Usalama
-
Kiongozi wa Wanazuoni wa Imamiyya Pakistan: Vikwazo kwa Mazuwwari wa Arubaini ni Sehemu ya Mardi wa Kuwadhoofisha Mashia
Kiongozi wa Baraza la Wanazuoni wa Imamiyya Pakistan, Hujjatul Islam Dkt. Sayyid Shafaqat Hussein Shirazi, amesema vikwazo vinavyowakabili mahujaji wa Pakistan kuelekea Arubaini si suala la kiusalama pekee, bali ni sehemu ya mpango wa kudhoofisha uhusiano wa wafuasi wa Ahlul-Bayt (as) na Iran, Iraq pamoja na utamaduni wa A'shura.
-
Iran: Kuwaadhibu waliohusika na mauaji ya Kiongozi Shahidi ni haki ya taifa
Naibu wa Baraza Kuu la Usalama wa Taifa la Iran amesema kuwa kuwawajibisha waliopanga, kutekeleza na kushiriki katika mauaji ya Kiongozi Shahidi wa Mapinduzi ya Kiislamu pamoja na mashahidi wengine ni haki halali ya taifa la Iran.
-
IRGC yatangaza kufungwa kwa muda kwa Mlango wa Bahari wa Hormuz baada ya tukio la meli kupuuza maonyo
Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu (IRGC) limetangaza kufungwa kwa muda kwa Mlango wa Bahari wa Hormuz, likisema hatua hiyo imechukuliwa kufuatia kile lilichodai kuwa ni ukiukaji wa maelekezo ya usalama wa baharini na kuendelea kwa uingiliaji wa mataifa ya kigeni katika eneo hilo.
-
Katibu wa Baraza Kuu la Usalama wa Taifa Iran: Shambulio la Miundombinu Litajibiwa kwa Hatua Kama Hiyo
Katibu wa Baraza Kuu la Usalama wa Taifa la Iran, Mohammad Baqer Zolqadr, amesema kuwa shambulio lolote dhidi ya miundombinu ya Iran litajibiwa kwa hatua kama hiyo, akisisitiza kuwa Israel haitakwepa majibu ya wapinzani wake.
-
Kaimu Waziri wa Ulinzi wa Iran: Uwezo wa Ulinzi wa Taifa Hauko Kwenye Majadiliano
Kaimu Waziri wa Ulinzi wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran, Brigedia Jenerali Ebn al-Reza, amesema uwezo wa Iran katika sekta ya ulinzi, makombora na ndege zisizo na rubani ni sehemu ya usalama wa taifa na hauwezi kujadiliwa katika mazungumzo yoyote.
-
Makamu wa Kwanza wa Rais wa Iran: Elimu ya Akili Bandia na Usalama wa Mtandao ni Muhimu Shuleni
Makamu wa Kwanza wa Rais wa Iran, Mohammad Reza Aref, amesisitiza umuhimu wa kufundisha akili bandia (AI) na usalama wa mtandao katika shule kwa mtazamo wa vitendo na unaojenga ujuzi, akieleza kuwa teknolojia za kisasa zina nafasi muhimu katika kukabiliana na changamoto za kisasa.
-
Iran Yaeleza Mkutano wa Usalama wa Marekani na Nchi za Kanda ni Maonyesho ya Kisiasa
Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran, Esmail Baghaei, amesema mkutano wa kile kilichoitwa "Mazungumzo ya Usalama wa Kikanda" ulioandaliwa na Marekani nchini Bahrain ni wa maonyesho tu na unalenga kuficha sera ambazo, kwa mujibu wake, zinachochea ukosefu wa utulivu katika eneo la Asia Magharibi.
-
Balozi wa Iran katika Umoja wa Mataifa Aitaka Baraza la Usalama Kuepuka Hatua za Uchochezi
Mwakilishi wa Kudumu wa Iran katika Umoja wa Mataifa, Amir Saeid Iravani, amesema Baraza la Usalama linapaswa kuunga mkono diplomasia na kuepuka hatua zinazoweza kuchochea mvutano au kudhoofisha mazungumzo yanayoendelea.
-
Umoja wa Ulaya Washindwa Kufikia Makubaliano Kuhusu Kumuwekea Vikwazo Itamar Ben-Gvir
Msemaji wa masuala ya nje wa Tume ya Ulaya amesema kuwa nchi wanachama wa Umoja wa Ulaya hazikufikia mwafaka kuhusu pendekezo la kumuwekea vikwazo Waziri wa Usalama wa Ndani wa Israel, Itamar Ben-Gvir, huku zikilaani kauli zake za uchochezi dhidi ya Lebanon.
-
Iran Yasitisha Mazungumzo ya Nyuklia na Marekani Kufuatia Mashambulizi ya Israel Lebanon
Iran imesitisha safari ya ujumbe wake kwenda Geneva kwa ajili ya duru ya kwanza ya mazungumzo ya nyuklia na Marekani, ikieleza kuwa kuendelea kwa mashambulizi ya Israel kusini mwa Lebanon kumekiuka mazingira ya kusitisha mapigano. Kufuatia msimamo huo, Makamu wa Rais wa Marekani, JD Vance, naye ameripotiwa kusitisha safari yake, huku hali hiyo ikiweka mashaka juu ya kuanza kwa mazungumzo yaliyokuwa yanatarajiwa kuwa hatua ya kwanza ya utekelezaji wa makubaliano ya hivi karibuni kati ya Tehran na Washington.
-
Iran na Oman Zasisitiza Umuhimu wa Usalama wa Mlango wa Hormuz Kufuatia Makubaliano ya Hivi Karibuni
Mawaziri wa Mambo ya Nje wa Iran na Oman wamejadili kwa njia ya simu umuhimu wa kulinda usalama wa Mlango wa Hormuz, kuimarisha usalama wa usafiri wa baharini, na kupanua ushirikiano wa pande mbili kufuatia makubaliano ya hivi karibuni kati ya Tehran na Washington.
-
Mamilioni ya Wairaq Kuitikia Wito wa Kushiriki Mazishi ya Kiongozi Shahidi wa Mapinduzi
Takribani Wairaq milioni moja wanatarajiwa kushiriki mazishi ya kiongozi shahidi wa Mapinduzi, huku zaidi ya nusu milioni wakitarajiwa kuingia Iran kupitia mpaka wa Mehran kuelekea Tehran, Qum na Mashhad kwa ajili ya maombolezo.
-
Iran: Kuachiliwa kwa Fedha Zilizozuiwa, Kuondoka kwa Majeshi ya Kigeni Mashariki ya Kati na Kulipa Ushuru wa Hormuz ni Miongoni mwa Masharti ya Iran
Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran amesema kuachiliwa kwa fedha za Iran zilizozuiwa ni sehemu muhimu ya makubaliano yoyote yajayo, huku akisisitiza kuwa mazungumzo ya sasa yanajikita katika kumaliza vita na masuala ya Lebanon, na kwamba uwepo wa majeshi ya kigeni katika eneo unapaswa kukomeshwa.
-
Chanzo Chafichua Rasimu ya Vipengele 14 vya Makubaliano Yanayodaiwa Kupendekezwa kati ya Iran na Marekani
Chanzo kilicho karibu na timu ya mazungumzo ya Iran kimefichua rasimu ya makubaliano yenye vipengele 14 vinavyohusisha usitishaji wa uhasama, kuondolewa kwa vikwazo, kufunguliwa kwa Mlango wa Hormuz, pamoja na kuachiliwa kwa mabilioni ya dola za mali za Iran zilizogandishwa.
-
Kundi la “Hanzala” Latuma Onyo Kali kwa Jeshi la Wanamaji la Marekani, Latishia Majibu Makali
Kundi la mtandao linalojiita “Hanzala” limetoa onyo kali kwa wanamaji wa Jeshi la Wanamaji la Marekani, likiwataka kuwasiliana na familia zao, likidai kuwa makombora yako tayari na likitahadharisha kujibu kwa nguvu iwapo kutatokea uchokozi dhidi ya Iran.
-
Iran Yaukosoa Mkutano wa Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa, Yasema Azimio 2231 Lilikoma Mwaka Jana
Ujumbe wa Iran katika Umoja wa Mataifa umeelezea kikao cha Baraza la Usalama kuhusu Iran kuwa ni “onyesho jingine la unafiki na viwango viwili,” ukisisitiza kuwa Azimio Na. 2231 la Baraza la Usalama lilimalizika rasmi Oktoba 18, 2025 na kwamba hakuna tena msingi wa kisheria wa vikwazo vya Umoja wa Mataifa dhidi ya Iran.
-
Qaani: Kuanzia Hormuz hadi Bab al-Mandab kutaundwa “ukanda mpya wa kiusalama wa Muqawama”
Kamanda wa Kikosi cha Quds katika Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu, Ismail Qaani, amesema kuwa hatua za wakati muafaka na za “busara” zinazochukuliwa na Yemen zinaonyesha uimara na mshikamano wa mhimili wa Muqawama. Amesema pia kuwa, endapo kutahitajika, pande nyingine zinaweza kujiunga katika hatua hizo.
-
Nchi Wanachama wa D-8 Zakubaliana Kupanua Ushirikiano wa Nishati Kupitia Azimio la Baku
Mawaziri na wawakilishi wa nchi wanachama wa D-8 wamepitisha Azimio la Baku, wakisisitiza kuimarisha ushirikiano katika usalama wa nishati, nishati jadidifu na maendeleo ya miundombinu ya pamoja ili kukabiliana na changamoto za sasa za sekta ya nishati duniani.
-
IRGC: Kuvuka Mipaka Miekundu ya Lebanon na Gaza Kutachukuliwa Kama Vita vya Moja kwa Moja Dhidi ya Iran
Shirika la Ujasusi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu (IRGC) limesema kuwa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran itachukulia hatua yoyote ya kuvuka mipaka myekundu nchini Lebanon na Gaza kuwa sawa na kutangaza vita vya moja kwa moja dhidi yake, huku likisisitiza utayari wake wa kuchukua hatua za kujihami na kufungua nyanja mpya za mapambano ikiwa hali hiyo itatokea.
-
Iran Yatoa Onyo Kali kwa Walowezi wa Kaskazini mwa Israel Endapo Beirut Itashambuliwa
Iran imeonya kuwa kushambuliwa kwa vitongoji vya kusini mwa Beirut kutakabiliwa na majibu makali, huku ikiwataka walowezi wa Kaskazini mwa Israel kuondoka katika maeneo hayo kwa ajili ya usalama wao iwapo mashambulizi hayo yatatekelezwa.
-
WSJ Yadai UAE Ilifanya Mashambulizi ya Anga Dhidi ya Iran Wakati wa Vita
Ripoti ya Wall Street Journal imedai kuwa Umoja wa Falme za Kiarabu ulifanya makumi ya mashambulizi ya anga dhidi ya Iran kuanzia siku za mwanzo za vita na kuendelea hadi baada ya kutangazwa kwa usitishaji mapigano mwezi Aprili, madai yaliyoibua mjadala kuhusu nafasi ya mataifa ya Ghuba katika mzozo huo.
-
Iran Yalaani Vitisho vya Marekani dhidi ya Oman, Yasema Usalama wa Hormuz Unalindwa kwa Mujibu wa Sheria za Kimataifa
Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran, Abbas Araghchi, amelaani kauli za vitisho za Marekani dhidi ya Oman akisisitiza kuwa ushirikiano wa Iran na Oman katika kulinda usalama wa usafiri wa majini katika Mlango wa Hormuz unafuata sheria za kimataifa na unalenga kulinda maslahi ya jamii ya kimataifa.
-
Iran Yapendekeza Mfumo Mpya wa Usalama wa Kikanda katika Mkutano wa BRICS Moscow
Naibu Katibu wa Baraza Kuu la Usalama wa Taifa la Iran, Ali Bagheri, amesema pendekezo la Iran la kuanzisha mfumo mpya wa usalama katika eneo limepokelewa vyema katika mkutano wa kimataifa wa viongozi wa usalama wa BRICS uliofanyika Moscow, huku akisisitiza umuhimu wa kuondoa ushawishi wa Marekani na utawala wa Kizayuni katika eneo.
-
CNN: Trump Ametishia au Kushambulia Taifa Moja Kati ya Kila Mataifa 13 Duniani
Ripoti ya CNN imesema matamshi ya Donald Trump kuhusu kuitishia Oman kwa mashambulizi yameongeza wasiwasi wa kimataifa kuhusu matumizi ya vitisho vya kijeshi katika sera za nje za Marekani na athari zake kwa usalama wa dunia.
-
Ali Bagheri: Marekani Haiwezi Kuaminika, Inavunja Ahadi na Makubaliano ya Kimataifa
Naibu Katibu wa Baraza Kuu la Usalama wa Taifa la Iran, Ali Bagheri, amesema kuwa Marekani haiwezi kuaminika kutokana na tabia yake ya kuvunja ahadi, akisisitiza kuwa Iran inategemea uwezo wake wa ndani na vikosi vyake vya ulinzi katika kukabiliana na vitisho, huku akilaumu Marekani na Israel kwa kuchochea ukosefu wa utulivu katika eneo.
-
Vita Dhidi ya Iran Vyatikisa Usalama wa Chakula Sudan
Kupanda kwa bei za mafuta na mbolea kutokana na mzozo unaoongozwa na Marekani dhidi ya Iran kunatishia uzalishaji wa chakula nchini Sudan, huku zaidi ya watu milioni 19.5 wakikabiliwa na njaa kali.
-
Ongezeko lisilo la kawaida la kesi za ujasusi kwa manufaa ya Iran ndani ya Israel
Gazeti la The Jerusalem Post limeripoti kuongezeka kwa wasiwasi wa vyombo vya usalama vya Israel kufuatia ongezeko lisilo la kawaida la kesi za ujasusi zinazodaiwa kuwa kwa manufaa ya Iran. Kwa mujibu wa ripoti ya Shin Bet, zaidi ya kesi 150 zimefunguliwa ndani ya miaka miwili iliyopita, hali inayoelezwa kuwa ni kipindi chenye msongamano mkubwa zaidi wa shughuli za kijasusi za Iran ndani ya Israel, na inayoibua maswali kuhusu udhaifu wa kiusalama na changamoto za kukabiliana na upenyezaji.
-
Iraq yakataa kuruhusu matumizi ya anga lake kwa mashambulizi dhidi ya Iran
Tamko la Iraq linaonyesha kuwa Iraq inalinda mamlaka yake na haitaki kuhusishwa na migogoro ya kijeshi katika eneo hilo, ikisisitiza sera ya kudumisha usalama na utulivu wa kikanda.
-
Mwendesha Mashtaka wa Tehran afungua mashtaka dhidi ya wanasiasa wanaounga mkono mikondo hasimu
Mwendesha Mashtaka wa Tehran ametangaza mashtaka dhidi ya baadhi ya wanasiasa kwa tuhuma za kushirikiana na Marekani na utawala wa Kizayuni, ambapo watu 4 wamekamatwa kwa madai ya kuchochea vurugu na kudhoofisha usalama wa ndani.
-
Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran Abbas Araghchi Aongoza Ujumbe wa Mazungumzo na Marekani Muscat
Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran, Abbas Araghchi, ameongozana na ujumbe wake wa kidiplomasia kuelekea mjini Muscat, Oman, kwa ajili ya mazungumzo na Marekani. Mazungumzo hayo yanatazamwa kuwa na umuhimu mkubwa katika kujadili masuala ya nyuklia, vikwazo vya kiuchumi na usalama wa kikanda, kwa lengo la kufungua ukurasa mpya wa maelewano ya kisiasa.