meli
-
Jeshi la Wanamaji la IRGC: Meli Mbili Zagongana Baada ya Kuvuka Mlango wa Hormuz kwa Njia Isiyo Salama
Jeshi la Wanamaji la IRGC limetangaza kuwa meli mbili zimegongana baada ya kuvuka Mlango wa Hormuz kwa njia isiyo salama, huku meli nyingine mbili zikizuiwa kuendelea na safari ya kuvuka njia hiyo.
-
Jeshi la Iran latangaza hatua ya 13 ya Operesheni "Saa'iqah"; lasema limelenga meli ya Marekani kwa kombora la cruise
Jeshi la Iran limetangaza kuwa katika hatua ya 13 ya Operesheni "Saa'iqah", vikosi vyake vya majini vilirusha kombora la cruise kuelekea meli ya kijeshi ya Marekani kaskazini mwa Bahari ya Hindi, likisema hatua hiyo ilisababisha meli hiyo kujiondoa kutoka eneo hilo.
-
Iran yaokoa mabaharia 23 baada ya meli mbili kugongana katika Ghuba ya Uajemi
Mamlaka ya Bandari na Usafiri wa Baharini ya mkoa wa Hormozgan nchini Iran imefanikiwa kuwaokoa mabaharia 23 baada ya meli mbili za mizigo kugongana katika maji ya pwani ya Bandar Abbas.
-
IRGC Yatangaza Mashambulizi Makali zaidi ya Makombora na Ndege zisizo na Rubani Kujibu Uchokozi wa Marekani
Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu la Iran (IRGC) limetangaza kuanzisha operesheni za makombora na ndege zisizo na rubani kujibu kile lilichokiita uchokozi wa Marekani, huku likionya kuwa litachukua hatua kali zaidi dhidi ya meli zitakazokiuka maelekezo yake.
-
Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi la Iran Latangaza Kufungwa kwa Mlango wa Bahari wa Hormuz
Jeshi la Wanamaji la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu (IRGC Navy) limetangaza kuwa Mlango wa Bahari wa Hormuz umefungwa kwa meli zote na kuonya kuwa chombo chochote kitakachoukaribia kitakuwa kinahatarisha usalama wake.
-
Iran Yadai Meli za Marekani Zimeondoka Bahari ya Oman Baada ya Onyo la Kijeshi
Jeshi la Majini la Iran limetangaza kuwa meli za kivita za Marekani, USS Truxtun na USS Mason, zimeondoka Bahari ya Oman kuelekea Bahari ya Hindi kufuatia kile Iran inachokiita hatua za onyo za kijeshi zilizochukuliwa dhidi yao.
-
IRGC: Meli 28 Zavuka Mlango wa Hormuz ndani ya Saa 24 kwa Uratibu wa Awali
Jeshi la Wanamaji la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu limetangaza kuwa meli 28, zikiwemo meli za mafuta na makontena, zimevuka Mlango wa Hormuz katika saa 24 zilizopita baada ya kupata vibali na kuratibiwa mapema, huku uangalizi wa usalama ukiendelea kwa kutumia mifumo ya kisasa ya kidijitali.
-
-
Marekani Yatwaa Meli ya Mafuta ya Kirusi Iliyo Husiana na Mafuta ya Venezuela
Hali hii inachangia kuongeza mvutano wa kimataifa, huku washirika wa Venezuela na Urusi wakionya kuhusu matokeo yanayoweza kutokea kutokana na hatua hizo za Marekani.
-
Venezuela yaamuru Jeshi la Wanamaji kuandamana na meli za mafuta katikati ya mzingiro wa baharini wa Marekani
Rais wa Venezuela Nicolás Maduro ameagiza jeshi la wanamaji kuandamana na meli zinazobeba mafuta ghafi ya Venezuela kuelekea masoko ya Asia, ikiwa ni hatua ya moja kwa moja ya kujibu kile ambacho Caracas inakiita mzingiro wa baharini uliowekwa na Marekani chini ya Rais Donald Trump.
-
Shamkhani: Sisi sote tuko kwenye meli moja / Inasikitisha ikiwa meli itapata doa au udhaifu
Mwakilishi wa Kamanda Mkuu wa Vikosi vya Ulinzi katika Baraza Kuu la Ulinzi, akisisitiza umuhimu wa kudumisha umoja na mshikamano wa ndani, alisema: "Sisi sote tuko kwenye meli moja ambayo mashahidi wa Mapinduzi ya Kiislamu waliizindua, na inasikitisha ikiwa, kwa bahati mbaya, tofauti zetu zitasababisha doa au pengo katika meli hii."
-
Marekani imeweka vikwazo dhidi ya watu 100 na taasisi mbalimbali kwa sababu ya kununua mafuta kutoka Iran
Serikali ya Donald Trump imeweka vikwazo vipya dhidi ya takriban watu 100, makampuni, na meli. Watu na taasisi hizi wanashutumiwa kushiriki katika ununua na usafirishaji wa mafuta na bidhaa za petrochemical za Iran.
-
Ombi la Kikosi cha Uthabiti na Uimara cha Muqawama kwa Serikali za Dunia: “Tuunge Mkono”
Waandaji wa Kikosi cha Uthabiti na Uimara cha Muqawama wametoa wito kwa Serikali za Dunia kusaidia harakati za meli za kikosi hiki kuelekea Ukanda wa Gaza.