jamhuri ya kiislamu ya Iran
-
Nchi 11 zalaani uvamizi wa Israel dhidi ya Iran katika kikao cha Baraza la Magavana
Katika taarifa ya nchi kumi na moja wanachama wa Bodi ya Magavana, inachukulia kuwa "shambulio lolote la silaha au tishio dhidi ya vituo vya nyuklia vinavyotolewa kwa madhumuni ya amani ni ukiukaji wa kanuni za Mkataba wa Umoja wa Mataifa, sheria za kimataifa na Mkataba wa Shirika la IAEA."
-
Waisraeli 24 wauawa na 592 kujeruhiwa katika mashambulizi ya makombora ya Iran katika maeneo yanayokaliwa kwa mabavu
Ofisi ya habari ya Israel imeripoti kuwa, tangu kuanza mashambulizi ya makombora mazito ya Jamhuri ya Kiislamu ndani ya Palestina inayokaliwa kwa mabavu, Wazayuni 24 wameuawa na wengine 592 wamejeruhiwa.
-
Uchokozi wa Israel: Rais wa Iran aitaka Iraq kulinda mipaka yake, anga
Picha ya mchanganyiko inawaonyesha Rais wa Iran Masoud Pezeshkian (Kulia) na Waziri Mkuu wa Iraq Muhammad Shayya al-Sudani.
-
Safari za ndege zimehairishwa hadi ilani nyingine/Shule, Misikiti, na njia za chini ya ardhi zitafunguliwa kwa umma saa 24 kwa siku kuanzia leo usiku
Msemaji wa Serikali amesema: "Hakuna shida katika kusafirisha bidhaa, dawa, chakula, na mahitaji ya watu, haswa mafuta."
-
Iran inaendelea Kuichakaza Israel kwa Makombora Hatari ya Balistiki
Wazayuni wanahaha na kutangatanga baada ya Iran kutuma shambulizi la wimbi jipya la Makombora ya Balistiki.
-
Wimbi la Makombora ya Iran Limelenga Ngome za Israel
Mashambulizi haya ya makombora ya balestiki yamesababisha hali ya taharuki kubwa, huku ving’ora vya hatari vikipigwa kote katika maeneo ya utawala huo ghasibu.
-
Mashambulizi makubwa ya makombora ya Iran dhidi ya Israel, watu 204 wameuawa na kujeruhiwa, uharibifu mkubwa usiokuwa na kifani katika Mji wa Tel Aviv
Iran, kuanzia usiku wa jana hadi sasa, imevurumisha takriban makombora ya masafa marefu 200 kuelekea malengo mbalimbali katika maeneo ya kati na kaskazini mwa Israel.
-
Tamko la Jumuiya ya Kimataifa ya Ahlul-Bayt (a.s) kuhusu mashambulizi ya utawala wa Kizayuni dhidi ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran
Jumuiya ya Kimataifa ya Ahlul-Bayt (a.s) imesisitiza katika tamko lake kwamba: kuanzisha vita dhidi ya Iran ya Kiislamu ni sawa na kuvamia harem (makao matakatifu) ya Ahlul-Bayt (a.s). Katika hali hii, wanaharakati wote wa haki duniani, hasa mashirika na jumuiya zilizo chini ya mwavuli wa Ahlul-Bayt na wale wanaohusishwa na Jumuiya hii, wanaweza sasa kwa sauti kubwa kuliko wakati wowote kusema wazi kuwa utawala wa Kizayuni ni wa kigaidi na mvamizi. Aidha, taifa la Iran, likiwa limeungana zaidi na thabiti kuliko wakati wowote, litatoa jibu kali na la wazi kwa utawala huu wa kihalifu na muuaji wa watoto.
-
Brigedia Jenerali Sayyid Majid Mousavi Ateuliwa Kuongoza Kikosi cha Anga cha IRGC
Katika amri rasmi ya uteuzi, Ayatullah Khamenei amesisitiza umuhimu wa: Kuimarisha uwezo wa makombora na ndege zisizo na rubani
-
Maneno ya Ayatullah Ustadh Abdullah Jawadi Amuli: “Rudisha jiwe, kokote kule lilipotoka"
Ujumbe wa muhimu wa Ayatollah Jawad Amuli kuhusu Jinai ya Kizayuni dhidi ya Iran umetolewa hivi punde.
-
Kiongozi Mkuu wa Mapinduzi ya Kiislamu: Utawala wa Kizayuni Lazima Usubiri Adhabu Kali – Mkono wa Nguvu wa Jeshi la Iran Hautauacha Salama
Kiongozi Mkuu wa Mapinduzi ya Kiislamu: Mkono wa Nguvu wa Jeshi la Kiislamu Hautauacha Utawala wa Kizayuni - Kwa idhini ya Mwenyezi Mungu
-
Kiongozi Mkuu: Msimamo Usioyumba wa Taifa la Iran Ni Ishara ya Uwezo na Dhamira ya Kitaifa – Wabunge Wahimizwa Kulinda Hadhi ya Bunge la Kiislamu
Katika mkutano na Spika na wabunge wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran, Kiongozi Mkuu wa Mapinduzi ya Kiislamu amesema: "Iran Haijawahi Kuyumba Mbele ya Mashinikizo ya Kimataifa".
-
Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran: Haki za Nyuklia za Iran Lazima Ziheshimiwe Katika Mazungumzo
Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran: Uhuru wa Kisiasa ni Asili ya Sera ya Kigeni ya Jamhuri ya Kiislamu – Haki za Nyuklia Lazima Zihifadhiwe Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran katika mazungumzo maalum amesisitiza kuwa uhuru wa kisiasa ni nguzo kuu ya sera ya kigeni ya Iran, akieleza kuwa taifa hilo limekuwa likijitahidi daima kujiepusha na utegemezi au kuingiliwa na madola ya kigeni.
-
Rais wa Baraza la Wawakilishi la Iran Awasilisha Zawadi ya Familia ya Shahidi Soleimani kwa Rais Maduro wakati wa Ziara Caracas
Rais wa Bunge | Baraza la wawakilishi la Iran akutana na Rais Maduro Caracas, na kumkabidhi sanamu ya Jenerali Shahidi Qasem Soleimani, iliyotumwa na familia ya Shahidi Soleimani kama zawadi.
-
Naibu Waziri wa Elimu na Utamaduni atembelea Shirika la Habari la ABNA / Entemani: Tofauti za ABNA ndizo Nguvu yake
Naibu Waziri wa Elimu na Utamaduni wa Jamhuri ya Kiislamu wa Iran, alipokuwa akitembelea Shirika la Habari la ABNA, alieleza kwamba vyombo hivi vya habari vina sifa za kipekee na vina athari kubwa katika jamii.
-
Raundi mpya ya mazungumzo kati ya Iran na Marekani itafanyika Ijumaa hii Mjini Rome, Italia
Raundi ya tano ya mazungumzo kati ya Iran na Marekani inatarajiwa kufanyika siku ya Ijumaa mjini Rome, Italia. Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran ametangaza kuwa nchi yake imekubali pendekezo la Oman kwa ajili ya kikao hiki. Aidha, alisisitiza kuwa ujumbe wa Iran katika mazungumzo haya umejikita katika kulinda haki za taifa hilo na kuhakikisha kuondolewa kwa vikwazo vilivyowekwa dhidi ya Iran.
-
Naibu Waziri wa Mambo ya Nje:Vikwazo vya upande mmoja ni Ukiukaji wa Haki za Binadamu | Vikwazo na Haki za Binadamu;Mazungumzo Muhimu Yafanyika Tehran
Katika Pembeni mwa Mkutano wa Kimataifa Kuhusu Vikwazo vya Kijedwali huko Tehran: Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran katika Masuala ya Kisheria na Kimataifa amekutana na Bi. Alena Douhan, Mtaalamu Maalum wa Umoja wa Mataifa kuhusu Athari za Vikwazo kwa Haki za Binadamu. Katika mazungumzo hayo, Ali Bagheri Kani (au Garibabadi, kulingana na jina halisi) alisisitiza kuwa: Vikwazo vya upande mmoja (vya kijedwali) ni kinyume cha sheria za kimataifa. Nchi zinazoweka vikwazo hivyo zinapaswa kubeba dhamana ya kisheria kwa madhara yanayotokana na hatua zao. Na kwamba ni lazima waathirika wa vikwazo hivyo wawe na fursa ya kupata haki kupitia vyombo vya sheria.
-
Waziri wa Mambo ya Nje wa Taliban akiwa Tehran: Haki ya maji ya Iran imekuwa ikitiririka kwa mwezi mmoja sasa
Amir Khan Muttaqi, Waziri wa Mambo ya Nje wa Serikali ya Muda ya Afghanistan, amesema saa chache zilizopita katika “Jukwaa la Mazungumzo ya Tehran” kwamba: “Kwa mwezi mmoja sasa, haki ya maji ya Iran kutoka Afghanistan imekuwa ikielekezwa kuelekea Sistan na Baluchestan.”
-
Waziri wa Mambo ya Nje wa Afghanistan na Iran wamekutana na kufanya mazungumzo Mjini Tehran
Waziri wa Mambo ya Nje wa serikali ya muda ya Afghanistan, ambaye yuko Iran kwa ajili ya kushiriki katika Jukwaa la Mazungumzo ya Tehran, amekutana na Sayyid. Araghchi na kufanya mazungumzo kuhusu ushirikiano wa pande mbili, masuala ya kiusalama, hali ya wakimbizi na haki ya maji ya Iran.
-
Trump: Iran ina drone hatari sana
Iran ina droni Mzuri Sana na hatari.
-
Kwa mujibu wa Qur'an Tukufu: Kundi la Mwenyezi Mungu, linalomtii Mwenyezi Mungu, Mtume Wake, na waliokuwa Waumini wa kweli, Hao ndio washindi wa kweli
"Hezbollah" humaanisha: Kundi lililojifunga na miongozo ya Mwenyezi Mungu, linalosimama na kutetea haki, hata likiwa ni dogo au linakabiliwa na maadui wakubwa. Aya hii imekuwa nembo ya Harakati za Muqawama (Upinzani wa Kiislamu) kama vile Hezbollah ya Lebanon, Ansarullah ya Yemen, na wengineo wanaopambana dhidi ya dhulma ya mabeberu ya Kimataifa.
-
Iran yarusha Kombora la Michezo Kenya | Ni katika Kuimarisha Uhusiano Kupitia Michezo – Kati ya Iran na Kenya
Akizungumza katika kipindi cha Sports Extravaganza kinachorushwa na TV47 na kuendeshwa na Tony Kwalanda, Dkt. Gholampour alisema kuwa michezo ni daraja muhimu la kuunganisha mataifa na jamii.
-
Kuimarishwa kwa uhusiano wa kibiashara kati ya Iran na Afrika / Isfahan kuwa mwenyeji wa Mkutano wa Ushirikiano wa Kiuchumi kati ya Iran na Afrika
Waziri wa Viwanda wa Mali, katika hafla ya kufunga Mkutano wa Ushirikiano wa Kiuchumi kati ya Iran na Afrika, alisisitiza umuhimu wa kuimarisha uhusiano wa kibiashara na uwekezaji wa pamoja katika nyanja mbalimbali. Alieleza matumaini kwamba mkutano huu utasababisha mshikamano na maingiliano yenye tija kati ya pande hizo mbili, na akatambua kuwa sekta binafsi ina nafasi muhimu katika mchakato huu.
-
Serikali ya Muda ya Afghanistan Yatoa Pole kwa Watu wa Iran Kufuatia Mlupuko wa Bandar Abbas
Baada ya mlipuko uliotokea jana katika Bandari ya Shahid Rajaei iliyopo katika Mji wa Bandar Abbas, Serikali ya Muda ya Afghanistan, sambamba na mataifa mengi duniani, imetoa pole kwa watu na Serikali ya Iran.
-
Iran | Kesho ni Siku ya Maombolezo ya Kitaifa Nchini Iran / Idadi ya Waliopoteza Maisha Yafikia 28
Baada ya tukio la kusikitisha katika Bandari ya Shahid Rajaei lililosababisha vifo vya makumi ya raia wapenzi wa Iran, Baraza la Mawaziri limetangaza kuwa kesho kutakuwa na maombolezo ya kitaifa kote nchini.
-
"Hezbollah ya Lebanon imetoa pole kwa Kiongozi wa Mapinduzi na Taifa la Iran kufuatia tukio la Mlipuko wa Bandar Abbas"
Baada ya tukio la kusikitisha katika Bandari ya Shahid Rajaei Bandar Abbas lililosababisha mashahidi na majeruhi kadhaa, Hezbollah ya Lebanon imetoa taarifa ya kuonesha mshikamano na Jamhuri ya Kiislamu ya Iran.
-
Kiongozi wa Mapinduzi: Uhusiano kati ya Iran na Saudi Arabia utakuwa wa manufaa kwa nchi zote mbili / Kupanua uhusiano kati ya nchi hizi 2 kuna maadui
Katika kikao hicho Ayatollah Khamenei akiashiria baadhi ya maendeleo ya Iran amesema: Jamhuri ya Kiislamu iko tayari kuisaidia Saudi Arabia katika maeneo hayo.
-
Mshauri wa Utamaduni wa Ubalozi wa Iran, Nairobi Dkt. Ali Pourmarjan amtembelea Mwenyekiti wa Tume ya Kitaifa ya Usawa wa Jinsia ya Kenya Mhe. Rehema
Dk. Pourmarjan, mtetezi kwa bidii wa elimu, alieleza dhamira ya Ubalozi wa Iran Nchini Kenya kuwa ni kutoa ufadhili wa masomo kwa Wanafunzi wanaoishi katika mazingira magumu, kwa lengo la kuwapa fursa bora zaidi kwa maisha yao bora ya baadaye.
-
Imam Khamenei afanya ziara muhimu ya kuonesha mafanikio ya sekta binafsi mjini Tehran
Kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu Ayatullah Sayyid Ali Khamenei siku ya Jumanne amefanya ziara katika hafla iliyofanyika ili kuonesha mafanikio ya sekta binafsi.
-
Adui amechanganyikiwa na ana hofu kuhusu maendeleo ya Jamhuri ya Kiislamu / Kudumisha utayari wa hali ya juu na uboreshaji wa maunzi na programu
Ayatullah Khamenei amehusisha hasira za watu wasio na mapenzi mema (wenye nia mbaya) na mabishano yao kwenye vyombo vyao vya habari kuwa ni kuzidisha maendeleo ya Iran na kusema: "Wanabainisha mambo (matakwa) ambayo ni sehemu ya matamanio yao kwa anuani kuwa ni habari na uhakika, na ni lazima kubuni njia za kukabiliana na dhana na propaganda hizi."