mazishi
-
Wizara ya Usalama ya Iran Yapongeza Mahudhurio Makubwa ya Umma wa Kiislamu Katika Mazishi ya Kiongozi Shahidi
Wizara ya Usalama ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran imetoa taarifa ya kupongeza ushiriki mkubwa wa wananchi, Marjaa wa dini, serikali na wajumbe kutoka nchi mbalimbali za Kiislamu katika mazishi ya Kiongozi Shahidi wa Mapinduzi ya Kiislamu, ikieleza kuwa tukio hilo limeonyesha umoja, uaminifu na mshikamano wa Umma wa Kiislamu.
-
Kamanda Mkuu wa IRGC: Mazishi ya Kihistoria Iran na Iraq Yamehuisha Ahadi kwa Njia ya Kiongozi Shahidi
Kamanda Mkuu wa Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu (IRGC) amesema kuwa ushiriki wa mamilioni ya watu katika mazishi ya Kiongozi Shahidi wa Mapinduzi ya Kiislamu nchini Iran na Iraq ulikuwa ni ishara ya kuhuisha ahadi kwa misingi na njia yake, pamoja na kudhihirisha mshikamano wa Umma wa Kiislamu.
-
Rais Pezeshkian Aishukuru Iraq kwa Kuandaa Mazishi ya Kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu Sayyid Ali Khamenei (ra)
Rais wa Iran, Masoud Pezeshkian, ameishukuru serikali na wananchi wa Iraq kwa mapokezi na ushirikiano walioutoa wakati wa shughuli za kuaga na kusafirisha mwili wa Kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu, Ayatullah Sayyid Ali Khamenei, akisema taifa la Iran halitasahau kamwe mshikamano huo.
-
Iraq Yaandaa Mazishi ya Kihistoria ya Kiongozi Shahidi wa Mapinduzi ya Kiislamu Ayatollah Sayyid Ali Khamenei (ra)
Marasimu ya kihistoria ya mazishi ya mwili mtukufu wa Kiongozi Shahidi wa Mapinduzi ya Kiislamu, Ayatullah Sayyid Ali Hussein Khamenei, pamoja na mashahidi wa familia yake, yanafanyika leo nchini Iraq kwa ushiriki wa maelfu ya waombolezaji.
-
Rais wa Iran Masoud Pezeshkian Awasili Najaf Kushiriki Mazishi ya Kiongozi Shahidi Ayatullah Sayyid Ali Khamenei
Rais wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran, Dkt. Masoud Pezeshkian, amewasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Najaf nchini Iraq kwa ajili ya kushiriki katika mazishi ya Kiongozi Shahidi Ayatullah Sayyid Ali Khamenei, ambapo alipokelewa na Waziri Mkuu wa Iraq pamoja na viongozi wengine waandamizi wa nchi hiyo.
-
Makao Makuu ya Khatam al-Anbiya: Iran Haitaruhusu Uingiliaji wa Usimamizi wa Mlango wa Bahari wa Hormuz
Makao Makuu ya Khatam al-Anbiya (s) yametangaza kuwa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran haitaruhusu kwa hali yoyote uingiliaji wa mamlaka yoyote katika usimamizi wa Mlango wa Bahari wa Hormuz, huku yakiahidi kutoa jibu kali dhidi ya kile ilichokitaja kuwa uchokozi wa Marekani.
-
Jenerali Qaani: Mazishi ya Sayyid Ali Khamenei Nchini Iraq Yataimarisha Umoja Dhidi ya Fitna na Kuhuisha Wito wa Haki
Kamanda wa Kikosi cha Quds amesema marasimu ya mazishi ya Sayyid Ali Khamenei nchini Iraq yataonyesha mshikamano wa wananchi wa Iraq na Iran, na kuimarisha msimamo wa pamoja dhidi ya fitna na migawanyiko.
-
Mkuu wa Mhimili wa Mahakama Awashukuru Waombolezaji wa Mazishi ya Kiongozi Shahidi Ayatollah Sayyid Ali Khamenei
Mkuu wa Mhimili wa Mahakama wa Iran amesema mahudhurio ya mamilioni ya wananchi katika mazishi ya Kiongozi Shahidi Ayatollah Sayyid Ali Khamenei yameandika ukurasa mpya wa historia ya mshikamano, heshima na uimara wa taifa la Iran.
-
Washington post: Familia Nyingi Zilishiriki Katika Mazishi ya Kiongozi Shahidi wa Iran
Gazeti la Washington Post limesema kuwa Mazishi ya Kiongozi Shahidi wa Iran yalishuhudia ushiriki mkubwa wa wananchi, wakiwemo familia zilizofika na watoto wao, huku yakieleza kuwa tukio hilo lilidhihirisha mshikamano wa kitaifa na uthabiti wa wananchi.
-
Sheikh Isa Qassim: Kiongozi Shahidi alisimama kwa ajili ya Uislamu, Umma na ubinadamu
Mwanazuoni mashuhuri wa Bahrain, Ayatullah Sheikh Isa Ahmad Qassim, amesema kuwa Kiongozi Shahidi Ayatullah Sayyid Ali Khamenei alijitolea maisha yake kwa ajili ya Uislamu, Umma wa Kiislamu na ubinadamu, huku akieleza kuwa urithi wake utaendelea kuongoza njia ya Muqawama na umoja wa Waislamu.
-
Panahian: Iran Itasimama Imara Kulipiza Kisasi cha Kiongozi Shahidi Sayyid Ali Khamenei
Mwanazuoni wa Kiislamu wa Iran, Alireza Panahian, amesema wakati wa mazishi ya Kiongozi Shahidi Sayyid Ali Khamenei kwamba Iran iko tayari kujitolea kwa gharama kubwa ili kuhakikisha kisasi kwa kuuawa kwa kiongozi huyo, akisisitiza kuwa jambo hilo halitaachwa bila majibu.
-
Mshauri wa Kamanda wa IRGC: Mazishi ya Kiongozi Shahidi Ayatullah Sayyid Ali Khamenei Yatakuwa Chachu ya Mabadiliko Makubwa Kanda ya Mashariki ya Kati
Mshauri wa Kamanda wa Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu (IRGC) amesema kuwa mazishi ya Kiongozi Shahidi wa Mapinduzi ya Kiislamu, Ayatullah Sayyid Ali Khamenei, yatakuwa hatua muhimu itakayochochea maendeleo na mabadiliko ya kisiasa katika eneo la Mashariki ya Kati.
-
Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran Akutana na Mwenzake wa Kazakhstan Kujadili Uhusiano wa Nchi Mbili
Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran, Sayyid Abbas Araghchi, amekutana na Waziri wa Mambo ya Nje wa Kazakhstan, Yermek Kosherbayev, ambapo viongozi hao wamejadili kuimarisha ushirikiano wa kidiplomasia na kiuchumi kati ya nchi hizo mbili.
-
Mamia ya Waandishi wa Habari wa Kimataifa Kuutangaza Msiba wa Mazishi ya Kiongozi Shahidi Tehran
Mkuu wa Mkoa wa Tehran ametangaza kuwa kati ya waandishi wa habari 500 hadi 600 wa kimataifa wanatarajiwa kushiriki katika kuripoti hafla ya mazishi ya Kiongozi Shahidi wa Mapinduzi ya Kiislamu, sambamba na maandalizi makubwa ya kiafya na kiusalama kwa ajili ya kuhudumia umati mkubwa wa waombolezaji.
-
Iran: Mabadiliko ya Serikali Hayataathiri Mahusiano Mazuri Kati ya Tehran na Baghdad
Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran amesisitiza kuwa mahusiano kati ya Iran na Iraq ni ya kihistoria na ya kina, yakijengwa juu ya misingi ya kidini, kitamaduni na ujirani, akieleza kuwa mabadiliko ya serikali hayataathiri uhusiano huo wa karibu kati ya mataifa hayo mawili.
-
Iraq Yajitayarisha kwa Mazishi ya Kihistoria na ya Mamilioni ya Waombolezaji kwa Kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu
Kwa mujibu wa taarifa zilizotolewa, kufuatia kuuawa shahidi kwa Kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu, Imam Sayyid Ali Khamenei, na kutokana na maombi ya mara kwa mara ya wanazuoni, viongozi wa makabila na wasomi wa Iraq, miji mitakatifu ya Najaf na Karbala inajiandaa kupokea mamilioni ya waombolezaji katika mazishi ya kihistoria yatakayofanyika tarehe 8 Julai.
-
Ratiba ya Mazishi ya Kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu Iran na Iraq Yatangazwa Rasmi
Msemaji wa Kamati ya Maandalizi ya Kuaga, Kusindikiza na Kuzika mwili wa Kiongozi Shahidi wa Mapinduzi ya Kiislamu, Ayatullah Sayyid Ali Khamenei, ametangaza ratiba kamili ya shughuli hizo zitakazofanyika katika miji ya Tehran, Qum, Mashhad, Najaf na Karbala. Shughuli hizo zinatarajiwa kushuhudiwa na mamilioni ya waombolezaji kutoka Iran na mataifa mbalimbali duniani.
-
Mamilioni ya Wairaq Kuitikia Wito wa Kushiriki Mazishi ya Kiongozi Shahidi wa Mapinduzi
Takribani Wairaq milioni moja wanatarajiwa kushiriki mazishi ya kiongozi shahidi wa Mapinduzi, huku zaidi ya nusu milioni wakitarajiwa kuingia Iran kupitia mpaka wa Mehran kuelekea Tehran, Qum na Mashhad kwa ajili ya maombolezo.
-
Mazishi ya Kamanda Mwandamizi wa Muqawama wa Lebanon yamefanyika katika eneo la Dhahiya;
"Mwenyekiti wa Baraza Kuu la Uongozi wa Hizbullah: Kwa kuuawa kwa maagenti wetu, azma yetu inazidi kuwa imara kuliko hapo kabla”
Sheikh Ali Damuush amesema: “Kulegeza msimamo au kukubali mashinikizo na maagizo ya Marekani na Israel hakutaleta matokeo yoyote. Sisi hatutasalimu amri; hata ikiwa maadui wataweka juhudi zao zote kutuangamiza, kamwe hatutaacha njia ya muqawama (mapambano) wala kujitoa katika kuilinda nchi yetu.”
-
Mazishi ya Mashahidi 300 Wasiojulikana Kufanyika Siku ya Kumbukumbu ya Shahada ya Bi.Fatima(sa); Dalili ya Umoja wa Kitaifa Baada ya Vita vya Siku 12
Kamanda wa Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi (IRGC) wa Mkoa Mkuu wa Tehran, Sardar Hassanzadeh, amesema kuwa miili ya mashahidi 300 wasiojulikana—ikiwa ni pamoja na 200 kwa mikoa mbalimbali na 100 kwa jiji la Tehran—iko tayari kwa ajili ya mazishi ya kitaifa. Mazishi haya yatafanyika Jumatatu tarehe 3 Azar, sambamba na kumbukumbu ya shahada ya Bibi Fatima Zahra (a.s), ambapo msafara maalumu wa “Lale za Fatima” utaanza saa 2:00 asubuhi mbele ya Chuo Kikuu cha Tehran kuelekea kwenye kituo cha "Meraje’ Shohada".