22 Julai 2026 - 19:49
Chanzo cha kijeshi: Iran Ina Azma ya Chuma Kulinda Mamlaka Yake Katika Mlango wa Hormuz

Chanzo cha kijeshi kimenukuliwa na Shirika la Habari la Ahlul-Bayt (as) –ABNA– Kikisema kuwa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran ina azma ya chuma katika kutekeleza mamlaka yake juu ya Mlango wa Hormuz na haitaruhusu eneo hilo la kimkakati kugeuzwa kuwa chanzo cha tishio dhidi yake.

Kwa mujibu wa Shirika la Habari la Ahlul-Bayt (as) –ABNA– Imeripoti kwa kunukuu chanzo cha kijeshi kwamba Iran itaendelea kusimamia kwa uthabiti usalama wa Mlango Bahari wa Hormuz, na kwamba usafiri wa meli kupitia eneo hilo utakuwa salama iwapo utaendeshwa kwa uratibu na Iran na kwa mujibu wa taratibu itakazoweka.

Chanzo hicho kimesisitiza kuwa Iran haitatelekeza azma yake ya kudhibiti Hormuz, kikibainisha kuwa hatua hiyo inalenga kuhakikisha usalama wa muda mrefu wa njia hiyo muhimu ya kimataifa.

Lebo

Maoni yako

You are replying to: .
captcha