meli
-
Iran: Shule ya Minab, Meli ya Dena na Harusi ya Sirik ni ushahidi wa wazi wa uhalifu wa kivita wa Marekani
Naibu Rais wa Iran anayeshughulikia masuala ya kiutendaji, Mohammad Jafar Qaem-Panah, amesema mashahidi wa vita vya siku 12, pamoja na wahanga wa Shule ya Minab, Meli ya Dena na sherehe ya harusi ya Sirik, ni ushahidi wa wazi wa uhalifu wa kivita unaodaiwa kufanywa na Marekani.
-
Iran: Kulenga Meli za Kivita za Marekani ni Sehemu Ndogo tu ya Uwezo Wetu wa Kijeshi
Naibu Spika wa Bunge la Iran, Ali Nikzad, amesema kuwa kulenga meli za kivita za Marekani na kuharibu vituo ambako makamanda wa kijeshi wa Marekani wanapatikana ni sehemu ndogo tu ya uwezo wa kijeshi wa Iran.
-
IRGC: Meli za Kivita za Marekani Zamelazimika Kusogea Kilomita 400 kutoka Mlango-Bahari wa Hormuz
Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu nchini Iran (IRGC) limesema meli za kivita za Marekani zimelazimika kusogea umbali wa takribani kilomita 400 kutoka Mlango-Bahari wa Hormuz, huku mvutano wa kijeshi kati ya Iran na Marekani ukiendelea kuongezeka katika eneo hilo.
-
Iran Yafanya Jaribio la Kombora la Onyo Dhidi ya Meli ya Kivita ya Marekani
Katibu wa Baraza Kuu la Usalama wa Taifa la Iran, Mohsen Rezaei, amesema Iran imefanya jaribio muhimu la kombora dhidi ya meli ya kivita ya Marekani katika kipindi cha saa 48 zilizopita, akilitaja kama hatua ya kuimarisha uwezo wa kuzuia mashambulizi.
-
Tume ya Haki za Binadamu Iran Yalaani Mashambulizi ya Marekani Dhidi ya Meli za Iran
Tume ya Kitaifa ya Haki za Binadamu ya Iran imelaani mashambulizi ya Marekani dhidi ya meli za Iran katika Ghuba ya Uajemi na Bahari ya Oman, ikisema hatua hizo zinakiuka wazi misingi ya sheria za kimataifa, haki za binadamu na juhudi za kulinda amani na usalama wa kimataifa.
-
Iran Yaionya Marekani: Ikiwa Mzingiro wa Baharini Utaendelea, Jeshi la lran Litafanya Mashambulizi Makali Zaidi Dhidi ya Meli za Kijeshi za Marekani
Msemaji wa Makao Makuu ya Khatam al-Anbiya (saww) ya Iran ameionya Marekani kwamba endapo itaendelea kuzuia na kusumbua meli za Iran baharini, Jeshi la Wanajeshi la Iran litazidisha mashambulizi makali zaidi dhidi ya meli za kijeshi za Marekani katika eneo hilo.
-
Iran Yarusha Makombora ya Kupambana na Meli Kuelekea Mlango-Bahari wa Hormuz
Vikosi vya Iran vimeripotiwa kurusha makombora ya kupambana na meli kuelekea Mlango-Bahari wa Hormuz na kulenga meli za kivita za Marekani, huku mvutano wa kijeshi katika eneo hilo ukiendelea kuongezeka.
-
Iran: Njia ya muda ya kupitisha meli katika Mlango wa Hormuz imekubaliwa na Oman
Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran, Kazem Gharibabadi, amesema Iran na Oman zimekubaliana kuhusu njia ya muda ya kupitisha meli katika Mlango wa Hormuz, yenye upana wa maili 7. Amesema ufunguaji kamili wa mlango huo utategemea masharti na mipangilio itakayowekwa na Iran, huku akisisitiza kuwa Tehran bado iko katika hali ya vita.
-
Iran: Meli zitakazoshirikiana na meli zinazokiuka taratibu za Hormuz zitaongezwa kwenye orodha ya wanaokiuka
Mamlaka ya Usimamizi wa Njia ya Maji ya Ghuba ya Uajemi imetangaza kuwa meli zitakazoshirikiana na meli zilizowekwa kwenye orodha ya wanaokiuka taratibu za Iran katika kupita Mlango wa Hormuz zitaongezwa kwenye orodha hiyo na kukabiliwa na vikwazo.
-
USNI: Iran Yavuruga Mnyororo wa Usambazaji wa Meli ya Kubeba Ndege za Kivita USS Abraham Lincoln ya Marekani
Kwa mujibu wa USNI, uharibifu wa kituo kikuu cha logistiki cha Jeshi la Wanamaji la Marekani nchini Bahrain umeathiri mnyororo wa usambazaji wa USS Abraham Lincoln. Meli hiyo imelazimika kupata tena mahitaji yake kutoka Diego Garcia, umbali wa takribani kilomita 3,540. Ripoti hiyo inadai kuwa Waziri wa Vita wa Marekani, Pete Hegseth, ameficha ukubwa halisi wa hasara hizo.
-
Iran: Mlango wa Hormuz Bado Haujafunguliwa, Hakuna Mabadiliko katika Sera ya Tehran
Chanzo cha kisiasa na kiusalama nchini Iran kimesema Mlango wa Hormuz bado haujafunguliwa, huku kikisisitiza kuwa Iran haijafanya mabadiliko yoyote katika sera na taratibu zake kuhusu upitishaji wa meli katika njia hiyo muhimu ya baharini.
-
Yemen Yaongeza Mashambulizi dhidi ya Meli za Mafuta za Saudi, Iran Yasisitiza Vitisho Havitafungua Mlango wa Hormuz
Jeshi la Yemen limetangaza kushambulia meli nyingine ya mafuta ya Saudi katika Bahari Nyekundu na kuahidi kuendelea na operesheni zake za kuzuia usafirishaji wa mafuta. Wakati huo huo, Iran imesema vitisho vya Marekani havitabadilisha msimamo wake kuhusu Mlango wa Hormuz, huku matumaini ya mazungumzo kati ya Tehran na Muscat yakiongezeka.
-
Mvutano wa Hormuz na Bab al-Mandab Waongezeka; Iran Yaweka Masharti ya Usafiri wa Baharini, Yemen Yatangaza Shambulio dhidi ya Meli ya Mafuta ya Saudi
Iran imesema imefikia uelewano wa awali na Oman kuhusu njia inayopendekezwa katika Mlango wa Hormuz, huku ikisisitiza usajili wa kila meli inayoingia na kutoka katika eneo hilo. Wakati huo huo, Yemen imetangaza kushambulia meli ya mafuta ya Saudia katika Ghuba ya Aden, huku ripoti zikionyesha kupungua kwa meli zinazopita Bab al-Mandab na kuongezeka kwa mvutano wa usafiri wa baharini.
-
IRGC: Meli Mbili za Mafuta Zasimamishwa Baada ya Kupuuzia Onyo; Nne Zabadilisha Njia Zao
Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu (IRGC) limesema meli mbili za mafuta zilizodaiwa kukiuka taratibu zilisimamishwa baada ya kupuuza maonyo, huku meli nyingine nne zikibadili mkondo na kurejea zilipotoka. IRGC pia imezitaka kampuni za meli na bima kutopuuzia taarifa zake kwa kutegemea matamko ya Jeshi la Marekani.
-
Zakharova: Shambulio la Ukraine dhidi ya Meli ya Iran ni Mfano wa Wazi wa Kitendo cha Kigaidi
Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Urusi, Maria Zakharova, amekosoa hatua ya Ukraine baada ya kile alichodai kuwa ni shambulio dhidi ya meli ya Iran katika Bahari ya Caspian, akisema tukio hilo ni mfano wa wazi wa ugaidi kwa mujibu wa viwango vya kimataifa.
-
Baghaei: Shambulizi la Ukraine dhidi ya Meli ya Iran ni Uchokozi Hatari, Hatutaacha Bila Jibu
Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran, Esmaeil Baghaei, amelaani shambulizi la Ukraine dhidi ya meli ya Iran, akisema kuwa ni kitendo kisicho halali, kinachokiuka Mkataba wa Umoja wa Mataifa na ni uchokozi hatari ambao Jamhuri ya Kiislamu ya Iran haitauacha bila jibu.
-
Upinzani wa Iraq Waunga Mkono Mkakati wa Yemen wa Kufunga Mlango wa Bab al-Mandab
Abu Alaa al-Wala’i: “Yemen ina haki ya kufunga Mlango wa Bab al-Mandab ili dunia isikie kwamba wananchi wa Yemen hawatakufa kimya.”
-
Chanzo cha kijeshi: Iran Ina Azma ya Chuma Kulinda Mamlaka Yake Katika Mlango wa Hormuz
Chanzo cha kijeshi kimenukuliwa na Shirika la Habari la Ahlul-Bayt (as) –ABNA– Kikisema kuwa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran ina azma ya chuma katika kutekeleza mamlaka yake juu ya Mlango wa Hormuz na haitaruhusu eneo hilo la kimkakati kugeuzwa kuwa chanzo cha tishio dhidi yake.
-
Jeshi la Wanamaji la IRGC: Meli Mbili Zagongana Baada ya Kuvuka Mlango wa Hormuz kwa Njia Isiyo Salama
Jeshi la Wanamaji la IRGC limetangaza kuwa meli mbili zimegongana baada ya kuvuka Mlango wa Hormuz kwa njia isiyo salama, huku meli nyingine mbili zikizuiwa kuendelea na safari ya kuvuka njia hiyo.
-
Jeshi la Iran latangaza hatua ya 13 ya Operesheni "Saa'iqah"; lasema limelenga meli ya Marekani kwa kombora la cruise
Jeshi la Iran limetangaza kuwa katika hatua ya 13 ya Operesheni "Saa'iqah", vikosi vyake vya majini vilirusha kombora la cruise kuelekea meli ya kijeshi ya Marekani kaskazini mwa Bahari ya Hindi, likisema hatua hiyo ilisababisha meli hiyo kujiondoa kutoka eneo hilo.
-
Iran yaokoa mabaharia 23 baada ya meli mbili kugongana katika Ghuba ya Uajemi
Mamlaka ya Bandari na Usafiri wa Baharini ya mkoa wa Hormozgan nchini Iran imefanikiwa kuwaokoa mabaharia 23 baada ya meli mbili za mizigo kugongana katika maji ya pwani ya Bandar Abbas.
-
IRGC Yatangaza Mashambulizi Makali zaidi ya Makombora na Ndege zisizo na Rubani Kujibu Uchokozi wa Marekani
Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu la Iran (IRGC) limetangaza kuanzisha operesheni za makombora na ndege zisizo na rubani kujibu kile lilichokiita uchokozi wa Marekani, huku likionya kuwa litachukua hatua kali zaidi dhidi ya meli zitakazokiuka maelekezo yake.
-
Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi la Iran Latangaza Kufungwa kwa Mlango wa Bahari wa Hormuz
Jeshi la Wanamaji la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu (IRGC Navy) limetangaza kuwa Mlango wa Bahari wa Hormuz umefungwa kwa meli zote na kuonya kuwa chombo chochote kitakachoukaribia kitakuwa kinahatarisha usalama wake.
-
Iran Yadai Meli za Marekani Zimeondoka Bahari ya Oman Baada ya Onyo la Kijeshi
Jeshi la Majini la Iran limetangaza kuwa meli za kivita za Marekani, USS Truxtun na USS Mason, zimeondoka Bahari ya Oman kuelekea Bahari ya Hindi kufuatia kile Iran inachokiita hatua za onyo za kijeshi zilizochukuliwa dhidi yao.
-
IRGC: Meli 28 Zavuka Mlango wa Hormuz ndani ya Saa 24 kwa Uratibu wa Awali
Jeshi la Wanamaji la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu limetangaza kuwa meli 28, zikiwemo meli za mafuta na makontena, zimevuka Mlango wa Hormuz katika saa 24 zilizopita baada ya kupata vibali na kuratibiwa mapema, huku uangalizi wa usalama ukiendelea kwa kutumia mifumo ya kisasa ya kidijitali.
-
-
Marekani Yatwaa Meli ya Mafuta ya Kirusi Iliyo Husiana na Mafuta ya Venezuela
Hali hii inachangia kuongeza mvutano wa kimataifa, huku washirika wa Venezuela na Urusi wakionya kuhusu matokeo yanayoweza kutokea kutokana na hatua hizo za Marekani.
-
Venezuela yaamuru Jeshi la Wanamaji kuandamana na meli za mafuta katikati ya mzingiro wa baharini wa Marekani
Rais wa Venezuela Nicolás Maduro ameagiza jeshi la wanamaji kuandamana na meli zinazobeba mafuta ghafi ya Venezuela kuelekea masoko ya Asia, ikiwa ni hatua ya moja kwa moja ya kujibu kile ambacho Caracas inakiita mzingiro wa baharini uliowekwa na Marekani chini ya Rais Donald Trump.
-
Shamkhani: Sisi sote tuko kwenye meli moja / Inasikitisha ikiwa meli itapata doa au udhaifu
Mwakilishi wa Kamanda Mkuu wa Vikosi vya Ulinzi katika Baraza Kuu la Ulinzi, akisisitiza umuhimu wa kudumisha umoja na mshikamano wa ndani, alisema: "Sisi sote tuko kwenye meli moja ambayo mashahidi wa Mapinduzi ya Kiislamu waliizindua, na inasikitisha ikiwa, kwa bahati mbaya, tofauti zetu zitasababisha doa au pengo katika meli hii."
-
Marekani imeweka vikwazo dhidi ya watu 100 na taasisi mbalimbali kwa sababu ya kununua mafuta kutoka Iran
Serikali ya Donald Trump imeweka vikwazo vipya dhidi ya takriban watu 100, makampuni, na meli. Watu na taasisi hizi wanashutumiwa kushiriki katika ununua na usafirishaji wa mafuta na bidhaa za petrochemical za Iran.