Rais Salva Kiir na kiongozi wa waasi, Riek Machar, walisaini makubaliano hayo ambayo sasa yanazileta pamoja kambi mbili zinazopingana ndani ya chama tawala cha Vuguvugu la Ukombozi wa Sudan Kusini (SPLM).
Waziri wa mambo ya kigeni wa jamhuri ya kiislamu ya Iran Mohammad Javad Zarif amesema leo kwamba kuhusika zaidi kwa Urusi kunaweza kuharakisha mazungumzo yenye lengo la kufikia makubaliano muhimu juu ya mzozo unaohusisha mpango wake wa kinyuklia.