Usalama
-
Katika mazungumzo ya simu kati ya Mawaziri wa Mambo ya Nje wa Iran na Pakistan:
Araghchi alisema: “Azimio namba 2231 la Baraza la Usalama linapaswa kuchukuliwa kuwa limekamilika na kuhitimishwa kwa wakati uliopangwa.”
Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran, huku akishukuru msimamo wa uwajibikaji wa Pakistan katika Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa kwa kupinga matumizi mabaya ya nchi tatu za Ulaya, alisisitiza kwamba Azimio namba 2231 lazima, kwa mujibu wa masharti yake na maandiko ya makubaliano ya nyuklia (JCPOA), lichukuliwe kuwa limekamilika katika muda uliopangwa, yaani tarehe 26 Mehr 1404 (18 Oktoba 2025).
-
Ismail Baghaei – Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran:
Amesema kuwa taarifa ya Kundi la G7 kuhusu kurejesha vikwazo vya Baraza la Usalama dhidi ya Iran ni ya kinafiki na yenye upotoshaji.
Ismail Baghaei, Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran, amelaani na kulikemea tamko la Kundi la G7 kuhusu suala la nyuklia la Iran, akilitaja kuwa ni la kinafiki na kupotosha ukweli.
-
Hasira ya Viongozi wa Kizayuni Kufuatia Hatua ya Uingereza, Australia na Canada Kutambua Nchi ya Palestina
Hatua ya nchi tatu — Uingereza, Australia na Canada — kutambua rasmi nchi huru ya Palestina, imeibua hasira na ghadhabu kubwa miongoni mwa viongozi wa utawala wa Kizayuni.
-
Upigaji kura wa leo katika Baraza la Usalama kuhusu kurejesha vikwazo dhidi ya Iran
Uanzishaji wa ‘mfumo wa kichocheo’ (Snapback mechanism / Triger Machanism) na Ulaya umeiweka Baraza la Usalama katika hali nyeti; ambapo kupinga azimio jipya kunamaanisha kurejea kwa vikwazo vyote dhidi ya Iran.
-
Kuanza kwa Operesheni ya Kijeshi Katika Bonde la Al-Shay, Kirkuk kwa Lengo la Kuangamiza Maficho ya ISIS
Vyanzo vya usalama vya Iraq vimetangaza kuwa operesheni maalum ya kijeshi imeanza katika sehemu ya mashariki ya Bonde la Al-Shay, karibu na mji wa Kirkuk.
-
Mshauri wa Usalama wa Taifa wa Iraq alisema:
"Hatutaruhusu mtu yeyote kuzungumza kuhusu kuvunjwa kwa Hashd al-Shaabi"
Mshauri wa Usalama wa Taifa wa Iraq alitangaza:Hatutaruhusu Marekani au wengine kuzungumza nasi kuhusu kuvunjwa kwa Hashd al-Shaabi.
-
Kutoka kwa Udanganyifu wa Shetani hadi Mapambano ya Gaza: Nafasi ya Vyombo vya Habari Katika Kufichua Ukweli
Vyombo vya habari vya upinzani vimefanikiwa kugeuza mapambano ya Palestina kutoka katika simulizi ya ndani hadi kuwa gugufumu wa kimataifa wa haki. Kwa kutumia mbinu za kisasa na uelewa wa kihistoria, vyombo hivi vimeweza kuibua mwamko wa umma wa dunia – na jukumu hili linahitaji kuimarishwa kila siku kwa nguvu, mshikamano na ukweli.
-
JMAT Yatangaza Mafunzo ya Msingi ya Itifaki na Ustaarabu (J-PEC) Jijini Dar es Salaam
Taarifa zinaeleza kuwa, mafunzo hayo yatafanyika kuanzia tarehe 16 – 18 Septemba 2025, katika Ukumbi wa Nefaland Hotel Hall, Manzese – Argentina, Dar es Salaam, kuanzia saa 2:00 asubuhi hadi saa 11:00 jioni kila siku.
-
Utabiri wa Mazuwwari 8 Milioni Katika Siku za Mwisho za Mwezi wa Safar
Naibu wa Kitengo cha Utamaduni, Jamii na Hija wa Mkoa wa Khorasan Razavi, Hojjatoleslam Ali Asgari, amesema kuwa idadi ya mazuwwari katika siku za mwisho za mwezi Safar imeongezeka kwa kiasi kikubwa ikilinganishwa na mwaka uliopita. Kwa kuzingatia likizo zinazokaribia, inatarajiwa kuwa idadi ya mazuwwari itafikia takriban milioni 8.
-
Katibu wa Usalama wa Taifa Iran: “Muqawama ni Hazina Kuu kwa Eneo na Umma wa Kiislamu"
Larijani alitembelea Iraq na Lebanon kwa mazungumzo na viongozi wakuu, akiwemo Rais Joseph Aoun na Spika Nabih Berri.
-
Kabla ya kuondoka Tehran kuelekea Iraq na Lebanon;
LariJani: Mkataba wa usalama kati ya Iran na Iraq unaandaliwa / Kusisitiza umoja wa kitaifa wa Lebanon
Katibu wa Baraza Kuu la Usalama la Kitaifa alisema kwamba usalama wa Iran unategemea usalama wa majirani zake na kuongeza: “Mkataba wa usalama kati ya Iran na Iraq unaandaliwa na utaasainiwa katika safari hii.”
-
Baghdad yamuita Balozi wa Uingereza kufuatia matamshi yake kuhusu Hashd al-Shaabi
Wizara ya Mambo ya Nje ya Iraq imemuita balozi wa Uingereza mjini Baghdad kutokana na matamshi yake kuhusu nafasi ya Hashd al-Shaabi katika mfumo wa usalama wa Iraq, na imeonyesha majibu makali juu ya kauli hizo.