jamhuri ya kiislamu ya Iran
- 
                                    
                                    Dkt. Pezeshkian katika Mazungumzo na Waziri wa Mambo ya Ndani wa Oman:
Iran na Oman zimekuwa zikisaidiana daima katika nyakati za mivutano ya eneo
Hamad bin Faisal Al-Busaidi alielezea furaha yake kwa ziara yake nchini Iran na kukutana na Rais Pezeshkian, akisema kuwa uhusiano wa Iran na Oman ni wa kipekee, wa kihistoria, wa kina na wa ukweli, usio na mashaka. yoyote.
 - 
                                    
                                    Waziri wa Mambo ya Nje:
Ulinzi Usio wa Kijeshi lazima uwe makini na wenye umakini wa hali ya juu
Kauli hiyo imetolewa katika ujumbe wake maalum kwa mnasaba wa Wiki ya Kuheshimu Ulinzi Usio wa Kijeshi, ambapo amesema kuwa kipindi hiki ni fursa muhimu ya kueleza umuhimu wa mikakati na mipango ya kuongeza usalama, uimara, na kinga ya miundombinu ya taifa dhidi ya kila aina ya vitisho vya maadui.
 - 
                                    
                                    Jeshi la Israel ladaiwa kumuua “Muhammad Akram Arabiyeh” mwanachama wa Kikosi cha Rizwan cha Hezbollah
Kwa mujibu wa vyanzo vya Kizayuni, katika kuendeleza uvamizi wake ndani ya ardhi ya Lebanon na mashambulizi dhidi ya wapiganaji wa muqawama, mwanachama wa Kikosi Maalumu cha Ridhwan cha Hezbollah ameuawa shahidi katika shambulizi la anga lililofanywa na Israel katika eneo la al-Qulay‘a, kusini mwa Lebanon.
 - 
                                    
                                    Enayati: Miezi Miwili Ijayo Itakuwa Kipindi Chenye Harakati Nyingi katika Uhusiano wa Tehran–Riyadh
Balozi wa Iran nchini Saudi Arabia ametangaza kuwa kutakuwa na harakati kubwa za kidiplomasia katika miezi miwili ijayo, akibainisha kuwa angalau mawaziri watatu wa Iran watahudhuria mikutano ya kimataifa na ya kikanda itakayofanyika Riyadh.
 - 
                                    
                                    Barua ya Iran, Urusi na China kwa Grossi: Wajibu wa Kuripoti wa IAEA Umefikia Mwisho
Wawakilishi wa kudumu wa Iran, Urusi na China katika Wakala wa Kimataifa wa Nishati ya Atomiki (IAEA) wamemwandikia barua rasmi Rafael Grossi, Mkurugenzi Mkuu wa wakala huo, wakisisitiza kuwa kwa kumalizika kwa muda wa utekelezaji wa Azimio la 2231 la Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa, jukumu la IAEA la kuwasilisha ripoti chini ya azimio hilo limefikia mwisho, na kwamba hatua yoyote mpya katika mwelekeo huo haina uhalali wa kisheria.
 - 
                                    
                                    Mahojiano na Mwanaharakati Mnyemeni na Shirika la Habari la ABNA;
Kuhusu Utambulisho wa Kiyemen na Sifa za Sayyid al-Houthi hadi kwenye “Bendera ya Yamen” / Kizazi kijacho nchini Yemen kitakuwa kizazi imara
Sisi na Iran ni Mwili Mmoja Uhusiano wetu na Jamhuri ya Kiislamu ya Iran ni wa kindugu uliyojengwa juu ya msingi wa Uislamu, si madhehebu. Tunafuata aya tukufu isemayo: «إِنَّمَا الْمُؤْمِنُونَ إِخْوَةٌ» - “Hakika waumini ni ndugu.”
 - 
                                    
                                    Kamanda Mkuu wa Majeshi ya Iran, Meja Jenerali Abdolrahim Mousavi:
“Vikosi vya Ulinzi vya Iran vimewapiga maadui zao Kofi lisilosahaulika”
Jenerali Mousavi alisema kuwa kipindi cha masomo ya kijeshi kwa wanafunzi hao kilitokea katika wakati wa kipekee - wakati ambao muqawama ulithibitisha ushindi wa imani juu ya dhulma na ubabe wa kimataifa.
 - 
                                    
                                    Kiongozi Mkuu wa Mapinduzi ya Kiislamu:“Wazayuni hawakutarajia nguvu ya makombora ya Iran / Marekani haina haki kujihusisha na teknolojia ya Iran"
Ayatollah Sayyid Ali Khamenei amebainisha kwamba: Marekani haina haki kujihusisha na suala la teknolojia ya nyuklia ya Iran - na akahoji kuhusiana na Trump akisema: Wewe ni nani hasa?”.
 - 
                                    
                                    Rais wa Shirika la Nishati ya Atomiki: Teknolojia ya nyuklia ni viwanda na mwanga wa afya kwa wananchi wa Iran
Rais wa Shirika la Nishati ya Atomiki ya Iran katika hafla ya ufunguzi wa Kituo cha Mionzi kaskazini-magharibi mwa nchi, alieleza kwamba teknolojia ya nyuklia ni tasnia ya kisasa, na matumizi ya mionzi ni hatua muhimu katika kuboresha afya na usalama wa chakula nchini. Pia alisisitiza kuwa teknolojia hii inaweza kuleta baraka nyingi kwa wananchi wa Iran.
 - 
                                    
                                    Iran Yazindua Makombora Mapya Yenye Uwezo wa Kuongozwa Angani
Wataalamu wa kijeshi wanaona kuwa teknolojia ya kuongozwa kwa Makombora yakiwa angani inafanya makombora hayo kuwa na faida kubwa kutokana na uwezo wake wa kurekebisha au kubadilisha mwelekeo kwa wakati halisi na Sahihi, jambo linaloongeza usahihi na kupunguza uwezekano wa kuruka hadi mbali bila kufikia shabaha yake.
 - 
                                    
                                    Wizara ya Ulinzi ya Iran: Hakuna Nguvu Yenye Haki ya Kuingilia Uwezo wa Makombora ya Iran
Kwa mujibu wa taarifa ya Wizara ya Ulinzi, Brigedia Talaeinik alibainisha kuwa Marekani na washirika wake wanasisitiza mazungumzo kuhusu programu ya makombora na wanataka kupunguza umbali wa makombora ya Iran. Hata hivyo, alisema kuwa msingi wa uwezo wa makombora ya Iran ni kulinda usalama na maslahi ya kitaifa ya wananchi wake.
 - 
                                    
                                    Jeshi la Iran Lathibitisha kuendelea kutoa Msaada wa Kimkakati kwa wana Harakati za Uhuru za kuyakomboa Mataifa yao dhidi ya Ukoloni na Ukandamizaji
Hatua hii ya Iran inaashiria msimamo wake thabiti katika kuhimiza uhuru na kuunga mkono harakati za kupinga ukandamizaji wa kigeni na ukoloni duniani kote.
 - 
                                    
                                    Kiongozi wa Mapinduzi katika hotuba ya televisheni kwa taifa la Iran:
''Umoja wa Kitaifa wa Iran ni ule ule wa Tarehe 13 Juni 2009; Wote wanawajibika''
Mheshimiwa Ayatollah Khamenei, Kiongozi Mkuu wa Mapinduzi ya Kiislamu, usiku huu katika hotuba ya televisheni akiwahutubia watu, aliueleza umoja na mshikamano wa kudumu wa taifa la Iran kuwa ni ngumi ya chuma juu ya kichwa cha adui.
 - 
                                    
                                    Je, ilikuwa sahihi kutumia vijana baleghe wachanga katika Vita vya Kulazimishwa (Vita vya Iran na Iraq)?
Nchi kadhaa za Ulaya, ikiwemo Ujerumani, zimeruhusu kisheria ajira ya zaidi ya watoto askari 1,500 chini ya utaratibu wa kipekee wa jeshi.
 - 
                                    
                                    Mkuu wa Majeshi: Vikosi vya Ulinzi vya Iran Vitatoa Jibu Kali Zaidi ya Mawazo ya Wavamizi
“Kwa msaada wa Mwenyezi Mungu na kwa mwongozo wa Kiongozi Muadhamu Ayatollah Imam Khamenei (Mwenyezi Mungu amlinde), vikosi vya ulinzi vya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran viko tayari kugeuza tishio lolote kuwa fursa ya kustawisha nguvu za taifa na kuinua hadhi ya Iran katika mizani ya kimkakati ya kikanda na kimataifa. Jibu letu kwa maadui litakuwa la wakati, kali, la kuumiza na zaidi ya walivyowahi kufikiria.”
 - 
                                    
                                    Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu (IRGC) Lalaani Mauaji ya Kinyama ya Wazayuni Dhidi ya Yemen-Laahidi Jibu Kali kutoka kwa Muqawama wa Kiislam
"Kinyume na matarajio ya Wazayuni na waungaji mkono wao, jinai hizi hazitaweza kudhoofisha irada ya mapambano ya wananchi wa Yemen, bali damu ya mashahidi hawa watukufu itachochea zaidi hasira na mwamko wa upinzani dhidi ya ukoloni na utawala wa Kizayuni kote katika eneo".
 - 
                                    
                                    Jeshi la Iran:
"Majibu ya Iran yatakuwa makali zaidi iwapo adui atafanya kosa”
Jeshi Kuu la Iran lilibainisha kuwa katika tukio la kosa la kimahesabu kutoka kwa adui, kile kilichozuia operesheni kubwa wakati wa vita vya siku 12 vilivyopita hakitarudiwa tena.
 - 
                                    
                                    Usimamizi wa Uingiaji wa Maashura ya Kiirani Nchini Iraq Kufanywa na Ataba Tukufu ya Husseiniyya
Kitengo cha Forodha na Mipaka kinachohusiana na Idara ya Mahusiano ya Umma cha Ataba Tukufu ya Husseiniyya, ambacho kimepewa majukumu haya, kina uzoefu wa zaidi ya miaka 8 katika uwanja huu na kimekuwa kikifanya kazi kwa ufanisi mkubwa hata katika mazingira magumu zaidi ili kuhakikisha kuingia kwa maashura mjini Karbala kunafanyika kwa utaratibu na urahisi.
 - 
                                    
                                    Hashd ni nguzo ya hema, na Muqawama ni heshima ya Umma wa Iraq / Hatutapatanishwa na Wavamizi
Al_Walaiy: “Tunaiweka hai Gaza ndani ya nyoyo zetu na tuko tayari daima kuwasaidia.” Alieleza kuwa ushindi wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran ni furaha kwao, na kwamba ndugu zao wa Lebanon ni mfano wa ushindi - ushindi uliotabiriwa na Qur’an Tukufu.
 - 
                                    
                                    Madrasa Hazrat Zainab (sa) | Dini na Afya: Dkt. Beshteri Azungumzia Umuhimu wa Lishe Sahihi kwa Muislamu
Dkt. Beshteri alieleza kuhusu adabu za kula chakula kulingana na mafundisho ya Imam Ja’far Sadiq (a.s), akitaja riwaya mbalimbali zinazoelekeza namna bora ya kula kwa mujibu wa maadili ya Kiislamu.
 - 
                                    
                                    Mafanikio Makubwa ya Iran: Yarusha Satelaiti (Nahid-2) katika Obiti na Kufanikiwa Kutesti Kombora la Khorramshahr-5 lenye uwezo wa kufika hadi 12000KM
Iran imejiweka kwenye orodha ya mataifa 9 duniani yaliyofanikiwa kubuni, kutengeneza na kurusha satelaiti yake kwa uwezo wa ndani kabisa.
 - 
                                    
                                    Pezeshkian: Madai ya Trump kuhusu kukomesha mpango wa Nyuklia wa Iran ni Udanganyifu
Katika mahojiano na gazeti la Al-Jazeera, Rais wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran sambamba na kusisitiza utayarifu wake wa kukabiliana na utawala wa Kizayuni, aliyataja mazungumzo ya kuhitimisha mpango wa nyuklia wa Iran kuwa ni ndoto na njozi. Aidha, alisema: Hatutaki Vita, lakini Tuko Tayari Kujilinda kwa Nguvu Zetu Zote.
 - 
                                    
                                    Lariyani: “Mazungumzo Sio Kipaumbele Sasa – Adui Lazima Kueleza Kwanza Sababu ya Vita”
Mazungumzo ni (Taktiki) mbinu tu ya Kisiasa inayotumika kufikia lengo Maalum. “Muachieni Kiongozi wa Mapinduzi aamue ni wakati gani na wapi ni sahihi kutumia mbinu hii.”
 - 
                                    
                                    Ripoti ya ABNA kuhusu Kongamano la Kitaifa la Dini za Ki_Mungu na Uvamizi wa Wazayuni:
Umuhimu wa kuchukuliwa hatua za kivitendo dhidi ya uvamizi wa utawala wa Kizayuni;Kunyongwa kwa Trump na Netanyahu na kuunda Upinzani wa Kimataifa
Kufuatia uvamizi wa hivi karibuni wa utawala wa Kizayuni dhidi ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran, baadhi ya viongozi wa dini zinazomuamini Mungu nchini walikusanyika katika Kongomanano la Kitaifa la “Dini za Ki_Mungu na suala la Uvamizi wa Kizayuni na Magharibi dhidi ya Iran”. Katika Kongamano hilo, walilaani vikali kitendo hicho na kusisitiza umuhimu wa kusimama kidete dhidi ya dhuluma, umoja wa dini za Mwenyezi Mungu Mmoja, na kusherehekea mchango wa kipekee wa utamaduni wa Kiarabu katika kuhifadhi heshima, amani, na upinzani.
 - 
                                    
                                    Himaya thabiti ya Allama Sajid Naqvi kwa Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi/Syed Khamenei Shkhsia wa Kimataifa anayeheshimika katika Ulimwengu wa Kiislamu
Akikosoa matamshi ya hivi karibuni ya kimatusi dhidi ya Ayatullah Sayyid Ali Khamenei amesema kuwa, Kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu ya Iran ni Shakhsia mwenye hadhi ya Kimataifa katika Umma wa Kiislamu, na kauli yoyote ya kumtusi inaweza kuwa na matokeo mabaya na ya kutia wasiwasi.
 - 
                                    
                                    Wayahudi Wanaopinga Uzayuni Wametoa Pongezi kwa Mashahidi wa Mashambulizi ya Israel Dhidi ya Iran
Mayahudi wanao uchukia Uzayuni huko New York, walihudhuria katika Ofisi ya Ujumbe wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran katika Umoja wa Mataifa mjini New York na kutoa heshima zao kwa Mashahidi wa Mashambulizi ya Utawala wa Kizayuni.
 - 
                                    
                                    Mchambuzi wa Kiyahudi: "Kwa Nini Tumeshindwa Vita na Iran Imeshinda Vita?"
Mchambuzi huyu wa Kiyahudi, Goldberg alisisitiza zaidi kuwa Makombora ya Iran yalilenga kwa usahihi mno Shabaha zake, na yameibuka kwa heshima kubwa kimataifa. Badala ya kusambaratika, Iran imeonekana kuwa Taifa thabiti na lenye msimamo wa kupambana na uonevu wa yeyote.
 - 
                                    
                                    Ikiwa hatari itatishia Iran, Wairaq hawatanyamaza kimya
Iran haijaomba msaada kwa makundi ya Muqawama ya Iraq, lakini iwapo wananchi wa Iraq wanahisi kwamba hatari ya kweli inatishia Iran, mashujaa watanyanyuka kutoka katika kila nyumba nchini Iraq na kuiangamiza Marekani na utawala wa Kizayuni.
 - 
                                    
                                    Rais wa Iran Dkt.Pezeshkian: "Tumejifunza kutoka kwa Hussein bin Ali (AS) namna ya Kutonyenyekea, Kutokuwa dhalili na kusujudia dhulma"
Rais wa Iran amesisitiza: Tumejifunza kutoka kwa Imam Hussein ibn Ali (AS) kutonyenyekea, kutojidhalilisha na kutosujudia dhulma.
 - 
                                    
                                    Televisheni yenye kufuata mrengo wa Kizayuni "Iran International" imeanguka, na sasa BBC imechukua nafasi yake
Katika dunia ya sasa, ni vigumu kujua ukweli kamili kwa urahisi, hivyo ni muhimu kuwa na vyombo vya habari vya kuaminika vinavyotumia vyanzo vya haki na kuthibitisha taarifa kabla ya kuzisambaza. Hivyo ndio Vyombo vya kufuatilia na kusikiliza. Na sio kufuata kila chombo cha Habari bila kujua kuwa hiki chombo kinatumiwa na waovu wa uistikbari wa Dunia au la.