Rais wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran, Dkt. Masoud Pezeshkian, katika ujumbe wake kwa kongamano la kuheshimu wahifadhi na wahudumu wa Markazi ya Qur’ani Tukufu, amesema kuwa Aya za Qur’ani ni mwaliko wa kutafakari kwa undani, mwaliko unaoweza kuangazia na kuongoza maisha na mienendo ya mwanadamu.
Rais wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran, amesema kuwa Iran, hii ndiyo ustaarabu wa kale zaidi unaoendelea duniani, na daima imesimama imara mbele ya dhoruba za historia. Taifa hili, kwa roho kuu na azma isiyokoma, mara nyingi limethibitisha kwamba haliinamii mbele ya wavamizi; na leo pia limesimama kwa heshima mbele ya wanyakuzi, likitegemea nguvu ya imani na mshikamano wa kitaifa