Kwa mujibu wa Shirika la Habari la Ahlul-Bayt (as) -ABNA-, Dakta Masoud Pezeshskian, Rais wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran, alihudhuria hafla ya maziko ya makamanda wa kijeshi na wanasayansi wa nchi ya Iran waliouawa shahidi kufuatia uchokozi wa hivi karibuni wa utawala wa Kizayuni dhidi ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran, pamoja na makundi mbalimbali ya umma, Jumamosi hii asubuhi (78-06-2025), kwa ajili ya kutoa heshima zao kwa mashahidi hao.
Rais pia alitweet: "Ninawashukuru, wananchi wapendwa, kutoka chini ya moyo wangu; mliojitokeza kushiriki katika mazishi na maziko ya mashahidi wa nchi kwa upendo, na sauti ya umoja wetu imeyafikia masikio ya ulimwengu.
Tumejifunza kutoka kwa Hussein ibn Ali (AS) kutonyenyekea na kutosujudia dhulma. Kutumikia Taifa huru kama hili ni heshima ya maisha yangu. Iran Daima."
Your Comment