Pezeshkian
-
Rais Pezeshkian Aishukuru Iraq kwa Kuandaa Mazishi ya Kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu Sayyid Ali Khamenei (ra)
Rais wa Iran, Masoud Pezeshkian, ameishukuru serikali na wananchi wa Iraq kwa mapokezi na ushirikiano walioutoa wakati wa shughuli za kuaga na kusafirisha mwili wa Kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu, Ayatullah Sayyid Ali Khamenei, akisema taifa la Iran halitasahau kamwe mshikamano huo.
-
Rais Pezeshkian: Marekani Inakiuka Sheria katika Siasa na Michezo, Iran Itatetea Haki Zake
Rais wa Iran, Masoud Pezeshkian, amesema ukiukaji wa sheria na udanganyifu ni sifa zinazotawala mwenendo wa Marekani katika siasa na michezo, akisisitiza kuwa Iran haitakubali vitendo hivyo na itaendelea kutetea haki zake kwa uthabiti.
-
Rais Pezeshkian: Juhudi za Pakistan za Kuimarisha Amani Zimejikita Katika Utamaduni Wake Tajiri
Rais wa Iran Masoud Pezeshkian amesema kuwa juhudi za Pakistan katika kuimarisha amani katika eneo la Mashariki ya Kati na Asia zina mizizi katika utamaduni wake tajiri, akisisitiza uhusiano wa karibu na malengo ya pamoja kati ya Tehran na Islamabad.
-
Pakistan: Ziara ya Rais Pezeshkian Islamabad Yaakisi Dhamira ya Pamoja ya Amani na Maendeleo ya Kikanda
Wizara ya Mambo ya Nje ya Pakistan imesema ziara rasmi ya Rais wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran, Masoud Pezeshkian, nchini Pakistan inaonesha azma ya pamoja ya Tehran na Islamabad ya kuimarisha uhusiano wa kihistoria na kitamaduni, pamoja na kuendeleza amani, utulivu na maendeleo endelevu katika eneo.
-
Pezeshkian: Ujumbe wa Kiongozi wa Mapinduzi ni Ramani ya Kulinda Maslahi ya Taifa katika Mazungumzo
Rais Masoud Pezeshkian amesema ujumbe wa hivi karibuni wa Kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu unaweka dira ya mazungumzo yajayo na kuhakikisha maslahi ya taifa la Iran yanalindwa kikamilifu.
-
Rais Pezeshkian: Ushirikiano wa Kimkakati kati ya Iran na Urusi Unaendelea Kupanuka
Rais wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran, Masoud Pezeshkian, amesema ushirikiano wa kimkakati kati ya Tehran na Moscow unaendelea kuimarika na kupanuka, akisisitiza dhamira ya kuendeleza mahusiano hayo kwa manufaa ya mataifa yote mawili.
-
Rais Pezeshkian: Umoja wa Kitaifa Ndiyo Mtaji Mkubwa Zaidi wa Iran Katika Kipindi Hiki
Rais Masoud Pezeshkian amesema mshikamano wa kitaifa ndio msingi wa maendeleo ya Iran, akisisitiza matumizi ya uwezo wa wataalamu na kujibu mahitaji ya wananchi ili kutatua changamoto zinazoikabili nchi.
-
Rais Pezeshkian: Vitisho vya Kulenga Miundombinu Vinadhihirisha Udhaifu Dhidi ya Uamuzi wa Taifa
Rais wa Iran Masoud Pezeshkian amesema kuwa vitisho vya kushambulia miundombinu muhimu ya nchi hiyo vinaonyesha udhaifu wa wapinzani mbele ya uamuzi na mshikamano wa wananchi wa Iran.
-
Pezeshkian: Aya za Qur’ani ni mwaliko unaoleta mwanga katika maisha na tabia njema
Rais wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran, Dkt. Masoud Pezeshkian, katika ujumbe wake kwa kongamano la kuheshimu wahifadhi na wahudumu wa Markazi ya Qur’ani Tukufu, amesema kuwa Aya za Qur’ani ni mwaliko wa kutafakari kwa undani, mwaliko unaoweza kuangazia na kuongoza maisha na mienendo ya mwanadamu.
-
Pezeshkian: Iran daima imesimama imara mbele ya Dhoruba za Historia / Watenda jinai ambao mwenendo wao ni kuua watoto, hawastahili kuitwa Binadamu
Rais wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran, amesema kuwa Iran, hii ndiyo ustaarabu wa kale zaidi unaoendelea duniani, na daima imesimama imara mbele ya dhoruba za historia. Taifa hili, kwa roho kuu na azma isiyokoma, mara nyingi limethibitisha kwamba haliinamii mbele ya wavamizi; na leo pia limesimama kwa heshima mbele ya wanyakuzi, likitegemea nguvu ya imani na mshikamano wa kitaifa