Kwa mujibu wa Shirika la Habari la Ahlul-Bayt (as) –ABNA– Imeripoti kwa kunukuu chanzo cha kijeshi kwamba Iran itaendelea kusimamia kwa uthabiti usalama wa Mlango Bahari wa Hormuz, na kwamba usafiri wa meli kupitia eneo hilo utakuwa salama iwapo utaendeshwa kwa uratibu na Iran na kwa mujibu wa taratibu itakazoweka.
Chanzo hicho kimesisitiza kuwa Iran haitatelekeza azma yake ya kudhibiti Hormuz, kikibainisha kuwa hatua hiyo inalenga kuhakikisha usalama wa muda mrefu wa njia hiyo muhimu ya kimataifa.
Maoni yako