wananchi
-
Akili ya Marekani inapokuwa inapanga uadui inapungua ghafla
Tarehe 11 Februari 2026, maelfu ya Wairani walikusanyika kuonyesha mshikamano wao na taifa na kuthibitisha kwamba Marekani ni adui wa Umma wa Kiislamu. Tukio hili linaonyesha wazi kwamba mbinu za adui hazina nafasi mbele ya mshikamano wa wananchi wa Iran na jitihada za kuharibu taifa hilo hazina mafanikio.
-
Mchambuzi wa kisiasa wa Lebanon katika mahojiano na shirika la habari la ABNA amesema:
“Kufanya mazungumzo na Iran ni jambo la lazima kwa Trump / Utayari wa Iran kwa vita unapunguza uwezekano wa kutokea kwa vita”
Wissam Nasif Yassin anaamini kuwa hali bado inaelekea zaidi kwenye suluhisho la mazungumzo lililo imara. Anasema kuwa chaguo la vita haliwezi kuondolewa kabisa, lakini kwa kuzingatia uwezo wa Iran, utayari wake na uungwaji mkono wa wananchi kwa uongozi wa Iran, inaonekana kuwa ni vigumu kwa upande wa pili kuthubutu kutumia chaguo la kijeshi.
-
Shahidi Sajad Zabihi: Alijitoa Muhanga Kulinda Usalama wa Wananchi wa Maeneo yenye uhitaji (Vijijini)
Wananchi na viongozi mbalimbali wamemuenzi Shahidi Zabihi kama shujaa wa taifa aliyesimama kulinda heshima, usalama na ustawi wa jamii. Tukio hilo limeacha huzuni kubwa, lakini pia limeongeza ari ya kulinda amani na mshikamano wa kitaifa.
-
Sababu za Sayyid Ali Khamenei Kukubalika Hata Ndani ya Jamii za Wananchi wa Ulaya
Sayyid Ali Khamenei hakubaliki kwa sababu ya utaifa au dini tu, bali kwa sababu: 1_Anawakilisha kupinga dhulma. 2_Anaonekana kuwa na msimamo. 3_Na anazungumza lugha ya waliodhulumiwa ambayo huvuka mipaka ya dini na rangi.
-
Rais Samia Afanya Mazungumzo na Viongozi wa Wizara ya Ulinzi na JKT Zanzibar
Mazungumzo hayo yamezingatia masuala mbalimbali ya usalama, ulinzi wa taifa, na maendeleo ya majeshi, huku akisisitiza umuhimu wa ushirikiano kati ya majeshi na wananchi katika kuhakikisha amani na utulivu wa taifa.
-
-
Rais wa Taasisi ya Tafiti za Kistratejia “Naba’” ya Iraq katika mazungumzo na ABNA:
Uamuzi wa mwisho ni wa Iraq, si wa Marekani / Mfumo wa Uratibu wa Kishia una mkono wa juu
Sambamba na kuongezeka kwa harakati za kisiasa kwa ajili ya kubainisha muundo wa serikali ijayo ya Iraq, Hashim Al-Kandi ameeleza kurejea kwa mshikamano wa Mfumo wa Uratibu wa Kishia, kuundwa kwa kamati maalumu za kumchagua Waziri Mkuu, pamoja na kukaribiana kwa mikondo ya Kisunni na Kikurdi, na kusisitiza kuwa hakuna kikwazo kikubwa katika njia ya kuunda serikali.
-
Kamanda wa Jeshi la Ardhi la IRGC:
Umoja wa Shia na Sunni ni rasilimali ya kimkakati ya Taifa la Iran
Kamanda wa Jeshi la Ardhi la IRGC katika sherehe ya kuapishwa na kualikwa kwa kamanda mpya wa Kituo cha Medinah Munawwarah, akiwa ameisisitiza umuhimu wa kudumisha mshikamano wa kitaifa, alitaja umoja wa Shia na Sunni kama rasilimali ya kimkakati ya taifa la Iran.
-
Imamu wa Ijumaa wa Michigan:Dunia imejifunza kutokana na uongozi wa Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi /Ushindi wa kuvutia wa Iran katika vita vya siku 12
Hujjatul-Islam wal-Muslimin Basim Al-Shar’i amesema kuwa hatari kuu kwa Jamhuri ya Kiislamuinatokana na mambo ya ndani, na akaongeza: “Nguvu ya wananchi wa Iran imo katika umoja wao na kushikamana kwao na uongozi wenye busara wa Ayatullah Khamenei. Umoja huu ndio heshima na mtaji halisi wa Jamhuri ya Kiislamu.”
-
Rais wa Shirika la Nishati ya Atomiki: Teknolojia ya nyuklia ni viwanda na mwanga wa afya kwa wananchi wa Iran
Rais wa Shirika la Nishati ya Atomiki ya Iran katika hafla ya ufunguzi wa Kituo cha Mionzi kaskazini-magharibi mwa nchi, alieleza kwamba teknolojia ya nyuklia ni tasnia ya kisasa, na matumizi ya mionzi ni hatua muhimu katika kuboresha afya na usalama wa chakula nchini. Pia alisisitiza kuwa teknolojia hii inaweza kuleta baraka nyingi kwa wananchi wa Iran.
-
Mashambulizi ya Kipuuzi Zaidi Kufuatia Kuongezeka kwa Umaarufu na Ushindi wa Mamdani katika Uchaguzi wa Awali wa Umeya wa New York
Zahran Mamdani, Mbunge wa jimbo na mgombea wa chama cha Demokratik katika uchaguzi wa Umeya wa New York, kupitia kampeni za wananchi amefanikiwa kuwashinda wapinzani maarufu kama Andrew Cuomo katika kinyang’anyiro cha awali na kuwa mgombea wa kwanza Mwislamu kwa nafasi hiyo. Ushindi huo, hata hivyo, umekumbwa na mashambulizi ya chuki na matusi ya Uislamu kutoka kwa baadhi ya wanasiasa, lakini yeye pamoja na wafuasi wake wametangaza kuwa hawatarudi nyuma mbele ya chuki na ubaguzi.
-
Kiongozi wa Mapinduzi atazungumza na wananchi usiku wa leo
Sambamba na Wiki Takatifu ya Ulinzi (au Wiki ya Utetezi Mtukufu - Sacred Defence), Ayatollah Khamenei atazungumza na Wananchi wa Iran na Ulimwengu mzima Usiku wa leo akidadavua masuala mbalimbali ya kitaifa na kimataifa.
-
Kupigwa kwa Kengele ya Ujasiri katika Shule 1300 za Mkoa wa Gilan Wakati wa Wiki ya Ulinzi wa Kiutukufu
Naibu Mratibu wa Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi (Sepah Qods) – Mkoa wa Gilan, Kanali Ahmad Reza Manshouri, ameeleza kuwa sambamba na maadhimisho ya Wiki ya Ulinzi wa Kiutukufu, shule 1300 katika mkoa huo zitashiriki katika kupiga kengele ya ujasiri na kuimba kwa pamoja wimbo wa uzalendo "Ey Iran".
-
Muqtada al-Sadr Ataka Iraq Ianzishe Mazungumzo na Uturuki Kuhusu Mgogoro wa Maji
Kufuatia kupungua kwa vyanzo vya maji nchini Iraq, Muqtada al-Sadr ametoa wito wa kuanzishwa kwa mazungumzo na Uturuki ili kuongeza mgao wa maji, na ametahadharisha kuhusu athari za mgogoro wa maji kwa afya na kilimo cha wananchi.
-
Maduro: Mamilioni ya Wavenezuela wako tayari kwa vita na kukabiliana na wavamizi wa Kimarekani
Rais wa Venezuela, huku akilaani shambulio la utawala wa Kizayuni dhidi ya Qatar, ametangaza kuwa wananchi wa nchi hiyo wako tayari kwa vita dhidi ya wavamizi wa Marekani.
-
Ujumbe wa Rambirambi kutoka kwa Ayatullah Dori Najafabadi kwa Watu wa Yemen: "Ushujaa wa Mashahidi Utaimarisha Umoja Dhidi ya Adui wa Kizayuni"
Ninawapa pole familia za mashahidi hawa wapendwa na wananchi wote wa Yemen. Tunawakumbuka mashahidi wote wa Uislamu: kuanzia mashahidi wa tukio la Fakh, mashahidi wa Palestina, Lebanon, na mashahidi wetu wa Iran kama vile Shahidi Qassem Soleimani na wengine.
-
Maafisa wa Kiyemeni katika mazungumzo na Abna:
"Madai ya Israel ni udanganyifu na kupindisha mambo ili kufidia udhaifu katika uwanja wa mapambano / Msaada kwa Gaza hautasitishwa"
"Abdulaziz al-Bakr", Katibu Mkuu wa chama cha "Ujamaa wa Kitaaluma wa Kiyemen" na "Hizam al-Asad", mjumbe wa ofisi ya kisiasa ya harakati ya Ansarullah ya Yemen, katika mazungumzo na shirika la habari la Abna wamesisitiza kuwa: Kila shambulio linalolenga raia wasio na hatia huko Sana'a linageuka kuwa mafuta ya ziada kwa ajili ya harakati ya mapambano ya wananchi wa Yemen.
-
Katika Kumbukizi ya Imam Reza (a.s): Kiongozi Mkuu Atoa Wito wa Kulinda Umoja na Kukemea Jinai za Kizayuni
Ayatollah Khamenei: "Marekani Haitaki Iran Isimame Imara, Bali Itii Amri Zake".
-
Beirut - Wananchi wa Lebanon Wamiminika Mitaani Kuiunga Mkono Hizbullah na Mapambano ya Muqawama
Wakisambaza ujumbe wao kwa sauti na maandamano, wananchi hao wamesisitiza kuwa Hizbullah si tu harakati ya kijeshi, bali pia ni nguzo muhimu ya taifa katika ulinzi wa mipaka na heshima ya Lebanon. Kwao, wazo la kuondoa silaha za harakati hiyo ni sawa na kuiweka Lebanon mikononi mwa maadui wake.
-
Kukamatwa kwa Mawakala 87 wa Utawala wa Kizayuni katika Mkoa wa Lorestan, Magharibi mwa Iran
Watu hao 87 waliotiwa mbaroni wanatuhumiwa kwa kueneza hofu miongoni mwa raia, kufanya vitendo vya uharibifu, kuwasiliana na mashirika ya kijasusi ya kigeni, na kumiliki vilipuzi.
-
Mafanikio mawili ya Yemen ndani ya siku moja; Mashambulizi ya Kimaonyesho dhidi ya Hodeidah yazimwa na kushindwa/Meli "Magic Seas" Yazamishwa Baharini
Yemen, imefanikiwa kuitwanga meli iliyokuwa ikielekea maeneo ya Palestina yanayokaliwa kwa mabavu na utawala haram wa Kizayuni, na kuizamisha baharini.
-
Rais wa Iran Dkt.Pezeshkian: "Tumejifunza kutoka kwa Hussein bin Ali (AS) namna ya Kutonyenyekea, Kutokuwa dhalili na kusujudia dhulma"
Rais wa Iran amesisitiza: Tumejifunza kutoka kwa Imam Hussein ibn Ali (AS) kutonyenyekea, kutojidhalilisha na kutosujudia dhulma.
-
Televisheni yenye kufuata mrengo wa Kizayuni "Iran International" imeanguka, na sasa BBC imechukua nafasi yake
Katika dunia ya sasa, ni vigumu kujua ukweli kamili kwa urahisi, hivyo ni muhimu kuwa na vyombo vya habari vya kuaminika vinavyotumia vyanzo vya haki na kuthibitisha taarifa kabla ya kuzisambaza. Hivyo ndio Vyombo vya kufuatilia na kusikiliza. Na sio kufuata kila chombo cha Habari bila kujua kuwa hiki chombo kinatumiwa na waovu wa uistikbari wa Dunia au la.
-
Sayyid Ali Khamenei: "Utawala wa Kizayuni haukufikiria kamwe kupokea mashambulizi kama haya kutoka kwa Jamhuri ya Kiislamu".
Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu - Leo akihutubia Taifa la Iran, ametoa ufafanuzi mzuri mno wa matukio yalivyojiri, na kauli imara za kutia moyo kwa wananchi wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran, ambazo kwa hakika zimeonyesha mshikamano wa kitaifa, ujasiri, na kukataa kuachia madikteta au nguvu za kigeni na kibeberu kutawala na kuidhibiti Kijeshi Mashariki ya Kati. Pia, kauli za Kiongozi huyu imara na mwenye busara na hekima ya hali ya juu, zinaonyesha msimamo wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran katika kukabiliana na mashambulizi ya nje, na kutotetereka katika suala zima la kuifyekelea mbali mikono ya adui yeyote yenye nia ovu dhidi ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran.
-
Umati wa Wananchi wa Malaysia wameandamana kuonyesha sapoti yao kwa Iran mbele ya Ubalozi wa Marekani Mjini Kuala Lumpur
Hivi karibuni Dunia itashuhudia Haki ikiishinda batili na Imani ikishinda ukafiri.
-
Kiongozi cha Ansarullah Yemen:
"Jinai dhidi ya Iran hata bada ya kusisitiza kuwa haina haja ya silaha za Nyuklia ni kwa sababu ya misimamo imara Iran juu ya kadhia ya Palestina"
Wamagharibi hatwaki kuona Iran ikiwa ni nchi huru, na hii ni kutokana na msimamo wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran katika kuwatetea wananchi wa Palestina na kukataa udhalimu wa uvamizi wa Kizayuni kwa ardhi za Taifa la Palestina.
-
Safari za ndege zimehairishwa hadi ilani nyingine/Shule, Misikiti, na njia za chini ya ardhi zitafunguliwa kwa umma saa 24 kwa siku kuanzia leo usiku
Msemaji wa Serikali amesema: "Hakuna shida katika kusafirisha bidhaa, dawa, chakula, na mahitaji ya watu, haswa mafuta."
-
Imam Khomein Akumbukwa: Mamia Wahudhuria Maadhimisho ya Kifo Chake Jamiat Al-Mustafa, Dar es Salaam
Imam Khomein (ra) anakumbukwa duniani kote kama mtetezi wa wanyonge, hususan kwa msimamo wake thabiti katika kuwatetea Waislamu wa Palestina na wananchi wa Palestina kwa ujumla.
-
Ukurasa wa Ukandamizaji wa Usalama huko Bahrain: Vita vya Serikali dhidi ya Wananchi vinaendelea
Serikali ya Bahrain imezidisha tena juhudi zake za kiusalama, kuanzisha wimbi jipya la ukandamizaji, kuwakamata na kuweka vizuizi vikali dhidi ya wapinzani, wanaharakati na hata wananchi wa kawaida; mkakati ambao umekuwa msingi wa kuendelea kwa utawala huu kwa miaka mingi.
-
Rais Museveni na Mkewe Waomba Radhi kwa Wananchi wa Uganda, Watoa wito wa Amani na Uwajibikaji
Hatua hii inaonyesha dhamira yao ya kuendelea kuongoza kwa uwazi na heshima.