ya usalama wa kimataifa, yakiwemo udhibiti wa silaha, upokonyaji wa silaha na kuzuia kuenea kwa silaha za nyuklia.
-
Uchambuzi: Mohsen Rezaei Ateuliwa Kuwa Mtu Muhimu wa Usalama wa Taifa Iran - Ni Jenerali Mkongwe Mwenye Uzoefu Mkubwa Katika Masuala ya Usalama
Mohsen Rezaei, Jenerali mstaafu wa Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu (IRGC) na mmoja wa viongozi mashuhuri wa kijeshi na kisiasa nchini Iran, ameteuliwa kuwa: Katibu wa Baraza Kuu la Usalama wa Taifa la Jamhuri ya Kiislamu ya Iran. Uteuzi huo unamrudisha mwanajeshi huyo mwenye uzoefu mkubwa katika nafasi nyeti ya kuratibu masuala ya usalama wa taifa wakati Iran ikiendelea kuandamwa na changamoto kubwa za kiusalama na kisiasa kutoka kwa maadui Marekani na Israel.
-
Rais Pezeshkian Amteua Mohsen Rezaei kuwa Katibu wa Baraza Kuu la Usalama wa Taifa la Iran
Rais wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran, Masoud Pezeshkian, amemteua Mohsen Rezaei kuwa Katibu wa Baraza Kuu la Usalama wa Taifa, akimtaka kuimarisha uratibu wa taasisi za usalama, kukabiliana na vitisho vipya na vya kiteknolojia, na kulinda umoja wa kitaifa, mamlaka na uadilifu wa ardhi ya Iran.
-
Aref: Iran Iongeze Usalama wa Mtandao na Ulinzi wa Kiraia Kukabiliana na Njama za Adui
Makamu wa Kwanza wa Rais wa Iran, Mohammad Reza Aref, amesisitiza umuhimu wa kuimarisha usalama wa mtandao na ulinzi wa kiraia, akieleza kuwa adui hatasitisha njama zake licha ya kushindwa kwake hivi karibuni mbele ya wananchi wa Iran, hivyo nchi inapaswa kuwa katika hali ya tahadhari na utayari kamili.
-
Kaimu Waziri wa Ulinzi: Uwepo wa viongozi wenye uzoefu katika nafasi za kimkakati ni faida kwa kulinda maslahi ya taifa
Kaimu Waziri wa Ulinzi wa Iran, Brigedia Jenerali Majid Ibn al-Reza, amempongeza Meja Jenerali Mohsen Rezaei kwa kuteuliwa kuwa Katibu wa Baraza Kuu la Usalama wa Taifa, akisema uwepo wa watu wenye imani, uzoefu, uelewa na historia ya kujitolea katika nafasi za kimkakati ni rasilimali muhimu kwa kulinda maslahi ya kitaifa na kuimarisha nguvu ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran.
-
Velayati: Maono ya kimkakati ya Mohsen Rezaei ni nguzo muhimu katika kulinda usalama na maslahi ya kitaifa ya Iran
Mshauri wa Kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu wa Iran katika masuala ya kimataifa, Ali Akbar Welayati, amesema kuwa uzoefu, maono ya kimkakati na moyo wa kimapinduzi wa Meja Jenerali Mohsen Rezaei vitakuwa nguzo muhimu katika kulinda usalama na maslahi ya kitaifa ya Iran.
-
Qalibaf: Waandishi wa Habari Ni Wapiganaji Wenye Maarifa Kama Ngome na Ukweli Kama Silaha
Spika wa Bunge la Iran, Mohammad Baqer Qalibaf, amesema kuwa hatima ya mataifa haiamuliwi tu katika uwanja wa vita, bali pia katika uwanja wa simulizi, akisisitiza kuwa waandishi wa habari wana jukumu la kulinda ukweli, usalama wa kisaikolojia, utambulisho wa kitaifa na nguvu ya kiutamaduni ya taifa.
-
Urithi wa Shahidi Nasirzadeh: Nguzo ya Usalama na Ulinzi wa Iran
Katika kuelekea Wiki ya Serikali nchini Iran, urithi wa mashahidi na watumishi wa taifa unakumbusha umuhimu wa kuchukulia dhamana ya uongozi kama amana ya Mwenyezi Mungu, na kutumia uwezo wote katika kulinda heshima, usalama na maslahi ya taifa.
-
Katibu wa Baraza Kuu la Usalama wa Taifa Iran: Mlango wa Hormuz Hautafunguliwa Marekani Isiporekebisha Mwenendo Wake
Katibu wa Baraza Kuu la Usalama wa Taifa la Iran, Mohammad Baqir Zolqadr, amesema kuwa Mlango wa Hormuz hautafunguliwa hadi Marekani itakaporekebisha mwenendo wake, akitaja masharti kadhaa ikiwemo kusitisha vitisho na mashambulizi dhidi ya Iran, kuondoa vikwazo na kulipa fidia ya uharibifu uliosababishwa na vita.
-
Mahakama ya Israel Yasitisha Pendekezo la Ben Gvir la Kuweka Mamba Kuzunguka Gereza la Ketziot
Mahakama ya Israel imesitisha pendekezo la Waziri wa Usalama wa Taifa, Itamar Ben Gvir, la kuweka mamba kuzunguka Gereza la Ketziot linalowashikilia wafungwa wa Kipalestina, kufuatia kesi iliyowasilishwa na shirika la kutetea haki za wanyama.
-
Iraq Yaanzisha Operesheni Kubwa ya Kupambana na Magaidi wa Daesh huko Ninawa
Kikosi cha Kupambana na Ugaidi cha Iraq kimeanzisha operesheni kubwa ya kiusalama katika mkoa wa Ninawa kwa lengo la kuwasaka mabaki ya kundi la kigaidi la Daesh, kubaini seli zilizojificha na kuimarisha usalama na utulivu katika eneo hilo.
-
Mhadhiri wa Sala ya Ijumaa Tehran: Makombora na Diplomasia Vimeimarisha Mizani ya Nguvu kwa Manufaa ya Iran
Mhadhiri / Khatibu wa Sala ya Ijumaa mjini Tehran amesema uwezo wa makombora ya Iran pamoja na diplomasia madhubuti ndivyo vilivyoimarisha mizani ya nguvu kwa manufaa ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran, huku akisisitiza umuhimu wa kulinda mshikamano wa kitaifa na kuimarisha imani ya wananchi.
-
Iraq yakemea mashambulizi ya anga ya Marekani na Saudi Arabia
Serikali ya Iraq imelaani mashambulizi ya Marekani na Saudi Arabia, ikisisitiza kuwa yanakiuka mamlaka yake. Baraza la Usalama wa Taifa limeagiza kuandaliwa kwa mpango wa kukabiliana na ukiukaji huo, huku Wizara ya Mambo ya Nje ikitakiwa kuchukua hatua kwa mujibu wa sheria za kimataifa. Iraq pia imeahidi kurekodi matukio hayo na kulinda haki na mamlaka yake ya kitaifa.
-
Radiamali ya Al-Wefaq kwa Mawasiliano ya Mfalme wa Bahrain na Rais wa utawala wa Kizayuni: Ushirikiano na Tel Aviv hauleti usalama
Jumuiya ya Al-Wefaq: Mawasiliano ya Mfalme wa Bahrain na Rais wa utawala wa Kizayuni yanakwenda kinyume na maslahi ya taifa Jumuiya ya Al-Wefaq imelaani vikali mawasiliano ya simu kati ya Mfalme wa Bahrain na Rais wa utawala wa Kizayuni, ikieleza kuwa hatua hiyo ni kujitenga na msimamo wa pamoja wa kitaifa na wa wananchi wa Bahrain. Katika taarifa yake, Al-Wefaq imesema kuwa kitendo hicho kinaonyesha utegemezi wa serikali ya Bahrain kwa ajenda za Marekani na utawala wa Kizayuni, na kwamba hakilingani na matakwa ya wananchi wala maslahi ya taifa. Aidha, jumuiya hiyo imeeleza kuwa hatua hiyo ni kinyume na maslahi na usalama wa Bahrain, ulimwengu wa Kiarabu na Umma wa Kiislamu, ikisisitiza kuwa kuimarisha uhusiano na utawala wa Kizayuni hakutaleta amani wala utulivu katika eneo, bali kutaongeza migogoro na kuhatarisha usalama wa kikanda.
-
Dhu al-Qadr: Mashambulizi Endelevu Yataendelea Hadi Adui Asalimu Amri Kikamilifu
Katibu wa Baraza Kuu la Usalama wa Taifa la Iran: “Mashambulizi endelevu na yaliyoelekezwa ya wapiganaji wetu yataendelea hadi adui asalimu amri kikamilifu na kulipiza kisasi kwa damu za watoto wasio na hatia wa Minab na Lamerd.”
-
Ujumbe wa Kidiplomasia wa Oman Wawasili Tehran Kujadili Usalama wa Usafiri katika Mlango wa Hormuz
Ujumbe wa kidiplomasia wa Oman unatarajiwa kuwasili Tehran leo kwa ajili ya kufanya mashauriano kuhusu taratibu za kusimamia usafiri wa majini katika Mlango wa Hormuz. Ziara hiyo ni sehemu ya mashauriano yanayoendelea kati ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran na Usultani wa Oman. Mashauriano hayo yanalenga kufikia taratibu zinazofaa za kusimamia na kuratibu mwenendo wa usafiri wa majini katika Mlango wa Hormuz.