Kwa mujibu wa Shirika la Habari la Kimataifa la Ahlul-Bayt (AS) -ABNA-, Rais wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran, Masoud Pezeshkian, amesema kuwa ujumbe wa hivi karibuni wa Kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu umeweka ramani ya njia ya kulinda maslahi ya taifa katika mchakato wa mazungumzo yajayo.
Katika taarifa yake iliyotolewa kufuatia ujumbe wa kimkakati wa Kiongozi wa Mapinduzi uliotolewa Alhamisi jioni kuhusu mwelekeo wa mazungumzo na makubaliano ya kumaliza vita, Rais Pezeshkian alieleza shukrani zake kwa mwongozo na uungwaji mkono huo.
Alisisitiza kuwa maelekezo hayo yanafafanua mfumo wa jumla wa mchakato wa mazungumzo, yanaainisha wajibu wa taasisi husika, na yanatoa dira ya kuhakikisha maslahi ya taifa la Iran yanalindwa kikamilifu katika hatua zote za mazungumzo yajayo.
Your Comment