mapinduzi
-
Jeshi la Wanamaji la IRGC: Meli Mbili Zagongana Baada ya Kuvuka Mlango wa Hormuz kwa Njia Isiyo Salama
Jeshi la Wanamaji la IRGC limetangaza kuwa meli mbili zimegongana baada ya kuvuka Mlango wa Hormuz kwa njia isiyo salama, huku meli nyingine mbili zikizuiwa kuendelea na safari ya kuvuka njia hiyo.
-
Kwa Nini Iran Ililenga Kambi ya Al-Tanf? Ujumbe wa Kisiasa Unaozidi Ewanja wa Vita
Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu nchini Iran (IRGC) wameripotiwa kulenga kambi ya kijeshi ya Marekani ya Al-Tanf, kusini mwa Syria, katika awamu ya 11 ya operesheni ya “Nasr 2”, huku wachambuzi wakisema umuhimu wa shambulizi hilo unaweza kuwa mkubwa zaidi katika ujumbe wake wa kisiasa na kimkakati kuliko matokeo yake ya moja kwa moja ya kijeshi.
-
Khatibu wa Ijumaa Tehran: Imam Shahidi alivunja nguvu za ubeberu wa kimataifa
Khatibu wa Swala ya Ijumaa mjini Tehran amesema kuwa Imam Shahidi Ayatullah Sayyid Ali Khamenei (r.a.) alichagua njia ya jihadi katika njia ya Mwenyezi Mungu na, kupitia mapambano yake kabla na baada ya ushindi wa Mapinduzi ya Kiislamu, aliweza kuvunja nguvu za ubeberu wa kimataifa.
-
IRGC Yathibitisha kuharibu rada za Marekani za udhibiti wa baharini na anga nchini Oman
Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu (IRGC) limedai kuharibu rada za Marekani za udhibiti wa baharini katika Miamba ya Salamah na rada ya udhibiti wa anga katika eneo la Ghanam nchini Oman, katika mwendelezo wa operesheni iliyopewa jina la "Nasr 2 / Ushindi 2".
-
Iran yatangaza kufungwa kwa muda kwa Mlango wa Bahari wa Hormuz hadi itakapotolewa taarifa nyingine
Jeshi la Wanamaji la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu (IRGC) limetangaza kufungwa kwa muda kwa Mlango wa Bahari wa Hormuz, likisema hatua hiyo inalenga kulinda usalama wa eneo hilo kufuatia matukio ya hivi karibuni ya kijeshi na baharini.
-
Brigedia Jenerali Ali Fadavi: Ushahidi wa Imam Shahidi Khamenei Umeufanya Njia ya Mapinduzi ya Kiislamu Kuwa Wazi Zaidi
Mkuu wa Kundi la Washauri wa Makao Makuu ya Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu (IRGC), Brigedia Jenerali Ali Fadavi, amesema kuwa ujasiri ulikuwa sifa kuu ya Imam Shahidi Sayyid Ali Khamenei na kwamba ushahidi wake umeifanya njia ya Mapinduzi ya Kiislamu kuwa wazi zaidi.
-
Chuo cha Al-Mustafa (s) Tanzania Kuaandaa Kongamano la Kielimu Kumuenzi Imam Shahidi Sayyid Ali Khamenei(ra)
Kitengo cha Utafiti wa Kisayansi cha Chuo Kikuu cha Al-Mustafa (s) Tawi la Dar es Salaam - Tanzania kitaandaa Kongamano la Kielimu lenye anuani "Imam Khamenei: Kutoka Jihadi hadi Ushahidi," likiwa na lengo la kuchambua kwa ufupi Maisha ya Kiongozi huyo wa Mapinduzi ya Kiislamu, na hatimaye kukuachia msikilizaji na mfuatiliaji Nafasi ya kupata mazingitio na masomo mbalimbali ya kimaisha kutoka katika kumbukumbu ya Maisha yake Matukufu, katika muktadha ule ule wa Maelekezo ya Qur'an Tukufu aliposema Mwenyezi Mungu: Hakika kuna mazingatio ndani ya visa vyao (Historia Yao) kwa watu wenye Akili"
-
Rais Pezeshkian Aishukuru Iraq kwa Kuandaa Mazishi ya Kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu Sayyid Ali Khamenei (ra)
Rais wa Iran, Masoud Pezeshkian, ameishukuru serikali na wananchi wa Iraq kwa mapokezi na ushirikiano walioutoa wakati wa shughuli za kuaga na kusafirisha mwili wa Kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu, Ayatullah Sayyid Ali Khamenei, akisema taifa la Iran halitasahau kamwe mshikamano huo.
-
Kamanda Abdollahi: Tutawalipiza Kisasi Waliomuua Kiongozi Shahidi Sayyid Ali Khamenei (ra)
Kamanda wa Makao Makuu ya Khatam al-Anbiya (s), Luteni Jenerali Ali Abdollahi, amesema Iran itaendelea kufuatilia na kuwaadhibu waliomuua Kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu aliyeuawa shahidi pamoja na mashahidi wengine.
-
Jeshi la Wanamaji la Walinzi wa Mapinduzi: Wageni Hawana Haki katika Mlango wa Hormuz
Jeshi la Wanamaji la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu (IRGC Navy) limesema kuwa mataifa ya kigeni hayana haki yoyote katika eneo la Iran na Mlango wa Hormuz, likionya kuwa hatua za kijeshi za Marekani zinatishia usalama wa njia hiyo muhimu ya kimataifa.
-
Kisa cha Kihistoria:Jinsi na Kwa Nini Shahidi Hujjatul Islam Sayyid Abdul Karim Hashimi Nejad Aliuawa na Shirika la Kigaidi la Mujahideen-e Khalq /MEK
Kwa mujibu wa simulizi za kihistoria, kuuawa kwa Shahidi Hujjatul Islam Sayyid Abdul Karim Hashimi Nejad mnamo mwaka 1981 kulikuwa sehemu ya mfululizo wa mauaji yaliyotekelezwa na Shirika la Kigaidi la Mujahideen-e Khalq (MEK), likiwa na lengo la kuwaondoa viongozi waliokuwa na mchango mkubwa katika kuimarisha Mapinduzi ya Kiislamu nchini Iran.
-
IRGC Yatangaza Kushambulia Malengo 85 ya Kijeshi ya Marekani kwa Kujibu Mashambulizi ya Marekani
Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu nchini Iran (IRGC) limetangaza kuwa limeanzisha hatua ya awali ya kujibu mashambulizi ya Marekani kwa kushambulia malengo 85 ya kijeshi ya Marekani katika eneo la Mashariki ya Kati kwa kutumia makombora na ndege zisizo na rubani.
-
Msanii wa Iran: Shahidi Sayyid Ali Khamenei alitupanda ndani yetu mapenzi ya sanaa na ukweli
Msanii wa Iran Hussein Esmati amesema kuwa kufariki shahidi kwa Sayyid Ali Khamenei kumewaathiri kwa kina wasanii wa Iran, jambo lililoonekana katika kazi nyingi za kisanii zinazoakisi maombolezo, mapenzi na maadili aliyoyasimamia.
-
kamanda wa jeshi la majini la Iran: muqawama haujafungwa tena na mipaka ya kijiografia
Kamanda wa Jeshi la Majini la Iran, Admiral Shahram Irani, amesema kuwa Muqawama sasa umevuka mipaka ya kijiografia, akisisitiza kuwa mataifa na vikosi vya Muqawama vinaendelea kuimarisha umoja na mshikamano katika kukabiliana na changamoto.
-
Ayatollah Makarim Shirazi: Waliomuua Kiongozi Shahidi Hawataepuka Adhabu ya Mwenyezi Mungu
Ayatollah Nasser Makarim Shirazi amesema wahusika na wapangaji wa mauaji ya Kiongozi Shahidi wa Mapinduzi ya Kiislamu, pamoja na waliohusika na umwagaji damu wa viongozi, raia wasio na hatia na watoto, hawataokoka adhabu ya Mwenyezi Mungu, huku akisisitiza kuwa damu zao takatifu haitasahaulika kamwe.
-
Mshauri wa Kamanda wa IRGC: Mazishi ya Kiongozi Shahidi Ayatullah Sayyid Ali Khamenei Yatakuwa Chachu ya Mabadiliko Makubwa Kanda ya Mashariki ya Kati
Mshauri wa Kamanda wa Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu (IRGC) amesema kuwa mazishi ya Kiongozi Shahidi wa Mapinduzi ya Kiislamu, Ayatullah Sayyid Ali Khamenei, yatakuwa hatua muhimu itakayochochea maendeleo na mabadiliko ya kisiasa katika eneo la Mashariki ya Kati.
-
Araghchi apongeza msimamo wa Jamhuri ya Congo wa kuiunga mkono Iran katika majukwaa ya kimataifa
Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran, Sayyid Abbas Araghchi, ameishukuru Jamhuri ya Congo kwa msimamo wake wa kuendelea kuiunga mkono Iran katika majukwaa ya kimataifa, huku Waziri wa Mambo ya Nje wa Kongo akiwasilisha salamu za rambirambi na mshikamano kwa taifa la Iran.
-
Picha ya Kihistoria ya Mwili Mtukufu wa Kiongozi Shahidi Imam Sayyid Ali Khamenei Yashuhudiwa Jijini Tehran
Shirika la Habari la Kimataifa la Ahlul-Bayt (as) – ABNA – limechapisha picha ya karibu zaidi ya mwili mtukufu wa Kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu, Shahidi Ayatullah Mkuu Imam Sayyid Ali Khamenei (Qudsallahu Nafsahu Az-Zakiyyah), katika ukumbi wa Msikiti wa Imam Khomeini (Quds Sirruh), huku mamilioni ya watu duniani wakiendelea kuomboleza na kumuenzi kama “Imamu wa Wanyonge”.
-
Iran: Mabadiliko ya Serikali Hayataathiri Mahusiano Mazuri Kati ya Tehran na Baghdad
Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran amesisitiza kuwa mahusiano kati ya Iran na Iraq ni ya kihistoria na ya kina, yakijengwa juu ya misingi ya kidini, kitamaduni na ujirani, akieleza kuwa mabadiliko ya serikali hayataathiri uhusiano huo wa karibu kati ya mataifa hayo mawili.
-
Mazingira ya Mazishi ya Imam Shahidi (r.a) Kufanyika kwa Maelekezo ya Kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu
Katibu wa Kamati ya Kitaifa ya Kuaga na Kusimamia Mazishi ya Imam Shahidi (r.a) amesema kuwa maandalizi ya mazishi hayo yanafanyika kwa uongozi na maelekezo ya Kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu, Ayatullah Sayyid Mujtaba Husseini Khamenei, huku akizitaka vyombo vya habari kuhifadhi tukio hilo la kihistoria kwa ajili ya vizazi vijavyo.
-
Chuo cha Kiislamu cha Wafuasi wa Ahlul-Bayt (a.s) Chafanya Majlisi ya Maombolezo ya Muharram - Dar es Salaam
Jamiatul Mustafa International Foundation - Chuo cha Kiislamu cha Wafuasi wa Ahlul-Bayt (a.s.) jijini Dar es Salaam kimefanya majlisi ya maombolezo ya Muharram, ambapo mhadhiri alikuwa Dkt. Reihan Yasin.
-
Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi la Iran Latangaza Kufungwa kwa Mlango wa Bahari wa Hormuz
Jeshi la Wanamaji la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu (IRGC Navy) limetangaza kuwa Mlango wa Bahari wa Hormuz umefungwa kwa meli zote na kuonya kuwa chombo chochote kitakachoukaribia kitakuwa kinahatarisha usalama wake.
-
Majlisi ya kuhuisha kumbukumbu ya Imam Hussein (a.s) katika Shule ya Wasichana ya Bibi Zaynab (s.a) – Kigamboni, Dar es Salaam
Katika shule ya wasichana ya Shule ya Bibi Zaynab (sa) kumefanyika hafla ya kuhuisha kumbukumbu ya Imam Hussein (a.s) kwa lengo la kuimarisha utamaduni wa Ashura na kuelimisha nafasi ya mwanamke katika Uislamu.
-
Araghchi: Ujumbe wa Kiongozi wa Mapinduzi ni Mwanga wa Njia kwa Diplomasia ya Iran
Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran, Abbas Araghchi, amesema ujumbe wa hivi karibuni wa Kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu ni mwongozo muhimu kwa maafisa wote wa sera za nje na utasaidia kulinda heshima ya taifa pamoja na haki za wananchi wa Iran.
-
Qalibaf: Tutatekeleza Maelekezo ya Kiongozi wa Mapinduzi na Kulinda Haki za Taifa la Iran
Spika wa Bunge la Iran, Mohammad Baqer Qalibaf, amesema ujumbe wa Kiongozi wa Mapinduzi ni ramani ya njia ya kurejesha haki za taifa la Iran na Kambi ya Muqawama, akisisitiza kuwa hawataruhusu upande mwingine kukiuka ahadi wala kukanyaga haki za wananchi wa Iran.
-
Pezeshkian: Ujumbe wa Kiongozi wa Mapinduzi ni Ramani ya Kulinda Maslahi ya Taifa katika Mazungumzo
Rais Masoud Pezeshkian amesema ujumbe wa hivi karibuni wa Kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu unaweka dira ya mazungumzo yajayo na kuhakikisha maslahi ya taifa la Iran yanalindwa kikamilifu.
-
Kiongozi wa Mapinduzi Atoa Ujumbe kwa Wairan Kuhusu Makubaliano kati ya Iran na Marekani
Kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu amesema aliruhusu kutiwa saini kwa hati ya makubaliano kati ya Iran na Marekani baada ya kupokea dhamana kutoka kwa Rais wa Iran kwamba haki za wananchi wa Iran na Kambi ya Muqawama zitalindwa, huku akisisitiza kuwa mazungumzo ya baadaye hayatamaanisha kujisalimisha kwa matakwa ya Marekani.
-
Diplomasi wa Iraq Athibitisha Ushiriki wa Raia Wake na Kujadili Mradi wa Reli Kati ya Iran–Iraq
Balozi Mkuu wa Iraq katika Mji wa Kermanshah, Saadoun Al-Saadi, amesema makundi mbalimbali ya wananchi wa Iraq yako tayari kushiriki katika shughuli za kijamii na pia amejadili na viongozi wa Iran kuhusu mradi wa reli unaounganisha Kermanshah na Baghdad kwa ajili ya kurahisisha usafiri na kuimarisha ushirikiano wa kiuchumi.
-
IRGC: Vikosi vya Iran Viko Tayari Kujibu Uchokozi Wowote kwa Nguvu
Naibu Kamanda wa Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu, Brigedia Jenerali Yadollah Javani, amesema silaha yenye nguvu zaidi ya Iran ni imani na itikadi ya wananchi wake, akisisitiza kuwa diplomasia na uwezo wa kijeshi vinaenda sambamba katika kulinda haki na maslahi ya taifa.
-
IRGC Yadai Kushambulia Malengo Manne ya Kijeshi ya Marekani Nchini Jordan
Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu ya Iran (IRGC) wamedai kufanya mashambulizi ya makombora yaliyolenga maeneo manne muhimu ya kijeshi ya Marekani katika kambi ya Al-Azraq nchini Jordan, ikiwa ni pamoja na kituo cha amri na udhibiti.